THBUB yapokea Malalamiko ya uvunjwaji wa haki na ukiukwaji ya misingi ya utawala bora Kigoma

THBUB yapokea Malalamiko ya uvunjwaji wa haki na ukiukwaji ya misingi ya utawala bora Kigoma

Joined
Sep 17, 2024
Posts
21
Reaction score
16
IMG-20250212-WA0000.jpg
Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imepokea malalamiko ya uvunjwaji wa haki za binadamu na ukiukwaji wa misingi ya utawala bora kwa mkoa wa Kigoma.

Malalamiko hayo yamewasilishwa na wananchi wakati wa Mkutano wa hadhara wenye lengo la kutoa elimu ya haki za binadamu na misingi ya utawala bora uliofanyika katika Mtaa wa Kamala, kata ya Bangwe, Manispaa ya Kigoma Februari 10, 2025.

Akizungumza mara baada ya kupokea malalamiko hayo Kamishna wa THBUB Mhe. Amina Talib Ali amesema kuwa, kwa utaratibu, Tume inatoa siku tisini kupata mrejesho wa malalamiko yanayowasilishwa mbele yake. Hivyo, kuahidi kuyafanyia kazi malalamiko yaliyowasilishwa mbele ya Tume katika Mkutano huo na kutoa mapendekezo kwa Serikali.
Screenshot 2025-02-12 103154.jpg

Screenshot 2025-02-12 103134.jpg
Ziara ya Ujumbe wa THBUB Mkoani Kigoma ina lengo la kuitambulisha Tume, kutoa elimu ya Haki za binadamu na misingi ya utawala bora na kupokea malalamiko.

THBUB inalenga kuzifikia Wilaya za Buhigwe, Kakonko, Kibondo, Kigoma Manispaa na Wilaya ya Kigoma.
Screenshot 2025-02-12 103121.png
 
Back
Top Bottom