TFF yatoa maamuzi sakata la Ramadhani Singano 'Messi' na timu yake Simba

TFF yatoa maamuzi sakata la Ramadhani Singano 'Messi' na timu yake Simba

Messi fanya haya ili uwe mchezaji huru na uende kokote upatakapo.
1.Kaa meza moja na Simba ili mzungumze mkataba mpya.
2.Wambie wakupe dau la $50,000
3.Wambie wakupe mshahara wa $4000 kwa mwezi.
4.Mkataba usizidi mwaka1.
Najua hawa "mambumbu FC hawatakubali,kisha utakua huru na utaenda kwa "MDOGO WAKE WA KIKE" AZAM.
TOPIC CLOSED!!
 
Acha tu kumbe dogo mbwembwe zote zile uwanjan kumbe analala kwa bro daaah so shame? Jaribu kukumbuka samatta ilikuaje

Shame gani wakati dogo anafight kwa ajili ya maisha? Uwezo wake ndo huo, hajapata fursa.
 
Hapa hakuna kutumia busara hata kidogo. Yaani wameficha jinai halafu tunawasifu wametumia busara? Hili suala ilibidi liende kwenye vyombo vya sheria ili kutoa onyo wa wapuuzi wengine wasijaribu kufanya forgery. Simba wameforge mkataba na kuongeza mwaka mwingine mmoja. Huu ni uhuni na ni jinai.

Tiba

Umenena vyema bro!!

Huyo messi atafute wanasheria wa maana waipeleke simba mahakamani watiwe adabu.
 
Tuwekeeni barua waliyopewa Simba na Messi kutoka TFF kuhusiana na kikao chao cha leo, sio kujadili kwa kufuata alichokiandika Shaffih Dauda.
 
Aende hana jipya. Msuva mdogo atacover nafasi yake. mtu hata kitanda huna unataka m50 na gari??
 
Acha tu kumbe dogo mbwembwe zote zile uwanjan kumbe analala kwa bro daaah so shame? Jaribu kukumbuka samatta ilikuaje

Ndo maana dogo Kaamua kukomaa kwenda kwenye mshahara mnono.
 
Taarifa.jpg
 
Messi fanya haya ili uwe mchezaji huru na uende kokote upatakapo.
1.Kaa meza moja na Simba ili mzungumze mkataba mpya.
2.Wambie wakupe dau la $50,000
3.Wambie wakupe mshahara wa $4000 kwa mwezi.
4.Mkataba usizidi mwaka1.
Najua hawa mambumbu FC hawatakubali,kisha utakua huru na utaenda kwa "MDOGO WAKE WA KIKE" AZAM.
TOPIC CLOSED!!


1. Mezani wamekaa mara kibao, hawakukubaliana ndo mana wakakimbia TFF.
2. Kama ilishindkana kumpatia hilo dau kocha Goran, itawezekanaje kwa Messi?!
3. Kama "mtalamu" Okwi anapata dola 3000 kwa mwezi.. Huyu dogo ana ubavu gani wa kupewa zaidi?!
4. Kama kutaka mkataba wa mwaka 1, ilikua ni sababu ya kunyimwa mkataba Goran.. itakuaje kwa huyu dogo ambae amekua na kiwango cha kupanda na kushuka?!
Hadi sasa TFF wamekiri kua Messi yupo huru.. hivyo namtakia changamoto njema katika safari yake.
 
mpira wa kibongo magumashi sana. sheria zinatumika kwa wachache tu
 

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limetangaza kwamba klabu ya Simba na kiungo Ramadhani Singano ‘Messi' watakaa na kujadili mkataba wao upya.



Katibu Mkuu wa TFF, Mwesigwa Selestine amesema wamegundua mikataba miwili alionao Messi na walionao Simba, ina matatizo.

"Hivyo tumekubaliana waanze mwanzo kujadili tena ingawa ni muhimu kuzingatia mkataba mama," alisema Mwesigwa.

Suala la kuzingatia mkataba mama ambao ndiyo ule wa Simba, nalo limeonekana kuzua utata jambo ambalo limezidi kuwachanganya hata waandishi lakini katibu huyo alipoulizwa, alijibu.

"Hatujaja hapa kutangaza mshindi ni nani, kwa kifupi ni vizuri waanze upya na kujadili kuhusiana na mkataba mpya," alisema.

Messi alikuwa na mkataba unaoiisha 2015, wakati Simba wana mkataba unaoisha 2016 jambo lililozua tafrani kati yao.

Licha ya Mwesigwa kukiri kulikuwa na mapungufu pande zote mbili baada ya kikao hicho cha pande zote pamoja na Sputanza, bado alishindwa kuweka wazi kama Messi bado ni mchezaji wa Simba au makubaliano yanamfanye awe huru.

"Siwezi kuweka hadharani masuala yanayohusu mkataba, hiyo ni siri kati ya mchezaji na klabu," alisisitiza.

Hiyo ni nukuu kutoka kwenye Blog ya Salehjembe.
 
siyo lazima washushe kibano kwa mchezaji kwa kuwa anataka kwenda timu yenye maslahi nao sasa wakimfungia itakuwaje?
 
Yaani hawa tff, sasa huo ndio uamuzi gani??!! na inaoneka Messi ameshinda kwenye hili, sasa ili kuwasaidia simba ina bidi walete magumashi mengine, yaani ni shida tu kumbe kina hans walikuw wana mtisha dogo tu, kumbe wao ndio magumashi!!! kweli soka la bongo sina hamu nalo. Na siku zote mwisho wa ubaya ni aibu.

Huyo ndio Malinzi bwana..na huyo ndio muwakilishi wetu kwenye kumchagua Blatter..akili za kima kabisa hizi
 
fununu zulizopo tff mkataba wa miaka 3 wa simba ndio wenye makosa , tff wameamua kutumia busara zaidi ili kutoweka wazi nani mwenye makosa

Hapana kama ni kweli basi TFF hawakutumia busara ila wamemlaghai (deceive) kijana. Ilibidi wapelekwe mahakani iwe fundisho kwa wengine. Kwa mchezo huu wa TFF soka la Tanzania haliwezi kusogea. Limejaa ujanja ujanja tu.
 
Hata hao viongozi wa chama cha wachezaji wa mpira wa miguu (SPUTANZA) nao hovyo tu, sioni kama wametetea maslahi ya singano
 
duh, mkataba wa halali ndio unaotakiwa kufuatwa acheni blah blah
 
Mkia wana historia ya kufoji mikataba,walifanya hivyo kwa Chuji pia
 
Sio simba tu, timu nyingi za bongo zimekaa kihunihuni tu ndo maana wanapokutana na wale wenye proffession zao wanaambulia kipigo.
Nadhani hilo la Singano ni la Simba.
 
Back
Top Bottom