Mad Max
JF-Expert Member
- Oct 21, 2010
- 26,961
- 77,890
Wakuu.
Hii nchi ni huru, kila mtu ana ruksa ya kuvaa nguo yoyote anayopenda kikubwa asivunje sheria tu za nchi.
Ila kuna baadhi ya mavazi, mwanaume sio vizuri kuvaa na kutoka nje kutembea nje mbele ya kadamnasi. Hapa ni baadhi ya mifano mitano (5):
1. Vipensi kuonesha Mapaja.
Kuna watu wanavaa pensi fupi sana na za kubana, zinaonesha mapaja nje nje. Na wanatembea comfortably kwenye malls au mitaani.
Ni kweli hatuwapangii maisha, ila sio vizuri Mwanaume kuonesha mapaja yako nje nje.
Mbadala:
Kama ni mdau wa pensi tafuta dude pana linaficha ata magoti ukiwa umekaa. Unaweza tupia jeans, au kama za basketball.
Hayo ni mawazo yangu tu.
2. Jeans za kubana au kuchanika chanika.
Hii inaendana na vipensi, sio poa kijana unavaa jeans la kubana sana au lilochanika chanika.
Mbadala vaa tu slim jeans, au track inayokufit ila sio kukubana ivo wala imechanwa.
Iko poa itakupendeza.
3. Crocks na ndala.
Hizi Crocks kuna wanaume wanavaa hafu wanatoka out kabisa comfortably.
Hapa unaweza kuvaa ndani na mtaani tu labda unaenda shop, au upo beach.
Mbadala:
Kuna sandals za kiume unaweza ukavaa na ukaonekana vizuri sana.
Huna haja ya kuvaa madude aya kitoto au kivulana mitaani.
4. T-shirt zenye maandishi au Alama za ajabu.
Kuna hizi Tshirt either by coincidence au purpose unakuta ina maneno na wewe una nunua inaivaa.
Mwanaume vaa tu plain tshirt au simple one word kama unataka maneno mengi vaa zako jezi tosha kabisa.
5. Nguo za Mfanano na Mpenzi wako kipindi cha Matukio.
She is my Queen. Au My Valentine. nk. Tuwaachie madogo wa Magufuli Hostel.
Asanteni.
Narudia kusema, ayo ni mawazo binafsi. Karibuni kwa mawazo yenu.
Hii nchi ni huru, kila mtu ana ruksa ya kuvaa nguo yoyote anayopenda kikubwa asivunje sheria tu za nchi.
Ila kuna baadhi ya mavazi, mwanaume sio vizuri kuvaa na kutoka nje kutembea nje mbele ya kadamnasi. Hapa ni baadhi ya mifano mitano (5):
1. Vipensi kuonesha Mapaja.
Kuna watu wanavaa pensi fupi sana na za kubana, zinaonesha mapaja nje nje. Na wanatembea comfortably kwenye malls au mitaani.
Ni kweli hatuwapangii maisha, ila sio vizuri Mwanaume kuonesha mapaja yako nje nje.
Mbadala:
Kama ni mdau wa pensi tafuta dude pana linaficha ata magoti ukiwa umekaa. Unaweza tupia jeans, au kama za basketball.
Hayo ni mawazo yangu tu.
2. Jeans za kubana au kuchanika chanika.
Hii inaendana na vipensi, sio poa kijana unavaa jeans la kubana sana au lilochanika chanika.
Mbadala vaa tu slim jeans, au track inayokufit ila sio kukubana ivo wala imechanwa.
Iko poa itakupendeza.
3. Crocks na ndala.
Hizi Crocks kuna wanaume wanavaa hafu wanatoka out kabisa comfortably.
Hapa unaweza kuvaa ndani na mtaani tu labda unaenda shop, au upo beach.
Mbadala:
Kuna sandals za kiume unaweza ukavaa na ukaonekana vizuri sana.
Huna haja ya kuvaa madude aya kitoto au kivulana mitaani.
4. T-shirt zenye maandishi au Alama za ajabu.
Kuna hizi Tshirt either by coincidence au purpose unakuta ina maneno na wewe una nunua inaivaa.
Mwanaume vaa tu plain tshirt au simple one word kama unataka maneno mengi vaa zako jezi tosha kabisa.
5. Nguo za Mfanano na Mpenzi wako kipindi cha Matukio.
She is my Queen. Au My Valentine. nk. Tuwaachie madogo wa Magufuli Hostel.
Asanteni.
Narudia kusema, ayo ni mawazo binafsi. Karibuni kwa mawazo yenu.