Thabo Bester maarufu 'Mbakaji wa Facebook' na Dkt. Nandipha Magudumana wakamatiwa Arusha Tanzania. Wafahamu kwa undani wapenzi hawa

Thabo Bester maarufu 'Mbakaji wa Facebook' na Dkt. Nandipha Magudumana wakamatiwa Arusha Tanzania. Wafahamu kwa undani wapenzi hawa

Mm nikiwa Rais ntahakikisha natekeleza adhabu ya kifo, kwakweli ni muhimu sana. Yaan mtu auwe watu afu afungwe tu kifungo cha maisha, anakula na kulala bure wakati aliowaua wanaoza makaburini? Kwangu hapana, ni Utanyongwa au kupigwa Risasi.
Na hiyo kunyongwa au kupigwa risasi anatakiwa achague yeye mwenyewe anayetakiwa kuuliwa.
 
Hii ni mbaya sana yaani unaratibu mauji ya mtu asiye na Hatia Kwa kuchoma gereza Ili tuu wewe utoroke gerezani.

Kuna mashaka sana na security appatus za Afrika Kusini.

Reference: Thabo Bester and Spouse Dr Nandipha Magadugula.

=======

Tanzania Police have confirmed the arrest of South African prison escapee Thabo Bester and his accomplice Dr. Nandipa Magudumana and one other person by the name of Zakaria Alberto.

In a short statement released by the Police Spokesperson David A Misime, Tanzania Police said they are finalizing, “other international and national procedures” for the case.

Thabo Bester, a serial rapist, scammer, and murderer was confirmed to have escaped Mangaung Prison in South Africa in March 2023 after a viral Twitter picture that showed him shopping. It was later learned that Bester had escaped prison in May 2022 in a ploy that involved fake suicide.

Prison cell where Bester was kept had caught fire only for his corpse to be found burnt beyond recognition. Bester was pronounced dead, only for the news to resurface on social media that he was living large with South African celebrity Doctor, Nandipa Magundumana.

Reports show it was a complex scheme that involved Dr Nandipa Magundumana who collected the burnt corpse from prison, claiming she was the wife of Thabo Bester.

Confirming the arrest of Thabo Bester, South Africa Minister of Justice and Correctional Services Ronald Lamola, says he is expecting to be in Tanzania on Sunday, April 09, 2023, to follow up on the case.

“We have confirmed with all relevant authorities in Tanzania which include the national Police in Tanzania and Interpol that fugitives have been processed in the Tanzania criminal justice system,” said Lamola in a press statement.
Huyo aliyechomwa huko gerezani mna uhakika gani alikuwa mzima au ni mtu wa kweli? Hii habari inasema tu huyu dada alichukuwa mabaki yaliyoungua kiasi cha kutotambulikana. Hapa nimejiuliza mengi: 1. Je, walichukuwa mtu aliye hai wakamchoma? Je, waliingiza maiti kutoka sehemu nyingine wakaichoma? Je, inawekana wala siyo binadamu aliyeunguzwa?
 
Hao ni majasusi wa dunia.

Mbaya kuua mtu ili wewe uokoke, mbaya zaidi mbele za Mungu pia.

All in all polisi wa tz wako vizuri, naogopa kusema CONGRATULATIONS.

Angesogea hapo kwa Uhuru asingekamatwa mpaka afe kweli kweli.
Kwanini unasema wako vizuri? Hapa walipewa tip tu na wenzao wa S. Africa kuwa huyu mtu amekuja huko! Halafu inaonekana baada ya kufeki kuwa amejiunguza alijiamini sana akawa anajiachia mitaani akidhani watu wote wameamini kuwa ameshafariki hivyo siyo rahisi kuhisiwa.
 
Moja: Aliyechomwa moto kuna uhakika kwamba alikuwa hai ? (Issue kama hii sio mpya ishafanyika sana lakini wengi huwa wanachukuwa mwili mortually especially mwili wa Jane au John Doe hii inarahisisha kupunguza maswali ya fulani kapotea....

Mbili: hayo ya security naomba yawe kama alert hususan kwa sisi tunaopenda kubinafsisha kila kitu (hayo magereza ni private run); Kwahio hayo mambo yakija huku na watu kuleta miswada yao ili waendelee kupiga kwa kubinafisha magereza taomba tukumbushie hii kwenye reference ya why not to......
Actally naona hiki ndicho kilichofsnyika maana ingekuwa ni mfungwa mwingine ndio kauawa na kuchomwa ili huyo mhalifu atoroke, ni wazi mamlaka za jela zingegundua kupotea kwa mfungwa mmoja humo ndani. Umewaza vyema kabisa.
 
Sijaelewa toa habari kamili
Nadhani kutakua na nyama zaidi next time watakapoletwa mahakamani, wote tunaelewa kuwa Mr.Bester hakufa pale jela kuna mtu ambaye kuna dalili kuwa aliuliwa ili ionekane aliyekufa ni Mr.Bester ,inawezekana Dr Nandipa father amehusika na mauaji ya mtu huyu, ngoja tuendelee kusoma news24.com na eNCA
 
... SA walifuta adhabu ya kunyonga adhabu pekee aliyostahili Bester! Angekatiwa hiyo adhabu na ikatekelezwa inavyopaswa bila figisu shida zote hizi za kuhangaika naye zingeshasahaulika zamani. Adhabu ya kunyonga bado ina umuhimu mkubwa duniani.
Omba kazi hiyo. Ninani ameruhusu kuua? USIUE NDIO AMRI. HAKUNA MBADALA
 
Walikubali kwavile walihongwa pesa
Actually tangu weusi washike hatamu za uongozi hapo South, kuna ujinga mwingi sana umezaliwa. Hao viongozi wenyewe wa ANC kuanzia Rais mpaka viongozi waandamizi chamani ni wala rushwa/mafisadi wakubwa kabisa. Sasa wale wa chini wataacha kuiga matendo yao!?
 
Nadhani kutakua na nyama zaidi next time watakapoletwa mahakamani, wote tunaelewa kuwa Mr.Bester hakufa pale jela kuna mtu ambaye kuna dalili kuwa aliuliwa ili ionekane aliyekufa ni Mr.Bester ,inawezekana Dr Nandipa father amehusika na mauaji ya mtu huyu, ngoja tuendelee kusoma news24.com na eNCA
Tunasubiri
 
Good question mkuu, naona tumekubaliana kuwa iliyoingizwa mle ni maiti, sio mtu hai then akachomwa moto na kuuliwa mle, elewa SA ni moja ya nchi hapa duniani zenye mauaji mengi na ya kutisha, kupata maiti sio big issue hapo SA, huyu binadamu anaweza alikua ameuliwa kule kwa township kwa kupigwa hivyo na maiti yake ikatumika au walikwenda mortuary na kununua maiti ili kufanikisha mpango wao, inawezekana hii maiti ni ya foreigner, means kutakua hakuna madai kutoka kwa SA family, na kuna sitofahamu kuwa Dr.Nandipa aliiomba maiti hii aizike yeye!,Tanzania we need to have a DNA forensics lab as sooner as possible, iwe chini ya jeshi letu la police, hii ya mkemia mkuu kwangu ni utapeli fulani
Criminals wana akili nyingi sana. Laiti wangezitumia kufanyia mambo mazuri. Ila good observation Mkuu.
 
Waliingia na full documents ila walidanganya details, yaan walikuja na majina tofauti kwenye Passport zao. Sio kwamba wameingia bila passport kabisa kiongozi.
Hawawezi kutumia passport watu wanaotafutwa kwa maana Nchi zote wanakua na taarifa ukipeleka Passport tuu wanakamata ndio maana wao walitumia gari mpaka Harare kwa kupita kwa kuhonga mpaka wanaingia Tanzania na kutoka...
 
Criminals wana akili nyingi sana. Laiti wangezitumia kufanyia mambo mazuri. Ila good observation Mkuu.
Huyu jamaa alitoka muda jela mwaka jana akajisahau akaanza kwenda kula bata watu wakamuona Centurion na kusema mbona pana mtu kaonekana akilipia vitu Mall moja hapo wazee walipoenda kuangalia CCTV za pale wakagundua kweli ikabidi waanze kumsaka kimya kimya ndio akaona akimbie kumbuka alitumia zaidi ya 5milion katoa kama rushwa wale waliopokea rushwa wanampa taarifa zinazoendelea maana karibu wengi wao walishaanza kuhojiwa baada ya kuchunguzwa account zao na mawasiliano ya Simu...
 
Mkuu jadili hoja sio kumjadili Nkanini, na tuna haki ya kutofautiana,our former PM Mr.Pinda naye hapendi death sentence na amelisema hili public,ni msimamo wake, nami death sentence it's a NO ndio msimamo wangu, nami ninayajua matusi but usinifanye nikutukane
Hapo kuna tusi mkuu? Mi nimekueleza kwa uhalisia aliuemchinya mama yako au Baba yako, utapendelea afungwe kifungo cha maisha badala ya kunyongwa?
Msifunge akili zenu kisa mko upande ambao hamjafikiwa na hiyo kadhia ya kuuawa kwa mtu wako wa karibu.

Mimi mtu akimuua tu ndugu yangu, hata kabla ya mahakama kuamua nahikikisha namuua. Siwezi kulea ujinga
 
Hiyo ni kazi ya Interpol, ndiyo wanaotoa descriptions na ndiyo wanao ongoza msako lakini arresting hufanywa na askari wa nchi husika (aliyokamatiwa) hata taarifa hutolewa na nchi ambapo mharifu amekamatiwa.
Wakati mwingine inaweza isiwe interpol lakini ikawa ni joint mission
We ukisikia INTERPOL unadhani ni wazungu, waamerika, siyo? Ungejua katika nchi wanachama wa Interpol kazi za Interpol zinafanywa na askari police wa nchi husika ambao wapo kitengo cha Interpol.

Yani kiufupi, hatoki askari New Zealand, US, Urusi au UK ndo awe Interpol. Ndani ya police Tanzania kuna kitengo cha Interpol pale makao makuu ya polisi kama vilivyo vitengo vingine Traffic, FFU, GD, STPU, intelligence, CID nk. Hao INTERPOL wa police Tz ndo hufanya kazi na Interpol wengine nchi nyingine huko duniani. Arrest ya mhalifu wa kimataifa hufanywa na yeyote hapa nchini, aweza kuwa local police au hata huyo Interpol police kwa kuwa na yy ni mmoja wa local police ila yupo katika kitengo cha interpol
 
P
Hivi uliwahi kusome shule kweli? Toka lini shuleni mwalimu akauliza swali afu mwanafunzi na yeye akajibu kwa kumuuliza mwalimu swali? Imanaa jibu la swali ni swali lingine?

Badala ya wewe kuweka fact ya lini waliingia nchini na lini walianza kutafutwa na kukamatwa, na jinsi interpol walifanikisha njia ya kukamatwa kwao ili kujibu swali langu eti na wewe tena unaniuliza swali kabla ya kujibu swali. Aisee elimu yetu inabidi ipitiwe upya ili watu waweze kujua namna ya kujibu kwanza swali kisha ndio kuuliza swali 😂😂😂
😂😂😂 huwa nacheka mtu anaponambia kuwa nimepotosha swala fulani ambalo hata na yeye hakuwepo kuliona.

Sasa wewe ambae haupotoshi utuwekee evidence inayoonesha kuwa unachoongea ni kweli. Nikimaanisha fact ambazo zitaonesha kuwa interpol ndio waliohusika na ukamataji huo, au ushahidi kuwa walitoa saini yoyote kwa jeshi letu la polisi kuwakamata hao jamaa.

Kuna msemo unaosema kuwa usimkate mtoto wako mkono kisa ameshika kinyesi. Nikimaanisha kwamba usitengeneze chuki kwa polisi kisa tu kuna watu wameifanya akili yako iwachukie hata pale wanapofanya mazuri, wewe uone mabaya.
Polisi wa Tz walijuaje kuwa hawa jamaa ni wahalifu kama hawakupewa taarifa zao na movement zao!? Binafsi naona walichofanya ni kusaidia tu kazi ya kukamata.
 
Hapo kuna tusi mkuu? Mi nimekueleza kwa uhalisia aliuemchinya mama yako au Baba yako, utapendelea afungwe kifungo cha maisha badala ya kunyongwa?
Msifunge akili zenu kisa mko upande ambao hamjafikiwa na hiyo kadhia ya kuuawa kwa mtu wako wa karibu.

Mimi mtu akimuua tu ndugu yangu, hata kabla ya mahakama kuamua nahikikisha namuua. Siwezi kulea ujinga
Nimekuelewa mkuu na ninaomba hiyo kitu ISITOKEE ili nawe usiwe murderer kama Mr.Bester
 
We ukisikia INTERPOL unadhani ni wazungu, waamerika, siyo? Ungejua katika nchi wanachama wa Interpol kazi za Interpol zinafanywa na askari police wa nchi husika ambao wapo kitengo cha Interpol.

Yani kiufupi, hatoki askari New Zealand, US, Urusi au UK ndo awe Interpol. Ndani ya police Tanzania kuna kitengo cha Interpol pale makao makuu ya polisi kama vilivyo vitengo vingine Traffic, FFU, GD, STPU, intelligence, CID nk. Hao INTERPOL wa police Tz ndo hufanya kazi na Interpol wengine nchi nyingine huko duniani. Arrest ya mhalifu wa kimataifa hufanywa na yeyote hapa nchini, aweza kuwa local police au hata huyo Interpol police kwa kuwa na yy ni mmoja wa local police ila yupo katika kitengo cha interpol
Yaani ma wewe japo ndiyo umeelekeza? Unashindwa hata kuelewa hoja unakimbilia kuelezea vitu obvious?
Sasa hayo unayoyaelezea hapo ni nani asiyeelewa?
Muwe mnajifunza kuelewa kitu kabla ya kukimbilia kuongea ili mradi, halafu unaelezea mpaka unarudia niliyoyaelezea.
Majibu yako ungetafuta wa kumuelezea lakini siyo mimi, kwangu labda kama ungekuja ku topup
 
P

Polisi wa Tz walijuaje kuwa hawa jamaa ni wahalifu kama hawakupewa taarifa zao na movement zao!? Binafsi naona walichofanya ni kusaidia tu kazi ya kukamata.
Hivi unafikiri mambo yanayofanyika duniani polisi wetu hawayajui? Hawafuatilii taarifa habari za nje na kujua wauaji na wafungwa wanaokamatwa na kuoneshwa kwenye vyombo vya habari?

Kesi ya huyo kijana ilikuwa ya wazi na watu wengi waliifatilia. Na hata hilo tukio la jamaa kushtukiwa kwamba ile maiti hauhusiani na huyo mfungwa pia lilitangazwa na msako nchini Afrika kusini ukaanza.

Cha kushangaza baada ya jamaa kugundua kwamba ishajulikana kuwa yeye hakufa kifo cha moto aliamua kutoroka bila kukamatwa na hao wanaowatafuta, pia nchi zote walizopita hawakuweza kugundulika na kukamatwa, ila walipofika kwetu ndo walipoanza kufuatiliwa na askari wetu waliobobea katika nyanja hizo na kufanikiwa kukamatwa.

Ndio maana kuna mchangiaji alisema laiti kama wangefanikiwa kuvuka kuingia Kenya basi mpaka leo wangekuwa bado wanatafutwa na hao interpol wenu. Kwa sababu inaaminika vyema askari wa Kenya wanavyopenda rushwa bila kujali madhara yatokanayo na rushwa.

Kama askari wetu wangekuwa mbumbumbu basi na hapo wangepita salama kama walivyopita huko kwengine.
 
Bongo kuna ma pimbi wengi sana wanadhani Interpol ni polisi wengine toka ughaibuni, hawajui kua hio Interpol inatokana na hao hao polisi wa bongo ila jina tu. Informations zote zinatokana na polisi wa bongo, na ndio kazi walioifanya ya kuwakamata. Interpol ni jina tu, local police ndio wenye kazi yao kuna kitengo tu hapo..
"Informations zote zinatokana nan polisi wa Bongo" !? Hao Polisi Wa Bongo walijuaje kama hao jamaa ni wahalifu waliotoroka huko SA!?
 
Back
Top Bottom