The Advantage of being a latecomer: Yanga tunalo la kujifunza kwa Simba

The Advantage of being a latecomer: Yanga tunalo la kujifunza kwa Simba

WakatibRoman anainunua Chelsea hakukuwa na Cole,Terry wala Super Frank mkuu.

Labda Uweke Zola, Flo na Petrescu
Screenshot_20231126-095602.jpg
Screenshot_20231126-095544.jpg
 
Miaka ya 2000 Mwanzoni, Mpira wa Uingereza—ligi fuatiliwa zaidi duniani—ulikuwa umetawaliwa na Klabu Mbili tu; ARSENAL na MANCHESTER UNITED.

Liverpool alikuwa msindikizaji, Manchester City alikuwa bado 'chandimu'. Chelsea walikuwa na timu nzuri sana—Frank Lampard, John Terry, Joe Cole, Petr Cech—lakini haikuwa chochote mbele wakubwa hao wawili. Lakini mambo yalibadilika mwaka 2003, Roman Abrahamovich alipoinunua timu hiyo. Kuingia kwa tajiri huyo wa kirusi kulifuatiwa na Kuja klabuni hapo, kutoka Man U, kwa Peter Kenyon kama Mtendaji Mkuu.

Watu hao wawili walipoingia Klabuni ulikuwa ndio mwanzo wa mafanikio ya Timu ya Chelsea hadi kuwa hivi ilivyo leo. Uwepo wa watu hawa, ukakamilisha mawili ya LAZIMA—mbali na wigo mpana wa mashabiki—ya maendeleo ya timu yoyote ile dunia; FEDHA YA KUTOSHA na UTAWALA WA KIWELEDI (FINANCIAL MUSCLES and PROFESSIONALISM IN MANAGEMENT).
View attachment 2825231

Turejee kwetu. Toka mwaka 2018, club ya Simba imekuwa na mafanikio makubwa sana ya Mpira barani africa. Leo inacheza African Football League, kama kigogo wa Kanda hii ya Africa Mashiriki kutokana na record yake ya miaka mitano nyuma. Mafanikio haya yametokana na Uwekezaji Mkubwa wa fedha uliofanywa na Mohamed Dewji ambao wote tunaufahamu. Amekuwa na CEOs bora kama Senzo na Babra Gonzalez ili tu kukamilisha Utatu Mtakatifu wa mafanikio ya timu yoyote (Mashabiki, Muwekezaji/Tajiri na Utawala). Lakini sasa Simba inashuka. NDIO SIMBA INASHUKA. AMELETWA BENCHIKHA, LAKINI BADO SIAMINI KAMA ITAFANYA LOLOTE.

Mohamed Dewji ni tatizo. Ukitazama upangaji wa makundi ya CAFCC, Utaona kuna Teams 1, 2, 3 na 4 haya ni madaraja ya ubora.

Timu kama Al Ahly, Mamelodi, Wydad Na Esperence de Tunis hawa ni Daraja 1, Teams kama Simba ni Daraja la 2, Yanga ni Daraja la 3, Medeama ni daraja la 4. Sasa hapa Simba ilipo, ni matokeo ya uwekezaji mkubwa wa kifedha wa Mohamed Dewji—Kusajili, Kuhudumia na Miundombinu ya michezo ya timu. Ili Simba, iwe ya daraja la kwanza (African level kuwa sambamba na kina Al Ahly, Mamelodi, Wydad au ES Tunis), inabidi tajiri wa Timu afungue Pochi haswa.

Mfano, kwa mujibu wa Tovuti ya Transfermarket, Mamelodi na Al Ahly vikosi vyao vina thamani ya Shilingi Bilioni 80, Wydad na ES Tunis zina Shilingi Bilioni 47. Kikosi cha Simba kina thamani ya Shilingi Bilioni 8 tu. Huku Yanga kikosi chake kina thamani ya Bilioni 4 tu. Tazama maana zaidi ya hizi namba; Simba yeye ni wa Pili kwa ubora, wa chini yake (watatu) Asec Mimosas wa Ivory Coast kikosi chake kina thamani ya Shilingi Bilioni 3 na wanne kwake ni Jwaneng Galaxy ya Botwasana ina kikosi chenye thamani ya Milioni 210.

Hivyo ukweli ni kuwa ili tufike viwango vya juu kabisa Africa, ni lazima tuwe na vikosi vyenye thamani kubwa sana. Tutaweza sajili wachezaji wenye hadhi ya juu kabisa wa ndani na nje ndipo hapo tutaweza kaa meza moja na kina Al Ahly na Mamelodi. Mohamed Dewji amewekeza kuifikisha Simba Daraja la Pili-Chini au tuseme Daraja la Tatu-Juu. Hakuna uwekezaji anaofanya sasa wa kuipeleka daraja la Kwanza. Simuoni kama Mohamed Dewji ni muwekezaji serious wa kuifikisha Simba Daraja hilo. Kwanini simuoni kama ni muwekezaji Serious, Bilioni 50 kwake ni kiasi anachokimudu, kwani utajiri wake Trilioni 3 kwa mujibu wa Forbes. Namuona kama ni mfanyabiashara aliyeridhika/aliyehitaji/anayehitaji nafasi hii tu iliyopo sasa—kwake inamlipa kibiashara ndio maana anafanya mambo ya kijanja janja ya kupumbaza mashabiki na kuzima moto ili kumantain Status quo. Ni aidha Mo abadilishe mindset na kuwaza Daraja la Kwanza au Simba itafakari muwekezaji Mpya mwenye kuweza kutupa Squad yenye thamani ya walau Bilioni 50.

2. Utawala wenye weledi.
Mwaka jana, aliyewahi kuwa mchezaji wa Super Sport United wa Africa Kusini, alihojiwa na Gazeti la The Citizen la Afrika Kusini hlompho Kekana, akielezea mafanikio ya Timu ya Mamelodi Sundowns. Maoni ya kekana ni kuwa mafanikio ya Mamelodi, sehemu kubwa yaliletwa na kuwa na Scouting Team nzuri, yenye mtandao mpana iliyoleta wachezaji wazuri na sahihi kuweza kutengeneza timu imara.


Kwenye timu yoyote ya mpira, kimsingi Mtendaji Mkuu (Chief Executive Office) huyu ndiye injini ya kuendesha timu. Kwa Simba ni mtu kama Imani Kajula, kwa Yanga ni Andrew Mitine kwa Azam ni Abdulkarim Amin au Popat. Sasa, hawa Kimsingi huongozi idara tatu—Idara ya Uendeshaji ( utawala, mapato na matumizi ya Timu mfano kutafuta wadhamini, kulipa mishahara n.k), Huduma za klabu (Ustawi wa klabu mfano Ulinzi, matibabu n.k) na Tatu ni Idara ya maendeleo ya Mpira (soka lenyewe kwa ujumla). Sasa kwenye Hizi idara kunakuwa na Vitengo mbalimbali, Mfano Kitengo cha Michezo, ambacho Kocha wa Timu huwa chini ya kitengo hiki, Pia kuna Kitengo cha Kutafuta wachezaji (Scouting Team). Sasa ili timu iwe na kikosi kizuri, rejea maneno ya Kekana hapo juu kuhusu Scouting. Na Scouting team ili ipate wachezaji wazuri wa kufit na timu lazima wawe na masikilizano na kocha, pia lazima wawe na mtandao mpana, yaani wasambae maeneo mengi duniani hivyo lazima wawezeshe kifedha (IDARA YA UENDESHAJI & TAJIRI), wawe na utaalamu na weledi na wawe na Usimamizi bora wa kiweledi (CEO COMPETENT). Ndio maana unaona Mamelodi wamefanikiwa hapo walipo—HELA ZA PATRICE MOSEPE na MANAGEMENT BORA. Ndio maana Chelsea iliamka kuanzia 2004—HELA ZA KUTOSHA ZA ROMAN ABRAHAMOVIC na MENAGEMENT BORA YA PETER KENYON. Bahati mbaya sana Management bora inategemea na Utashi na Ufanisi wa Tajiri. Hivyo, Simba inaenda kuporomoka hapa ilipo, isipoachana na Mohamed Dewji huyu wa sasa—mjanjamjanja na kuwa Mohamed Dewji Mpya—Serious Investor au kutafuta Tajiri mwingine aliye serious kuweka mzigo wa maana.

Sasa, sisi Yanga tuna bahati kubwa. Tumechelewa. Ukichelewa una faida ya kujifunza kwa aliyetangulia. Simba ametutengenezea nafasi ya 'heshima'. Sasa tujifunze kwake, anapokosea! Sina shaka na trend ya Yanga, lakini kila nikitazama. Nikirejea hulka za 'kikariakoo', nahisi nasi tutapita njia ya Simba.

Muda ni muamuzi mzuri.
Mimi nafikiri nguvu kubwa tuiweke hapo kwenye scouting. Tuwe sharp kuwaona wachezaji wazuri na kuwqsajiri kwa gharama ndogo kabla hawajaonwa na hao wakubwa lakini ukisema tumwage hela kushindana na hao wakina al ahly na mamelod hatuwezi. Kumbuka uchumi wa nchi zao ni mkubwa ukilinganisha na uchumi wetu na uchumi wa nchi unaeleza uchumi wa vilabu. Ukimuweka pembeni Mamelod sundowns kwa sasa Yanga anaweza kuzipiga klabu zote za South afrika lakini ukija kwenye msuli wa pesa kuna klabu kama orlando pirates, keizer chiefs ambazo zimemuacha yanga mbali sana kiuchumi. Tukitaka kushindana kiuchumi na hao jamaa hatuatweza tuimalishe tu vitengo vyetu vya scouting.
 
WakatibRoman anainunua Chelsea hakukuwa na Cole,Terry wala Super Frank mkuu.

Labda Uweke Zola, Flo na Petrescu
Uache ujuaji... Terry alikuwapo, Lampard alikuwapo, Cole alikuwapo ... Wote hao walikuwapo pamoja na Petit, Carlton Cole, Jimmy Floyd Hasselbaink, Crespo, Gronkjaer, Makelele, eidur gudjohsen, Adrian Mutu, Scott parker , veron wengi mnooo .... Acha kudanganya watu...
 
Mimi nafikiri nguvu kubwa tuiweke hapo kwenye scouting. Tuwe sharp kuwaona wachezaji wazuri na kuwqsajiri kwa gharama ndogo kabla hawajaonwa na hao wakubwa lakini ukisema tumwage hela kushindana na hao wakina al ahly na mamelod hatuwezi.
Nakubaliana na wewe. Lakini hii inahitaji Scouting Network kubwa na yenye weledi sana, ambavyo vyote hivi vinahitaji ADMINISTRATION NZURI YA CLUB & ADEQUATE FINANCING—Ambayo haya ni matatizo yetu makuu.
Kumbuka uchumi wa nchi zao ni mkubwa ukilinganisha na uchumi wetu na uchumi wa nchi unaeleza uchumi wa vilabu. Ukimuweka pembeni Mamelod sundowns kwa sasa Yanga anaweza kuzipiga klabu zote za South afrika lakini ukija kwenye msuli wa pesa kuna klabu kama orlando pirates, keizer chiefs ambazo zimemuacha yanga mbali sana kiuchumi. Tukitaka kushindana kiuchumi na hao jamaa hatuatweza tuimalishe tu vitengo vyetu vya scouting.
Hivi chief, ni kweli kabisa kwa football culture iliyopo Tanzania, hatuwezi pata uwekezaji wa kufikia level ya walau ¾ ya Mamelodi?
 
Natamani huu uchambuzi ufanyike pale Azam Tv na usiongezewe Wala kueditiwa chochote.
 
Miaka ya 2000 Mwanzoni, Mpira wa Uingereza—ligi fuatiliwa zaidi duniani—ulikuwa umetawaliwa na Klabu Mbili tu; ARSENAL na MANCHESTER UNITED.

Liverpool alikuwa msindikizaji, Manchester City alikuwa bado 'chandimu'. Chelsea walikuwa na timu nzuri sana—Frank Lampard, John Terry, Joe Cole, Petr Cech—lakini haikuwa chochote mbele wakubwa hao wawili. Lakini mambo yalibadilika mwaka 2003, Roman Abrahamovich alipoinunua timu hiyo. Kuingia kwa tajiri huyo wa kirusi kulifuatiwa na Kuja klabuni hapo, kutoka Man U, kwa Peter Kenyon kama Mtendaji Mkuu.

Watu hao wawili walipoingia Klabuni ulikuwa ndio mwanzo wa mafanikio ya Timu ya Chelsea hadi kuwa hivi ilivyo leo. Uwepo wa watu hawa, ukakamilisha mawili ya LAZIMA—mbali na wigo mpana wa mashabiki—ya maendeleo ya timu yoyote ile dunia; FEDHA YA KUTOSHA na UTAWALA WA KIWELEDI (FINANCIAL MUSCLES and PROFESSIONALISM IN MANAGEMENT).
View attachment 2825231

Turejee kwetu. Toka mwaka 2018, club ya Simba imekuwa na mafanikio makubwa sana ya Mpira barani africa. Leo inacheza African Football League, kama kigogo wa Kanda hii ya Africa Mashiriki kutokana na record yake ya miaka mitano nyuma. Mafanikio haya yametokana na Uwekezaji Mkubwa wa fedha uliofanywa na Mohamed Dewji ambao wote tunaufahamu. Amekuwa na CEOs bora kama Senzo na Babra Gonzalez ili tu kukamilisha Utatu Mtakatifu wa mafanikio ya timu yoyote (Mashabiki, Muwekezaji/Tajiri na Utawala). Lakini sasa Simba inashuka. NDIO SIMBA INASHUKA. AMELETWA BENCHIKHA, LAKINI BADO SIAMINI KAMA ITAFANYA LOLOTE.

Mohamed Dewji ni tatizo. Ukitazama upangaji wa makundi ya CAFCC, Utaona kuna Teams 1, 2, 3 na 4 haya ni madaraja ya ubora.

Timu kama Al Ahly, Mamelodi, Wydad Na Esperence de Tunis hawa ni Daraja 1, Teams kama Simba ni Daraja la 2, Yanga ni Daraja la 3, Medeama ni daraja la 4. Sasa hapa Simba ilipo, ni matokeo ya uwekezaji mkubwa wa kifedha wa Mohamed Dewji—Kusajili, Kuhudumia na Miundombinu ya michezo ya timu. Ili Simba, iwe ya daraja la kwanza (African level kuwa sambamba na kina Al Ahly, Mamelodi, Wydad au ES Tunis), inabidi tajiri wa Timu afungue Pochi haswa.

Mfano, kwa mujibu wa Tovuti ya Transfermarket, Mamelodi na Al Ahly vikosi vyao vina thamani ya Shilingi Bilioni 80, Wydad na ES Tunis zina Shilingi Bilioni 47. Kikosi cha Simba kina thamani ya Shilingi Bilioni 8 tu. Huku Yanga kikosi chake kina thamani ya Bilioni 4 tu. Tazama maana zaidi ya hizi namba; Simba yeye ni wa Pili kwa ubora, wa chini yake (watatu) Asec Mimosas wa Ivory Coast kikosi chake kina thamani ya Shilingi Bilioni 3 na wanne kwake ni Jwaneng Galaxy ya Botwasana ina kikosi chenye thamani ya Milioni 210.

Hivyo ukweli ni kuwa ili tufike viwango vya juu kabisa Africa, ni lazima tuwe na vikosi vyenye thamani kubwa sana. Tutaweza sajili wachezaji wenye hadhi ya juu kabisa wa ndani na nje ndipo hapo tutaweza kaa meza moja na kina Al Ahly na Mamelodi. Mohamed Dewji amewekeza kuifikisha Simba Daraja la Pili-Chini au tuseme Daraja la Tatu-Juu. Hakuna uwekezaji anaofanya sasa wa kuipeleka daraja la Kwanza. Simuoni kama Mohamed Dewji ni muwekezaji serious wa kuifikisha Simba Daraja hilo. Kwanini simuoni kama ni muwekezaji Serious, Bilioni 50 kwake ni kiasi anachokimudu, kwani utajiri wake Trilioni 3 kwa mujibu wa Forbes. Namuona kama ni mfanyabiashara aliyeridhika/aliyehitaji/anayehitaji nafasi hii tu iliyopo sasa—kwake inamlipa kibiashara ndio maana anafanya mambo ya kijanja janja ya kupumbaza mashabiki na kuzima moto ili kumantain Status quo. Ni aidha Mo abadilishe mindset na kuwaza Daraja la Kwanza au Simba itafakari muwekezaji Mpya mwenye kuweza kutupa Squad yenye thamani ya walau Bilioni 50.

2. Utawala wenye weledi.
Mwaka jana, aliyewahi kuwa mchezaji wa Super Sport United wa Africa Kusini, alihojiwa na Gazeti la The Citizen la Afrika Kusini hlompho Kekana, akielezea mafanikio ya Timu ya Mamelodi Sundowns. Maoni ya kekana ni kuwa mafanikio ya Mamelodi, sehemu kubwa yaliletwa na kuwa na Scouting Team nzuri, yenye mtandao mpana iliyoleta wachezaji wazuri na sahihi kuweza kutengeneza timu imara.


Kwenye timu yoyote ya mpira, kimsingi Mtendaji Mkuu (Chief Executive Office) huyu ndiye injini ya kuendesha timu. Kwa Simba ni mtu kama Imani Kajula, kwa Yanga ni Andrew Mitine kwa Azam ni Abdulkarim Amin au Popat. Sasa, hawa Kimsingi huongozi idara tatu—Idara ya Uendeshaji ( utawala, mapato na matumizi ya Timu mfano kutafuta wadhamini, kulipa mishahara n.k), Huduma za klabu (Ustawi wa klabu mfano Ulinzi, matibabu n.k) na Tatu ni Idara ya maendeleo ya Mpira (soka lenyewe kwa ujumla). Sasa kwenye Hizi idara kunakuwa na Vitengo mbalimbali, Mfano Kitengo cha Michezo, ambacho Kocha wa Timu huwa chini ya kitengo hiki, Pia kuna Kitengo cha Kutafuta wachezaji (Scouting Team). Sasa ili timu iwe na kikosi kizuri, rejea maneno ya Kekana hapo juu kuhusu Scouting. Na Scouting team ili ipate wachezaji wazuri wa kufit na timu lazima wawe na masikilizano na kocha, pia lazima wawe na mtandao mpana, yaani wasambae maeneo mengi duniani hivyo lazima wawezeshe kifedha (IDARA YA UENDESHAJI & TAJIRI), wawe na utaalamu na weledi na wawe na Usimamizi bora wa kiweledi (CEO COMPETENT). Ndio maana unaona Mamelodi wamefanikiwa hapo walipo—HELA ZA PATRICE MOSEPE na MANAGEMENT BORA. Ndio maana Chelsea iliamka kuanzia 2004—HELA ZA KUTOSHA ZA ROMAN ABRAHAMOVIC na MENAGEMENT BORA YA PETER KENYON. Bahati mbaya sana Management bora inategemea na Utashi na Ufanisi wa Tajiri. Hivyo, Simba inaenda kuporomoka hapa ilipo, isipoachana na Mohamed Dewji huyu wa sasa—mjanjamjanja na kuwa Mohamed Dewji Mpya—Serious Investor au kutafuta Tajiri mwingine aliye serious kuweka mzigo wa maana.

Sasa, sisi Yanga tuna bahati kubwa. Tumechelewa. Ukichelewa una faida ya kujifunza kwa aliyetangulia. Simba ametutengenezea nafasi ya 'heshima'. Sasa tujifunze kwake, anapokosea! Sina shaka na trend ya Yanga, lakini kila nikitazama. Nikirejea hulka za 'kikariakoo', nahisi nasi tutapita njia ya Simba.

Muda ni muamuzi mzuri.
Ndugu yangu ubarikiwe Umeongea Fact tupu mwenye Masikio na asikie
 
Nakubaliana na wewe. Lakini hii inahitaji Scouting Network kubwa na yenye weledi sana, ambavyo vyote hivi vinahitaji ADMINISTRATION NZURI YA CLUB & ADEQUATE FINANCING—Ambayo haya ni matatizo yetu makuu.

Hivi chief, ni kweli kabisa kwa football culture iliyopo Tanzania, hatuwezi pata uwekezaji wa kufikia level ya walau ¾ ya Mamelodi?
kutengeneza scoting nzuri tunaweza kumudu mfano usajiri wa Mayele tuliweza kumuona kabla ya wakubwa lakini kwenye kushindana nao kumchukua mchezaji hatutaweza watatuzidi tu kwenye dau kuhusu wawekezaji wa level za mamelod bado hatujafika uko mkuu. Uchumi wa nchi tia maji tia maji kwaiyo tuna kundi kubwa la wananchi masikini wenye hali za kawaida ni wale wanaoweza kupata mahitaji muhimu tu mfano mimi jezi ya mwisho ya yanga kununua ni ya msimu juzi sio kwamba sipendi kununua jezi ya kila msimu lakini uchumi wangu unanikwamisha kufanya ivyo, tukija kwa hao wawekezaji kumbuka lazima waangalie na faida yao pia. Sasa mashabiki hawalipi kadi za uanachama, hawanunui jezi origino, kujaza uwanja ndio mpaka wakutane simba na yanga. Hao wakina mamelod na al ahly uchumi wa nchi zao ni mkubwa kwaiyo automaticaly hata expending power ya mashabiki ni kubwa.
 
Mnaweza mkanishukia kama mwewe ila mimi siamini sana thamani ya fedha kwenye kikosa ndio ubora wa timu. Ubora wa timu inachangiwa na vitu vyingi sana hasa uongozi na wale wanaohusika na usajili. Pyramid kikosi chao ghali sana lakini hamna lolote alkadhalika PSG na Man U.
Sawa lakini uhalisia unabaki kwamba Katika Ligi alilopo Man utd,.... Man city ndo hubeba kombe sambamba na Liverpool ambao wote hao wana misuli ya kiuchumi na Vikosi ghali sana,

Kwa upande wa Psg wao uwekezaji wao umezaa matunda kidogo maan kwenye ligi lao yeye ndo mwenye makombe mengi na pia Hata Uefa hayuko mbali sana maan alifika fainali ya Uefa japokuwa akafungwa ila kimalengo yupo karibu sana kufanikisha lengo la kuwa bingwa ulaya,

Ukitaka kuamini hilo Angalia katka mitandao mbalimbali ya Football Prediction & statistics utaona katka Timu 8 zinazopewa Uwezekano wa Kubeba Uefa basi Psg ipo kwenye List,

Ila Tukija upande wa Caf hata katka Timu nne zinazopewa uwezekano wa kubeba Caf champions League Simba wala Yanga Haipo.

Tukirejea Uefa jarbu kuangalia washindi wa Uefa kuanzia miaka ya 2009 mpak leo ? Utagundua washindi wote ni vilabu vyenye Squad ya gharama sana... Na ukitak kuamin hilo angalia Atletico alifungwa mara mbili Fainali na Madrid....ni kutokana na Squad quality tu na si vinginevyo.

Mpira kuanzia miaka ya 2005 kupanda juu umebadilika sana ni mwenye kikosi ghali na Team management nzuri ndo hupata Mafanikio tofaut na hapo Ni Kwenda kuzuga tu kwenye mashindano.
 
kutengeneza scoting nzuri tunaweza kumudu mfano usajiri wa Mayele tuliweza kumuona kabla ya wakubwa lakini kwenye kushindana nao kumchukua mchezaji hatutaweza watatuzidi tu
Sasa hapa hatuwezi endelea.
Kama tunakuwa tunasajiri wachezaji wenye viwango kisha hatuwezi wamantain tunaingia gharama kubwa zaidi tukimuuza kuliko kummantain—Kwanza tunasajiri mchezaji hatuna guarantee ya mchezaji kuperfom mf Konkon, pili inahitaji muda kuingia kwenye mfumo wa Timu— fikiria Gharama za Konkon kumsajiri, kumvunjia mkataba na tatu tunasajiri mwingine AMA Kuongeza kile alichokuwa anakitaka mayele kama ongezeko la malipo yake ipi ni maamuzi ya busara zaidi? Hii ndio ninaita Ukariakoo uliopo kwenye uongozi wa Simba na Yanga—KARIAKOISM.
 
Kuhusu wawekezaji wa level za mamelod bado hatujafika uko mkuu. Uchumi wa nchi tia maji tia maji kwaiyo tuna kundi kubwa la wananchi masikini wenye hali za kawaida ni wale wanaoweza kupata mahitaji muhimu tu mfano mimi jezi ya mwisho ya yanga kununua ni ya msimu juzi sio kwamba sipendi kununua jezi ya kila msimu lakini uchumi wangu unanikwamisha kufanya ivyo, tukija kwa hao wawekezaji kumbuka lazima waangalie na faida yao pia. Sasa mashabiki hawalipi kadi za uanachama, hawanunui jezi origino, kujaza uwanja ndio mpaka wakutane simba na yanga. Hao wakina mamelod na al ahly uchumi wa nchi zao ni mkubwa kwaiyo automaticaly hata expending power ya mashabiki ni kubwa.
Kwanza ni dunia nzima, washabiki ni wengi kuliko wanachama.

Nchini kwetu Wanachama ni wachache kwa sababu hizi:
1. Hakuna uwajibikaji vilabuni.
Hakuna mtu anayeweza lipa hela yake bila kujua inaenda fanyia nini na aone kweli kitu hicho kimefanyika. Bila kuwa na uwajibikaji mzuri, bado mashabiki watakuwepo ila si wanachama hai.

2. Hakuna Engagement kubwa ya Wanachama na Timu zao. (Huku matawini).

3. Shabiki hatuoni faida ya kuwa na kadi.
Mfano, Timu zikiweka utaratibu kuwa ukinunua tiketi au jezi kwa Kadi unapata punguzo fulani, unadhani shabiki ataacha kuwa na hiyo kadi?

Kitu kingine bado vilabu vijafanya vya kutosha, kugeuza huu Usimba na Uyanga kuwa hela. Mfano, Hivi unajua Simba au Yanga wakiingia mkataba tu na Dume Condoms na wakatengeneza Condoms zenye pakiti yenye usimba na Uyanga, ni revenue kubwa kwa Club?

Ni kweli wengi hatuwezi nunua jezi ya sh elfu 50. Lakini hatushindwi nunua Jambo Juice/Sayona ya sh 500 ikiwa na usimba au Uyanga ndani yake.

Ushawahi waza kuwa unaweza shawishi waajiriwa, kila mwisho wa mwezi wakuchangie hata Buku tu kwenye mishahara yao? Kwa hiari kwa kutengeneza automated systems ambazo vilabu vinapokea moja kwa moja kama vile NHIF wanavyoipokea?

Bado naamini katika 'ujero jero' wetu huu, bado vilabu vinaweza tengeneza mabilioni ya Shilingi na kuwa na financial power kubwa.

Shida iko wapi, Simba/Yanga ikaajiri Consultant, si lazima atoke nje, hata Chuo Kikuu chochote hapa hapa Bongo chenye uwezo, wakafanya tafiti namna gani ya kutumia Fan base yetu kuongeza mapato ya Timu.
 
Sasa hapa hatuwezi endelea.
Kama tunakuwa tunasajiri wachezaji wenye viwango kisha hatuwezi wamantain tunaingia gharama kubwa zaidi tukimuuza kuliko kummantain—Kwanza tunasajiri mchezaji hatuna guarantee ya mchezaji kuperfom mf Konkon, pili inahitaji muda kuingia kwenye mfumo wa Timu— fikiria Gharama za Konkon kumsajiri, kumvunjia mkataba na tatu tunasajiri mwingine AMA Kuongeza kile alichokuwa anakitaka mayele kama ongezeko la malipo yake ipi ni maamuzi ya busara zaidi? Hii ndio ninaita Ukariakoo uliopo kwenye uongozi wa Simba na Yanga—KARIAKOISM.
Ndio gharama za kuwa masikini izo mkuu. Hauwezi kuafford kuwa na kitu kizuri ambacho mwenye pesa anakitaka. Hata yanga hakupenda kumuuza Mayele ndio ivyo mchezaji anataka kwenda kwenye malisho mema
 
Kwanza ni dunia nzima, washabiki ni wengi kuliko wanachama.

Nchini kwetu Wanachama ni wachache kwa sababu hizi:
1. Hakuna uwajibikaji vilabuni.
Hakuna mtu anayeweza lipa hela yake bila kujua inaenda fanyia nini na aone kweli kitu hicho kimefanyika. Bila kuwa na uwajibikaji mzuri, bado mashabiki watakuwepo ila si wanachama hai.

2. Hakuna Engagement kubwa ya Wanachama na Timu zao. (Huku matawini).

3. Shabiki hatuoni faida ya kuwa na kadi.
Mfano, Timu zikiweka utaratibu kuwa ukinunua tiketi au jezi kwa Kadi unapata punguzo fulani, unadhani shabiki ataacha kuwa na hiyo kadi?

Kitu kingine bado vilabu vijafanya vya kutosha, kugeuza huu Usimba na Uyanga kuwa hela. Mfano, Hivi unajua Simba au Yanga wakiingia mkataba tu na Dume Condoms na wakatengeneza Condoms zenye pakiti yenye usimba na Uyanga, ni revenue kubwa kwa Club?

Ni kweli wengi hatuwezi nunua jezi ya sh elfu 50. Lakini hatushindwi nunua Jambo Juice/Sayona ya sh 500 ikiwa na usimba au Uyanga ndani yake.

Ushawahi waza kuwa unaweza shawishi waajiriwa, kila mwisho wa mwezi wakuchangie hata Buku tu kwenye mishahara yao? Kwa hiari kwa kutengeneza automated systems ambazo vilabu vinapokea moja kwa moja kama vile NHIF wanavyoipokea?

Bado naamini katika 'ujero jero' wetu huu, bado vilabu vinaweza tengeneza mabilioni ya Shilingi na kuwa na financial power kubwa.

Shida iko wapi, Simba/Yanga ikaajiri Consultant, si lazima atoke nje, hata Chuo Kikuu chochote hapa hapa Bongo chenye uwezo, wakafanya tafiti namna gani ya kutumia Fan base yetu kuongeza mapato ya Timu.
Ni kweli mkuu uwajibakaji na uwazi ni mdogo sana kwenye masuala ya hela lakini naamini ni mwanzo tutazidi kupiga hatua ila kumshawishi mtanzania atoe hela ni rahisi kwa kuongea lakini kwa vitendo ni ngumu sana.
 
Ndio gharama za kuwa masikini izo mkuu. Hauwezi kuafford kuwa na kitu kizuri ambacho mwenye pesa anakitaka. Hata yanga hakupenda kumuuza Mayele ndio ivyo mchezaji anataka kwenda kwenye malisho mema
Chief, mimi naamini Yanga haikushindwa mlipa hiyo M47—inayosemwa—hatukuwa na final say na huyu mchezaji. Haiingii akilini ushindwe mlipa nyongeza ya M300 kwa Mwaka halafu unaanza hangaika sajili tena.
 
Back
Top Bottom