The Buzwagi Saga: Karamagi aenda kusaini Mkataba wa ULAJI London

The Buzwagi Saga: Karamagi aenda kusaini Mkataba wa ULAJI London

Yaani nawaonea huruma hawa wanasiasa vijana...the Malima (yeye anaamini Zitto ni mmoja wa maadui zake katika sakata la NSSF/Manji/Mengi/Malima),Peter Selukamba (mpinzani wake kisiasa Kigoma na mpambe poa wa EL), na wengineo ...kwa kujianika hivi kwa watanzania. Wenzao wanakusanya pensheni zao na wengine ndio wanazila wakiwa kwenye jumba letu hili.

Kibano wao tunaokumbana mitaani kwa mika mingi inayokuja.

Tanzanianjema
 
Wewe, acha kutumia exclamation marks nyingi kiasi hicho.

...tatizo liko wapi..wewe huoni kwamba tunaliwa..si bora madini yetu yabaki ardhini ..mwalimu alisema hayaozi!!!..huko vijijini mwisho tutaachiwa mashimo tu..hulioni hilo..nina kilio namna walalahoi tunavyokosa utetezi!! tutetee basi..
 
...tatizo liko wapi..wewe huoni kwamba tunaliwa..si bora madini yetu yabaki ardhini ..mwalimu alisema hayaozi!!!..huko vijijini mwisho tutaachiwa mashimo tu..hulioni hilo..nina kilio namna walalahoi tunavyokosa utetezi!! tutetee basi..

Haina neno. Nimekupata.
 
Looh! Zitto amewazidi kabisa hawa CCM, naona walichofanya ni uonevu mkubwa.

Hivi Watanzania hatuwezi kuona bunge letu ni kichaka?
 
Binafsi nilijua ngoma itakuwa nzito kwa sababu kuu moja:
Wakati Ndugu Zitto anatoa hoja/swali kabla ya kuwasilisha hoja hii iliripotiwa kuwa huyo waziri wakati anasaini huo mkataba huko Uingereza, alikuwa safarini na mkuu wa kaya. Kwa hali hiyo, niliamini kuwa bosi mwenyewe alitoa baraka zake. Isingekuwa rahisi waziri asaini, akiwa ziarani na rais, pasi na rais kujua au kubariki, ilhali ni yeye aliyesema mikataba mipya sasa basi mpaka kieleweke!

Hata hivyo, kwa upande mwingine, ikiwa ni kweli mkataba huu una masharti mazuri KIDOGO kuliko ile mingine ya awali, basi ni afadhali.

Taarifa nilizonazo ni kwamba hawa jamaa walitaka kusainisha mkataba huu mwishoni mwishoni mwa utawala wa MJASIRIAMALI, somehow, ikashindikana. Alipokuja Muungwana wakataka kusaini chapchap, lakini jamaa somehow akachelewesha kubariki zoezi hilo. Binafsi nilipata habari hizi za mzee "kuwakwepa" hao wawekezaji kuhusu mradi huo tangu mwaka jana kwani walitaka akazindue mradi huo tangu mwaka jana. Najua vyombo vya habari (magazeti ya BONGO) vimekuwa vikiandika siku nyingi kwa kurudia rudia habari ya mradi huo (hata pale kulipokuwa hamna kitu kipya) kwa nia ya kuweka msukumo fulani kwa serikali (mtazamo wangu).

Kuchelewa kusainiwa kulikuwa kukinipa faraja kuwa serikali kwa ujumla na Muungwana in particular, wameamua kusimamia kidete mikataba safi katika sekta hiyo. Sasa hili la kusaini katika mazingira ambayo kidogo (kama si sana!) yameleta maswali kumenichanganya. NDIYO MAANA NAAMINI KUWA MZEE ALIBARIKI ZOEZI HILO!
 
Wanabodi,
Naomba darasa hapa kidogo!
Hivi wabunge wanaweza kumsimamisha mbunge aliyechaguliwa na wananchi kwa sababu ya Hoja yake?... I mean hao wananchi wa Kigoma leo hii wanawakilishwa na nani - on his behalf! Je, ndio kusema jimbo la Kabwe limesimamisha Uraia wake hadi hapo January?...

Ebu nipeni darasa hapa maanake ikiwa chama tawala chenye wabunge zaidi ya asilimia 80 wanaweza kusimamisha mbunge mmoja... naona kama kuna uwezekano wa bunge hilo hilo kusimamisha wapinzani wote inapobidi!..
 
Mzee Malecela naye eti anaongea kwa uchungu, hawa wazee kweli wana uchungu wowote? Ndio maana Nyerere aliwaita wahuni.

Mimi hili bunge nitaacha kulisikiliza maana unaweza kuchukia
na kufanya mambo ya ajabu.

Mimi imeniudhi sana maana nilitegemea watu kama akina Malecela angalau wangelikuwa na busara ya kuwashauri wabunge wao lakini yeye ndio anaongoza kumfungia mtu ambaye mchango wake ni mkubwa kuliko wengi wao?
 
nimetoka kuangalia recorded ya star tv ...na tena malecela amemalizia kwa kutoa onyo kwa wapinzani kuwa ..atakayefuata nyayo au njia ya zitto..dawa ni hiyohiyo waliyompa zitto..kwa kweli inasikitisha sana..ni bora basi bunge lifutwe maana anaonekana bunge linatumikia siasa...hata yule waziri asiyejua kujieleza batilda burian..kati ya sababu za kutaka zitto aadhibiwe ni eti huwa imekuwa kawaida yake kutoa hoja za kuwakalia mawaziri kooni..so mpinzani anatakiwa awe bubu??
 
Nataka kuamini kuwa hii ni nafasi nzuri kwa Zitto kujipanga zaidi lakini experiance ya issue ya Dada yetu Amina ambayo mwanzoni niliamini kuwa naye angeweza kujipanga baada ya ushenzi ule aliofanyiwa inanifanya nijiulize zaidi.

Baada ya kufuatilia mjadala huo ambao nakubaliana na Zitto kuwa umeonyesha jinsi gani demokrasia inavyofanya kazi (tanzania style) nataka kuamini kuwa kilichotokea jana ni kurutubisha self destructive tendency ya tabaka tawala ama WALADAU katika nchi yetu. Tunaweza tusione matunda (matamu ama machungu leo) kwa sasa lakini yanakuja.

Kwa upande wa Spika ambaye nimekuwa nikiamini ni victim wa mfumo wa kisiasa lakini ni mwenye nia njema, uendeshaji wa mjadala wa leo umenifanya nijiulize zaidi na zaidi.

Kwa Zitto, jitahidi kuepuka maneno makali ambayo ni rahisi kutumiwa kukugeuzia kibao hata kama utakuwa umesimama katika mstari wa haki.

Lakini zaidi ya yote HONGERA kaka kwani mwisho wa siku ni kuwa yote yanayotokea ni sehemu ya kukomaza kwa majukumu makubwa zaidi hapo mbeleni na zaidi umeweza kufanikisha kile ambacho tunaamini ni moja ya mbionu za kisiasa.....Kuwaanika ndugu zangu ambao hivi karibuni tu walikuwa wakijidai kulilia maslahi ya wananchi na kufikia kudai kuwa wanabanwa kutetea maslahi ya watanzania kwa ajili ya kulinda maslahi ya chama tawala.

Nampa pole Dada yangu Dr Batilda Salha Burian kwa majukumu mazito ambayo kwa jinsi ninavyomjua ni wazi kuyatekeleza kimahiri kama alivyofanya ilikuwa adhabu kubwa moyoni mwake....
 
Mimi kwa maoni yangu wapinzani wote should walk out of the Parliament!...Maneno ya Malecela ni tishio kubwa ambalo linavunja kabisa demokrasia! His is out of line kabisaaa! sikutegemea hata kidogo, Duh!
Wapizani waondoke bungeni na wafanye kila njia kukutana na rais wa nchi..
Kitendo cha kumsimamisha Zitto ni kashfa kubwa kwa wananchi na sidhani kama Malecela anaweza kusimama mbele yetu kutuhakikishia kwamba Wabunge ni wawakilishi wa wananchi sio serikali wala chama tawala kuwajibisha mbunge wa upoinzani!.
Kifupi wanabodi nashindwa kabisa kuona logic ktk heria hii ambayo mbunge kiongozi wa chama tawala anaweza kumsimamisha mbunge wa Upinzani!.. Mimi nachofahamu ni Uongozi wa Chadema ambao unaweza kumsimamisha mbunge wake!..

Ndugu zangu bado naomba somo ktk hili
 
Mimi kwa maoni yangu wapinzani wote should walk out of the Parliament!...Maneno ya Malecela ni tishio kubwa ambalo linavunja kabisa demokrasia! His is out of line kabisaaa! sikutegemea hata kidogo, Duh!
Wapizani waondoke bungeni na wafanye kila njia kukutana na rais wa nchi..
Kitendo cha kumsimamisha Zitto ni kashfa kubwa kwa wananchi na sidhani kama Malecela anaweza kusimama mbele yetu kutuhakikishia kwamba Wabunge ni wawakilishi wa wananchi sio serikali wala chama tawala kuwajibisha mbunge wa upoinzani!.
Kifupi wanabodi nashindwa kabisa kuona logic ktk heria hii ambayo mbunge kiongozi wa chama tawala anaweza kumsimamisha mbunge wa Upinzani!.. Mimi nachofahamu ni Uongozi wa Chadema ambao unaweza kumsimamisha mbunge wake!..

Ndugu zangu bado naomba somo ktk hili

Sheria na kanuni za bunge zinasemaje? Hili swala lilizuka wakati mkono alipokuwa anamtetea Dito na Bunge halikufanya kitu lakini hili la ujinga ati amedanganya bunge. Hivi kweli sheria inasema Mbunge anaweza kusimamishwa kwa flimsy argument kama hii? MWENYE HIYO DOCUMENT ATUWEKEE HAPA.
 
mi naona hapa watu mnashindwa kueleza hasa nini kimetokea,inamaana huu mkataba mpya ni ruksa sasa wabunge kuuona,je nchi sasa inamufaika kivipi,wanalipa kodi sawasawa,kahama kama sehemu ya machimbo yalipo inanufaikaje ktk huu mkataba,
mwisha sioni kama kuna sababu ya kuwa na bunge,sijaona mafanikio ya bunge letu,kama yapo naomba nifahamishwe.
 
Wewe ni nani kuamuru watu hapa....

Members can use whatever the heck they want...

Au unadhani vikao vya chama hapa?

This Mugongo x 2 sounds like a corrupt arrogant CCM fellow who still thinks this is 1980's.Its high time he woke up to realise times have changed and you cannot terrorise people into believing that CCM owns the country.
This is a sad day for democracy in Tz.I wonder if this goverment realises that the whole world can see how rotten they are.
They silence the opposition and then dare to talk of heshima kwenye bunge letu. What a joke.One of these days they will tell us that we cant say their shit stinks and will have to say inanukia baadala ya kunuka.
 
..haya maswali yako hayana majibu sahihi!

..sababu hii issue ishakuwa siasa tayari!

..mwana si rizki tena huyu!


Kwa hili nakubaliana na wewe kabisa....kama ni Bwawa basi Luba Kibao na kama ni kitumbua basi kishaingia mchanga...
 
Mimi kwa maoni yangu wapinzani wote should walk out of the Parliament!...Maneno ya Malecela ni tishio kubwa ambalo linavunja kabisa demokrasia! His is out of line kabisaaa! sikutegemea hata kidogo, Duh!
Wapizani waondoke bungeni na wafanye kila njia kukutana na rais wa nchi..
Kitendo cha kumsimamisha Zitto ni kashfa kubwa kwa wananchi na sidhani kama Malecela anaweza kusimama mbele yetu kutuhakikishia kwamba Wabunge ni wawakilishi wa wananchi sio serikali wala chama tawala kuwajibisha mbunge wa upoinzani!.
Kifupi wanabodi nashindwa kabisa kuona logic ktk heria hii ambayo mbunge kiongozi wa chama tawala anaweza kumsimamisha mbunge wa Upinzani!.. Mimi nachofahamu ni Uongozi wa Chadema ambao unaweza kumsimamisha mbunge wake!..

Ndugu zangu bado naomba somo ktk hili

Mkandara Salute..

Kwa mimi nadhani wapinzani wote wangeungana katika hoja kama hizi...lakini zaidi Chadema wangalisimama kidete na kumtetea Zitto, mfano wangefanya Ziara fupi kule jimboni kwake kuwapa moyo wapiga kura wake kwamba ni kazi nzuri ya Mbunge wao ambayo imewafanya CCM wamchukie. Vyovyote watakavyofanya Chadema wana nafasi nzuri ya kupata kila faida ya kisiasa kwenye suala hili.
 
yy,
hii mibunge yetu mitutusa sijui hatala kusema,hivi unajua mpaka leo hii wilaya ya kahama haina maji,watu wanatumia maji ya visima
 
Katibu Tarafa,
Unasema Kahama!. Sema robo tatu ya nchi nzima!...
Ukerewe ambacho ni kisiwa kimezungukwa na maji.. ni majuzi tu wameanza kufufua upya mradi wa maji ambao ulikufa toka 1984!..tena baada ya kashfa nyingi ambazo zilitokea ktk uchaguzi uliopita..Yaani kufufua tu mitambo na kubadilisha mabomba ilikuwa ngoma ya miaka 13!, hadi sasa ni robo ya mji mkuu wa kisiwa hicho - Nansio maji yanapatikana!..
 
Mkandara Salute..

Kwa mimi nadhani wapinzani wote wangeungana katika hoja kama hizi...lakini zaidi Chadema wangalisimama kidete na kumtetea Zitto, mfano wangefanya Ziara fupi kule jimboni kwake kuwapa moyo wapiga kura wake kwamba ni kazi nzuri ya Mbunge wao ambayo imewafanya CCM wamchukie. Vyovyote watakavyofanya Chadema wana nafasi nzuri ya kupata kila faida ya kisiasa kwenye suala hili.

This is what we call constructive engagement. Zitto arudi jimboni na kauli yake kuhusiana na sakata hili akaitolee huko kuwapa heshima wapiga kura wake. Halafu wenziwe wawe naye karibu "SOLIDARITY FOREVER" strategy.

Halafu achukue muda kupumzika kidogo maana hicho kichwa bado tunakihitaji...labda awatembelee kina MKANDARA ughaibuni kubadilishana nao mawazo....kama uchumi unaruhusu..

Tanzanianjema
 
Tanzanianjema,
Mtu kama Zitto nitaitoa mimi ticket wala hana haja ya kuuliza mara mbili!.. wangu hawa Chadema damu damu - ManU au sio! heee heee heee!
 
Back
Top Bottom