TCRA yasimamisha kipindi cha EFATHA cha Nabii Josephat Elias Mwingira kwa miezi mitatu, Star TV yapewa onyo

TCRA yasimamisha kipindi cha EFATHA cha Nabii Josephat Elias Mwingira kwa miezi mitatu, Star TV yapewa onyo

Mwambieni huyo mbweha kuwa nipo hapa siku 3 then nitaondoka.
yani hapo Yesu anawaambia watu wamwambie mtawala. Anamuita rais au mfalme mbweha .
kama mfalme aliitwa mbweha huyu mama tumuite jina la mnyama gani?
Kahaba
 
Tanzania kuna wajinga wengi sana iku hizi iwapo mtu kama huyu naye eti ana wafuasi wanaompa hela za sadaka. Ukishasikia mtu anajiita Mtume au Nabii ujua ana tatizo wala usimsikilize kabisa.

Vile vile wanaoitwa Askofu bila kuwa na structure yoyote ujue pia ni tatizo, kwani askofu hupatikana kwa structure fulani; kwa mfano huwezi kuwa na waziri mkuu pasipokuwapo mawaziri.

Lakini Tanzania leo imejaa hawa mitume, manabii na maaskofu wasioelewaka na bado wana wafuasi sana.
 
Hivi chui jike anaelewa outcome ya kila jambo analolifanya? 🤣 🤣 Napata tabu sana kuelewa uwezo wa washauri wake wa karibu kwa haya yanayoendelea
Mshauri wa rais ni waziri mwenye dhamana.
 
Zilongwa Mbali, Zitendwa Mbali
Choni Mnyangu!!!
 
Mwambieni huyo mbweha kuwa nipo hapa siku 3 then nitaondoka.
yani hapo Yesu anawaambia watu wamwambie mtawala. Anamuita rais au mfalme mbweha .
kama mfalme aliitwa mbweha huyu mama tumuite jina la mnyama gani?
"Chui jike" ushaga sikia sauti yake?...ng'weeu ng'weeeu!
 
ndiyo maana watu kama hawa huwaga wanapotea tu na wapotee tu maana hawana maana kuendelea kuwepo anaacha kuhubiri anaanza mapambano na serikali ngoja ushauri wa kagame utumike muone sasa mtakuwa mnaongelea wapi ujinga wenu huo kweli mamlaka mnayaona kama shangazi zenu?huyo siyo mtumishi maana hata vitabu vinasema tutii mamlaka yeye anatukana mamlaka senzi sana huyo jamaa
Mkuu,,,,, Kama wewe sio mmoja kati ya waliofungia kipindi Basi utakuwa chawa kindakindaki wa bimkubwa wa ikulu!!

Ungeacha tu watawala wapewe vidonge vyao , maana huu ndyo uzalendo
 
Tatizo binadamu wa siku hizi ni wabishi sana...
 
Hawa TCRA inaonesha uwezo wao wa kung'amua mambo ni mdogo sana.Hawaoni kuwa tozo,kufukuza machina na kuporomoka kwa uchumi ni upiumbavu unaofanywa na serikali?ifike mahali taasisi za serikali ziajili watu wenye uwezo na sio hawa wa kusifusifu hata kwenye upumbavu na upuuzi

Sent using Jamii Forums mobile app

Kama namba moja anapenda kuabudiwa na kusifiwa kwa kufanywa "mungu - mtu" hata wangepewa wenye uwezo kama malaika bado hali ingekuwa hivi hivi.

Tatizo la Tanzania sio watu,tatizo la Tanzania ni "namba moja".
 
Nimpongeze Raisi Mama Samia kufanya mabadiliko ya mawaziri na kumtoa Simbachawene mambo ya ndani waziri aliyepo Masauni katumia hekima kubwa Ku deal na hilo tatizo tofauti na yule mwehu Simbachawene waziri aliyekuwepo ambaye hekima hana hata asilimia moja

Mwingira kakosea lakini Masauni katoa solution peaceful
 
TCRA mimekifungia kwa muda wa miezi 3 kipindi cha Nabii na Mtume Josephat Mwingira wa Efatha Ministry kinachorushwa mubashara kila Jumapili kupitia Star tv.

Aidha TCRA imewataka Star tv kuomba radhi siku 3 mfululizo kwa kushindwa kusimamia maadili ya habari.

Inadaiwa Nabii Mwingira alitoa maneno yenye ukakasi kuihusu serikali katika mahubiri yake.

Source: Chomoza tv
 
Kamati ya Maadili ya TCRA imesema Kituo cha Star Tv kimeonesha uzembe na udhaifu katika kusimamia kipindi cha EFATHA Ministries ambacho hurushwa kwa matangazo ya moja kwa moja, kwa kuruhusu maudhui yenye ukakasi ambayo ni kinyume na Kanuni za Mawasiliano...
Mbona Sasa nawewe umerudia Hayo maneno yenye ukakasi hapa?

"Serikali fanyeni upuuzi wenu Mungu amewaruhusu, lakini muda sio mrefu atakuja kumalizana na upumbavu wenu"

Hutasababisha tufungiwe?
 
Back
Top Bottom