TEC: Mhashamu Baba Askofu Wolfgang Pisa, Rais Mpya TEC. Rais Samia atuma salamu za pongezi

TEC: Mhashamu Baba Askofu Wolfgang Pisa, Rais Mpya TEC. Rais Samia atuma salamu za pongezi

ABC ZA 2025

JF-Expert Member
Joined
May 2, 2018
Posts
1,299
Reaction score
832
20240623_125317.jpg
Askofu Wolfgang Pisa

Rais Samia kupitia mitandao yake ya kijamii ameandika haya kumpongeza Mhashamu Askofu Wolfgang Pisa

Pongezi za dhati kwa Mhashamu Askofu Wolfgang Pisa, Askofu wa Jimbo Katoliki Lindi kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC). Kuchaguliwa kwako katika nafasi hii ya uchungaji kwa Kanisa Katoliki nchini ni matokeo ya imani na matarajio ya Kanisa kwa utumishi wako.

Nanukuu maneno mawili toka katika Biblia Takatifu kwenye Injili ya Yohana 19:28, “...Naona kiu” ambayo pia uliyachagua kuwa kaulimbiu yako ya Uaskofu. Katika utumishi huu nakuombea kiu ya kuendelea kufanya kazi ya kujenga Kanisa kwenye misingi ya upendo, haki, kweli, kujali masikini, umoja, amani, mshikamano, utu na kuhudumia jamii na Watanzania kwa ujumla, ndani na nje ya Kanisa Katoliki.

Nakutakia kila la kheri. Mwenyezi Mungu akushike mkono na kukuongoza.
 
Wametoa waraka kulaani mauaji ya mtakatifu Asimwe yaliyoratibiwa na kasisi wao Padre Elpidius ?
 
kanisa katoliki limechafuliwa sana na hili la paroko kutuhumiwa mauwaji ya mtoto albino

wanaonekana kama kuna mambo mengi ndani yao hayako sawa
 
kanisa katoliki limechafuliwa sana na hili la paroko kutuhumiwa mauwaji ya mtoto albino

wanaonekana kama kuna mambo mengi ndani yao hayako sawa
Tangu lini katoliki ilikuwa safi. Huduma na makanisa yote ni vichaka vya maovu kwa miaka mingi.

1. Ufiraji na unajisi ndani ya katoliki ni suala sugu.
2. Migogoro ya kugomabania madaraka na fedha ndani ya KKKT ni suala sugu.
3. Migawanyiko inayosababishwa na fedha ndani ya Pentecostal churches inayopelekea kuibuka kwa huduma za mtu mmoja mmoja (ministries) ni suala sugu.
4. Biashara ya madawa ya kulevya na ulozi ndani ya ministries ni suala sugu
 
Kuna viongozi wakichaguliwa hakuna hata anayejua wala chombo chochote Cha habari kuripoti sababu Hawana uzito mfano akiteuliwa kiongozi wa Baraza la Maulamaa la Anwsar sunna hata hakuna anayejua wanajua wenyewe lakini Mufti wa Bakwata akichaguliwa mpya magazeti na vyombo vyote vya habari lazima vitangaze
 
Back
Top Bottom