Teknolojia isiathiri utu wetu, Polisi Tanzania msifanye kazi kwa mhemko. Trafiki 2 warudi Ofisini haraka

Teknolojia isiathiri utu wetu, Polisi Tanzania msifanye kazi kwa mhemko. Trafiki 2 warudi Ofisini haraka

Moja ya matukio ya Hovyo ni kuchukua Trafiki video wanapokusanya mapato ya kuchomwa na jua la siku nzima hizi video zinalengo la kudhalilisha Trafic na sio sawa na yeyote mwenye hii Tabia aache… na jeshi la polisi Tz hili lichukuliwe kwenye Taswira ya kudhalilisha jeshi.

Trafic hajawahi kumlazimisha mtu kuchangia mapato ya kuchomwa na jua ! It is your choices ni ulipe fine ya 30,000 au umalizane nae hapo hapo yote ni sawa.

Ni makosa mapato ya kuchomwa na jua yatafsiriwe kama rushwa !! Kama polisi -Tanzania mnataka kweli ku deal na rushwa nendeni kwenye mikataba ya hiyo nchi kama DP World, Mikataba ya madini, Ujenzi wa SGR, ujenzi wa mwendokasi…. Huko ndio kuna Big fish Corruption

Mshahara wa Rais ni 139M ….. ambae 24 hours yupo kwa AC, , mshahara wa mawaziri ni mnono and yet wanapiga deal fake na muda wote wanakula mema ya nchi, watoto wa marais na mawaziri kama kina Abdul ambao hawana history ya nchi…. Wanakula mema na kupiga deal fake…. Goli moja linanunumia kwa 5M na chanzo cha fedha hakijulikana. Polisi yote hayo hamdeal nayo mnaenda ku deal na vi elf mbili mbili wanavopewa trafic kama mapato ya kuchomwa na jua !

Soma Pia: Trafiki wawili wakamatwa baada ya kunaswa kwenye video wakipokea Rushwa hadharani

Polisi TZ acheni mihemko ya kila kitu cha mitandao mkitolee ufafanuzi au ku deal nacho au kuwachukulia hatua watendaji wenu ! Mengine ni hayana msingi dilini na mambo makubwa yanayoikabili nchi kama vile Rushwa zinazofanywa na viongozi wakuu, utekaji n.k

Pamoja na mambo mengine mnatakiwa ku deal na watu wanao rekodi trafic wanapokuwa kwenye majukumu yao ya kukusanya mapato ya kuchomwa na jua, hao watu wakamatwe na wafanywe mfano maana wanadhalilisha watendaji wa jeshi la usalama wa barabarani. HAIKUBALIKI

Otherwise hao trafic warudi Ofisin haraka na ni aibu kamanda mkuuu kusimama kwa media kuongelea mambo kama hayo, ni kukosa weledi

Ni Nani aliyemuua Ali Kibao?

Yupo wapi Ben Saane?

Amekufa au yupo hai; kwenye mila zetu za Kichaga hii damu italipwa kwa namna yoyote mpaka
Mtuletee majivu yake tuyazike with our ritual proceedures or else the game is not over and our hearts are still bleeding

Tunataka kusikia ni nani aliyempiga Tundu Lissu risasi in the government yard ?

Tunataka kusikia Soka yupo wapi ?

Tunataka kusikia wabakaji wa binti wa Dovya wapo wapi ? Tunataka kusikia nani alimteka Nondo?

Hayo ndio majukumu yenu ya msingi

N.K
Hayo mengine ni hayana ishu kwa taifa;

Dr Megalodon, PhD Candidate
WHO Regional Office
Rue 52 , Ottawa
Canada
Eeeh
 
Wale nao walijiachia sana bhana, yaan hadi vibegi wamebeba na traffic kwa kucheza mchezo huwaambii kitu😆😆, uhakika wa kupata laki mbili kwa siku wanao,

Hata hivyo hao hawawezi kufukuzwa kazi zaidi zaidi wataondolewa road wabaki vituoni
Acha utani, laki mbili kwa hizo buku mbilimbili na sio gari zote ni daladala tu na wengine huwa hawato na hapo kuna ganji ya mkulu
 
Hili jambo limeinbua mitazamo finyu san kwa wa Tz wengi walioandk kutoa thread jamii forum.

Naendelea kuamin kuw kwa akili hiz tutaisubr haki itufate nyumbn na mae deleo.
Huu utetezi unaouona humu sio kwamba watu wanatetea uhalifu na wahalifu la hasha !
Bali watu wanajua vizuri kabisa kwamba wanyonge ndio waathirika wakuu wa kushughulikiwa na hizo sheria zilizopo kwa sababu wao ndio soft target na ndio wako wazi zaidi wanaoweza kupatikana kwa urahisi zaidi katika hayo makosa kutokana na hali halisi ya vipato na maisha yao kwa ujumla !
Ilihali lile tabaka jingine haligusiki kutokana na Mazingira jinsi yalivyo !
 
Traffic wanatusadia Sana barabarani hata kama wanatuandikia notification ni moja ya kazi zao..
Huyo jamaa aliyerekodi video ni mshamba Tu , kuna matukio mengi yanafanyika barabarani lkn hatuna muda wa kijinga WA kurekodi video.

Kama kila kosa wangekuwa wanatupiga faini watu wasingeingiza magari Yao barabarani, mara nyingi traffic wanakuwa watu wema Sana tena sanaa
Jamaa aliyerekodi hiyo video ni mtu anayejiekewa sana, akili kubwa. Kila anayekuwa katika eneo anapoweza kurekodi uhalifu(criminal activities) kama huo wa kupokea/kutoa rushwa afanye hivyo kwani huwa wanasaidia kwa namna moja au nyingine kuuweka bayana ushahidi wa uhalifu. Ingekuwa vizuri kama serikari ingekuwa inawafikiria wazalendo wa aina hii(to motivate the mass) kwa kuirahisishia serikali/vyombo vya ulinzi na usalama katika upelelezi wake.
Uhalifu uwe mkubwa au mdogo una madhara katika jamii yetu. Kama kuna makosa ambayo watu hupaswa kilulipa kihalali na kupewa stakabathi pesa ikaingia serikalini lakini badala yake inatoka rushwa na kuingia mifukoni mwa wahuni/majizi in uniforms.
 
Trafiki hawana mambo mengi
(Wasio trafiki)Polisi wana mambo mengi
Aliyerekodi alitakiwa awarekodi hawa polisi au wanaoitwa wasiojulikana au watekaji
Atawarekodi vipi wakati hajawaona wakifanya huo uhalifu? Kila raia mwema arekodi uhalifu anaouona. Mtu yuko Kawe, anawezaje kurekodi uhalifu unaofanyika Tabata?
 
Ruge alisema hakuna kitu anaogopa kama Mungu na texnolojia.Police ifike sehem wabadilishe mifumo yao ya utendaji kazi.Ukiangali taasisi zingine zimeadvance sana lakin Jeshi letu bado linaendelea na mifumo ileile ya mwaka 47.Tabia ya matraffic kuchukuachukua elfu 2 au tano barabaran ni tangu watu tuko watoto na tunakaribia miaka 50 sasa hv.
Mpaka leo serikali imeashindwa kuweka mfumo wa kuzuia rushwa na kuboresha maisha ya askari wake.
Kwann tusiweke camera zinazocharge faini automatically kwa makosa flanflan kupunguza human interaction.
Daladala nyingi ni mbovu sana na hazifai kuwa barabarani.
Tunaweza kabisa kuforce level seat na mabasi yakaongezwa (refer kipindi cha Covid).
Vituo vya daladala havieleweki/vidogo sana bila uwepo wa traffic daladala wanaziba njia.
Najiuliza hv police hawajapata IGP mwenye maono makubwa?,Au ni political post so anayeteuliwa anafuata amri za wateule.Lakin taasisi zingine pia wakuu wake wanateuliwa. Au police haina competent personnel.
 
Mimi nadhan Polisi wa deal na watu wanaorekedi; hao wawe termed kama wadhalilishaji wa jeshi la polisi



Ila ya Ali kibao aaanh
Nondo aanh
Kwa upande mwingine ninaweza kukubaliana na wewe kwamba police walipaswa kuanza na hao big fishes wanaosomwaga na CAG mara Kwa nara, ila kwenye hiki kipande umeandikia upumbavu mtupu.

Kwa hiyo Sasa hivi mtu akirecord vitendo viovu vinayofanywa na civil servants ni mdhalilishaji? Na waliodhalilishwa ni hao wafanya maovu(wapokea rushwa Kwa hii case hapa)???

Kwa hiyo hapa mtu aliyechukua hiyo video kuonesha umma jinsi Gani jeshi letu la usalama barabarani lisivyotimiza wajibu wake ipasavyo Kwa kuendekeza rushwa ndogo ndogo ni criminal na anastahili kishughulikiwa? Halafu hao askari ni victims wa udhalilishaji WA huyo mchukua video??

Aisee yaani umeishi nchi iliyostaharabika kama Canada na pia ni mwanafunzi wa PHD Lakini una reasoning ya kipumbavu kiasi hiki??

Halafu hapo hapo unaongelea suala la mzee ALLY KIBAO kwamba waliomuua wako wapi, haya tukitumia hii hii reasoning yako huoni kwamba wangetokea watu waku record tukio la ALLU KIBAO kukamatwa na wenyewe pia ungewaita ni wadhalilishaji WA jeshi la police? Maana tunaambiwa hata waliomkamata huyo KIBAO ni hao hao jeshi la police..!!

Wewe akili huna kabisa, siungi mkono adhabu kutolewa Kwa hao askar, ila kitendo Cha kusema huyo mchukua video amedhalilisha jeshi la police ni upumbavu na kuendekeza kasumba za kishenzi za kuficha maovu.
 
Mfumo wote wa jeshi la polisi umejaa failures, yamejazana majinga jinga mshahara mdogo, makazi duni, weledi hafifu, zero exposure. Zimejaa ng'ombe ambazo zimeridhika na maisha ya kifukara. Amkaa acheni kulinda wezi wachache wanao umiza mamilioni ya raia.

Pamoja na kwamba unaweza kuwa na hoja, nakushauri usidhalilishe taaluma za watu kwani PhD student/holder hawezi kuwakilisha hoja kwa namna hiyo.....
Nikusaidie tu kuwa; mambo ya kisheria ni taaluma nyingine na maanisha unaweza kuwa na mtazamo lakini usiwe na hoja kisheria au niseme, huwezi kuhalaisha kosa kwa kutumia kosa au ni seme huwezi kutetea kosa kwa kutumia kosa.....
 
Honestly, mimi sikutegemea mtu anayesema yuko Canada kutangaza hadharani kabisa kuwa anaunga mkono utoaji na upokeaji wa rushwa.
NIMESIKITIKA SANA!
Kaka huyu mleta mada licha ya kuishi kwenye nchi zenye civilization/ustaharabu ya Hali ya juu, lakini bado ana ujinga na unyani Mwingi sana kichwani, sijui hata kwenye hiyo level ya PHD amefika vipi.

Hawa ndio wale wasomi wakitoka huko nje hakuna Cha maana wanachokuja kuongeza Kwa taifa zaidi ya kututisha na lugha ya kingereza, na ndio wanakuwaga mafisadi wakubwa wanaolitia taifa hasara Kwa mikataba mibovu yenye mchanganyiko wa rushwa ndani yake..!!

Na ndio maana Magu Kuna muda alikuwa anawadharau sana Hawa wasomi na PHDs zao za Mchongo.

Mtu anashindwa hata kujua Moja ya sababu za kuongezeka Kwa ajali za barabarani ni madereva kuendesha vyombo vya moto vyenye makosa KIBAO, na hii ni Kwa sababu mamlaka za usimamizi wa sheria za barabarani hazifanyi kazi Yao kwa waledi zaidi ya kuendekeza rushwa.
 
Wale nao walijiachia sana bhana, yaan hadi vibegi wamebeba na traffic kwa kucheza mchezo huwaambii kitu😆😆, uhakika wa kupata laki mbili kwa siku wanao,

Hata hivyo hao hawawezi kufukuzwa kazi zaidi zaidi wataondolewa road wabaki vituoni
Tinaomba historia yako kuanzia ulivyo zaliwa mpaka sasa una zeeka lini uta itoa ewani
 
Huu utetezi unaouona humu sio kwamba watu wanatetea uhalifu na wahalifu la hasha !
Bali watu wanajua vizuri kabisa kwamba wanyonge ndio waathirika wakuu wa kushughulikiwa na hizo sheria zilizopo kwa sababu wao ndio soft target na ndio wako wazi zaidi wanaoweza kupatikana kwa urahisi zaidi katika hayo makosa kutokana na hali halisi ya vipato na maisha yao kwa ujumla !
Ilihali lile tabaka jingine haligusiki kutokana na Mazingira jinsi yalivyo !
Umeeleza vzr mkuu , ila tutakaa kwenye ujinga huu hadi lin ? ,
Unatak kusema kuw mmiliki alie nunua costa ya 90Million atashindwa kutimiza kanuni za barabarani ?
Unazan wote wanao toa hongo (daladala driver wanamakosa , ?) wengin wanatzmiza tuu mazoea kuepusha kubabikiwa na kusumbuliwa .



Ila mabadiliko yanapaswa yaanzie juu huko na chini (mifumo ya elimu) matumiz ya teknolojia yanawez kupunguz rushwa na urasimu kwa 90%
 
Mfumo wote wa jeshi la polisi umejaa failures, yamejazana majinga jinga mshahara mdogo, makazi duni, weledi hafifu, zero exposure. Zimejaa ng'ombe ambazo zimeridhika na maisha ya kifukara. Amkaa acheni kulinda wezi wachache wanao umiza mamilioni ya raia.
Naunga mkono hoja hasa nikikumbuka lile tukio la Gongo la Mboto siku ya kura.

Mwananchi anajaribu kuzuia mtu wa ccm kuingiza kura bandia ndani ya kituo cha kura, polisi anampiga risasi na kumuua ili kutetea na kulinda wizi, dah!!!
Na hadi sasa hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa!
Laana ya Polisi ni nzito na kubwa mno
 
Moja ya matukio ya Hovyo ni kuchukua Trafiki video wanapokusanya mapato ya kuchomwa na jua la siku nzima hizi video zinalengo la kudhalilisha Trafic na sio sawa na yeyote mwenye hii Tabia aache… na jeshi la polisi Tz hili lichukuliwe kwenye Taswira ya kudhalilisha jeshi.

Trafic hajawahi kumlazimisha mtu kuchangia mapato ya kuchomwa na jua ! It is your choices ni ulipe fine ya 30,000 au umalizane nae hapo hapo yote ni sawa.

Ni makosa mapato ya kuchomwa na jua yatafsiriwe kama rushwa !! Kama polisi -Tanzania mnataka kweli ku deal na rushwa nendeni kwenye mikataba ya hiyo nchi kama DP World, Mikataba ya madini, Ujenzi wa SGR, ujenzi wa mwendokasi…. Huko ndio kuna Big fish Corruption

Mshahara wa Rais ni 139M ….. ambae 24 hours yupo kwa AC, , mshahara wa mawaziri ni mnono and yet wanapiga deal fake na muda wote wanakula mema ya nchi, watoto wa marais na mawaziri kama kina Abdul ambao hawana history ya nchi…. Wanakula mema na kupiga deal fake…. Goli moja linanunumia kwa 5M na chanzo cha fedha hakijulikana. Polisi yote hayo hamdeal nayo mnaenda ku deal na vi elf mbili mbili wanavopewa trafic kama mapato ya kuchomwa na jua !

Soma Pia: Trafiki wawili wakamatwa baada ya kunaswa kwenye video wakipokea Rushwa hadharani

Polisi TZ acheni mihemko ya kila kitu cha mitandao mkitolee ufafanuzi au ku deal nacho au kuwachukulia hatua watendaji wenu ! Mengine ni hayana msingi dilini na mambo makubwa yanayoikabili nchi kama vile Rushwa zinazofanywa na viongozi wakuu, utekaji n.k

Pamoja na mambo mengine mnatakiwa ku deal na watu wanao rekodi trafic wanapokuwa kwenye majukumu yao ya kukusanya mapato ya kuchomwa na jua, hao watu wakamatwe na wafanywe mfano maana wanadhalilisha watendaji wa jeshi la usalama wa barabarani. HAIKUBALIKI

Otherwise hao trafic warudi Ofisin haraka na ni aibu kamanda mkuuu kusimama kwa media kuongelea mambo kama hayo, ni kukosa weledi

Ni Nani aliyemuua Ali Kibao?

Yupo wapi Ben Saane?

Amekufa au yupo hai; kwenye mila zetu za Kichaga hii damu italipwa kwa namna yoyote mpaka
Mtuletee majivu yake tuyazike with our ritual proceedures or else the game is not over and our hearts are still bleeding

Tunataka kusikia ni nani aliyempiga Tundu Lissu risasi in the government yard ?

Tunataka kusikia Soka yupo wapi ?

Tunataka kusikia wabakaji wa binti wa Dovya wapo wapi ? Tunataka kusikia nani alimteka Nondo?

Hayo ndio majukumu yenu ya msingi

N.K
Hayo mengine ni hayana ishu kwa taifa;

Dr Megalodon, PhD Candidate
WHO Regional Office
Rue 52 , Ottawa
Canada
Binafsi nafurahishwa sana na kamanda mkuu wa usalama barabarani na wasaidizi wake wanaopita mikoa mbalimbali kuwasimamia kwa umakini madereva wa mabasi masafa marefu.

mtoa mada nikupe mfano umepanda basi unatoka moshi kuja Dar halafu dereva wa basi akaovateki Kwenye mteremko mkali na mbele kuna Kona Kali akakoswa na Lori la mafuta halafu mbele kama mita 500 kuna trafiki wa tochi akamsimamisha Dreva akaanza kujitetea ni nini kingekuwa sahihi kwa uelewa wako?

Dereva ajitete kwa trafiki kwa njia yoyote Trafiki amsamehe au trafiki ampige faini Kali ya risiti ya tra na kufungiwa leseni ?
 
Moja ya matukio ya Hovyo ni kuchukua Trafiki video wanapokusanya mapato ya kuchomwa na jua la siku nzima hizi video zinalengo la kudhalilisha Trafic na sio sawa na yeyote mwenye hii Tabia aache… na jeshi la polisi Tz hili lichukuliwe kwenye Taswira ya kudhalilisha jeshi.

Trafic hajawahi kumlazimisha mtu kuchangia mapato ya kuchomwa na jua ! It is your choices ni ulipe fine ya 30,000 au umalizane nae hapo hapo yote ni sawa.

Ni makosa mapato ya kuchomwa na jua yatafsiriwe kama rushwa !! Kama polisi -Tanzania mnataka kweli ku deal na rushwa nendeni kwenye mikataba ya hiyo nchi kama DP World, Mikataba ya madini, Ujenzi wa SGR, ujenzi wa mwendokasi…. Huko ndio kuna Big fish Corruption

Mshahara wa Rais ni 139M ….. ambae 24 hours yupo kwa AC, , mshahara wa mawaziri ni mnono and yet wanapiga deal fake na muda wote wanakula mema ya nchi, watoto wa marais na mawaziri kama kina Abdul ambao hawana history ya nchi…. Wanakula mema na kupiga deal fake…. Goli moja linanunumia kwa 5M na chanzo cha fedha hakijulikana. Polisi yote hayo hamdeal nayo mnaenda ku deal na vi elf mbili mbili wanavopewa trafic kama mapato ya kuchomwa na jua !

Soma Pia: Trafiki wawili wakamatwa baada ya kunaswa kwenye video wakipokea Rushwa hadharani

Polisi TZ acheni mihemko ya kila kitu cha mitandao mkitolee ufafanuzi au ku deal nacho au kuwachukulia hatua watendaji wenu ! Mengine ni hayana msingi dilini na mambo makubwa yanayoikabili nchi kama vile Rushwa zinazofanywa na viongozi wakuu, utekaji n.k

Pamoja na mambo mengine mnatakiwa ku deal na watu wanao rekodi trafic wanapokuwa kwenye majukumu yao ya kukusanya mapato ya kuchomwa na jua, hao watu wakamatwe na wafanywe mfano maana wanadhalilisha watendaji wa jeshi la usalama wa barabarani. HAIKUBALIKI

Otherwise hao trafic warudi Ofisin haraka na ni aibu kamanda mkuuu kusimama kwa media kuongelea mambo kama hayo, ni kukosa weledi

Ni Nani aliyemuua Ali Kibao?

Yupo wapi Ben Saane?

Amekufa au yupo hai; kwenye mila zetu za Kichaga hii damu italipwa kwa namna yoyote mpaka
Mtuletee majivu yake tuyazike with our ritual proceedures or else the game is not over and our hearts are still bleeding

Tunataka kusikia ni nani aliyempiga Tundu Lissu risasi in the government yard ?

Tunataka kusikia Soka yupo wapi ?

Tunataka kusikia wabakaji wa binti wa Dovya wapo wapi ? Tunataka kusikia nani alimteka Nondo?

Hayo ndio majukumu yenu ya msingi

N.K
Hayo mengine ni hayana ishu kwa taifa;

Dr Megalodon, PhD Candidate
WHO Regional Office
Rue 52 , Ottawa
Canada
Unahoja Mkuu... Naomba usikilizwe
 
Back
Top Bottom