Tetemeko kubwa lazikumba Uturuki na Syria. Watu zaidi ya 36,257 Wafariki Dunia

Tetemeko kubwa lazikumba Uturuki na Syria. Watu zaidi ya 36,257 Wafariki Dunia

Nasikia eti ukichomewa Qur'an wewe unaelalamikia kuchomewa Qur'an unapigwa na tetemeko la sekunde 90, kweli au uongo?
Huna akili ,tokea wewe ndiye mwanzilishi wa mambo ya kidini humu na tokea mwanzo mpaka sasa bado unaendelea udini katika masuala mazito kama haya na kuandika ili watu waandike negative kuhusu uislamu na tukio hili.

Kumbuka haujui Kesho yako hivyo haipendezi siku wewe ufiwe na Baba yako Mzazi ,Mama yako Mzazi ,Mwanafamilia nk halafu mtu akuletee kejeli za kidini .Jiheshimu angalau kidogo majanga waliyopata hawajaomba wala kusababisha wao.
 
Yalitabiriwa haya Kutokea.

Ni kati ya Oct 20 mwaka 2022 Hadi March 20 mwaka 2023.

Bado yatatokea mengi.

Tuendelee kuomba REHEMA na TOBA.

Aaamen.
 
Huna akili ,tokea wewe ndiye mwanzilishi wa mambo ya kidini humu na tokea mwanzo mpaka sasa bado unaendelea udini katika masuala mazito kama haya na kuandika ili watu waandike negative kuhusu uislamu na tukio hili.

Kumbuka haujui Kesho yako hivyo haipendezi siku wewe ufiwe na Baba yako Mzazi ,Mama yako Mzazi ,Mwanafamilia nk halafu mtu akuletee kejeli za kidini .Jiheshimu angalau kidogo majanga waliyopata hawajaomba wala kusababisha wao.

Ningelikua admin watu kama hawa wanaokejeli na kuchagua race za kuwapa pole ningelikua nawalima life ban.
 
Erdogan katangaza hali ya hatari kwa miezi 3

Hotel za Kitalii kubadilishwa kwa muda na kuwa sehemu ya makazi.

Nchi zaidi ya 70 zimepeleka watu kusaidia, kati ya hizo nchi hakuna nchi moja ya Afrika.

Tanzania yatoa salamu twitter masaa 17 baada ya tukio
 
Jiheshimu angalau kidogo majanga waliyopata hawajaomba wala kusababisha wao
Ila km Qur'an isingechomwa na Sweden na Turkey isingekua msitari wa mbele kulalamika yote haya yasingetokea, hapo pia utapinga?

Erdogan anasema zaidi ya watu 5000 wamefariki dunia, pole kwa Marehemu walale wanapostahiri
 
Erdogan katangaza hali ya hatari kwa miezi 3

Hotel za Kitalii kubadilishwa kwa muda na kuwa sehemu ya makazi.

Nchi zaidi ya 70 zimepeleka watu kusaidia, kati ya hizo nchi hakuna nchi moja ya Afrika.

Tanzania yatoa salamu twitter masaa 17 baada ya tukio
Kwenye hizo 70 Sweden ipo au haipo?
 
Kwenye epicenter destruction Huwa ni ndogo ukilinganisha na nje kule mawimbi yanapoenda kuishia..... epicenter ni huko Syria.
Mkuu naona somola Jiografia ulililidharau kabisa.

Nawakaribiksha wadau wenzangu wanokumbuka Physical Georgrapy ya Forms Six Topic ya Earthquake.

Epicentre ni kitovu cha tetemeko yaani pale katikati ya Uturuki na karibu kabisa na mji wa Gaziantep.

Sasa Uturuki ipo ndani ya sahani iitwayo "Anatolia Plate" na hii sahani yakinzana na sahani ingine iitwayo "Arabian Plate".

Hivyo tetemeko la ardhi husababishwa na kukinzana kwa sahani hizi mbili yaani movement of tectonic plates na pale zinapokuwa zikisogea ndipo husababisha ardhi kuinuka na kutokea tetemeko la ardhi.

Ule mtikisiko au "tremor" waweza kuenea hadi katika maeneo mengine "provided yamo ndani ya ule mkanda au mkondo wa tetemeko uitwao "faultline".

Tetemeko laweza kutembea umbali mrefu na ndo maana limeweza kufika kilomita hadi 18 na kuingia Syria na pia kutetesha maeneo kama Lebanon Israel, Ugiriki na Cyprus kwa sabau ya ule mkanda.

Kinachoshangaza ni uwezo wa uturuki kama nchi ilipoyo barani Ulaya lakini yashindwa kuwekeza katika sayansi na kuwa na vituo vya kusoma alama za nyakati kuhusu matetemeko na majanga mengine, na hivyo kuwa wamejiandaa kwa kuokoa maisha ya watu.

Japan ambayo nayo huathirika na matetemeko wana somo kabisa la disaster na uokozi pale tetemeko linaposomwa au kugundulika kutaka kutokea.

Watoto wa shule hufundishwa namna ya kujikinga endapo tetemeko linatokea.

Tetemeko la ardhi pia laweza kusababisha tsunami na ndo maana nchi ya Italia yajiandaa kwa hilo.
 
Tetemeko la ardhi pia laweza kusababisha tsunami na ndo maana nchi ya Italia yajiandaa kwa hilo.
Kuna mjinga atakua anachimba madini huko dunia ya pili kalipua baruti kwenye mkanda ili apate Ruby, nimehisi tu
 
Tetemeko kubwa la ardhi la kipimo cha 7.9 limepiga katikati mwa Uturuki na Kaskazini-Magharibi mwa Syria siku ya Jumatatu, na kuua maelfu ya watu na kujeruhi mamia wakati majengo yakiporomoka


Uokoaji wa walionusurika kwenye vifusi katika eneo hilo lenye theluji unaendelea.

Shirika la maafa la Uturuki limesema watu 76 wameuawa, na 440 wamejeruhiwa, wakati mamlaka ilipotawanya timu za uokoaji na kusambaza ndege katika eneo karibu na mji wa Kahramanmaras, huku ikitangaza "kiwango cha 4 ya uokoaji" inayotaka usaidizi wa kimataifa.

Vyombo vya habari vya serikali ya Syria vimesema kuwa idadi kubwa ya majengo yameporomoka katika jimbo la Aleppo, huku chanzo cha habari katika utumishi wa umma cha Hama kikisema kuwa majengo pia yameporomoka huko.

UPDATES
Vifo zaidi ya 100 upande wa Uturuki, 39 Upande wa Syria huku watu wengi wakiwa bado chini ya vifusi.

Italia yaonya kuwa tsunami yaweza tokea kutokana na tetemeko hilo

UPDATE: WALIOFARIKI KWA TETEMEKO LA ARDHI UTURUKI NA SYRIA WAFIKIA 1500

Wakati shughuli za Uokoaji zikiendelea baada ya kutokea Tetemeko lenye kipimo cha Richa 7.8, zoezi hilo linaanza kukabiliwa na ugumu kutokana na Mamia ya Watu kunaswa kwenye vifusi

Zaidi ya watu 5000 wamejeruhiwa na wengine bado hawajulikani walipo na wana hali gani. Nchi za Cyprus, Misri na maeneo ya Lebanon yamepata Mtikisiko kutokana na Tetemeko hilo.

---
UPDATE: IDADI YA WALIOFARIKI KWA TETEMEKO LA ARDHI UTURUKI YAFIKIA WATU 1,800

Vifo zaidi vinazidi kuripotiwa kufuatia Tetemeko la ukubwa wa Richa 7.8 kuzipiga Uturuki na Syria usiku wa kuamkia Februari 6, 2023 na kuporomosha mamia ya Majengo wakati watu wakiwa wamelala

Idara ya Dharula Nchini Uturuki imeomba msaada kwa Jumuiya za Kimataifa baada ya kutokea Matetemeko mengine mawili yenye kipimo cha 7.5. Uingereza tayari imetuma Wataalamu 76 wa Utafutaji na Uokoaji.


UPDATE: Zaidi ya watu 2,300 wamepoteza maisha huku waokoaji wakiendelea kutafuta manusura
Zaidi ya watu 2,300 wamepoteza maisha huku waokoaji wakiendelea kutafuta manusura kutoka chini ya vifusi vya majengo yaliyoporomoka kutokana na Tetemeko kubwa la ardhi lililozikumba Uturuki na Syria leo Februari 6, 2023 na kuacha majeruhi zaidi ya 10,000 na wengine wakiwa hawana makazi.

UPDATE: Staa wa zamani wa Chelsea Christian Atsu akwama kwenye kifusi

View attachment 2508725
Staa wa zamani wa Chelsea na Newcastle za England Christian Atsu (31) Raia wa Ghana ambaye kwa sasa anacheza Hatayspor ya Uturuki amekwama kwenye kifusi cha jengo lililoanguka baada ya tetemeko la ardhi.

Harakati za kumuokoa Atsu zinaendelea lakini kwenye tetemeko hilo lililotokea leo nchini Uturuki mitandao mbalimbali imeripoti kuwa watu zaidi ya 1400 wamefariki Dunia.

Atsu ambaye alijiunga na Chelsea 2013 na kuishia kutolewa kwa mkopo Newcastle na Everton, alikuwa sehemu ya mchezo wa Ligi Kuu Uturuki jana kati ya timu yake ya Hatayspor dhidi ya Kasimpasa ambapo aliisaidia kupata ushindi wa 1-0 akifunga goli dakika ya 90+

UPDATE: Matetemeko mengi madogo 100 yatokea baada ya lile kubwa
Takriban matetemeko 100 yenye ukubwa wa 4.0 au zaidi yametokea tangu tetemeko la ardhi lenye kipimo cha 7.8 lilipotokea Kusini mwa Uturuki Jumatatu asubuhi saa za huko, kulingana na Utafiti wa Jiolojia wa Kituo cha Marekani.

Kadiri muda kutoka kwa tetemeko la ardhi la asili unavyoongezeka, frequency na ukubwa wa matetemeko ya baadaye hupungua.

Hata hivyo, matetemeko ya kipimo cha 5.0 hadi 6.0 bado inaweza kutokea nchini humo na kuleta hatari ya uharibifu zaidi. Hii inaleta tishio kwa zoezi la uokozi linaloendelea na kwa timu za uokoaji na manusura.

UPDATE: WALIOFARIKI KWA TETEMEKO LA ARDHI UTURUKI, SYRIA NI ZAIDI YA WATU 4,300
Ripoti za idadi ya waliofariki inaendelea kuongezeka kufuatia Tetemeko la Ardhi la ukubwa wa 7.8 kwa kipimo cha Richa, kuzipiga Uturuki na Syria usiku wa kuamkia Februari 6, 2023.

Watu 2,921 wameripotiwa kufariki Nchini Uturuki huku zaidi ya 15,000 wakijeruhiwa, upande wa Syria imeripotiwa waliofariki ni watu 1,444; ikifanya jumla ya vifo kufikia 4,365, inaelezwa idadi inatarajiwa kuongezeka.

Rais wa Korea Kusini, Yoon Suk-yeol amesema Nchi yake itatuma timu ya waokoaji na vifaa vya matibabu ya dharura Nchini Uturuki ili kusaidia uokoaji unaoendelea.
Waache kumuudhi Mungu na shepu zao za bandia
 
Ila km Qur'an isingechomwa na Sweden na Turkey isingekua msitari wa mbele kulalamika yote haya yasingetokea, hapo pia utapinga?

Erdogan anasema zaidi ya watu 5000 wamefariki dunia, pole kwa Marehemu walale wanapostahiri
Elimu ya kujua yote hayo umeitoa wapi na unaweza kuweka ushahidi ?

Ni katika ujinga wa mtu kuzua na kuzungumza mambo pasipo na ushahidi.

Waliokufa wanahusika vipi na hilo wakati kuna wengine ni wakiristo na atheist na Waislamu wasiolalamika mbona wamefariki na hilo janga ?

Kwa kuongeza eneo liliotokea maana karibu na mpaani mwa Syria kwa asilimia kubwa linakaliwa na Kurdish people ambao Sweden inawaunga mkono na wanauhasama na serikali ya Turkey..
 
Kwa kuongeza eneo liliotokea maana karibu na mpaani mwa Syria kwa asilimia kubwa linakaliwa na Kurdish people ambao Sweden inawaunga mkono na wanauhasama na serikali ya Turkey
Mchezaji Christian Atsu ameokolewa kwenye kifusi huko Turkey amepona, mkurugenzi wao bado yupo chini ya kifusi hajatolewa hadi mda huu
 
Waliokufa wanahusika vipi na hilo wakati kuna wengine ni wakiristo na atheist na Waislamu wasiolalamika mbona wamefariki na hilo janga ?

Kwa kuongeza eneo liliotokea maana karibu na mpaani mwa Syria kwa asilimia kubwa linakaliwa na Kurdish people ambao Sweden inawaunga mkono na wanauhasama na serikali ya Turkey
Mbon kwenye video wengi walikua wanaimba

Railauraha Railauraha Railauraha

Vipi hapo?
 
Back
Top Bottom