The Buzwagi Saga: Karamagi aenda kusaini Mkataba wa ULAJI London

The Buzwagi Saga: Karamagi aenda kusaini Mkataba wa ULAJI London

"DUA"hakuna sheria kama hiyo kaka,hata usome mpaka asbh..........................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................
 
sitoshangaa kama mheshimiwa zitto akifanyiwa majungu asishinde uchaguzi 2010 ! suala je haki ipo wapi ? maskini wee, hivi kwa nini watu wenye uchungu na nchi yao siku zooote hupingwa vikali mno ?
 
yaaaani what the f*****KKKK !@ nimesoma kumbe jamaa kasimamishwa hadi 2008 ! what the..................mhm, aiseeeeeee, that needs to go to the records people.
 
kutukana na hoja ambazo zitto alizo wasilisha nimegundua kitu kimoja ambacho ni mtego kwa serikali,kama wangekubali kuundwa kwa tume basi mikataba yote ingekuwa adharani kitu ambacho wanakipinga kwa nguvu zote.kwani hawawezi kujadili hizo hoja bila kuwepo kwa hiyo mikataba.hapo ndipo palipo na utata ktk sakata lote hili.
 
Wewe uko nchi gani? Zitto amesema hagombei tena 2010. Siasa sio lelemama.

najua alisema hivyo, lakini yeye kama mwanasiasa lazima aonyeshe umahiri wake na sio kuvunja tamaa mapema, nadhani kama situation itakuwa life threatening, basi namuunga mkono kwamba asigombee !
 
Hii article ni tofauti na "hoja ya Zitto yatupwa na ageuziwa kibao" kwa maoni yangu inastahili kuwa independent. Tunajadili hoja muhimu kuhusu hatma ya nchi yetu. Hivyo article muhimu kama hii inabidi ziwe independent ili wachangiaji wapate nafasi ya kuiona na kuichangia. Natanguliza Shukrani.

Wananchi wamlilia Kabwe, wadai haki haikutendeka
*Wakosoa jibu la Waziri kuondoa shutuma
*Wanasiasa wasema Zitto ameibuka shujaa
*Mwenyewe asema hatakubali, atakata rufaa


Na Waandishi Wetu

SIKU moja tu baada ya kukabiliwa na adhabu ya kusimamishwa kuhuduria vikao vya Bunge kwa takribani miezi mitano, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (Chadema) amejizolea umaarufu mkubwa na baadhi ya wasomi, wanasiasa na wananchi wa kawaifa wamemchukulia kama shujaa kutokana na msimamo wake.

Wakizungumza na Mwananchi kwa nyakati tofauti wananchi mbalimbali, mmoja mmoja, taasisi na vyama vya siasa, wameelezea kutoridhishwa na hatua iliyochukuliwa dhidi ya mbunge huyo na kusema hatua hiyo haikuwa ya haki na inakandamiza uhuru na demokrasia Tanzania.

Profesa Mwesiga Baregu, mhadhiri mwandamizi wa masuala ya siasa na ushirikiano wa kimataifa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, alisema uamuzi wa Bunge kumsimamisha Kabwe kuhudhuria mikutano miwili ya Bunge haujamtendea haki.

Akizungumza na Mwananchi, ofisini kwake jana, Profesa Baregu alisema kwa kitendo hicho, Bunge halikumtendea haki Kabwe, halikutenda haki kwa demokrasia na pia halikutenda haki kwa wananchi.

Alisema kumwadhibu mbunge huyo hakujaweza kuondoa ukweli kwamba kuna mikataba mibovu inayoingiwa na serikali na suala la Buzwagi ni mfano tu kati ya mikataba mingi mibovu iliyoingiwa, hasa ya madini.

Wabunge wengi wanaonyesha kuwa hawana utashi wa kulinda maslahi ya wananchi na ndiyo maana wakakataa kuunda kamati kujadili suala lile muhimu,? alisema Profesa Baregu.

Alisema kuzimwa kwa jambo lile bungeni si dawa na wala kumuadhibu Kabwe kwa kuonyesha uzalendo wake hakusaidii kuliziba tatizo bali kilichofanyika ni kudhihirisha tu kwamba Bunge limetumika kuisigina demokrasia.

Profesa Baregu alisema kimsingi maswali ya Kabwe hayajajibiwa kwani jibu la kuwa kulikuwa na ulazima wa kuharakisha mkataba si jibu lenye mantiki.

Naye Dk Mohamed Bakari wa Idara ya Sayansi ya Siasa na Uongozi wa Umma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, alisema alichofanya Kabwe ni kutoa shutuma na njia muafaka ni anayeshutumiwa kutoa hoja mbadala na kuonyesha kwamba shutuma zilizotolewa si za kweli.

Alisema hilo ni jambo la kawaida hata katika uvumbuzi wa kisayansi, kinachoanza ni kuwa na wasiwasi na kitu, dhana ndiyo huzaa ukweli, sasa hakukuwa na ubaya wowote kuiacha dhana kujadiliwa ili hatimaye ukweli upatikane.

?Jibu la Waziri peke yake halijatosha kuondoa shutuma na kwa kweli kilichotendeka ni sawa na kuwazuia watu kusema. Kitendo kilichotendwa dhidi ya Kabwe ni cha aibu kwa Spika na hata kwa Bunge,? alisema Dk Bakari.

Umoja wa vyama vya upinzani mkoa wa Arusha, umempongeza Kabwe kwa kutoa hoja binafsi ya kutaka kuundwa kamati ya kuchunguza kusainiwa mkataba wa mradi wa madini ya Buzwagi wilayani Kahama na umemkaribisha mkoani Arusha kuzungumza na wananchi.

Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi, James Mbatia, amepinga hatua iliyochukuliwa na Bunge kumsimamisha Kabwe na kudai kuwa adhabu hiyo ni ya ukandamizaji wa demokrasia nchini.

Mbatia alisema pia kuwa hiyo ni picha halisi kuwa Bunge chini ya Spika Samwel Sitta, limekuwa ni la kuwaburuza wapinzani na pia kumlaumu Spika kwa kuruhusu kuingiza mjadala wa kiitikadi katika Bunge, suala ambalo alisema si sahihi.

"Zitto Kabwe ni shujaa, ninavyomjua mimi si mropokaji hata siku moja, lakini amedhihirisha pia ushujaa kwa kusimamia lile analoliamini mpaka dakika ya mwisho, adhabu aliyopewa haikufuata kanuni na misingi ya haki za binadamu kujitetea, ni maonevu ambayo yameweka kovu lisilofutika kwa makundi ya demokrasia," alisema.

Mwenyekiti wa Chama cha DP Mchungaji Christopher Mtikila pia ameungana na wenzake akisema Zitto hana kosa, adhabu aliyopewa ni uharamia wa demokrasia na suala ambalo kila Mtanzania anatakiwa kulitambua na kutotakubali kukaa kimya.

Akizungumza na Mwananchi kwa njia ya simu kutokea Mwanza, Mchungaji Mtikila alisema tayari ameshazungumza na mwanasheria wake aliyeko Dar es Salaam ambaye anaandaa kusudio la kupinga adhabu hiyo ili kulifikisha Mahakama Kuu mapema iwezekanavyo.

Mwenyekiti wa Tanzania Labour Party (TLP) Wilaya ya Arusha, Calist Lazaro, alisema licha ya kumwalika Kabwe kwenda Arusha kuzungumza na wananchi, juu ya hoja hiyo na watamuandalia mapokezi makubwa. ?Tayari tunajipanga kumpokea aje Arusha kwani wabunge wa CCM hawajamvua ubunge, sisi tutaendelea kumpa heshma yake.

Kwa upande wa Asasi za kiraia zimesema utaratibu uliotumika kumwadhibu Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe, ni batili kwa maelezo kuwa haukufuata maadili wala kanuni za Bunge.

Akizungumza kwa niaba ya viongozi wa taasisi hizo jana, Wakili wa Kujitegemea, Tundu Lissu, alisema adhabu iliyotolewa kwa Kabwe sio halali, huku akitaka mbunge huyo aruhusiwe kuendelea na vikao vyote vya Bunge.

Lissu alisema ni bora Bunge likaeleza mbunge huyo amepewa adhabu ya ngapi ili wananchi walinganishe na kufahamu adhabu ambayo ilikuwa inastahili kulingana na kosa, kama analo.

Naye Gema Akilimali wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), alisema Bunge sasa limegeuka kuwa serikali na siyo mhimili wa tatu wa serikali kama ilivyokuwa hapo mwanzo.

Spika aueleze umma, je Bunge lipo au halipo kwani, linatetea serikali badala ya wananchi hii ni ajabu!? alisema Akilimali.

Pia alipendekeza Bunge lielewe kuwa adhabu ya Zitto ni dhidi ya wananchi wa Kigoma Kaskazini kwani, kutokuwa na mwakilishi katika vikao viwili vya bunge ni hasara kubwa kwao.

Mbali na mahojiano na makundi hayo ya wanazuoni na viongozi wa kisiasa, wananchi kutoka sehemu mbalimbali za Tanzania, wametuma barua pepe na wengine kupiga simu chumba cha habari, wote wakilaani kusimamishwa kwa Mbunge huyo.

Wakati huo huo Kabwe ametangaza azma ya kukata rufaa Mahakama ya Rufaa kupinga adhabu ya kusimamishwa kujishughulisha na shughuli zote za Bunge hadi Januari mwakani kwa madai kwamba ameonewa.

Akizungumza na Mwananchi jana, Zitto alisema anawasiliana na mwanasheria wa chama chake, Tundu Lissu, pamoja na wanasheria wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kuiomba mahakama uwezekano wa kuipitia upya hukumu aliyopewa na Bunge.

Alisema adhabu aliyopewa ni ya uonevu kwa kuwa kanuni ya Bunge namba 59 iliyotumiwa kumpa adhabu hiyo, haihusiani na masuala ya adhabu, badala yake ilipindishwa makusudi ili kumkomoa.

Zitto alisema kanuni hiyo inahusu masuala ya amani na usalama bungeni tofauti na ilivyotumiwa na Bunge kumuadhibu.

"Walipindisha kanuni kunikomoa, wameshindwa kuthibitisha uongo wangu, najua nafsi zao zimejuta kwa sababu nimeibua uozo unaofanywa. Nitashtaki pia kwa wananchi, waamue la kufanya," alisema Zitto.

Alisema adhabu hiyo pia haikutokana na Spika bali na Bunge, kinyume na kanuni za Bunge.

Hata hivyo, Zitto alisema pamoja na adhabu aliyopewa, moyo wake ni mweupe kwa kuwa ametimiza wajibu wake wa kikatiba wa kuhakikisha analinda raslimali za nchi.

"Nimefanya kazi ambayo Mbunge anatakiwa kuifanya. Wengi walikuwa hawajui kama kuna mkataba uliosainiwa kimya kimya na serikali London. Hata wabunge walioshinikiza niadhibiwe pia walikuwa hawajui hilo," alisema Zitto.

Imeandikwa na Boniface Meena, Mussa Juma, Andrew Msechu, Hawra Shamte na Muhibu Saidi
 
yaaaani what the f*****KKKK !@ nimesoma kumbe jamaa kasimamishwa hadi 2008 ! what the.................

Sababu;...ili tusahau, maana kwa kusahau sie hatujambo!!! Baada ya wiki tu TUTASAHAU yote haya...!!!
 
Mida hii, chama cha mhe. Zitto (CHADEMA) kinamfanyia pati ya pongezi..

Why am I not surprised? Wabongo kwa pati! When Taifa Stars scores a remote goal, we throw a bash, when Flaviana Matata lands from Mexico, a party! When Mwisho Mwampamba comes second in voyeuristic contest, a party! When an MP is sacked for lying, a party! We are a nation of festivals. And we want to catch up with the rest of the world! A nation is as strong as the character of its people.
 
kama mtikila amesema anafungua kesi mahakama kuu kupinga adhabu ya zitto....i think it is strategically right..CHADEMA wamuunge mtikila mkono..kwani inapendeza kama kesi hiyo inafunguliwa na mtanzania yoyote aliyeona haki haikutendeka.........utakuwa mtihani wa kwanza kwa augustino ramadhan..ili tujue na yeye muhimili wake umeshatekwa kama ule wa sitta au la..
 
kama mtikila amesema anafungua kesi mahakama kuu kupinga adhabu ya zitto....i think it is strategically right..CHADEMA wamuunge mtikila mkono..kwani inapendeza kama kesi hiyo inafunguliwa na mtanzania yoyote aliyeona haki haikutendeka.........utakuwa mtihani wa kwanza kwa augustino ramadhan..ili tujue na yeye muhimili wake umeshatekwa kama ule wa sitta au la..

kama mtikila atafungua kesi ni sawa sawa, lakini cha kushangaza chadema wanafanya party, party ya nini ? au ndio fumbo hilo kwamba wanafanya vile kukimaliza ccm, ? mhm, labda party hiyo ni kusherekea mwanzo wa mwisho wa muungwana, we never know ! lets wait.
 
nimeona erasto tumbo ......mkurugenzi wa CHADEMA anaongelea mapokezi ya zitto jumamosi..wajitahidi kwa pamoja na wabunge wote wa upinzani na viongozi wao akiwemo mtikila wafanye rainball opposition meeting than ever....

nadhani vijana wanamapinduzi wengi waanze kuandaliwa kugombea wilayani/majimboni....kila jimbo lianze kulifikiria hili.........siku bunge likifikia wapinzani hata 100 tu ..basi nawahakikishieni tofauti itaonekana...maana wengi wa wabunge wa ccm ni mabubu wanaokula wanavimbiwa hadi wanatapikia viatu vyao,,...wanabaki kuchafua hewa na kulala bungeni kutwa nzima...
 
nimeona erasto tumbo ......mkurugenzi wa CHADEMA anaongelea mapokezi ya zitto jumamosi..wajitahidi kwa pamoja na wabunge wote wa upinzani na viongozi wao akiwemo mtikila wafanye rainball opposition meeting than ever....

nadhani vijana wanamapinduzi wengi waanze kuandaliwa kugombea wilayani/majimboni....kila jimbo lianze kulifikiria hili.........siku bunge likifikia wapinzani hata 100 tu ..basi nawahakikishieni tofauti itaonekana...maana wengi wa wabunge wa ccm ni mabubu wanaokula wanavimbiwa hadi wanatapikia viatu vyao,,...wanabaki kuchafua hewa na kulala bungeni kutwa nzima...

Mkubwa unatoa maagizo mtandaoni? Ila naomba unieleweshe "rainball" manake nini?
 
House resists Zitto's motion

DAILY NEWS Reporter in Dodoma
Daily News; Wednesday,August 15, 2007 @00:04

THE parliament was yesterday overwhelmingly opposed
to the formation a probe team over alleged mining deal
sealed in London last year by the Minister for Energy and
Minerals, Mr Nazir Karamagi.

As we went to the press last night, Mr Kabwe Zitto(Chadema-Kigoma North), who presented a private motion in the House, was defending his position that the deal smacked of shoddy deal.

Earlier the Minister for Energy and Minerals, Mr Nazir Mustafa Karamagi, told the National Assembly yesterday that there was ‘absolutely nothing wrong' in the signing of a mining contract between the state and Barrick Good Corporation in March this year.

The minister explained that the contract was prepared in Tanzania by competent local experts, taking all contractual requisites aboard, confirming that the contract got blessings from the Mining Advisory committee. He told the legislators that the government decided to offer Buzwagi project to Barrick Gold Corporation, which is a holding company.

The contract was supposed to be done in March, this year, short of which the prospect for investment in the project would have been lost. Mr Karamagi said all contractual arrangements prior to signing were made in Tanzania at a time the minister was on a long working tour abroad he saw no point in jeopardizing the investment opportunity which was in the best interest of the nation. He signed the contract in London, UK.

He outlined the benefits of the investment as including royalties and other taxes amounting to 168.9 million US dollars a year; Pay as You Earn (PAYE) in the tune of 50.3 million US dollars a year, and installation of power lines and power consumption costing 30 million dollars a year. The minister also said the investor would pay an estimated 818.3 million dollars to the government in variou s taxes during the lifespan of the project. He said the project would employ 696 workers of various disciplines on permanent terms, 630 of whom would be indigenous Tanzanians.

He told the House that the minister signed the contract with Barrick Gold Tanzania in respect of Buzwagi mines in the last week of February, this year, a few months before the National Environment Council appro ved the environment impact assessment report of the company. He said the approval was issued on May 11, this year. He demanded to know why Mr Karamagi signed the mining contract before the environment council had given its go-ahead to the signing. He said the minister should also have listened to the advice of the Mining Advisory Committee.

He said if a minister elects to reject the committee's advice on the opportune moment to sign a contract he is required to give reasons. Mr Zitto demanded that a select parliamentary committee be formed and charged with the duty of probing into ircumstances that surround the contract. He said the committee should investigate if there are any unlawful acts and consequent losses of financial income to the state. Discussing the motion, Ms Ruth Blasio Msafiri (Muleba North), said there was no need to form a select committee to investigate this matter.


Waziri anaongelea benefits, Je mabadiliko ya mkataba huu na ile ya zamani ni yapi? Hiyo ya kuweka idadi ya pesa sio kitu. kitu cha msingi ni mabadiliko kuonyesha kwamba huu ni mkataba bora kuliko ile ya mwanzo.
 
Mkubwa unatoa maagizo mtandaoni? Ila naomba unieleweshe "rainball" manake nini?


its rainbow.....macho na vidole vimekosa ushirikiano..i mean its typing error...vipi umeona hilo tu??....yule mbunge wenu eng stella aliwashauri vizuri sana pale alipotoa mfano wa biblia"..pakiwamo wenye haki 9 katika mji wenu nitawasamehe kwa ajili yao..yesu akashuka hadi akauliza kama kuna mwenye haki hata mmoja tu ili aunusuru mji wa sodoma na gomora..." eng stella alimalizia akasema pamoja na mabaya yote ya hoja za zitto kwa ccm "hawaoni hata hija moja ya muhimu??? ili wamsamehe kutokana na hiyo hoja moja nzuri.....wabunge wenzake wa ccm walim boow..hii ina maana wenzako wengi pale bungeni waliona sense kwenye hoja za zitto na kimsingi wanakubali kuwa zinahitaji kufanyiwa kazi..tatizo lipo kwa waitikiaji wa JSM Kama wewe.....
 
Back
Top Bottom