Thabo Bester maarufu 'Mbakaji wa Facebook' na Dkt. Nandipha Magudumana wakamatiwa Arusha Tanzania. Wafahamu kwa undani wapenzi hawa

Mm nikiwa Rais ntahakikisha natekeleza adhabu ya kifo, kwakweli ni muhimu sana. Yaan mtu auwe watu afu afungwe tu kifungo cha maisha, anakula na kulala bure wakati aliowaua wanaoza makaburini? Kwangu hapana, ni Utanyongwa au kupigwa Risasi.
Na hiyo kunyongwa au kupigwa risasi anatakiwa achague yeye mwenyewe anayetakiwa kuuliwa.
 
Huyo aliyechomwa huko gerezani mna uhakika gani alikuwa mzima au ni mtu wa kweli? Hii habari inasema tu huyu dada alichukuwa mabaki yaliyoungua kiasi cha kutotambulikana. Hapa nimejiuliza mengi: 1. Je, walichukuwa mtu aliye hai wakamchoma? Je, waliingiza maiti kutoka sehemu nyingine wakaichoma? Je, inawekana wala siyo binadamu aliyeunguzwa?
 
Hatari sana na kuna mambo yanasikitisha sana...
 
Hao ni majasusi wa dunia.

Mbaya kuua mtu ili wewe uokoke, mbaya zaidi mbele za Mungu pia.

All in all polisi wa tz wako vizuri, naogopa kusema CONGRATULATIONS.

Angesogea hapo kwa Uhuru asingekamatwa mpaka afe kweli kweli.
Kwanini unasema wako vizuri? Hapa walipewa tip tu na wenzao wa S. Africa kuwa huyu mtu amekuja huko! Halafu inaonekana baada ya kufeki kuwa amejiunguza alijiamini sana akawa anajiachia mitaani akidhani watu wote wameamini kuwa ameshafariki hivyo siyo rahisi kuhisiwa.
 
Actally naona hiki ndicho kilichofsnyika maana ingekuwa ni mfungwa mwingine ndio kauawa na kuchomwa ili huyo mhalifu atoroke, ni wazi mamlaka za jela zingegundua kupotea kwa mfungwa mmoja humo ndani. Umewaza vyema kabisa.
 
Sijaelewa toa habari kamili
Nadhani kutakua na nyama zaidi next time watakapoletwa mahakamani, wote tunaelewa kuwa Mr.Bester hakufa pale jela kuna mtu ambaye kuna dalili kuwa aliuliwa ili ionekane aliyekufa ni Mr.Bester ,inawezekana Dr Nandipa father amehusika na mauaji ya mtu huyu, ngoja tuendelee kusoma news24.com na eNCA
 
... SA walifuta adhabu ya kunyonga adhabu pekee aliyostahili Bester! Angekatiwa hiyo adhabu na ikatekelezwa inavyopaswa bila figisu shida zote hizi za kuhangaika naye zingeshasahaulika zamani. Adhabu ya kunyonga bado ina umuhimu mkubwa duniani.
Omba kazi hiyo. Ninani ameruhusu kuua? USIUE NDIO AMRI. HAKUNA MBADALA
 
Walikubali kwavile walihongwa pesa
Actually tangu weusi washike hatamu za uongozi hapo South, kuna ujinga mwingi sana umezaliwa. Hao viongozi wenyewe wa ANC kuanzia Rais mpaka viongozi waandamizi chamani ni wala rushwa/mafisadi wakubwa kabisa. Sasa wale wa chini wataacha kuiga matendo yao!?
 
Tunasubiri
 
Criminals wana akili nyingi sana. Laiti wangezitumia kufanyia mambo mazuri. Ila good observation Mkuu.
 
Waliingia na full documents ila walidanganya details, yaan walikuja na majina tofauti kwenye Passport zao. Sio kwamba wameingia bila passport kabisa kiongozi.
Hawawezi kutumia passport watu wanaotafutwa kwa maana Nchi zote wanakua na taarifa ukipeleka Passport tuu wanakamata ndio maana wao walitumia gari mpaka Harare kwa kupita kwa kuhonga mpaka wanaingia Tanzania na kutoka...
 
Criminals wana akili nyingi sana. Laiti wangezitumia kufanyia mambo mazuri. Ila good observation Mkuu.
Huyu jamaa alitoka muda jela mwaka jana akajisahau akaanza kwenda kula bata watu wakamuona Centurion na kusema mbona pana mtu kaonekana akilipia vitu Mall moja hapo wazee walipoenda kuangalia CCTV za pale wakagundua kweli ikabidi waanze kumsaka kimya kimya ndio akaona akimbie kumbuka alitumia zaidi ya 5milion katoa kama rushwa wale waliopokea rushwa wanampa taarifa zinazoendelea maana karibu wengi wao walishaanza kuhojiwa baada ya kuchunguzwa account zao na mawasiliano ya Simu...
 
Hapo kuna tusi mkuu? Mi nimekueleza kwa uhalisia aliuemchinya mama yako au Baba yako, utapendelea afungwe kifungo cha maisha badala ya kunyongwa?
Msifunge akili zenu kisa mko upande ambao hamjafikiwa na hiyo kadhia ya kuuawa kwa mtu wako wa karibu.

Mimi mtu akimuua tu ndugu yangu, hata kabla ya mahakama kuamua nahikikisha namuua. Siwezi kulea ujinga
 
We ukisikia INTERPOL unadhani ni wazungu, waamerika, siyo? Ungejua katika nchi wanachama wa Interpol kazi za Interpol zinafanywa na askari police wa nchi husika ambao wapo kitengo cha Interpol.

Yani kiufupi, hatoki askari New Zealand, US, Urusi au UK ndo awe Interpol. Ndani ya police Tanzania kuna kitengo cha Interpol pale makao makuu ya polisi kama vilivyo vitengo vingine Traffic, FFU, GD, STPU, intelligence, CID nk. Hao INTERPOL wa police Tz ndo hufanya kazi na Interpol wengine nchi nyingine huko duniani. Arrest ya mhalifu wa kimataifa hufanywa na yeyote hapa nchini, aweza kuwa local police au hata huyo Interpol police kwa kuwa na yy ni mmoja wa local police ila yupo katika kitengo cha interpol
 
P
Polisi wa Tz walijuaje kuwa hawa jamaa ni wahalifu kama hawakupewa taarifa zao na movement zao!? Binafsi naona walichofanya ni kusaidia tu kazi ya kukamata.
 
Nimekuelewa mkuu na ninaomba hiyo kitu ISITOKEE ili nawe usiwe murderer kama Mr.Bester
 
Yaani ma wewe japo ndiyo umeelekeza? Unashindwa hata kuelewa hoja unakimbilia kuelezea vitu obvious?
Sasa hayo unayoyaelezea hapo ni nani asiyeelewa?
Muwe mnajifunza kuelewa kitu kabla ya kukimbilia kuongea ili mradi, halafu unaelezea mpaka unarudia niliyoyaelezea.
Majibu yako ungetafuta wa kumuelezea lakini siyo mimi, kwangu labda kama ungekuja ku topup
 
P

Polisi wa Tz walijuaje kuwa hawa jamaa ni wahalifu kama hawakupewa taarifa zao na movement zao!? Binafsi naona walichofanya ni kusaidia tu kazi ya kukamata.
Hivi unafikiri mambo yanayofanyika duniani polisi wetu hawayajui? Hawafuatilii taarifa habari za nje na kujua wauaji na wafungwa wanaokamatwa na kuoneshwa kwenye vyombo vya habari?

Kesi ya huyo kijana ilikuwa ya wazi na watu wengi waliifatilia. Na hata hilo tukio la jamaa kushtukiwa kwamba ile maiti hauhusiani na huyo mfungwa pia lilitangazwa na msako nchini Afrika kusini ukaanza.

Cha kushangaza baada ya jamaa kugundua kwamba ishajulikana kuwa yeye hakufa kifo cha moto aliamua kutoroka bila kukamatwa na hao wanaowatafuta, pia nchi zote walizopita hawakuweza kugundulika na kukamatwa, ila walipofika kwetu ndo walipoanza kufuatiliwa na askari wetu waliobobea katika nyanja hizo na kufanikiwa kukamatwa.

Ndio maana kuna mchangiaji alisema laiti kama wangefanikiwa kuvuka kuingia Kenya basi mpaka leo wangekuwa bado wanatafutwa na hao interpol wenu. Kwa sababu inaaminika vyema askari wa Kenya wanavyopenda rushwa bila kujali madhara yatokanayo na rushwa.

Kama askari wetu wangekuwa mbumbumbu basi na hapo wangepita salama kama walivyopita huko kwengine.
 
"Informations zote zinatokana nan polisi wa Bongo" !? Hao Polisi Wa Bongo walijuaje kama hao jamaa ni wahalifu waliotoroka huko SA!?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…