TFF kilichoshindikana kwa Tuisila Kisinda kiliwezekana kwa Perfect Chikwende (double standard)

TFF kilichoshindikana kwa Tuisila Kisinda kiliwezekana kwa Perfect Chikwende (double standard)

Ilishawahi kutungwa kanuni ya bench la timu kuto vaa vipensi, Hii ikitokea baada ya aliyekua kocha wa Yanga kuwa ana vaa pensi akiwa uwanjani, Tff hii hii ya Karia, Baada ya Zahera kuondoka Yanga kwasasa kanuni iyo haifanyikazi, Matola kocha wa Simba anavaa pensi na abugudhiwi.
lakini katika yote huyu Wallace Karia ana shida gani na Yanga? au anaamini yeye ni Mkubwa kuliko Yanga?
 
Simba waliielekeza TFF ikate jina la Francis Kahata iweke la Perfect Chikwende. Sasa badala ya kuanza kulalamika, hebu tueleze kwa uwazi kabisa, ili nafasi ya Tuisila Kisinda ipatikane, Yanga waliieleza TFF ikate jina la mchezaji gani?
hahaha so issue ni kuwa yanga haijui nani wakumtoa? au hoja yako ni ipi hasa?
 
Karia hana shida na yanga wala yanga haina shida na karia. Ila kuna mtu ana shida na karia kwa maslahi yake binafsi na yanga ndo sehemu ya kufanikishia "dili" lake bahati mbaya wanayanga wamekubali kuingia mtegoni pasipo kujua kuwa kuna mtu anawafitinisha.

Yanga inatakiwa ifuate kanuni wao walishasajili wakamaliza na tff ikapitisha majina hayo ila kwa sasa kuna shida mahala kweye uongozi wa yanga wanaendesha mambo "kisela" mno bila kuzingatia kanuni na anayewapeleka hivyo yupo.

Angalia tu ishu ya yanga princess mpaka zimebaki siku mbili kabla dirisha kufungwa walikuwa hawajaingiza mchezaji yyte kwenye mfumo wa usajili na TFF ikawa kila siku inawakumbusha.
Viongozi wa yanga nawasihi fuateni kanuni.
 
Mwaka huo kanuni zilikuwa zinaruhusu wachezaji 12 CAF na wachezaji 10 wa ligi ya Bara, kwa hiyo ukipeleka majina ya wachezaji 12 TFF inabidi useme nani akatwe. Kanuni za mwaka huu zimebadilika kwa upande wa TFF, na zimeruhusu kusajili wachezaji 12 sawa na wa CAF. Sasa ukipeleka majina 13, huyo aliyezidi atacheza ligi gani? Na kama haujasema nani akatwe, si anakatwa wa mwisho? Au ulitaka TFF ichague yeyote ili Tuisila aingizwe, je TFF ingemchagua Mayele, si mngeenda hadi kwa Mama Samia? Kwa nini msikate wenyewe
Mchezaji anawezaje ku qualify kucheza michuano ya CAF Bila kwanza ku qualify kucheza ndani.
League inaruhusu kusajiri wachezaji 10 hata Kama CAF hawana hicho kigezo, hao 12 ili wacheze michuano ya CAF lazima kwanza wasajiriwe na Simba katika ligi ambayo inaruhusu kusajiri wachezaji 10 tu wa kigeni.
 
Watopolo mbona hamtaki kutumia akili au alivyosema Haji kuwa nyie ni hamnazo?
1662373971412.jpg
 
Kwahiyo shida ipo hapa!?
Hapana.shida ni KANUNI NA SHERIA NI MSUMENO.siku ukikukata usilalamike.wachezaji wa kigeni mwisho 12.mngemtoa Nani hapo?kwa akili zenu mngesema mngemtoa kwa mkopo mchezaji mmoja.mngempeleka wapi?
Screenshot_20220905-133847.png
 
Unapotoa hoja Uwe unajua ukweli wa unachoongea vinginevyo utaonekana kituko.. CAF haina idadi ya wachezaji wangapi wawe wa ndani wangapi wawe wa nje. Mwaka huu kutokana na Uviko timu imeruhusiwa hadi wachezaji 40 na si 12 kama unavyosema.
Kama chama cha soka cha nchi husika kinaruhusu ligi yake iwe na wachezaji 12, na CAF inaruhusu wawe 40, ni jukumu la klabu kutaja nani awemo kwenye ligi ya ndani na ya CAF, na nani awemo kwenye ligi ya CAF tu. Ukipeleka majina bila kutaja huo mchanganuo, TFF itakata kwenye mstari wake
 
CAF inaruhusu wachezaji 40 na Yanga iko CAF. Yanga ndo wamesema huyu na huyu watakuwa wa ndani na waliobaki watakuwa wa CAF. Hapo kanuni gani wamevunja Yanga?
Wataje kwa majina, usiseme huyu na huyu. Mbona Tuisila anatajwa kwa jina, hao au huyo anayekatwa kwa nini hatajwi? Na umejiuliza ni kwa nini haya madai hayatolewi na uongozi wa Yanga, ila yanatolewa na Manara?
 
Mchezaji anawezaje ku qualify kucheza michuano ya CAF Bila kwanza ku qualify kucheza ndani.
League inaruhusu kusajiri wachezaji 10 hata Kama CAF hawana hicho kigezo, hao 12 ili wacheze michuano ya CAF lazima kwanza wasajiriwe na Simba katika ligi ambayo inaruhusu kusajiri wachezaji 10 tu wa kigeni.
Kahata ilikuwa hivyo, usiseme haiwezekani. Alicheza ya kimataifa ila ndani alikuwa hachezi
 
hahaha so issue ni kuwa yanga haijui nani wakumtoa? au hoja yako ni ipi hasa?
Mtaje kwa jina, mbona wewe mwenyewe mwananchi lakini hujui ni nani amekatwa, ila unafuata tu anachosema Manara? Umesikia uongozi wa Yanga umelalamika?
 
Msije mkauana tuu naona sasa ni mapambano sio tena ushabiki.
 
Kama chama cha soka cha nchi husika kinaruhusu ligi yake iwe na wachezaji 12, na CAF inaruhusu wawe 40, ni jukumu la klabu kutaja nani awemo kwenye ligi ya ndani na ya CAF, na nani awemo kwenye ligi ya CAF tu. Ukipeleka majina bila kutaja huo mchanganuo, TFF itakata kwenye mstari wake
Na Yanga wametaja. Soma hiyo barua ya Clifford utagundua tatizo siyo kutaja ila ni kulazimisha wachezaji wawe 12. Ndo maana tusio na upande tunauliza Kahata na Chikwende ilikuwa nchi gani?
 
Mtaje kwa jina, mbona wewe mwenyewe mwananchi lakini hujui ni nani amekatwa, ila unafuata tu anachosema Manara? Umesikia uongozi wa Yanga umelalamika?
hio haiwez kuwa sababu, haiwezekan wao wenyew waombe kuongeza mtu halafu wasijue nanii wakumreplace, kutakua na sababu ya kikanuni tu na sio hio unayosema ww
 
Back
Top Bottom