The Buzwagi Saga: Karamagi aenda kusaini Mkataba wa ULAJI London

The Buzwagi Saga: Karamagi aenda kusaini Mkataba wa ULAJI London

hata hivyo maelfu ya watu na magari zaidi ya 200 yakipeperusha bendera za CHADEMA na vyama vingine ...yawliweka msafara mrefu kuanzia ubungo kuanzia saa saba ..maandamano yalipokewa jangawani saa 9...zittokabwe alikuwa kwenye gari pajero la wazi akiwa na nafikiri yule ni chacha wangwe ...alionekana akipunga kwa furaha kwa wananchi waliokuwa na chauku kubwa pamoja na mvua kunyesha...baaada ya dk 30 hapo saa 12.30 [*3 gmt]ingia kwenye mtandao wa bbc swahili service upate ma live cos mkutano ndio unaishaisha..maana bbc walionekana wakiwa busy kufanya coverage .....
 
kabwejangwanild8.jpg


Gari la Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe likisukumwa na mashabiki kwake kuelekea viwanja vya Jangwani jijini Dar es Salaam jana.

Maelfu wakubali mvua iwanyeshee kumsikiliza Kabwe Dar

*Asema mkataba ulisainiwa Hotelini London
Michael Matemanga, RCT na Boniface Meena

MAELFU ya wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam jana walijitokeza katika mapokezi na maandamano ya kumpokea Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema) Zitto Kabwe, aliyesimamishwa ubunge hadi Januari mwakani. Maandamano hayo, ambayo yalihudhuriwa na viongozi mbalimbali kutoka kambi ya upinzani, yalianzia eneo la Ubungo, baada ya Zitto Kabwe kuwasili akitokea mjini Dodoma. Maandamano hayo yalipitia barabara ya Morogoro na kuishia katika viwanja vya Jangwani ambako Kabwe alihutubia wananchi na kufafanua juu ya kile kilichotokea bungeni baada ya kuwasilisha hoja yake binafsi na baadaye kusimamishwa.

Katika hotuba yake kwa wananchi hao waliokusanyika Jangwani, Kabwe alisema iwapo mkataba wa madini wa mradi wa Buzwagi ungesainiwa nchini Uingereza ndani ya ubalozi wa Tanzania nchini humo, kusingekuwepo na tatizo. Alisema iwapo Kamati Teule ya Bunge aliyoomba iundwe kuchunguza mkataba huo uliosainiwa jijini London ingeundwa, ingegundua kuwa mkataba huo ulisainiwa hotelini.

"Niwaambieni tu ndugu zangu, hiki ni kitu ambacho sikukisema hapo mwanzo lakini kama kamati ingeundwa ingegundua kuwa mkataba huo ulisainiwa hotelini na hoteli yenyewe inaitwa hoteli ya Churchill iliyoko jijini London," alisema Kabwe. Alisema wakati Waziri Nazir Karamagi anasaini mkataba huo, Rais alikuwa hajui kama waziri wake alikwenda huko kusaini mkataba kinyume na maelekezo yake.

"Tukumbuke kuwa rais aliwahi kutangaza kuwa serikali itapitia mikataba yote ya madini, Mei mosi mwaka 2006 wakati wa sikukuu ya wafanyakazi na alikumbushia suala hilo, tarehe 17 mwezi Julai mwaka huo huo wakati Waziri wa Nishati na Madini wakati huo akiwa Dk Ibrahim Msabaha, ambaye alitangaza azma ya serikali kusitisha kusainiwa kwa mikataba ya madini na rais alipokuwa Afrika Kusini mwezi Februari 6 mwaka huu, huku akisema mikataba inaendelea kupitiwa, sasa hili inakuwaje?" alihoji Kabwe.

Alisema kutokana na hilo, wakati umefika kusimama kidete kuhakikisha rasilimali za Watanzania zinalindwa ili kuondokana na umasikini uliokithiri, huku akimtaka Kikwete kuangalia nyumbani kwake kwani kumeingiliwa na watu ambao hawajui kujenga nchi zaidi ya kushibisha matumbo yao.

"Rais aisafishe serikali yake mara moja ili ifanye kazi kwa maslahi ya wananchi, kwani wasaidizi wake wanamkosesha imani na Watanzania," alisema Kabwe. Kabwe alimaliza kwa kusema kuwa, mamlaka yote ya dola yapo mikononi mwa wananchi na Bunge ni wawakilishi wao tu, hivyo imani ikikosekana bungeni ni hatari kubwa na wajibu uko mikononi mwa wananchi.

Naye Mbunge wa Karatu (Chadema), Dk Wilbroad Slaa, ambaye alipanda jukwaani baada ya Kabwe kumaliza kuhutubia, alielezea suala la yeye kuamua kuichomoa bungeni hoja yake kuhusu ubadhilifu katika Benki Kuu ya Tanzania (BOT) na kuikabidhi kwa Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na kuifanya kuwa hoja ya kisiasa isiyopelekwa tena bungeni.


Bofya hapa
 
Ndo nimetoka Jangwani kwenye mkutano wa Zitto. Mvua imetunyeshea kishenzi, lakini tumesema ndiyo gharama ya harakati. Msishangae maksoa vidole vinatetema! Kwa umati ule na hamasa niliyoina pale, nakubali nchi inaanza kubadilika. Watu sasa wanaanza kujifunza kuitumia vema dhana ya NGUVU ya UMMA. Mke wangu naye ameguswa sana (si unajua ni mwanaCCM) na matukio ya wiki hii, na baada ya kumwona na kumsikiliza Zitto pale Jangwani anasema sasa naye anataka kujiunga CHADEMA!

Nimemwambia mimi naendelea na CUF yangu kwa ajili ya kukomaza mageuzi Visiwani, lakini katika masuala ya siasa za Bara nitawaunga mkono CHADEMA maana ndio wanaonekana kuwa na mwamko mpya, mithili ya ule uliokuwapo wakati wa ujana wa Nyerere na TANU. Dar es Salaam moto wa mageuzi unawaka kila sehemu!
 
jiji la dar limekabiliwa na mvua kubwa ya ghafla leo..pamoja na hayo imepungua muda simrefu na wana wa nchi wanaendelea na mkutano jangwani...

Sawasawa na ule ujio wa Mandela, baada ya kutoka tu gerezani alikuja Tanzania kwenye HIJA ya Taifa lililompa support kubwa. Mvua ilinyesha ile mbaya, nakumbuka tulilowana tepetepe lakini tulihakikisha tume mlaki mabarabarani.

SteveD.
 
Kichwamaji

Thanks for Info. Sisi tupo tunasikiliza habari za huko Maana magazeti wanachelewa.
 
Je, Wapinzani mmejifunza nini kutokana na muungano wenu ktk swala hili?...

Wananchi wamekusikieni na isiwe ndio imetoka!. Wapo nanyi kuliko wakati wowote!
UMOJA ni NGUVU hili liwe somo kwenu na namshuikuru sana Zitto kuwa kiamsho cha wananchi!
 
KWELI STEVE,

Wenzetu husema 'GOLDEN CHANCE' Jamani ee hapo hakuna kulala, Leteni herokopta huu ndo wakati wa mavuno na kujiimarisha vijijini!

Chapisha kadi za kutosha na biashara ya kukatisha shauri ianze mara moja kwa kwenda mbele MOTO MDUNDO mpaka 2010
 
Maelfu wakubali mvua iwanyeshee kumsikiliza Kabwe Dar
*Asema mkataba ulisainiwa Hotelini London

Michael Matemanga, RCT na Boniface Meena

MAELFU ya wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam jana walijitokeza katika mapokezi na maandamano ya kumpokea Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema) Zitto Kabwe, aliyesimamishwa ubunge hadi Januari mwakani.

Maandamano hayo, ambayo yalihudhuriwa na viongozi mbalimbali kutoka kambi ya upinzani, yalianzia eneo la Ubungo, baada ya Zitto Kabwe kuwasili akitokea mjini Dodoma. Maandamano hayo yalipitia barabara ya Morogoro na kuishia katika viwanja vya Jangwani ambako Kabwe alihutubia wananchi na kufafanua juu ya kile kilichotokea bungeni baada ya kuwasilisha hoja yake binafsi na baadaye kusimamishwa.

Katika hotuba yake kwa wananchi hao waliokusanyika Jangwani, Kabwe alisema iwapo mkataba wa madini wa mradi wa Buzwagi ungesainiwa nchini Uingereza ndani ya ubalozi wa Tanzania nchini humo, kusingekuwepo na tatizo.

Alisema iwapo Kamati Teule ya Bunge aliyoomba iundwe kuchunguza mkataba huo uliosainiwa jijini London ingeundwa, ingegundua kuwa mkataba huo ulisainiwa hotelini.

"Niwaambieni tu ndugu zangu, hiki ni kitu ambacho sikukisema hapo mwanzo lakini kama kamati ingeundwa ingegundua kuwa mkataba huo ulisainiwa hotelini na hoteli yenyewe inaitwa hoteli ya Churchill iliyoko jijini London," alisema Kabwe.

Alisema wakati Waziri Nazir Karamagi anasaini mkataba huo, Rais alikuwa hajui kama waziri wake alikwenda huko kusaini mkataba kinyume na maelekezo yake.

"Tukumbuke kuwa rais aliwahi kutangaza kuwa serikali itapitia mikataba yote ya madini, Mei mosi mwaka 2006 wakati wa sikukuu ya wafanyakazi na alikumbushia suala hilo, tarehe 17 mwezi Julai mwaka huo huo wakati Waziri wa Nishati na Madini wakati huo akiwa Dk Ibrahim Msabaha, ambaye alitangaza azma ya serikali kusitisha kusainiwa kwa mikataba ya madini na rais alipokuwa Afrika Kusini mwezi Februari 6 mwaka huu, huku akisema mikataba inaendelea kupitiwa, sasa hili inakuwaje?" alihoji Kabwe.

Alisema kutokana na hilo, wakati umefika kusimama kidete kuhakikisha rasilimali za Watanzania zinalindwa ili kuondokana na umasikini uliokithiri, huku akimtaka Kikwete kuangalia nyumbani kwake kwani kumeingiliwa na watu ambao hawajui kujenga nchi zaidi ya kushibisha matumbo yao.

"Rais aisafishe serikali yake mara moja ili ifanye kazi kwa maslahi ya wananchi, kwani wasaidizi wake wanamkosesha imani na Watanzania," alisema Kabwe.

Kabwe alimaliza kwa kusema kuwa, mamlaka yote ya dola yapo mikononi mwa wananchi na Bunge ni wawakilishi wao tu, hivyo imani ikikosekana bungeni ni hatari kubwa na wajibu uko mikononi mwa wananchi.

Naye Mbunge wa Karatu (Chadema), Dk Wilbroad Slaa, ambaye alipanda jukwaani baada ya Kabwe kumaliza kuhutubia, alielezea suala la yeye kuamua kuichomoa bungeni hoja yake kuhusu ubadhilifu katika Benki Kuu ya Tanzania (BOT) na kuikabidhi kwa Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na kuifanya kuwa hoja ya kisiasa isiyopelekwa tena bungeni.
 
Mwanzo wa mwisho wa udhalimu umewadia.Kama kuna atakaye wadharau wale waliokubali kunyeshewa mvua ili kupinga uozo uliopo basi asubiri haohao watakapo ishiwa uvumilivu na staha kisha kutumia nguvu kuleta mabadiliko (Mungu aepushie mbali maana tumeona kwa wenzetu)
 
1. Jana kwenye data zetu tulisema hivi,

Quote

1."Okay wazee niko njiani ninaendesha, lakini kewa hraka haraka, nilizozipata,

1. Mbunge wa Same East, alifikisha hoja ya madini bungeni, Zitto wakati wa break time akamwambia umeanzisha moto, subiri tukirudi uone nitakavyoiweka vizuri hoja ya madini!

2. Zitto, akaiweka inavyotakiwa kuwa Karimagi, amesaini mkataba na Barrick, London tena hotelini, hakuifahamisha kamati ya bunge ya uwekezaji, wala bunge zima kwa ujumla! hiyo mikataba ina utata!

3. Wabunge wote wakapigwa na shock ya umeme kusikia hayo maana waklikuwa hawajui kuhusu huo mkataba!"

2.Leo Mbunge Zitto, kwenye maandamano amesema hivi:

"Niwaambieni tu ndugu zangu, hiki ni kitu ambacho sikukisema hapo mwanzo lakini kama kamati ingeundwa ingegundua kuwa mkataba huo ulisainiwa hotelini na hoteli yenyewe inaitwa hoteli ya Churchill iliyoko jijini London," alisema Kabwe.


Je kuna mahali popote kwenye media zetu mlipoiona hii habari? Au kwenye hiyo kitu inaitwa ansard? Sasa haya maneno yalienda wapi na Zitto aliyasema ndani ya bunge? Ndio maana tunasema vijana muwe macho na data, na usanii wa serikali!
 
1. Jana kwenye data zetu tulisema hivi,

Quote

1."Okay wazee niko njiani ninaendesha, lakini kewa hraka haraka, nilizozipata,

1. Mbunge wa Same East, alifikisha hoja ya madini bungeni, Zitto wakati wa break time akamwambia umeanzisha moto, subiri tukirudi uone nitakavyoiweka vizuri hoja ya madini!

2. Zitto, akaiweka inavyotakiwa kuwa Karimagi, amesaini mkataba na Barrick, London tena hotelini, hakuifahamisha kamati ya bunge ya uwekezaji, wala bunge zima kwa ujumla! hiyo mikataba ina utata!

3. Wabunge wote wakapigwa na shock ya umeme kusikia hayo maana waklikuwa hawajui kuhusu huo mkataba!"

Leo Mbunge Zitto, kwenye maandamano amesema hivi:

"Niwaambieni tu ndugu zangu, hiki ni kitu ambacho sikukisema hapo mwanzo lakini kama kamati ingeundwa ingegundua kuwa mkataba huo ulisainiwa hotelini na hoteli yenyewe inaitwa hoteli ya Churchill iliyoko jijini London," alisema Kabwe.


Je kuna mahali popote kwenye media zetu mlipoiona hii habari? Au kwenye hiyo kitu inaitwa ansard? Sasa haya maneno yalienda wapi na Zitto aliyasema ndani ya bunge? Ndio maana tunasema vijana muwe macho na data, na usanii wa serikali!

I have fond memories of CHURCHILL HOTEL, LONDON
 
bubu....

time will tell us,hata mrema alivyohutubia UDSM alibebwa na wasomi wetu.matokeo yake amekuwa bogesti wa kutupwa.
 
bubu....

time will tell us,hata mrema alivyohutubia UDSM alibebwa na wasomi wetu.matokeo yake amekuwa bogesti wa kutupwa.

Wavutaji wa mashati hawakosi katika jamii. Mrema na Zitto hawalinganishwi kwa vigezo vyovyote vile. Tunachosema hapa ni kwamba times have changed baada ya "chaguo la Mungu" kuonekana mbabaishaji, mwizi (na amezungukwa na wezi) kama waliomtangulia. But cynics will always be there!
 
Prof. Kichuguu,

Uchambuzi safi kabisa.......

1.Ukiondoa hicho kipengele cha EIA ambacho waziri amejibu sawa................. nina mtizamo tofauti kuwa hii nayo ina mapungufu yake.......kwani tunatagulia kuwa na mkataba ambao ni binding.....na hapo baadaye EIA ikisema otherwise inakuwa kasheshe ktk EMP (environmental Management Plan) ambazo investors wengi hawatimizi mitigation measures kuepuka costs

2. Ni maoni yangu pia kuwa Waziri ana madaraka makubwa sana ya either kutuingiza mkenge ktk miradi mingi tu...........nafikiri ingekuwa vyema kuweka Kamati maalum itakayokuwa inatoa leseni (wadu wote wakishirikishwa) na sio waziri peke yake.

ukiondoa hilo la EIA majibu mengine ya waziri yamekuwa kama COVER UP ya mambo ambayo very hidden (UMAFIA).

Once again uchambuzi wako ni murua


Ogah,

maoni yako ni sahihi kabisa. Ndiyo maana kuna haja ya kufan ya marekebishoa katika sheria ya madini. Ila kwa sasa hivi sheria yetu inaruhusu maovu hayo kufanyika.
 
Labda hili litamsukuma JK kufanya mabadiliko na kupitia vitu kadha wa kadha...
 

Attachments

  • 1.jpg
    1.jpg
    57 KB · Views: 66
  • 2.jpg
    2.jpg
    47.8 KB · Views: 59
  • 3.jpg
    3.jpg
    19.9 KB · Views: 54
Hotuba ya Kabwe Zitto imeleta mengi mapya masikioni mwa Watanzania,Ambayo hatukuyasikia kwenye hotuba(Hoja) yake kule Dodoma Bungeni,Sio kwamba Mkataba ulisainiwa Hotelini na sio Ubalozini,bali pia Mkuu wa Kaya hakufahamishwa Ukweli kuhusu Mkataba huo.Pamoja na kwamba walikuwa pamoja ktk safari hiyo ya Uk na Japan.

Katika Hotuba yake kwenye sherehe ya Mei Mosi/2006,Jk alisema kwamba Utiaji saini mikataba yote ya madini umesimamishwa na serikali ya awamu ya NNE ili kutoa nafasi kwa Mabingwa wa mikataba kuipitia Upya kwani Mikataba iliyopita ina Utata,Alirudia maelezo hayo ya kusimamisha Utiaji saini Mikataba ya Madini huko Afrika kusini kwenye Seminar ya Madini.Sasa Mkataba huu uliotiwa Saini na Karamagi una utofauti na Mingine?

Kitendo cha Ndg Karamagi(Waziri mfanyabiashara)kutia saini Mkataba wa Uchimbaji Madini huko Kahama kinanipa wasiwasi kuwa kuna Mazingira ya Rushwa.Maelezo ya Zitto ni mwanzo tu wa ukweli mzima wa mambo.Na kama ni kweli Waziri alitia saini Mkataba huo bila Ufahamu wa Rais sioni kwanini Waziri asiwajibike!!
 
Mimi nilikuwa mchezaji wa soka enzi zangu.
Endapo mnaongoza kwa magoli 2 kwa nunge kisha ikatokea kwamba kazi yenu kubwa katika kipindi cha pili ni kujenga defensi ili kuzuia mashambulizi tu mjue dakika yeyote mnaweza kupoteza ushindi.
Timu inayoongoza kwa kawaida huendelea kudifendi na kushambulia kwa wakati mmoja.

Ndugu zetu wa CCM wanaongoza, ni washindi mapaka dakika hii. Lakini tangu awamu hii ianze kazi yao kubwa imekuwa ni kuzuia mashambulizi kutoka vyama vya upinzani.
Kibaya zaidi sasa wameanza kupiga vipepsi(Kufungia wabunge) ndani ya 18 na refa anawabeba. Wamesahau kwamba mechi inachukuliwa video wakati ukifika makamisaa( wananchi) watahakiki kama uchezaji wao mzima ulikuwa halali au vipi.

Sisi wananchi pia tunamatatizo bado kuna wenzetu kadhaa wamekata tamaa wanadhani wanadhani hapa ndiyo tumefika kwa vile kila mtanzania ni mwizi na hatuwezi kupata watu shujaa kutuongoza.

Nyerere alikuwa ni Mtanzania pia tena aliyeshika cheo cha juu kuliko Mtanzania yeyote kwa muda mrefu kabisa. Hakuiba hata shilingi.
Wako Watanzania wengi ambao wana uchungu na nchi yao. Lakini je unadhani wanaweza kufurukuta kati kati ya Fisi hawa wa CCM na kuweka mambo sawa?
Katika uwingi wetu wananchi tunaweza kubadiri mwelekeo tukikata tamaa hakuna wa kutupigania haki zetu kiuchumi.
Mwaka 2010 tutaingiza vijana wengi zaidi ndani ya Bunge na ikiwezekana tumshawishi MH Kabwe asiachie ngazi.

Wewe kijana huna haja ya kukata tamaa na kusema haiwezekani kwa sababu tu Mrema alishindwa.
Mrema ni mtumishi wa usalama wa taifa mpaka kesho.
Toka lini shushushu akastaafu???
CCM wametuandalia hila nyingi lakini katika kuzitekeleza hila hizo aibu na udhaifu wao utawekwa wazi.
Udhaifu wao ndiyo mtaji wetu.
Ukipta mtaji unautumia kuongeza faida.
 
Tanzania ni nchi yetu sote, malighafi zote ni za wananchi wote, serikali ni viranja wa kusimamia malighafi zetu, ili ziweze kutoa na kutupa maisha bora wote.

Waungwana wameshindwa kabisa kuzisimamia sasa washikadau wameshtuka, je tuwafanye nini hawa viranja???

Kijana Zito ameonyesha jinsi gani watanzania wa leo sio wa jana kwani kila mmoja kwa namna yake anaona ubovu, uzembe na uzandiki wa serikali, Kama kweli kauli za Kikwete zimekinzana na matendo ya waziri wake kkt utendaji , na tuone basi nini atakifanya, ila hii nisirikali sioni kitu hapa.

Hakuna rekodi ya kuwajibishana wala kuwajibika ndani ya nchi yetu, nchi imekuwa kama jeneza ambalo halifai kuzikwa wala halifufuki.

Huu ni wakati mzuri kwa kila mwenye kupenda maisha bora kuwaeleza wananchi wanaomzunguka ni nini wajibu wa serikali kwake. Ni nini maanaa ya tanzania kuwa na madini na uhusiano wake na maji safi , barabara bora, hospitali bora, shule bora pamoja na ajira za kutosha.

Wakati umefika watanzania wajue kusujudia mlarushwa na kumwona ni shujaa ni ujinga mkubwa, kwanza wachukieni wanaotuletea umaskini msiwaoonee haya wala kuwakumbatia.

Mikataba ya kihuni ambayo inatiwa saini kihuni inatuumiza sote, mwisho wa siku sote tunalipa tusichokijua. Leo madini yupo karamag kesho ni mwingine ila mkataba ukishasainiwa haufutiki kirahisi.

Tuwasaidie watanzania wenzetu kuondoa woga, tukubali kujaa magerezani kwa kutetea haki, hata ikibidi kufa kwani tusipofika hapo tutaendelea kuwa wa hanga ktk nchi yetu huku wachache wakisherehekea uhuru mchwara.

Bila ya kumwaga jasho la DAMU, maendeleo ni ndoto.
 
Back
Top Bottom