TEC toeni tamko kukemea ubaguzi kwenye elimu

TEC toeni tamko kukemea ubaguzi kwenye elimu

Issue sio TEC watoe tamko bali Wizara ya Elimu kama mtoto ulimchukua form one au darasa la kwanza kwamba ana uwezo kama akipwaya basi ameharibika mikononi mwako haya mambo ya kumfukuza ili wote wapate one hence kuongeza soko ni Upuuzi unaofanywa na shule nyingi sio Katoliki tu....

Elimu ni kumtoa mtu hatua moja mpaka nyingine sio kiwanda cha kuzalisha Division one...
Waanze na vyuo vikuu
 
Kumwondoa mwanafunzi anaesoma pale Tagaste kisha hajifukisha wastani wa A ni ubaguzi uliopitiliza
Ungeanza na serikali maana inabagua wanafunzi waliopata division zero form four kwenda form five.
 
Tunaomba baraza katoliki la maaskofu (TEC) kukemea kwa sauti moja ubaguzi unaofanyika chini ya shule ambazo zinaendeshwa na kanisa katoliki hapa nchini.

Ni muda sasa shule husika kuchagua wanafunzi kwa misingi ya kuhakikisha ya kwamba mwanafunzi yoyote yule ambae anaonekana kutokuwa na uwezo wa kimasomo anatengwa ama kwa kuhamishwa shule au kurejeshwa nyumbani.

Shule ambazo zimekuwa sugu kwa kutoa elimu kwa ubaguzi ni pamaja na Santa Augustine (Tagaste),St joseph na nyinginezo nyingi tu.

TEC ni taasisi kubwa hivyo tunawaombeni mtoe kauli moja kuhusu utoaji wa Elimu kwa misingi ya ubaguzi ambao umeota mizizi kwenye shule zinazomilikiwa na TEC na hata zile ambazo zimeamua kwa makusudi kabisa kuiga huu unyama kwenye utoaji elimu hapa nchini.

Tanzani yetu ni moja.
 
Wewe ndo hujitambui kabisa? Nani alikuambia ili uishi na ufanikiwe lazima usome shule za taasisi za dini? Kila shule ujiwekea vigezo ambavyo mzazi au mwanafunzi lazima kukizi, ukishindwa kosa si la taasisi bali ni lako mwenyewe! Shule ziko nyingi za kusoma! Nenda shule za umma/serikali kwani umekatazwa? Bichwa limejaa makamasi halina akili alafu unang'ang'ana usome shule za washua? Hiyo shule ya babaako? Shwaini! Kalaghabao!
Rubbish
 
Tunaomba baraza katoliki la maaskofu (TEC) kukemea kwa sauti moja ubaguzi unaofanyika chini ya shule ambazo zinaendeshwa na kanisa katoliki hapa nchini.

Ni muda sasa shule husika kuchagua wanafunzi kwa misingi ya kuhakikisha ya kwamba mwanafunzi yoyote yule ambae anaonekana kutokuwa na uwezo wa kimasomo anatengwa ama kwa kuhamishwa shule au kurejeshwa nyumbani.

Shule ambazo zimekuwa sugu kwa kutoa elimu kwa ubaguzi ni pamaja na Santa Augustine (Tagaste),St joseph na nyinginezo nyingi tu.

TEC ni taasisi kubwa hivyo tunawaombeni mtoe kauli moja kuhusu utoaji wa Elimu kwa misingi ya ubaguzi ambao umeota mizizi kwenye shule zinazomilikiwa na TEC na hata zile ambazo zimeamua kwa makusudi kabisa kuiga huu unyama kwenye utoaji elimu hapa nchini.

Tanzani yetu ni moja.
Mnafanya Waislamu waonekane wapuuzi kumbe kuna Waislamu Wana akili na busara kubwa. Shule imeset standards zake mwanafunzi asipofikia haruhusiwi kuendelea. Hapo kuna ubaguzi gani wewe kibaraka?
 
Huwezi elewa maana wewe inawezekana ni mmoja wa wale wanaondekeza ubaguzi kwenye utoaji wa Elimu
Peleka Mtoto wako kwenye shule za Mazuzu wenzio ziko nyingi tu usitupigie kelele.
 
Wamezoea kutumia Basha kupata nafasi, TEC hawana mchezo Kwa elimu.
Kuna shule za level zao, kila taasisi ina vigezo vyake. Au hilo no ajabu? Basi na shule za serikali zingekuwa zinachukua wanafunzi wote.
 
Unaelewa maana ya ubaguzi kwani shule za serikali siku hizi wanafunzi vilaza wanafanywaje, enzi zile usipofaulu tu mitihani wa kidato Cha nne ni umejifuta mwenyewe
 
Waanze na vyuo vikuu
Hapana Vyuo vikuu kuna standards sio lazima kila mtu aende kwenye fani fulani kama huko unapwaya unaweza kwenda VETA au sehemu tofauti..., huku chini ni msingi na moja kati ya kazi zao ni kuhakikisha mtu ana msingi mzuri na kumpatia training (after all kufeli ni zero) kwahio kama walimchukua mtoto baada ya la saba au vidudu wakiona kwamba yupo sawa kama akishuka kiwango basi ni wenyewe ndio wapo responsible na ushukaji kiwango chake kwahio waendelee nae....

Hii fukuza low graders ni ili shule zionekane hazina three ili zipate wateja (mwisho wa siku tume-focus kuna one ngapi kwa watu kukariri na kuiba mitihani kuliko mtu / watu wameelewa kiasi gani au tumewakwamua kiasi gani) Tunatengeneza a lot of uneducated certified students who have highly performed on paper
 
hapa watakuja na mapovu tu ,usitegemee majibu ya kueleweka
Mkuu hata Yanga au Simba wanasajili wachezani wenye uwezo mkubwa na sio Kila mchezaji. Na hao wenye uwezo mkubwa huendelea kuchezea team hizo, na uwezo ukishuka wanapigwa chini. Serekali ndio Ina wajibu wa kuchukua mwanafunzi yoyote maana ni jukumu la serekali kutoa elimu kwa wanachi wake. Taasisi binafsi Zina vigezo vyake.
 
Back
Top Bottom