TFF kilichoshindikana kwa Tuisila Kisinda kiliwezekana kwa Perfect Chikwende (double standard)

TFF kilichoshindikana kwa Tuisila Kisinda kiliwezekana kwa Perfect Chikwende (double standard)

Lyrics Master

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2016
Posts
479
Reaction score
670
Kuna swali najiuliza, hivi team ikisajili mchezaji na kabla ya deadline huyo mchezaji huyu akawa mgonjwa, inamaana hairuhusiwi tena kusajili mchezaji mwingine kabla ya hiyo deadline?

Kama ni ndio basi kuna mahala kanuni zetu hazipo vizuri.

Sipo hapa kusema nani yupo sahihi nan ani hayupo sahihi ila kwa namna hii team ya Yanga ninaweza kuipongeza kwa kuibua mapungufu katika kanuni zetu. Kwanini?

Haiwezekani mchezaji amesajiliwa katika muda sahihi na kufuata taratibu zote halafu iwepo kanuni ya kumzuia mchezaji huyo. Hiyo kanuni itakuwa na mapungufu makubwa sana au itakuwa imewekwa kimtego kwajili ya ‘’watu flani’’ na kwa bahati mbaya watu hao wameingia kwenye kumi na nane za ‘’watawala’’ ambao kwa siku za hivi karibuni wanasema wanaongoza kwa mawazo yao na si kanuni. Kanuni hutumika tu pale “unapoonekana kushindana na mamlaka.”

Kwanini?

Ni vile tu tumekuwa wasahaulifu sana hasa hawa ndugu wa TFF wamekuwa wasahaulifu mno kupindukia,

Mwaka jana 2021, katika usajili wa dirisha dogo, SIMBA SC ilimsajili Perfect Chikwende na kufanya idadi ya wachezaji wa kigeni kufikia wachezaji 13. Kilichofanyika Francis Kahata akatolewa kwenye usajili wa ligi ya ndani halafu Perfect Chikwende jina lake likaingizwa. Francis Kahata akasajiliwa kwenye mashindano ya kimataifa tu. Kitu ambacho this time around Yanga wamefanya hivyo hivyo.

Lakini wakati huo hatukusikia TFF ikikataa usajili huo.

Wachambuzi wenye ‘mbambamba’ nyingi kama akina Juma Ayo, Jemedari Said na Wilsom Oruma hatukuwasikia pia katika uchambuzi wa kujifanya wanajua kutetea sheria kama wanavyotetea sasa.

Hivyo hapa inaonekana kuna ‘ajenda’ ya siri kama ‘mungu mtu wa mpira’ alivyosema ukishindana na mamlaka wewe ndio utakaye umia. Ni wazi kuna watu wameanza kupata maumivu kwasasabu sheria ileile inayoibana team B sasa haikumbana team A.

Swali la msingi ni kujiuliza tu hizi sheria ni kwa team zote au kwajili ya team flani flani?
 
Case yako uliyorefer sidhani kama bado utakuwa sahihi ukiitumia leo, wakati wa usajili wa Chikwende CAF walitoa nafasi timu zisajili tena hasa zile zilizokuwa champions league kutokana na tatizo la uviko ili ikitokea baadhi ya wachezaji wana maambukizi timu zisiathirike wawepo wengine wa kucheza

Sasa hiyo kanuni bado ipo pamoja na kupungua kwa maambukizi ya uviko kama bado ipo utakuwa sahihi mkuu
 
Case yako uliyorefer sidhani kama bado utakuwa sahihi ukiitumia leo, wakati wa usajili wa Chikwende CAF walitoa nafasi timu zisajili tena hasa zile zilizokuwa champions league kutokana na tatizo la uviko ili ikitokea baadhi ya wachezaji wana maambukizi timu zisiathirike wawepo wengine wa kucheza

Sasa hiyo kanuni bado ipo pamoja na kupungua kwa maambukizi ya uviko kama bado ipo utakuwa sahihi mkuu
sasa kwanini Chikwende alisajiliwa kwa ligi ya ndani tu kama sababu ni hiyo ya UVIKO na idadi ya wachezaji?
 
Case yako uliyorefer sidhani kama bado utakuwa sahihi ukiitumia leo, wakati wa usajili wa Chikwende CAF walitoa nafasi timu zisajili tena hasa zile zilizokuwa champions league kutokana na tatizo la uviko ili ikitokea baadhi ya wachezaji wana maambukizi timu zisiathirike wawepo wengine wa kucheza

Sasa hiyo kanuni bado ipo pamoja na kupungua kwa maambukizi ya uviko kama bado ipo utakuwa sahihi mkuu
Elewa concept ya mleta mada. Mfano wake hauhusiani na Covid na hata 2021 haikuhusiana na Covid. Anachoongelea ni Chikwende kuruhusiwa kucheza ndani na kumtoa Kahata kubaki na mashindano ya nje pekee. Hiki ndo Yanga walichokifanya kwa sasa kumtoa Kambole ndani na kumbakiza nje pekee kisha kumleta Kisinda ndani na nje badala yake. Tofauti unaiona wapi hapo?
 
Mwaka jana 2021, katika usajili wa dirisha dogo, SIMBA SC ilimsajili Perfect Chikwende na kufanya idadi ya wachezaji wa kigeni kufikia wachezaji 13. Kilichofanyika Francis Kahata akatolewa kwenye usajili wa ligi ya ndani halafu Perfect Chikwende jina lake likaingizwa. Francis Kahata akasajiliwa kwenye mashindano ya kimataifa tu. Kitu ambacho this time around Yanga wamefanya hivyo hivyo.
Simba waliielekeza TFF ikate jina la Francis Kahata iweke la Perfect Chikwende. Sasa badala ya kuanza kulalamika, hebu tueleze kwa uwazi kabisa, ili nafasi ya Tuisila Kisinda ipatikane, Yanga waliieleza TFF ikate jina la mchezaji gani?
 
Simba waliielekeza TFF ikate jina la Francis Kahata iweke la Perfect Chikwende. Sasa badala ya kuanza kulalamika, hebu tueleze kwa uwazi kabisa, ili nafasi ya Tuisila Kisinda ipatikane, Yanga waliieleza TFF ikate jina la mchezaji gani?
Kambole
 
Mwaka jana 2021, katika usajili wa dirisha dogo, SIMBA SC ilimsajili Perfect Chikwende na kufanya idadi ya wachezaji wa kigeni kufikia wachezaji 13. Kilichofanyika Francis Kahata akatolewa kwenye usajili wa ligi ya ndani halafu Perfect Chikwende jina lake likaingizwa. Francis Kahata akasajiliwa kwenye mashindano ya kimataifa tu. Kitu ambacho this time around Yanga wamefanya hivyo hivyo.
Mwaka huo kanuni zilikuwa zinaruhusu wachezaji 12 CAF na wachezaji 10 wa ligi ya Bara, kwa hiyo ukipeleka majina ya wachezaji 12 TFF inabidi useme nani akatwe. Kanuni za mwaka huu zimebadilika kwa upande wa TFF, na zimeruhusu kusajili wachezaji 12 sawa na wa CAF. Sasa ukipeleka majina 13, huyo aliyezidi atacheza ligi gani? Na kama haujasema nani akatwe, si anakatwa wa mwisho? Au ulitaka TFF ichague yeyote ili Tuisila aingizwe, je TFF ingemchagua Mayele, si mngeenda hadi kwa Mama Samia? Kwa nini msikate wenyewe?
 
IMG-20220904-WA0012.jpg
 
Mwaka huo kanuni zilikuwa zinaruhusu wachezaji 12 CAF na wachezaji 10 wa ligi ya Bara, kwa hiyo ukipeleka majina ya wachezaji 12 TFF inabidi useme nani akatwe. Kanuni za mwaka huu zimebadilika kwa upande wa TFF, na zimeruhusu kusajili wachezaji 12 sawa na wa CAF. Sasa ukipeleka majina 13, huyo aliyezidi atacheza ligi gani? Na kama haujasema nani akatwe, si anakatwa wa mwisho? Au ulitaka TFF ichague yeyote ili Tuisila aingizwe, je TFF ingemchagua Mayele, si mngeenda hadi kwa Mama Samia? Kwa nini msikate wenyewe?
Kuna kitu hujakielewa Mkuu
 
Mwaka huo kanuni zilikuwa zinaruhusu wachezaji 12 CAF na wachezaji 10 wa ligi ya Bara, kwa hiyo ukipeleka majina ya wachezaji 12 TFF inabidi useme nani akatwe. Kanuni za mwaka huu zimebadilika kwa upande wa TFF, na zimeruhusu kusajili wachezaji 12 sawa na wa CAF. Sasa ukipeleka majina 13, huyo aliyezidi atacheza ligi gani? Na kama haujasema nani akatwe, si anakatwa wa mwisho? Au ulitaka TFF ichague yeyote ili Tuisila aingizwe, je TFF ingemchagua Mayele, si mngeenda hadi kwa Mama Samia? Kwa nini msikate wenyewe?
Unapotoa hoja Uwe unajua ukweli wa unachoongea vinginevyo utaonekana kituko.. CAF haina idadi ya wachezaji wangapi wawe wa ndani wangapi wawe wa nje. Mwaka huu kutokana na Uviko timu imeruhusiwa hadi wachezaji 40 na si 12 kama unavyosema.
 
Ndio, TFF wanafuata kanuni kama mlivyohitaji. Au sasa hivi mnataka wapindishe kidogo?
CAF inaruhusu wachezaji 40 na Yanga iko CAF. Yanga ndo wamesema huyu na huyu watakuwa wa ndani na waliobaki watakuwa wa CAF. Hapo kanuni gani wamevunja Yanga?
 
Back
Top Bottom