TFF yatoa maamuzi sakata la Ramadhani Singano 'Messi' na timu yake Simba

Tff ni tifutifu.. Huyo mwesiga kichwa cha majibu kama Rais wake..mlitegemea maamuzi gani zaidi ya haya. huyo barua yenyewe inakinzana na jinsi vyombo vya habari vilivyoreport kwani haisemi ni walichokubaliana imeishia katikati nadhani kaandika mbumbumbu mwesiga. ila kwa watu kwenye akili au Mimi kama ningekuwa ni huyo dogo maamuzi ya leo manake yupo huru....
 
Nadhani hilo la Singano ni la Simba.

Kufoji mikataba ni taaluma ya mikia. Kuna issue ikifia kwa Tabaigana. Aliwasave kwa kuwa yeye ni mikia damu. Ipo siku wataumbuka. Kuna watu mahakama zinawaita kwa hizi forgery.
 
Habari za chini zinasema TFF inaogopa kusema Simba imefoji mkataba wa miaka 3 maana itaharibu ''IMAGE'' ya klabu ya Simba na kusababisha kupoteza wadhamini wa klabu

acha uongo...
 
Kufoji mikataba ni taaluma ya mikia. Kuna issue ikifia kwa Tabaigana. Aliwasave kwa kuwa yeye ni mikia damu. Ipo siku wataumbuka. Kuna watu mahakama zinawaita kwa hizi forgery.

Swala LA Okwi mlifanyaje...
 

Tz haitaisha vituko eti naye siku hizi anajiita KOFI ANAN!!
 
Swala LA Okwi mlifanyaje...
Nani aliekuambia yanga walifoji mkataba wa okwi!!!
Mkuu unapaswa kuelewa mambo haya mawili;
1. Kuna kufoji mkataba, hii ina maana kuwa umeandika mkataba wa kubuniwa au ghushiwa, kama alivyofanyiwa Ramadhan Singano.

2.Kutotimiza matakwa au masharti ya mkataba. Hii ina maana kuwa pande mbili zimekubaliana jambo fulan lakin ikatokea upande mmoja ukashindwa kutimiza masharti ya makubaliano. Kama ilivyotokea kwa okwi-yanga au Hassan kessy-simba.
Nadhani umenielewa.
 
Huyu Hans Pope ndo bure kabisa, yan anavyojaribu kurubuni uma hv hv
 
Simba huwa ina uongozi mbumbumbu miaka yote...

Matatizo ya usajili na mikataba kwenye klabu hii hutokea karibu kila mwaka...

Hii mambo lazima itakuwa ilitokea wakati wa Msomali yule...
 
Huyu Hans Pope ndo bure kabisa, yan anavyojaribu kurubuni uma hv hv


Mkuu katika mkutano wa TFF ulioamua hili suala, wajumbe waliokuwapo ni;

1. Collin Frisch - Simba SC
2. Ramadhan Singano
3. Kisoki - Mwenyekiti Sputanza
4. Celestine - Katibu TFF

Sasa hapa Hans Pope anaingiaje Mkuu?
 
Mkuu katika mkutano wa TFF ulioamua hili suala, wajumbe waliokuwapo ni;

1. Collin Frisch - Simba SC
2. Ramadhan Singano
3. Kisoki - Mwenyekiti Sputanza
4. Celestine - Katibu TFF

Sasa hapa Hans Pope anaingiaje Mkuu?
Anaongea e FM
 
Shetangananaibebasimba. Kilasikunauhuni wakugushimikatabq singano nenda. Police kamalizekazi
 

Just one qn kwann TFF inaingilia hii kitu and y ianze kuita kikao wakat ina mkataba halali so wanajua messi alisign muda gani na lastly y kuna mikataba miwili inayotofautiana?
 
Habari za chini zinasema TFF inaogopa kusema Simba imefoji mkataba wa miaka 3 maana itaharibu ''IMAGE'' ya klabu ya Simba na kusababisha kupoteza wadhamini wa klabu

So inawahusu nn wakipoteza wadhamini?huu ni upuuzi usiopaswa kufumbiwa macho
 

Tusiwe wavivu wa kufikiri. TFF ina mkataba wa Simba, sio wa Messi. Kama wataenda mbele kisheria, mkataba utakaojadiliwa ni wa Simba kwani pamoja na makosa ulionao, ndio uliopo na unaotambuliwa na TFF. Kwa ufupi, mkataba wa Messi haupo TFF na kwa bahati mbaya zaidi hata alionao mkononi umepigwa photocopy, sio original. TFF hawakuwa wajinga kumlazimisha Messi akaongee na Simba kwani inajua kwamba kilichopo ofisini ni Messi kuwa na mkataba wa mwaka mzima mmoia zaidi.
 
Mimi kama ningekuwa ni huyo dogo maamuzi ya leo manake yupo huru....
Kinachoamua awepo au asiwepo huru ni mkataba uliopo ndani ya ofisi za TFF. Mkataba uliopo TFF ni wa miaka mitatu, sasa akisaini timu nyingine atashindwa tu kesi kama Ngasa alivyoshindwa, na atalazimika kukosa mechi sita, kuilipa fidia Simba na riba juu. Kumbukeni madhara yaliyomkuta Ngasa hadi akakopa hela benki na deni lile ndilo limemkimbiza Yanga kwa kuwa walimdanganya kuwa watasaidia kumlipia
 

hii mikataba inaandaliwa kishera na wanasheria au uhuni wa kitaani, haiingii akilini kugusihi mkataba, tuache blaablaa wabongo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…