The Bold Interview: Maisha, Intelijensia na mengi usiyoyajua

The Bold Interview: Maisha, Intelijensia na mengi usiyoyajua

Status
Not open for further replies.
Karibuni members wote wa Jf kwenye haya mahojiano ya moja kwa moja, Yaani ni Mubashara kabisaaaa ambayo yataendeshwa na kusimamiwa na mimi STUNTER !
-
Na kwa siku ya leo tutakuwa na Mbobezi wa masuala ya Intelijensia ambaye si mwingine ni Mr. The bold !!

Hii ni ile siku iliyokuwa inasubiriwa na wengi
hivyo
naomba kwa pamoja tutege masikio yetu na macho yetu na USIKUCOMMENT CHOCHOTE,
mpaka pale nitakapotoa ruhusa ya kuuliza maswali ya pamoja.
-
N.B
Hautakiwi kucoment chochote, na kama una swali basi subiri mpaka utakaporuhusiwa kuuliza
(maswali yote yatakayoulizwa nje ya utaratibu hayatojibiwa hatakama swali lako ni zuri kama MAKINIKIA).
popcorn please..!!!..
 
Eish eish This is so DEEP - it came too late

Kwanza nikupongeze mkuu sana The bold. Si kwasababu unajua sana kututeka akili ktk makala zako, hapana!! Bali nikupongeze katika kupambana kwako kutengeneza jina Person branding. That's the most difficult thing I may say - kwa sababu through the process unapata maadui wengi sana, sana, sana,for no any tangible reason. Naamini Bold umepata haters wengi - just because u can write and rewrite. So swali langu la kwanza ni 1. How do you deal with haters (usinambie unanyamazaga hahaa)

Mimi nilikua siandiki sana hapa JF - apparently nilikua naichikulia JF so second rated. Sikua nawaza kama nitakua napost post vitu, hata sikua nawaza kama JF itaeza kua inanichukulia muda... But kwasasa nahisi JF napita kuliko medias zingine zile when I am free. Na JF naipa tu heshima yake unconditionally kuweza kusimama hadi leo, coz najua wanatafutwa sana na watawala. Lkn JF hii hii ambayo mimi naikubali ilikuaje, kivipi ikakumistreat wewe bold. Kuna kipindi uliingia mzozo ukachezea ban za hapa na pale. Like The Bold alifanya nini hata apate kupishana na uingozi wa JF?!

Bold kuna siku nilikua naongea na Nifah whatsapp (sijui kama alikwambia). And actually kitu ambacho nilikua namwambia ni kua nataka kuandika uzi kuhusu huyu The Bold. Ni vile ubusy hata sasa sijaandika huo uzi. Presumably huo uzi nilitaka nigusie The business part ya kipaji ukichonacho... what I see and what I think. Mi naona unatembea na utajiri mkubwa sana juu ya kichwa chako... swali la 3 na la mwisho - as for now until now umeshawahi kufikiria kuturn kipaji chako kua a money printing machine... unaona kina messi na Ronaldo, they were just ordinary local players wakiwa na pesa miguuni mwao - leo wapo kwenye clubs kubwa wanaprint tu pesa watakavyo... vipi kuhusu hilo/wewe??

Kuna post nimeziruka, kama ulishajibu huko nyuma u may as well ignore my qns. Nitapitia uzi pole pole.

Zaidi ya yote nikupongeze sana mkuu the bold kwa kujua kututeka, maana si kwa sumu hizi unazotulisha, japo sijasoma threads hizi mpya mpya - lkn naamini mpk huu mwezi uishe ntakua nimepitia post zote. Hongera sana Sheikh Khabib!!


Chief,

Asante sana kwa compliments na pongezi za dhati...

1. Dealing with haters

Hili suala mwanzoni lilinipa shida sana... Kama ukisoma nyuzi zangu za mwaka Jana mwanzoni na mwaka juzi kuna muda mpaka nilitaka niache kuandika kabisa... Baadae nikaona nianze kuwastudy hawa haters... Kwa nini wanakuwa negative kiasi hiki?

Yani mimi humu huwa situkani, sibishani na mtu, sigombani, simuandami mtu, simchukii mtu... Najitahidi kadiri nijavyoweza kumuheshimu kila mmoja... But still kuna watu wanachuki...

Nikajisumbua kuanza kuwajua kwa undani... Kwanza kabisa nikajua tatizo lao ni WIVU ambao unatokana na Insecurities walizonazo...

Unajua kuna watu hawako satisfied na maisha yao, sasa wakikuona wewe unapeta tu wakati wao wako wamesimama pale pale kila uchwao, wanatengeneza chuki juu yako...

Mwanzoni nikawa nawaignore... Nikahisi labda watajirekebisha... Lakini hola! Nikaona bado wanaendelea... Watu wenyewe wako watano tu ndio vinara wa kampeni ya kumuandama The Bold... Tena mmoja ni binti anatumia IDs mbili

Nikasema 'no sweti'! Nikaanza kuwakimbiza kimya kimya... Unajua ile kama mwizi amekuibia usiku alafu umuitii mwizi, unamkimbiza tu kimya kimya ili ukimpata umfanye kitu ambacho hatothubutu kwenda kusimulia...

Nimewakimbiza kimya kimya for sometime... Plotting, planning... Nia yangu ni kuwaexpose rangi zao halisi zilivyo... Unajua kama watu wanaweza kuwa wapuuzi ndani ya JF that means hata mtaani wako hivyo ... Lazima wana makando kando

Hatimaye mwanzoni mwa wiki iliyopita nimewadungua wawili... Rangi zao halisi zimejulikana... Matapeli... Wamekazania kumuandama The Bold kumbe ni matapeli wakubwa humu... Niliombwa huko PM nitoe ushahidi nikamwaga ushahidi wa kutosha tu...

Mmoja amepewa ban (nadhani ni life ban) na mwingine amesema hataki tena kuwa mchangiaji humu...

Kwa nini nimefanya hivi??? Kuna haters una wapuuza... Lakini kuna wengine ukiwaona wamejipa mission kabisa ya kukuandama inabidi uwashughulikie kwa staili ile ile ya kihuni ambayo wanakufanyia wewe...

Sasa wamebaki wawili... Kuna huyo binti na mwenzake!! Alafu huyu binti ni mama ana watoto kabisa masikini ya Mungu, yeye hajui ila namjua mpaka anapokaa yani... Ana changamoto lukuki mwenye maisha yake halisi lakini yuko JF anashinda kumuandama The Bold ambaye hajawahi kumkosea chochote... Nawalia timing tu! Anytime nadeal nao

Bwamdogo Young dee kwenye wimbo wake # BongoBahatiMbaya kuna mstari anasema... "...ukiniona kama tozi, niguse nije na kikosi..."


2. MGOGORO NA JF

Yeah kuna kipindi nilichezea ban sana aisee mwezi ule April nadhani...

Ifike muda wajiamini na watuheshimu sisi member wao. Na watuache tufanye harakati zetu tukitaka kupiga hatua za kupeleka mbali vipaji vyetu...


KUHUSU KUWA KIBIASHARA

Yeah... Nifah aliniambia kuhusu hiyo convo yenu kama one month ago!

Unajua mkuu ili mtu mwenye kipaji unufaike na kipaji chake unapaswa uambatane na mtu mwenye jicho la kibiashara... Mwenye jicho la kutengeneza pesa! Mara nyingi wenye vipaji tunanyimwa jicho la biashara...

Ndio maana Ronaldo yuko na Jorge Mendez
Diamond yuko na Sallam SK
Etc

Jibu langu ni fupi tu mkuu...

Kwa heshima na taadhima, Mr. ONTARIO, najua you are a business tycoon... Be my 'Jorge Mendez'! Najua una akili ya biashara zaidi yangu... Tukiunganisha hiki kipaji changu na huo unguli wako wa biashara... Tunafanya mapinduzi Tanzania.

So, seriously! Mbele ya wanaJF wote nikuombe... Lets take this to another level...

Mwisho kabisa nikushukuru kwa ukarimu wako na ushirikiano wako na kuwa karibu na rafiki wa dhati kwetu familia ya The Bolds...

Salute chief!
 
Mkuu The Bold Kwa mujibu wa maelezo yako na flow nzima ya Elimu yako inaonesha kidato cha Sita umemaliza 2010...Kwa kumbukumbu zangu Darasa la PCB 2010 Tambaza sikumbuki kuwapo kwa jina Khabib
Unalizungumzia hili vp?
Ulikiwa PCB1 OR PCB2??

Kule PCB1 Unamjua Amney?? Yule binti wa Kiarabu??

Memory unamjua??

Evelyn unamjua?

Ester? Josephine? Au nikutajie darasa zima?

Ticha Mjuni wa Physics??

Unawajua hao??
 
nyieni dini mbili tofauti mliwezaje kumudu na kufikia hatua ya uchumba kuputia huu mlango wa dini zenu kua tofauti? wazazi wenu walilipokeaje na mlifanyaje had leo mmekua strong
 
1. Nimanza darasa la kwanza shule ya Msingi Kizuiani (Mbagala)... Nilipofika darasa la tatu Nilienda kusoma Lindi, Shule ya Msingu Stadium... Hapo nimesoma mpaka la tano nikaenda kusoma Shule ya Msingi Mzumbe, Morogoro.


O'Level Nimesoma Kibaha Boys Sec School...

Advance nimesoma Tambaza High School - PCB


Chuo nimesoma Mzumbe University, Uchumi

Nakuja kujibu swali la pili...
Shule ya Msingi Mzumbe IPO Mzumbe Campus.
1: Wazazi/walezi wako walifanya KAZI Mzumbe? Chuo au secondary?
2: Je,wakati unasoma degree, uliwahi kuwatumia watoto wa changarawe kukufanyia usafi? Chewa tribe ni kutoka nchi gani? (Zambia or Malawi?)
3: Mwisho, Maandalizi ya harusi/ndoa yakikaribia panapomajaaliwa tushirikishe wadau japo michango ya kufanikisha shughuli.
NB: Haniffa hongera kupata mchumba Kichwa. Mungu awajaalie mpate uzao bora
 
Ila STUNTER kwa interviews zako nilizowahi kufuatilia sijui kama utakuwa na nondo za kumpiga huyu zote atazipangua...,ngoja nifuatilie
yaaani...mualikwa anaehulizwa ndio anatawala jukwaa la mahojiano kuliko mwenye jukwaa la kuhoji...
yaani mgeni kafika na kuanza kugawa mboga mwenyeji yupo yupo tuuu..!!..
intelligence kama huyo si wa maswali mepesi kama hayo..!! .
 
Siwezi kusema kuna mbinu fulani kwa sababu uandishi ni kipaji kama ilivyo Mpira, kuimba, acting etc

Jambo la msingi unatakiwa uwe na passion... Andika kwa sababu unawiwa moyoni mwako kufanya hivyo... Yaani unajiona alive ukiwa unaandika... Usiandike ili upate hela au fame... Huwa nasemaga kuwa ukifanya kitu sahihi fame na hela zitakufuata tu... So usifukizie hela au fame... Focus on you writting and be passionate about it... Its will take time mpaka watu wakuelewe...


Mfano mimi Riwaya yangu ya kwanza kuandika ilikuwa ni 2006 niko kidato cha tatu inaitwa "Don't Make Her Cry"... Nilikuwa naandika nina fans watatu tu ndio wanajua naandika na ndio wanafutilia... Alikuwa binamu yangu anaitwa Aziza na marafiki zangu wawili...

Imagine tangu 2006 leo ndio watu wanaelewa The Talent I have....

Ndio maana nasema lazima uwe passionate about it!


Pili... Hardwork! Kipaji pekee hakitoshi... You also need to be a hard worker... Unapoandika zaidi ndio unakuwa bora zaidi...

Our brain is like a muscle! The more you exercise it, the stronger it gets...

Mwisho... Kuwa na subira! Usikate tamaa... Siku moja nguvu zote hizo unazowekeza sasa zitazaa matunda
jitihada mara nyingine hushinda kipaji...
hardwork ni muhimu sana...kuboresha kipaji....
 
Asante Stunter kutuletea chief the bold. At least tumemfahamu. Mr Khatibu.
 
NMEUNGANISHA DOTS KWA MAJIBU YOTE ULIYOTOA NAACHAJE KUAMINI SASA
90% NI TISS AU MPELELEZI YAAN UPO IDARA NYETI ZA USALAMA SERIKALINI NDO NAAMINI HIVO TUSUBIRI TU KUSHUHUDIA UKITEULIWA NA MTUKUFU
 
Thanks for that deep reply boss... Ni reply ndefu hivyo nimeamua kuiedit ili nisiwachoshe watumia smartphone.

Boss mimi nina personal business mentor wangu, ni mSA lkn mara nyingi yupo England coz he owns global businesses. Anaitwa Vusi Thembekwayo (unaweza mcheki YouTube, IG, Google), na hivi majuzi mwezi April aliuza large stake of his company shares for $30 mil... hii ni karibia Bil 68 Tsh. He's such a role model and a teacher. Siku nilikua na conversation nae Nyumbani kwake Centurion - Kati ya Jozi na Pretoria. Conversion ilikua kama hivi:-

Ontario: Vusi naomba unambia mtu anahitaji nini ili awe na mafanikio kama wewe ulivyofanikiwa

Vusi: Akanyoosha kidole (kama mtu akiwa anajibu swali darasani)

Ontario: kwanza nikashangaa sana... (Huyu jamaa vipi mbona hasomeki). Nikamuuliza kidole kimefanyaje?!

Vusi: ili ufanikiwa unahitaji kitu ki1, yani kimoja tu... then stick into it hadi mwisho. Akatolea mfn hizi poster stamp... kwamba zikibandikwa kwenye bahasha, zinastick into it muda wote jadi zinafika zinapoenda - hata kama ni kibiti ama mexico.

Ontario: nikamuuliza tena - what's that one thing??

Ndipo Vusi aliponambia - hilo ndio swali gumu zaidi... that 1 thing ni mtu kama mtu inabidi atambue hiko kitu then astick nacho.

Mimi chuo nilisoma 1 of the best courses, nasema best kwasababu ni best kweli kweli. Kama ningeajiriwa I'd be making hata mshahara wa madaktari kadhaa kwa mwezi. But niligundua that 1 thing kwangu ni Ujasiriamali na Biashara. Na nimedevelop into a person that whatever that crosses in front of my eyes naeza kuona fursa. Na naweza kudetect kua hii fursa ni pesa ndefu ama hii fursa ni ya kawaida ama fursa isiyokua na pesa kbs.

Boss kuna makala zako nilizisoma, kwanza ni ile ya DB Cooper, then ile ya Geromino Ekia kisha ya Escober... Nikaona kabisa hapa kuna mgodi unatembea, nikaona kbs kua hii ni pesa. Nothing else!!

Mimi mwaka jana Nov nilikutana na Chi Achebe Eastern Cape, Capetown. Chi Achebe ni mjukuu wa African Writer mashuhuri kabisa Chinua Achebe. Huyu dame kwakweli anajua sana biashara, yeye ni global business development expert and consultant. 1 kati ya vitu aliwahi kuniambia ni hii journalism opportunity untapped in Africa.

Pia mwaka huu mwanzoni katika annual conference ya global real leaders ambayo ilihitimishwa na TEDx talk nilikutana na mwanadada makini sana na my best writer of all times Chimamanda Ngozi Adichie aliyeandika vitabu kama we should all be feminists -kitabu ambacho kimefanywa learning syllabus nchini Australia pia ana vitabu kama Americana, half and a yellow moon, that thing around ut neck nk nk... nilizungumza nae vitu vingi sana nikapata kufahamu kuhusu the business part ya hii industry ya uandishi. Sasa hivi Chimamanda ni multimillionaire, tena kapewa honorary doctorate kutoka chuo fulani US. Na hata vitu anavyoandika ni vitu ambavyo ni very obvious, ni vile anajua tu kucheza na hisia ya msomani.

Let's keep in touch. Huu mwezi hyu nitakua busy mno, yani zaidi ya ubizy wa kawaida. Once am good, we will have a coffee talk.
 
The Bold
Hao waliokuandama sana mi nawafahamu wa2 ila jamaa kumbe umewafanyizia duh ....ila demu unayemsema anatumia ID mbili nae km namjua huwa anaandamana kukudiss na Mr Tapeli wake

Ila nimejifunza kitu waru wengi JF wapo kimaigizo maigizo....Binafsi Nifah ananijua kidogo ila siyo kwa sura(labda pia ananijua)
Kweli Usimchezee mtu usiyemjua.....utaumia
[emoji2] [emoji2] [emoji2]
 
Ulizeni bas maswali ili The bold ajibu.
Maana wengine hatun vipaji vya kuiliza maswali. So inabidi tusubiri maswali na majibu
 
Thanks for that deep reply boss... Ni reply ndefu hivyo nimeamua kuiedit ili nisiwachoshe watumia smartphone.

Boss mimi nina personal business mentor wangu, ni mSA lkn mara nyingi yupo England coz he owns global businesses. Anaitwa Vusi Thembekwayo (unaweza mcheki YouTube, IG, Google), na hivi majuzi mwezi April aliuza large stake of his company shares for $30 mil... hii ni karibia Bil 68 Tsh. He's such a role model and a teacher. Siku nilikua na conversation nae Nyumbani kwake Centurion - Kati ya Jozi na Pretoria. Conversion ilikua kama hivi:-

Ontario: Vusi naomba unambia mtu anahitaji nini ili awe na mafanikio kama wewe ulivyofanikiwa

Vusi: Akanyoosha kidole (kama mtu akiwa anajibu swali darasani)

Ontario: kwanza nikashangaa sana... (Huyu jamaa vipi mbona hasomeki). Nikamuuliza kidole kimefanyaje?!

Vusi: ili ufanikiwa unahitaji kitu ki1, yani kimoja tu... then stick into it hadi mwisho. Akatolea mfn hizi poster stamp... kwamba zikibandikwa kwenye bahasha, zinastick into it muda wote jadi zinafika zinapoenda - hata kama ni kibiti ama mexico.

Ontario: nikamuuliza tena - what's that one thing??

Ndipo Vusi aliponambia - hilo ndio swali gumu zaidi... that 1 thing ni mtu kama mtu inabidi atambue hiko kitu then astick nacho.

Mimi chuo nilisoma 1 of the best courses, nasema best kwasababu ni best kweli kweli. Kama ningeajiriwa I'd be making hata mshahara wa madaktari kadhaa kwa mwezi. But niligundua that 1 thing kwangu ni Ujasiriamali na Biashara. Na nimedevelop into a person that whatever that crosses in front of my eyes naeza kuona fursa. Na naweza kudetect kua hii fursa ni pesa ndefu ama hii fursa ni ya kawaida ama fursa isiyokua na pesa kbs.

Boss kuna makala zako nilizisoma, kwanza ni ile ya DB Cooper, then ile ya Geromino Ekia kisha ya Escober... Nikaona kabisa hapa kuna mgodi unatembea, nikaona kbs kua hii ni pesa. Nothing else!!

Mimi mwaka jana Nov nilikutana na Chi Achebe Eastern Cape, Capetown. Chi Achebe ni mjukuu wa African Writer mashuhuri kabisa Chinua Achebe. Huyu dame kwakweli anajua sana biashara, yeye ni global business development expert and consultant. 1 kati ya vitu aliwahi kuniambia ni hii journalism opportunity untapped in Africa.

Pia mwaka huu mwanzoni katika annual conference ya global real leaders ambayo ilihitimishwa na TEDx talk nilikutana na mwanadada makini sana na my best writer of all times Chimamanda Ngozi Adichie aliyeandika vitabu kama we should all be feminists -kitabu ambacho kimefanywa learning syllabus nchini Australia pia ana vitabu kama Americana, half and a yellow moon, that thing around ut neck nk nk... nilizungumza nae vitu vingi sana nikapata kufahamu kuhusu the business part ya hii industry ya uandishi. Sasa hivi Chimamanda ni multimillionaire, tena kapewa honorary doctorate kutoka chuo fulani US. Na hata vitu anavyoandika ni vitu ambavyo ni very obvious, ni vile anajua tu kucheza na hisia ya msomani.

Let's keep in touch. Huu mwezi hyu nitakua busy mno, yani zaidi ya ubizy wa kawaida. Once am good, we will have a coffee talk.
Interview inayofata ni yako mkuu
 
Yes and No...

Yes kwa kuwa nimeanza kulitumikia Taifa tangu niko chuo... So kwa namba fulani labda nilipata hiyo deal kwa sababu ya Elimu...

No kwa sababu nilichokisoma sikitumii sana katika utumishi wangu...

But again Yes kwa kuwa nilichosoma kinanisaidia kuwa na good reasoning na kuelewa mambo kwa mapana.
Hili jibu limenifungua mlango mmoja wapo wa kukufahamu wewe ni wa aina gani...??
kipepeo mweusi...
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom