Tendega asema Tanzania kutoruhusu uraia pacha kunaikosesha fursa nyingi za kiuchumi

Tendega asema Tanzania kutoruhusu uraia pacha kunaikosesha fursa nyingi za kiuchumi

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Mbunge wa Viti Maalum Grace Tendega amesema uamuzi wa Tanzania kutoruhusu uraia pacha kunaikosesha fursa nyingi za kiuchumi.

Tendega ametoa kauli hiyo leo Jumanne, Juni 1, 2021 bungeni wakati akichangia katika hotuba ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa mwaka 2021/22.

Suala la uraia pacha lilipata mashiko zaidi katika mjadala wa Bunge Maalum la Katiba ambapo rasimu ya awali ilipendekeza liruhusiwe kwenye Katiba hata hivyo katika Katiba inayopendekezwa liliondolewa

Hata hivyo limekuwa likijitokeza mara kwa mara katika mijadala hasa wakati wa Bunge la bajeti ingawa jambo hilo halijapatiwa ufumbuzi wa kudumu. Leo Tendega amesema kutoutambua au kukubali uraia pacha ni sawa na taifa kuendelea kujitenga na watu wake wakati mataifa mengine wanaendelea kuneemeka.

Mbunge huyo ametaka Tanzania kuwa na orodha kamili ya utambuzi kwa watu wake walio nje ili wasaidie kukuza uchumi ndani ya nchi. Ametolea mfano wa Kenya inapata zaidi ya Dola 2.7 bilioni ambayo ni asilimia 3 ya pato lao zinazotokana na watu wao kwenye uraia pacha.

Akizungumzia hadhi za Balozi za Tanzania amesema majengo ya balozi yamechoka hata kutia aibu lakini Serikali haipeleki fedha za ukarabati. Ameitaka Serikali kuwawezesha mabalozi katika masuala ya kidiplomasia ili walitangaze Taifa hata kwenye mambo ya uchumi.


Mwananchi
 
MBUNGE WA VITI MAALUM KUPITIA CHAMA GANI.

Anapata wapi uhalali wakuongelea mambo ya Nje ikiwa yeye amevunja mambo yetu ya ndani.

KULE KALENGA WALISHAKUDHARAU TEACHER.
 

Dual citizenship in Africa: 'Benefits outweigh disadvantages'​

29.01.2019​

16821087_101.jpg


Dual citizenship is illegal in a number of African countries. Authoritarian leaders regard people with a second nationality as potentially dangerous with their "foreign" ideas, analysts say.​

Several African countries, such as the Democratic Republic of Congo (DRC), Tanzania and Ethiopia, reject dual nationalities for their citizens. In these countries the fear of people with two citizenships seems to be acute.

There are a number of African heads of state and high-ranking politicians who have dual citizenship themselves or roots in another country. Somali President Mohamed Abdullahi Mohamed is a citizen of Somalia and the United States. Liberia's former head of state Ellen Johnson-Sirleaf has German and Liberian roots. Moise Katumbi, a leading DRC opposition politician, was an Italian citizen for 17 years. For this reason he was banned from running in the 2018 presidential election.

Pride or politics?

While the DRC does not recognize dual citizenship, an exception is made for children born abroad. They are allowed to keep both nationalities until they come of age at 21. Then they have a year to renounce one of their citizenships. An Ethiopian law of 1930 stipulates that Ethiopians acquiring another nationality will cease to be Ethiopians. Foreigners who want to become Ethiopians need to prove that they've already renounced or are able to renounce their original citizenship.

Tanzania also does not allow dual citizenship. In 2007, Tanzanian Foreign Minister Bernard Membe presented a report which recommended an amendment to this law. But the government argued that such a change represented a threat to peace, security and the Tanzanian population's livelihood.

47202378_7.png


"It's all a mystery, because the benefits outweigh the so-called disadvantages," Ahmed Rajab of the Pan-African Institute for Strategic Studies, told DW. "The main benefits are to the economies of these countries," he said. "Maybe it's a question of pride. Maybe these countries are so proud of their nationality that they don't want any of their citizens to acquire another citizenship." Legalization would not bring about any new problems. On the contrary: "It has been proved in the case of Ghana, for example, or even Kenya, that the country benefits from the inflow of funds from the countries of the citizens who have dual nationality." Ghana legalized dual citizenship in 2002. Kenya followed suit in 2011.

African leaders do not want to be challenged

Tanzanian analyst Gwandumi Mwakatobe believes there is more to the rejection of dual citizenship than mere pride. Many people often do not know where to get their information from so they believe whatever their president says. Mwakatobe believes that this works to the advantage of African heads of state. People with dual citizenship who live abroad "are exposed to so many things. They know so many issues regarding politics, regarding human rights. And they are very vocal. They criticize their country. They challenge the leaders from their original countries. Many African leaders don't want to be challenged," Mwakatobe told DW.


15670052_101.jpg


Mali is one of the African countries that allow dual nationality
"I think that is a threat," analyst Ahmed Rajab agrees. African leaders view people with dual citizenship as foreigners and don't want them to participate in politics. "Because they have ideas on democracy, democratic processes and on how to run politics. It goes against the grain of the Ethiopian political environment, for example," Rajab said. Dual citizens are banned from local politics in Ethiopia.

'We are world citizens'


Gwandumi Mwakatobe considers this to be a useless strategy. "There is nothing you can hide in this world today, due to the communication technology. Even in the DR Congo, where they cut the internet, they were still communicating," he said. The analyst also believes that states will benefit from allowing their citizens to have dual nationality. "We have to put in place good systems, good laws, that can guide us to make sure that we prosper," he said. Increased business, transport of goods and networking with people abroad are just a few advantages of dual citizenship, Mwakatobe pointed out.

He would like every African country to build a bridge to the diaspora, to ease the way home for people with dual citizenship. "That is very important, because we are all citizens of this world, and not from one nation or the other. The whole world is ours. We are world citizens."
 
Hii kitu sijawahi kuikubali hata kidogo Mimi

Yaani mtu uwe na uraia wa nchi mbili kiusalama hii haijakaa vizuri hata kidogo.
 
Mtu akiwa na uraia wa nchi mbili anaweza akaiuza nchi yake moja kiusalama sababu anajua anapo pa kukimbilia nchi yake ya pili
 
Cha ajabu hakuna nchi yoyote ile ya Africa ambayo inaruhusu uraia wa nchi mbili kuna ushahidi wowote wa kuonyesha hatari hiyo. Membe alipokuwa Foreign Affairs katika juhudi zake za kuhalalisha uDC alitembelea nchi mbali mbali za Africa na Caribbean kusikiliza prons and cons za uDC na katika nchi zote alizopita hakupata maoni yoyote mabaya kutoka Viongozi wa nchi na Mawaziri husika kuhusu dual citizenship.

Hii kitu sijawahi kuikubali hata kidogo Mimi

Yaani mtu uwe na uraia wa nchi mbili kiusalama hii haijakaa vizuri hata kidogo.
 
Tundu Lissu mbona ana uraia wa nchi mbili huko ubelgiji ni raia na huku Tanzania bado ni raia. Uraia zaidi ya nchi moja ni nzuri tu tena waafrika itatusaidia sana. Kuna watanzania wanaoishi marekani wamejenga majumba na kuwekeza biashara zao Tanzania, ni ngumu kuwafukuza raia kama hawa. Serikali ikubaliane na mabadiliko dunia ya sasa sio kama ya zamani watu hawaishi kuhama hama hasusan waafrika wanaoenda kutafuta maisha kwenye nchi zilizoendelea. Watanzania tuache uhafidhina.
 
Wasiruhusu uraia pacha.

Waanzishe utaratibu wa permanent residency.

Permanent residents wanakuwa na haki zote lakini hawaruhusiwi kushiriki ktk uchaguzi, na kutumikia ktk taasisi nyeti za serikali.
Mkuu wewe kama JokaKuu kama leo Tanzania ikiruhusu uraia pacha, utakuathiri vipi?

Mimi nadhani watanzania hatuna budi kukubali..wakati si milele. Uraia pacha utakuja tuu. ni swala la mda. Kikubwa , kama taifa tuwekane sawa.....tukiamua kuuruhusu..kipi kifanyike kulinda maslahi CORE ya taifa letu. Sioni sababu ya kuzuia uraia pacha.

Mfano kuna watanzania wengi wako nje, wengine walienda kusoma, wengine walijilipua. Hawa waote wameoa, wana familia zao huko ughaibuni. Na majority wanakuja bongo wakiwa na passport za nchi husika. Utawajuaje? Ukweli ni kwamba Uraia pacha hauruhusiwi kisheria lakini watanzania wengi wana passport za nje. Hata serikali hili wanalijua.

Ukweli ni kwamba uraia pacha upo..sema tuu kama kawaida, wadanganyika ukiwadanganya majukwaani...wanademka upepo unakodemkia.

Hata kwenye serikali yetu naamini wamo wengi wenye uraia pacha! Kikubwa serikali should recognize the obvious!
 
Hii kitu sijawahi kuikubali hata kidogo Mimi

Yaani mtu uwe na uraia wa nchi mbili kiusalama hii haijakaa vizuri hata kidogo.
Toa mfano unaoonyesha kuwa uraia pacha unaondoa usalama. Faida zake ni nyingi zaidi.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Mbunge wa Viti Maalum Grace Tendega amesema uamuzi wa Tanzania kutoruhusu uraia pacha kunaikosesha fursa nyingi za kiuchumi.

Tendega ametoa kauli hiyo leo Jumanne, Juni 1, 2021 bungeni wakati akichangia katika hotuba ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa mwaka 2021/22.

Suala la uraia pacha lilipata mashiko zaidi katika mjadala wa Bunge Maalum la Katiba ambapo rasimu ya awali ilipendekeza liruhusiwe kwenye Katiba hata hivyo katika Katiba inayopendekezwa liliondolewa

Hata hivyo limekuwa likijitokeza mara kwa mara katika mijadala hasa wakati wa Bunge la bajeti ingawa jambo hilo halijapatiwa ufumbuzi wa kudumu. Leo Tendega amesema kutoutambua au kukubali uraia pacha ni sawa na taifa kuendelea kujitenga na watu wake wakati mataifa mengine wanaendelea kuneemeka.

Mbunge huyo ametaka Tanzania kuwa na orodha kamili ya utambuzi kwa watu wake walio nje ili wasaidie kukuza uchumi ndani ya nchi. Ametolea mfano wa Kenya inapata zaidi ya Dola 2.7 bilioni ambayo ni asilimia 3 ya pato lao zinazotokana na watu wao kwenye uraia pacha.

Akizungumzia hadhi za Balozi za Tanzania amesema majengo ya balozi yamechoka hata kutia aibu lakini Serikali haipeleki fedha za ukarabati. Ameitaka Serikali kuwawezesha mabalozi katika masuala ya kidiplomasia ili walitangaze Taifa hata kwenye mambo ya uchumi.


Mwananchi
Naunga mkono hoja.
 
Back
Top Bottom