TCRA mchukulieni hatua huyu Nabii Tito, channel yake ya YouTube inamdhihaki Yesu

TCRA mchukulieni hatua huyu Nabii Tito, channel yake ya YouTube inamdhihaki Yesu

YEHODAYA

JF-Expert Member
Joined
Aug 9, 2015
Posts
36,902
Reaction score
52,001
TCRA na vyombo husika mchukulieni hatua huyu nabii Tito channel yake youtube kaandika YESU ni shetani

Hii ni hatari kwa jamii oneni wenyewe
1636349676600.png
 
Wanachafua picha ya nchi yetu kimataifa, imagine mtu ana blog inahoji matumizi ya serikali anatafutwa akamatwe ila kuna zumbukuku mmoja zao la milembe anatamba na mada zake za hovyo
 
Uhuru uliopitiliza siku zote una madhara tu kwahiyo hawa manabii na maaskofu wapewe utaratibu maalumu wa kupata mamlaka hayo na sio kujipachika vyeo kama vipi tuludi enzi za kupigana mawe hadharani
 
Kama kuna watu iwe binafsi au vyombo vya dola vinamtumia kwa kumdhamini huyu jamaa kuropoka ujinga wake kule youtube basi vinafanya vibaya sana

Wanafanya hivyo ili ku achieve kitu gani sijui! Uropokaji wake(maana yale sio mahubiri) unatia kinyaa. Sidhani kama ni jambo la busara kuacha mtu mmoja akashifu dini yenye waumini zaidi ya milioni ishirini hapa nchini

Mwaka ule wa uchaguzi(2020) nilipokua namuona huyu jamaa yupo pale round about ya Maringo Kawe akipeperusha bendera ya chama fulani nikajua hapa tayari yupo kwenye payroll. Ila lengo ka kumtumia bado sijalielewa na hakika halina maana
 
Huyu ni wa kupigwa fatwa. Na anafanya haya baada ya kusoma kuwa Wakristo hawana kuuna ukikashifu Yesu, wangelikuwa wenzetu angelikuwa maiti leo!
 
Imani zetu zinatofautiana sana, na ni lazima tuheshimu Imani za watu wengine tofauti na sisi tunavyo amini

TCRA tuanze na Ndugai aliyesema "Yesu na Mke wake walitembea kwa miguu hadi Galilaya"
 
Uyu chizi kwa nini walimtoa jela na uko milembe,angebaki uko waendelee kumtafuna kiboga
 
Hizi ndiyo gharama za haki za uhuru wa kutoa maoni! Haki inayoliliwa na wanademokrasia.

Tusicopy na kupaste aina za demokrasia zisizo na tija kwa taifa letu. Tujifunze kujitegemea.
 
Hawa wahuni akina tito washukuru Mungu kwenye ukristo hakuna munkari na jazba, wahuni wanakunya na kuharisha uharo kunuka wala hakuna mkristo anaoshughulika nao. Ole wao wangeidhihaki ile dini na mtume wao cha mtema kuni wangekiona
 
Nabii Tito
Nabii Shilla

MATHAYO 7: 15-21
Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali.

Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti?
Vivyo hivyo kila mti mwema huzaa matunda mazuri; na mti mwovu huzaa matunda mabaya.
Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mwovu kuzaa matunda mazuri.
Kila mti usiozaa tunda zuri hukatwa ukatupwa motoni.
Ndiposa kwa matunda yao mtawatambua.

Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.



EZEKIELI 22: 25-26
Fitina ya manabii wake imo ndani yake, kama simba angurumaye akirarua mawindo; wamekula roho za watu; hutwaa kwa nguvu hazina na vitu vya thamani; wameongeza hesabu ya wajane wake ndani yake.

Makuhani wake wameihalifu sheria yangu, wametia unajisi vitu vyangu vitakatifu; hawakuweka tofauti ya vitu vitakatifu na vitu vya kutumiwa sikuzote; wala hawakuwafundisha watu kupambanua vitu vichafu na vitu vilivyo safi, nao wamefumba macho yao, wasiziangalie sabato zangu, nami nimetiwa unajisi kati yao.


MIKA 3: 11
Makuhani wake hufundisha ili wapate ijara, na manabii wake hubashiri ili wapate fedha; ila hata hivyo watamtegemea Bwana, na kusema, Je! Hayupo Bwana katikati yetu? Hapana neno baya lo lote litakalotufikia.


NEHEMIA 6: 12-13
Nikatambua, na tazama, siye Mungu aliyemtuma; lakini amefanya unabii huu kinyume changu; nao Tobia na Sanbalati ndio waliomwajiri.


🙏
 
Back
Top Bottom