TCRA mchukulieni hatua huyu Nabii Tito, channel yake ya YouTube inamdhihaki Yesu

TCRA mchukulieni hatua huyu Nabii Tito, channel yake ya YouTube inamdhihaki Yesu

Huyu nabii Tito anamuita Yesu ni shetani kule nabii billionaire Shilla anamuita Yesu mwizi..basi ni tafrani

Uhuru wa kupitiliza ulio ktk ukristo unafanya baadhi ya watu kuhama katka reli na kuishia kudhalilisha dini

Sent from my CPH1923 using JamiiForums mobile app
Halafu mumu humu JF Don Namilison naye kaweka yake halafu Admin wapo kimya tu.
 
Nabii Tito
Nabii Shilla

MATHAYO 7: 15-21
Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali.
Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti?
Vivyo hivyo kila mti mwema huzaa matunda mazuri; na mti mwovu huzaa matunda mabaya.
Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mwovu kuzaa matunda mazuri.
Kila mti usiozaa tunda zuri hukatwa ukatupwa motoni.
Ndiposa kwa matunda yao mtawatambua.
Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.

[emoji120]

Mathayo 24:11 Na Manabii Wengi Wa Uongo Watatokea Na Kudanganya Wengi
 
Wanachafua picha ya nchi yetu kimataifa, imagine mtu ana blog inahoji matumizi ya serikali anatafutwa akamatwe ila kuna zumbukuku mmoja zao la milembe anatamba na mada zake za hovyo
Ccm huyo hawez kukamatwa.
 
Kwani TCRA inasoma biblia? Inajuaje kama ni kweli ama si kweli?? Hebu acheni kuchanganya mambo. Mteteeni huyo Yesu wenu acheni kulia lia

Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app
vipi kuhusu mtume wenu adhalilishwe, utasema tcra haisomi quran? Kama hamjaanza kumtetea wenyewe kwa jazba.
 
Alipokuwa anaonesha Biblia imeandikwa CCM mbona mlikaa kimya? Nyoka mlimfuga wenyewe acheni awatemee mate.
Na yale magauni yake yenye rangi ya kijani kibichi kwa nakshi ya msaraba wa njano.

Kipindi cha kampeni 2020 alikua akishinda ma manguo ya kijani roundabout ya kawe, walikaaa kimyaaaa
 
Kwani TCRA inasoma biblia? Inajuaje kama ni kweli ama si kweli?? Hebu acheni kuchanganya mambo. Mteteeni huyo Yesu wenu acheni kulia lia
Siku watapokuja na mada ya mitume wako uje uandike hivi hivi.
 
Wako wapi madaktari wa afya akili watuainishie aina za watu wenye ukichaa? Maana wengine wanaonekana ni wazima si wachafu wala hawaokoti makopo kumbe ni vichaa wa uhakika
 
Hivi mbona kwenye uislam hakuna vituko kama hivi? Hakika ukristo umetamalaki uhuru
 
Back
Top Bottom