We nawe ndo wale mtu akifanya innovation mnakamata yeye na alicho innovate. Tonzonia nchi yangu!!Mh.Jokate yuko sahihi....
Hao ndio wanaharibu ELIMU YETU.....
Utaratibu uko hivi, mtu anayesoma degree au bachelor anatakiwa afundishwe na PhD holder au Associate Professor, watu wenye masters wanabaki kuwa kama ma Assistant Tutorial, Diploma anafundishwa na mtu wa degree + masters holder,PhD holder ana msaada gani kwenye ujasiliamali wa kitaaluma? Tatizo mmeweka mkazo kwenye vyeti kama kwamba ndivyo vinavyotoa elimu. Kuna PhDs lundo nchi hii hawana kabisa msaada zaidi ya kutumia vile vyeti kama kitegauchumi wakati wanapwaya kwenye nafasi walizopewa kusimamia.
Alitakiwa kufanya nini boss?Huyu naye ameanza ujinga ule ule wa kuweka watu ndani
VETA wapi chini ya NACTE maana NACTE wanasimamia vyuo vyote vya ufundiHizo zipo chini ya NACTE na VETA
Ufumbuzi ni nini sasa?Suala siyo kuruhusu ubunifu, wale wameendesha chuo bila kufuata sheria, hilo ndiyo kosa lao, ila pia mazingira yao hayaendani na viwango vya Serikali kama NECTA na NACTE.
Mkuu hao wanaojificha lazima wana sababu! Kwa vyovyote kuna mtu mwenye fani yake anafichwa hapo tena inawezeka yuko kwenye system!. Chunguzeni vizuri mtagundua kitu muhimu... Lakini sio kwa mtindo huo wa kufunga vyuo kama vile mnakomesha mtu, Huwezi kuanzisha chuo hivi hivi bila kuwa na A B C ya fani.Serikali ilishatoa muda kwa vyuo kama hivi kwenda kujisajili na kufuata taratibu zote ila wamiliki hawakufuata taratibu. Shida inakuja pale wamiliki hawataki kujulikana ili wasilipe kodi na kwa sababu wanajua uwezo wao kuwa kujiendesha ni mdogo ndiyo wanaamua kujifichaficha sana, mwisho wa siku elimu wanayotoa inakuwa haitambuliki na inakuwa ni hasara kwa wahitimu hasa wanapoambiwa vyeti vyao havitambuliki.
Elimu maana yake kuelimishana ili miundombinu ya elimu iliyopo iweze kutoa matokeo tunayoyataka. Kufungia wajasiliamali siyo suruhisho. Kwani hao wanaofungiwa si wana vigezo vya kuajiriwa na Serikali kama kweli huko ndiko kwenye elimu bora?.Mh.Jokate yuko sahihi....
Hao ndio wanaharibu ELIMU YETU.....
Hapana! Angeweza kufanya zaidi kwa kujua kiini cha kukaidi agizo. Kama kiongozi anatakiwa kuwa smart sio kuamua kwe mihemuko. Hao watu wanashiriki kujenga, Sasa kama fito wanazotumia kama haziko sawa si wanaelekezwa tu?.Hayo yote unayoyasema yalishafanywa na kutolewa maelekezo, sema wabongo ni wagumu kutii sheria na kufuata utaratibu uliowekwa na Mamlaka zao. Serikali kwa upande wake ilishajitahidi kuweka utaratibu wa kumiliki taasisi za Elimu binafsi. DC JOKATE amefanya kwa mujibu wa Sheria.
Hayo wazungumza ni ya huko nje ya Afrika.Huyu dada kachemka vibaya!!!
mambo ya kuwekana ndani ni ushamba....
Mkuu, acha mzaha yaani mtoto amenawiri kiasi hicho weye wasema ana njaa?DC ameanza kujifunika mashuka kama yule muimba taarab, njaa kitu mbaya sana
Na hakuna tamshi kuhusu wanafunzi waliopo chuoni. Serikali ipo kuanzia ngazi ya Mtaa na haikuliona kwa miaka. Alichokifanya ni kupata simple popularity, au mgao wa hongo umeyeyuka.Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mhe. JOKATE MWEGELO Aagiza Kuwekwa Chini ya Ulinzi Mkali Viongozi wa Chuo cha LUBANDO TRAINING COLLEGE
Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Jokate Mwegelo ameagiza kuwekwa chini ya ulinzi kwa Viongozi wa Chuo cha Lubando Training College kilichopo Mtaa wa Butiama, Kata ya Mtoni Kijichi baada ya kubaini Chuo hicho kinaendeshwa kinyume cha Sheria.
DC Jokate ametoa agizo hilo wakati alipoungana na Wataalamu katika ziara ya kutembelea maeneo mbalimbali ya Wilaya hiyo ambapo aliambatana pia na Mkurugenzi-Uthibiti, Ufuatiliaji na Tathmini kutoka NACTE Dkt. Joefrey Oleke.
Baada ya kufanya mahojiano na Mkuu wa Chuo hicho, DC Jokate alibaini kuwa kwa muda sasa Chuo hicho kimekua kikitoa mafunzo bila kupata usajili, pamoja na kutoa mafunzo kwenye mazingira yasiyo rasmi .
"Hamna kitu kibaya kama kufanya utapeli halafu ukadhani hutagundulika, Serikali ina macho kila sehemu, NACTE kaeni hapa na Polisi, lazima tupate 'information', Chuo hakijasajiliwa lakini hata mandhari yake haistahili, kuna Watu wanatoa huduma ambazo kiuhalisia hawastahili kutoa, tushirikiane katika ufuatiliaji, hawa wachukuliwe hatua kali huu ni utapeli"βββ-DC Jokate
Kwa upande wake Dkt. Jofrey Oleke amesitisha shughuli zote zinazoendelea katika chuo hicho, huku akielekeza taratibu nyingine za kisheria kufuatwa huku akisema kwa ukaguzi uliofanyika, chuo hicho hakitambuliki NACTE wala VETA.
View attachment 1919666