TEC toeni tamko kukemea ubaguzi kwenye elimu

TEC toeni tamko kukemea ubaguzi kwenye elimu

hapa watakuja na mapovu tu ,usitegemee majibu ya kueleweka
kwamba unataka majibu gan ya kueleweka ? kwan TEC ndo wanashughulikia swala la elimu , kwama hakuna elimu nje ya shule za TEC ? anza kumsimamia mwanao sio kumlea kijinga
 
Tunaomba baraza katoliki la maaskofu (TEC) kukemea kwa sauti moja ubaguzi unaofanyika chini ya shule ambazo zinaendeshwa na kanisa katoliki hapa nchini.

Ni muda sasa shule husika kuchagua wanafunzi kwa misingi ya kuhakikisha ya kwamba mwanafunzi yoyote yule ambae anaonekana kutokuwa na uwezo wa kimasomo anatengwa ama kwa kuhamishwa shule au kurejeshwa nyumbani.

Shule ambazo zimekuwa sugu kwa kutoa elimu kwa ubaguzi ni pamaja na Santa Augustine (Tagaste),St joseph na nyinginezo nyingi tu.

TEC ni taasisi kubwa hivyo tunawaombeni mtoe kauli moja kuhusu utoaji wa Elimu kwa misingi ya ubaguzi ambao umeota mizizi kwenye shule zinazomilikiwa na TEC na hata zile ambazo zimeamua kwa makusudi kabisa kuiga huu unyama kwenye utoaji elimu hapa nchini.

Tanzani yetu ni moja.
hizo shule nazo ni za umma kama bandari?
Kama bharesa asivyoingiliwa kwenye kutoa ajira,kadharika na shule za watu binafsi ziachiwe kufanya waonavyo kikubwa wasivunje sheria za nchi.
 
Back
Top Bottom