TFF yatangaza kuipoka Simba pointi tatu, yazirudisha kwa Kagera Sugar

TFF yatangaza kuipoka Simba pointi tatu, yazirudisha kwa Kagera Sugar

Kagera walikata rufaa kua mchezaji wao hana kadi 3 leo imezibitika kweli alikua ana kadi 3 alafu point wanapewa only in bongo
 
huyu jamaa kafungiwa kwa kulilia point za mezani.

Aibu ya Maandamano Sc.

Breaking Newzz: TFF yamfungia Haji Manara miezi 12
MUUNGWANA BLOG / 12 minutes ago


Kamati ya Nidhamu ya TFF, imetangaza kumfungia miezi 12 Msemaji wa Simba, Haji Manara.Pia nakulipa faini ya Shilingi milioni 9.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Nidhamu ya TFF, Wakili Jerome Msemwa amesema Manara amefungiwa miezi 12 kutokana na utovu wa nidhamu.
 
Mpira Tz kwishaaaa. Simba tunajiondoa kwenye ligi na kuwaachieni timu zenyu. Sote tunahamia UAR kwenda jiandikisha huko na tutakutana kwenye ligi ya dunia. Lazima alogwe mtu hapa. Aalah! Mnatuchezea?? Yanga mtafungwa goli 20 kila mechi ambayo mtacheza tangu leo. Mtaona
Hahahaa! Sio kwa hasira hizo mkuu inabidi mkubali tu ndio mpira huo.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Swala nimchezaji alikua na kadi au hana? mbona alivyoitwa kuhojiwa pamoja na viongozi wao kagera wanasema alikua na kadi 2 leo Tff wanasema ana kadi 3 ataitumikia mechi ijayo...wewe kiazi malinzi acha ukabila
Mkuu, umenifanya nirudie kuusoma uzi upya; hapo kweny bold umepatoa wapi?
 
Soka la bongo madudu matupu! Hata hao wanaotuwakilisha si vilabu sio timu ya taifa! Ni umbumbumbu tu! Na kuanzia Leo sishabikii soka la bongo maana Mimi huwa sipangiwi!
 
Simba wanakumbushiwa tu sakata la Lufunga kuwa na red card akawepo kwenye kikosi dhidi ya Police Dar, kamati hii inayoongizwa na Simba ikaitupa rufaa ya Police kwa kigezo cha kuletwa nje ya muda na haikulipiwa ada leo hii Simba nao wanakosa kumbukumbu yaani wanakata rufaa nje ya muda na tena sio kwa maandishi na hawakulipa ada.
Ukiwa muongo uwe na kumbukumbu nzuri, ni Simba hawa walimchezesha Ajib akiwa na kadi 3 wakadai wameiandikia bodi ya ligi mchezaji awe anachagua mechi.
Muosha huoshwa japo siikubali tff ila simba ndio waasisi wa hii michezo ya kitoto.
 
  • Thanks
Reactions: MTK

Shirikisho la Soka la Tanzania (TFF) limetangaza kuipoka Simba pointi tatu na mabao matatu ambazo ilipewa kutokana na mchezo wao dhidi ya Kagera Sugar.

Wiki mbili zilizopita Simba ilipoteza mchezo dhidi ya Kagera kwa kufungwa mabao 2-1 kwenye Uwanja wa Kaitaba mkoani Kagera katika mchezo wa Ligi Kuu ya Bara lakini baadaye ilikata rufaa ikipinga Kagera kumtumia mchezaji Mohamed Fakhi ikidai alikuwa na kadi tatu za njano, ndipo ikapewa ushindi huo kupitia Kamati ya Saa 71.

Mara baada ya kamati hiyo kuipa Simba pointi Kagera ikaomba kupitiwa upya kwa suala hilo na nsipo TFF ikatangaza kuwa suala hilo sasa litakuwa chini ya Kamati ya Katiba, Sheria na Hadhi za Wachezaji ya TFF ambayo ndiyo imetoa maamuzi hayo.

Akizungumza na waandishi wa habari juu ya uamuzi huo, Katibu Mkuu wa TFF, Selestine Mwesigwa amesema kuwa kuna sababu kadhaa zimechangia kuchukuliwa kwa maamuzi hayo ambapo alisitaja kuwa ni:

“Malalamiko ya Simba hayakuwasilishwa kwa wakati muafaka tangu mchezo ulipochezwa, malalamiko yao hayakuwa katika njia ya maandishi, rufaa ya Simba haikulipiwa ada, kikao cha Kamati ya Saa 72 kilikosa uhalali kutokana na kuwashirikisha watu ambao hawana uhalali wa kuwa kwenye kikao.

“Kutokana na sababu hizo kamati imeamua kufuta maamuzi yaliyochukuliwa na Kamati ya Saa 72 na kurejesha matokeo kama yalivyokuwa, pia kamati imemuagiza katibu mkuu wa TFF kuwapeweleka baadhi ya wajumbe wa bodi ya ligi katika Kamati ya Maadili ya TFF kwa kosa la kwenda kinyume na kazi zao,” alisema Mwesigwa.
Kwa hiyo kwenye hukumu suala la mchezaji kupewa kadi 2,1,0 au tatu ni exclusive kabisa? Yaani ukweli wa idadi kadi alizopewa mchezaji limekuwa nullified na kasoro hizo?
Kazi ipo!
 
Mimi nilifikiri wameangalia SUBSTANCE ya madai yenyewe kumbe wamejikita kwenye FORM? irregularity hizo kisheria ni curable na ni maoni yangu kuwa wangetoa hukumu ya re trial tofauti na walivyofanya kuwatolea nje madai yao kwa technical ground.
 
daa masikini mnyama sasa hawezi kuwinda tena sasa usubiri ufe tuu
au wamtafute Bashite akaliibe kombe pale TFF
 
Poleni sana vikojozi, na hiii ndiyo hasara ya kutegemea ppkubebwa bebwa kwa mbeleko ya chuma, next time mjifunze kushinda uwanjani! Mliwa nyonga polisi dar sasa kamba hiyo hiyo imenyonga na nyinyi!
 
Ukiuwa utakufa kwa upanga hii hii sheria ndio iliwanyima haki police dar dhidi ya simba kwenye kombe la FA
 
Nasikia Simba wamepanga kuandamana ili utaratibu ubadilishwe - mpira uchezwe mezani na ugali uliwe uwanjani.....
 
  • Thanks
Reactions: MTK
Breaking Newzz: TFF yamfungia Haji Manara miezi 12
MUUNGWANA BLOG / 12 minutes ago


Kamati ya Nidhamu ya TFF, imetangaza kumfungia miezi 12 Msemaji wa Simba, Haji Manara.Pia nakulipa faini ya Shilingi milioni 9.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Nidhamu ya TFF, Wakili Jerome Msemwa amesema Manara amefungiwa miezi 12 kutokana na utovu wa nidhamu.
Huyu dogo mtoa povu miezi kumi na mbili haimtoshi.
 
  • Thanks
Reactions: MTK
Nasikia Simba wamepanga kuandamana ili utaratibu ubadilishwe - mpira uchezwe mezani na ugali uliwe uwanjani.....
[emoji3] [emoji3] [emoji3] [emoji3]
 
Back
Top Bottom