"Technically" Godbless Lema hawezi kurejea nchini mpaka baada ya miaka Mitano (5)

"Technically" Godbless Lema hawezi kurejea nchini mpaka baada ya miaka Mitano (5)

Kwahyo wakuu mnaojua hivi vitu inamaana Roma nae anaishi bure na kulipwa posho huko USA?

Hata ningekuwa mimi nisingerudi, mtu kama Roma hiyo ni chance ya maisha hakuwa na ndoto za kukanyaga USA achilia mbali kuishi bure.
 
Leo ngoja niandike kitu kimoja watu wapate uelewa hasa MATAGA wanaosema mbona Tundu Lisu na Lema hawarudi. Nitaongelea zaid kwa Lema.

Katika maisha wanasema "golden chance never comes twice" katika kitu Lema amekipata cha maisha yake yote ni kupata ukimbizi wa kisiasa "asylum seeker" inchini CANADA ndugu zangu hii deep down bwana Lema atamshukuru JPM mpaka kufa.(nitasema kwanini hapo mbele)

Nasema hivi kwasababu kwa hali ya kawaida kabisa kwa nchi yetu wenye uwezo wa kupata "Ukazi wa kudumu" kulingana na sifa na vigezo vya nchi hii moja kwa moja bila kupitia elimu (student pathways) ni wachache sana sana kwa sababu kupata CRS 463(MINIMUM POINT OF NOMINATION) sio kazi ya siku moja ni miaka hata 2 kujipanga ili uwe na vigezo vyote unapoomba via Express Entry (EE)

Vigezo kama;
  1. Umri.
  2. Elimu (lazima ithibitishwe na Canadian Institute inaitwa "ECA"),
  3. Uwezo wa kuzungumza Lugha (English/French) lazima ufanye test,
  4. SALIO la kutosha c$13,000 kwa mtu mmoja lazima ulionyeshe Bank + c$4,000 kwa kila member anaeongezeka kama ni familia ya watu 5 unatakiwa uonyeshe c$30,000.
  5. Afya ya mhusika na wanaomzunguka na n.k
Toka kuomba ahdi kukubaliwa muda hautapingua chini ya mwaka mmoja. nadhani unaona ilivo ngumu kwa nchi zetu ukitoa Rais na Makamu wake wengine woote kazi si ndogo hata uwe tajiri kiasi gani ukipitia EE pathways mfumo wenyewe unakutema mapema bila kutimiza vigezo.

Turudi kwa Lema.
Lema alipata "convetion refugee" akaingia nchi ya ahadi automatic huwezi kurudi nyumbani ndugu zangu sitaki niwafiche huu ndio ukweli, kwasababu
  1. watoto ambao angelipa ada ya 60m+ pale IST hapa anasoma bure bin bure tena gari linamfata na kumshusha mtoto mlangoni afu Pale Feza Int'l ada ni Ths 15m+ kwa chekechea kwa mwaka
  2. hapa mtoto wa miaka 18 yupo chuo kikuu mwaka wa 1 na tayari huyu anafanya kazi na analipwa pesa yake
  3. mazingira yamepangika, hakuna wahuni na wala rushwa
haya yote ananufaika nayo hata yoyote angenufaika nayo, sidhani kama ungerudi na unajua kabisa uwezo wa kulipa ada mwisho ni 2m kwa mwaka

Mwaka fulani wakatangaza wanarudi, nikasema "haiwezi tokea" nadhani LEMA alipata lawyer makini saana angetia mguu tu TANZANIA angekua salama angevunja kipengele cha "People in Need of Protection" hapa asingeweza kurenew visa via "asylum seeker" na wale CBSA office they are very well trained aisee.

Baada ya miaka 5+ toka GODBLESS LEMA atue CANADA ndio NAWAHAKIKISHIA ATARUDI TANZANIA ambapo atakua tayari ni PERMANENT RESIDENT kwasababu anaruhusiwa kuomba PR baada ya miaka 5 kama Asylum Seeker.


Mwisho; JPM wakati mwingine anashukuriwa chinichini.
Vipi madeni yake huku TZ Nani anapaswa kulipa kisheria?
 
Back
Top Bottom