TFF: Bei ya VAR ni Sh Bilioni 14.5, kamera ziwe 38, kila mechi timu zinalipia Sh milioni 7

TFF: Bei ya VAR ni Sh Bilioni 14.5, kamera ziwe 38, kila mechi timu zinalipia Sh milioni 7

John Haramba

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2022
Posts
365
Reaction score
1,374
Rais wa Shirikisho la Soka la Tanzania (TFF), Wallace Karia amezungumzia matumizi ya VAR wakati wa kufunga semina ya siku tatu ya Waamuzi wa Ligi Kuu ya NBC iliyomalizika jana Februari 17, 2022 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa.

Haya hapa ndiyo aliyoyasema Karia: “Unajua gharama za VAR? Sawa najua Serikali wanaliangaia hilo.

“Ili kupata ile VAR seti nzima ni karibu Sh bilioni 14.5, mbali ya kamera za Azam TV, VAR nao wanatakiwa kuwa na kamera zao kuanzia 33 hadi 38.

“Na tukiamua kuweka lazima tupate kibali kutoka kwao kwa kuwa siyo mali yetu, pia kila mechi klabu zinatakiwa kushea gharama ya kutumia hiyo VAR ambayo ni kama Sh milioni 7 hivi.”

Hatua hiyo inakuja kutokana na presha kubwa ambayo imekuwa ikiendelea hivi karibuni kutokana na waamuzi kadhaa wa soka kufanya makosa katika Ligi Kuu Bara msimu huu unaoendelea wa 2021/22.

Karia akaongeza kwa kusema: “Kuna mambo mengi yanazungumzwa, mengine kwa wadau kutojua sheria na mengine nayafanya makosa kweli.

“Mnafanya makosa nyie lawama zinakuja kwangu, sijawahi kutoa maelekezo kwa waamuzi hata mara moja.”

Kariaa.jpg
 
Hatutaki VAR kama za ulaya bali replay za Azam pekee zinatosha kwa mwamuzi kuangalia tukio uwanjani na kujiridhisha kama sisi tunaoangalia kwenye luninga tunavyopata wasaa kujiridhisha. Gharama hapo ni kununua tv na ving'amuzi vya Azam tu na kuviweka viwanjani. Na azam pia waongeze idadi za camera zao
 
Hiyo yote ili kuwaridhisha wana Yanga wanaohisi wanaonewa na waamuzi kwa makusudi na huenda wakaendelea kukosa kombe

Mwigulu akili zake anazijuaga mwenyewe Tu, waboreshe viwanja bana hayo mambo ya VAR na viwanja ni majaruba ya mpunga watafanya wote tuonekane wajinga
 
Hatutaki VAR kama za ulaya bali replay za Azam pekee zinatosha kwa mwamuzi kuangalia tukio uwanjani na kujiridhisha kama sisi tunaoangalia kwenye luninga tunavyopata wasaa kujiridhisha. Gharama hapo ni kununua tv na ving'amuzi vya Azam tu na kuviweka viwanjani. Na azam pia waongeze idadi za camera zao
Wewe ni jinga
 
Hatutaki VAR kama za ulaya bali replay za Azam pekee zinatosha kwa mwamuzi kuangalia tukio uwanjani na kujiridhisha kama sisi tunaoangalia kwenye luninga tunavyopata wasaa kujiridhisha.
Ndugu acha kujianika hadharani, mpira ni wa FIFA, standard zote zinatoka FIFA ikiwa ni pamoja na sheria 17 za mpira wa miguu. Huwezi kujipangia wewe eti unatumia camera za Azam, wewe ni nani?
 
Ukitaka uone TFF hawapo serious na mpira wa bongo angalia hiyo nembo ya GSM bado hadi leo inadisplay kama moja ya wadhamini wa Ligi kuu pamoja na mkataba kusitishwa wiki sasa.

Kila mwaka kuna fungu linatoka FIFA kwa ajili ya maendeleo ya soka kwa mashirikishi ya mpira lakini sioni TFF wanatumia vp fungu hilo ni bors wanunue hizo VAR tu
 
Hatutaki VAR kama za ulaya bali replay za Azam pekee zinatosha kwa mwamuzi kuangalia tukio uwanjani na kujiridhisha kama sisi tunaoangalia kwenye luninga tunavyopata wasaa kujiridhisha. Gharama hapo ni kununua tv na ving'amuzi vya Azam tu na kuviweka viwanjani. Na azam pia waongeze idadi za camera zao
Camera za Azam ndiyo chanzo za utata maana hazichukui angle zote......
 
Hiyo yote ili kuwaridhisha wana Yanga wanaohisi wanaonewa na waamuzi kwa makusudi na huenda wakaendelea kukosa kombe

Mwigulu akili zake anazijuaga mwenyewe Tu, waboreshe viwanja bana hayo mambo ya VAR na viwanja ni majaruba ya mpunga watafanya wote tuonekane wajinga
Mwigulu ni uto ambaye ameficha hisia zake kwenye kivuli cha uongozi na kujidai naye ni mkereketwa wa maamuzi wanayofanya marefa

Wakati huyu huyu tuliwahi kumuona akishangilia goli la mkono waliyoshinda yanga dhidi ya simba miaka ya nyuma
 
Ndugu acha kujianika hadharani, mpira ni wa FIFA, standard zote zinatoka FIFA ikiwa ni pamoja na sheria 17 za mpira wa miguu. Huwezi kujipangia wewe eti unatumia camera za Azam, wewe ni nani?
Ndio uwezo wako wa kufikiria umeishia hapo? Viwanja tunavyovitumia kwenye ligi yetu ni kwa mujibu wa standard ya FIFA? Je refarii akitumia replay za uwanjani atakuwa kavunja sheria ipi? Ikiwa lengo la kufanya hivyo ni kupata wasaa wa yeye kujiridhisha juu ya tukio husika? Usibabaike na neno V.A.R ukaona kama ni kitu cha ajabu sisi waafrica kushindwa kukifanya kwa namna yetu, ile ni Video Assistant Referee wakafupisha nakuita V.A.R hakuna cha ajabu hapo zaidi ya replay ya matukio na mwamuzi hupitia hiyo replay. Replay ya Azam inafaa kabisa
 
Ndio uwezo wako wa kufikiria umeishia hapo? Viwanja tunavyovitumia kwenye ligi yetu ni kwa mujibu wa standard ya FIFA? Je refarii akitumia replay za uwanjani atakuwa kavunja sheria ipi? Ikiwa lengo la kufanya hivyo ni kupata wasaa wa yeye kujiridhisha juu ya tukio husika? Usibabaike na neno V.A.R ukaona kama ni kitu cha ajabu sisi waafrica kukifanya ile ni Video Assistant Referee hakuna cha ajabu hapo zaidi ya replay ya matukio na mwamuzi hupitia hiyo replay. Replay ya Azam inafaa kabisa
Naunga mkono!
 
Ndio uwezo wako wa kufikiria umeishia hapo? Viwanja tunavyovitumia kwenye ligi yetu ni kwa mujibu wa standard ya FIFA? Je refarii akitumia replay za uwanjani atakuwa kavunja sheria ipi? Ikiwa lengo la kufanya hivyo ni kupata wasaa wa yeye kujiridhisha juu ya tukio husika? Usibabaike na neno V.A.R ukaona kama ni kitu cha ajabu sisi waafrica kushindwa kukifanya kwa namna yetu, ile ni Video Assistant Referee wakafupisha nakuita V.A.R hakuna cha ajabu hapo zaidi ya replay ya matukio na mwamuzi hupitia hiyo replay. Replay ya Azam inafaa kabisa
Haya basi, waambie waanze kureplay mechi ijayo maana AzamTV wapo tangu zamani tu, kwa kutumia taratibu za kiafrika
 
Usipaniki mkuu. Hii ni platform ya watu kujadiliana na pia kutoa maoni yao sijampangia mtu au kumshurutisha mtu afanye bali nimetoa maoni yangu kuwa ni jambo amabalo tunaliweza kutekeleza kwa bajeti ndigo sana
Sijapanic, ila mimi nilishakuelezea kwamba mpira tunaoucheza upo chini ya FIFA, na standards zikiwemo seria za mchezo tunaletewa na FIFA, nikadai kwamba hata standards za VAR tunalazimika kuletewa na FIFA au agent wake. Wewe ukakataa ukasema sisi Waafrika tuna standard zetu zinazotufaa. Basi mimi kama mdau nasubiri utekelezaji wa hiyo VAR ya AzamTV iliyo kiafrika zaidi
 
Sijapanic, ila mimi nilishakuelezea kwamba mpira tunaoucheza upo chini ya FIFA, na standards zikiwemo seria za mchezo tunaletewa na FIFA, nikadai kwamba hata standards za VAR tunalazimika kuletewa na FIFA au agent wake. Wewe ukakataa ukasema sisi Waafrika tuna standard zetu zinazotufaa. Basi mimi kama mdau nasubiri utekelezaji wa hiyo VAR ya AzamTV iliyo kiafrika zaidi

Kwa mashindano ya ndani kinachoangaliwa ni namna ya kufuata zile sheria za FIFA, kama ingekuwa kunakufuata standards za FIFA basi tungeona FIFA wanaingilia kati juu ya viwanja vyetu vibovu tunavyotumia kwenye ligi yet au unataka kusema kiwanja kama cha Manungu kipo kwenye standard ya FIFA? Lakini hawawezi kuingilia kati kwasababu ni mashindano ya ndani ila inapotokea mashindano ya kimataifa hapo ndipo kitu kinachoitwa standard hutumika. Halafu pili toa kichwani kwako dhana ya V.A.R kama limtambo likubwa kama la wazungu bali sisi tutumie tu replay inatosha sana na hakuna kosa litakalokuwa limekiukwa ndani ya sheria za FIFA eti kisa waamuzi kupitia replay kwenye mashindano yetu ya ndani
 
Kwa mashindano ya ndani kinachoangaliwa ni namna ya kufuata zile sheria za FIFA, kama ingekuwa kunakufuata standards za FIFA basi tungeona FIFA wanaingilia kati juu ya viwanja vyetu vibovu tunavyotumia kwenye ligi yet au unataka kusema kiwanja kama cha Manungu kipo kwenye standard ya FIFA? Lakini hawawezi kuingilia kati kwasababu ni mashindano ya ndani ila inapotokea mashindano ya kimataifa hapo ndipo kitu kinachoitwa standard hutumika. Halafu pili toa kichwani kwako dhana ya V.A.R kama limtambo likubwa kama la wazungu bali sisi tutumie tu replay inatosha sana na hakuna kosa litakalokuwa limekiukwa ndani ya sheria za FIFA eti kisa waamuzi kupitia replay kwenye mashindano yetu ya ndani
Lupweko amekariri standard za FIFA halafu hajui ukomo wa standards za FIFA zinahusika katika ngazi zipi. Standard za FIFA zinafanya kazi kwa ngazi za kimataifa pekee. Na ndio maana mechi yoyote iliyopo chini ya ratiba ya FIFA lazima uwanja hadi marefa wawe katika standards za FIFA. na ndio maana kuna marefa wanachezasha ligi yetu ya ndani lakini hauwezi kuwaona wakichezesha mechi za kimataifa kwasababu hawana standard za FIFA. tuna viwanja vingi tunavyochea mechi zetu za ligi kuu lakini ukija kuangalia wenye standard ya FIFA havizidi vitano lakini FIFA siyo jukumu lao kuangalia michuano ya ndani kikubwa kufuata kanuni zao na sheria zao 17 za mpira wa miguu.

Hii hapa Kenya pia walijaribu kufanya V.A.R ya kivyao vyao je walishtakuwa na FIFA?

 
Ndio uwezo wako wa kufikiria umeishia hapo? Viwanja tunavyovitumia kwenye ligi yetu ni kwa mujibu wa standard ya FIFA? Je refarii akitumia replay za uwanjani atakuwa kavunja sheria ipi? Ikiwa lengo la kufanya hivyo ni kupata wasaa wa yeye kujiridhisha juu ya tukio husika? Usibabaike na neno V.A.R ukaona kama ni kitu cha ajabu sisi waafrica kushindwa kukifanya kwa namna yetu, ile ni Video Assistant Referee wakafupisha nakuita V.A.R hakuna cha ajabu hapo zaidi ya replay ya matukio na mwamuzi hupitia hiyo replay. Replay ya Azam inafaa kabisa
Sema azam waboresha namna ya uchukuaji matukio.

Kwa maana ya wingi wa kamera zilizosetiwa vizuri na ubora wa picha.
 
Makosa mengi yanayolalamikiwa hutokea Uwanja wa Taifa almaarufu kwa Mkapa.

Kama tatizo ni gharama kubwa hawawezi kumudu viwanja vyote na waanzie hapo kwa Mkapa, hali ikiruhusu zaidi wataendelea na sehemu nyengine.
 
Back
Top Bottom