Thamani ya pesa yetu inazidi kuporomoka. Shida ni nini?

Leo dola moja ni Tsh 2350 mtandaoni. Gharama za vitu tunavyoagiza itazidi kupanda. Shida nini pesa yetu kuporomoka namna hii? Hivi kuna namna tunaweza kuachana na kuagiza vitu kwa dola?
we ulikuwa wapi siku zote hizo. Ulikuwa nje ya nchi. Dola ya marekani imekaa hapo (TShs 2350) muda mrefu sana nafikiri tangia kipindi cha Magu. Acha kukurupuka kuandika vitu usivyovijua.
 
Leo dola moja ni Tsh 2350 mtandaoni. Gharama za vitu tunavyoagiza itazidi kupanda. Shida nini pesa yetu kuporomoka namna hii? Hivi kuna namna tunaweza kuachana na kuagiza vitu kwa dola?
Huku tunaambiwa uchumi unakuwa,kwa Mwigulu tumepigwa
 
Kwani maduka ya kubadilisha fedha za kigeni yameruhusiwa tena?
 
ila story za dini zinatishia sana watu 😂😂🤣🤣
 
Mnazalisha nini na ku export? Zaidi ya raw materials wakati import mpaka mafuta ya Alizeti!
 

Hizi imani ndio mnaharibu, kwanini watu wafanye uzembe kwenye mambo ya kutumia akili zao na common sense tumsingizie Mungu? Uzembe wetu na tabia za kibinadamu usichanganywe na mambo ya imani! Tuseme nchi ambazo uchumi unakua ni watakatifu sana?


I agree to disagree, mambo ya matendo yetu turekebishe tusikimbilie imani!

Tumejaliwa akili, utashi na rasilimali vitumike vizuri kututoa hapa tulipo tusitafute blame game!
 
Huyo mungu wako ukiwa huna sadaka huendi kanisani
 
Siyo kweli
siyo kweli kitu gani, fuatilia taarifa kutoka vyanzo vya kuaminika. Leo hii tar 24.04.2023 dola ya Marekani ilinunuliwa kwa sh. 2301 na kuuzwa kwa sh 2324. Taarifa ya BOT. nenda hata kwenye tovuti yao siyo mnajidanganya vijiweni. Huyo mpotoshaji ana malengo yake maovu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…