The dark side of business

The dark side of business

Siku zote utajiri wa kiroho, kichawi, kishetani na kishirikina Husikika tu kwa waafrika maskini choka mbaya.

Kama kuna utajiri wa kishetani kwa nini usiutumie kwa nguvu zako zote, Uwazidi watu kama kina Mo Dewj, Bakhressa, Elon musk, Bill gates, warren Buffet, Jeff Bezos na matajiri wengine wakubwa.

Au huyo shetani na yeye pesa zake ni za kuunga unga?
kweli.

hata mtu mwenye imani za kishirikina anaweza kutajirika, juhudi binafsi na mambo yaliyo nje ya uwezo wake yakimuendea sawa anatajirika

shida mtu kama huyu atasambaza habari za uongo kuhusu utajiri na watu watamuamini, si wanaona hela anazo?

ila sio vibaya, si tunajua tayari kwamba utajiri haubagui imani/mitazamo ya kiroho?

kila mtu ashinde mechi zake
 
Siku zote utajiri wa kiroho, kichawi, kishetani na kishirikina Husikika tu kwa waafrika maskini choka mbaya.

Kama kuna utajiri wa kishetani kwa nini usiutumie kwa nguvu zako zote, Uwazidi watu kama kina Mo Dewj, Bakhressa, Elon musk, Bill gates, warren Buffet, Jeff Bezos na matajiri wengine wakubwa.

Au huyo shetani na yeye pesa zake ni za kuunga unga?
Hahahahahaha
 
Wangapi Wana mitaji na BIASHARA Zina wafia mikononi.

Mimi nacho jua BIASHARA nyingi Sana natolea mfano pharmaceutical industry companies za wahindi hapa bongo.

Wahindi wanatoa Sana kafara watachinja mambuzi na makondoo na kugawa NYAMA bureee watu weusi watagombania nyama zilizo somewa kisomo na manuizi

Inabidi uwe na mtaji lakini business Zinaendeshwa kwa invoices za siku 30's mpaka 90's days ziki mature ndio una pay..

BIASHARA ni MAARIFA na kua na taarifa nyingi za BIASHARA husika (information is power) Kuna Siri nyingi na nyingine huwezi ziona Wala kuambiwa Kuna nature of customers na mambo mengi mengi
sasa wanatajirika kwasababu ya imani/ibada zao au foul wanazojulikana kucheza kama kutolipa wafanyakazi na kutumia ile taswira kandamizi ya 'wahindi wana akili kuliko waafrika' kujizolea upendeleo kwa wanasiasa?

hayo yakiwa ni machache....
 
Tanzanian Dream huu muendelezo mboni km unatoka kwenye reli mkuu?

Tulichokitarajia na Heading inavyosoma na ulichoelezea mwanzo mboni kwenye muendelezo vinaanza kupingana pingana hivi, umeeleza in general summary kitu kilichotakiwa uelezee in detail unasema pale mwanzo Baba wa mshikaji wako alikua guru wa mambo fulani na wahindi wana mambo fulani meusi meusi ulipokuja kuendelea ukaficha white hujaelezea chochote na wala hujataka tujue chochote, simulizi inakosa utamu ndio maana nikakuuliza jamaa wamekuwahi PM usiwachome?

Sikia mkuu sisi hapa hatutaki hayo maelezo ya kwenye Ofisi yako madamu sijui kufukuza wafanyakazi na mengine tunataka urudi pale kwenye point ile ya mwanzo maana pale ndio umetuweka standby maana hii ya pili tunajua kilichofuata hukwenda kwa Mchungaji ulienda kwa Mganga, sasa acha hio rudi nyuma pale tuelezee kuhusu ulichoandika pale mwanzo kuhusu Mzee Fabi na Wahindi ulisema utaelezea mboni umeruka?
 
JamiiForums
Inaendelea................

Kuna uzi wangu niliutupia hapa unasema"experience ya miaka 15 ya kijiajiri(nadiriki kusema business is a sure way onto true riches)"kwenye huo uzi sikuelezea hiyo miaka 15 nilikuwa nafanya mishe gani, simply ilikuwa ni mishe ya vocha(wholesale)

Sasa baada ya kumaliza six,nilirudi mtaani na harakati za biashara zikaanza rasmi,kuna biashara ndogo nilianzisha lkn mawazo yangu yalikuwa ni mishe ya vocha za jumla, sema mtaji ulikuwa kipengele,so nikavutavuta siku mpk naingia chuo,ile biashara mdogo ilienda poa kimtindo,kuna dogo nilikuwa namwacha shop,mm naendelea na kitabu,nikapata boom(kwny intake yetu tulichelewa kupata,so tukapewa lumpsum ya mwaka mzima ilikuwa Kama 2.4M),chap nikaigeuza kuwa mtaji wa Biashara ya ndoto zangu,hii biashara ya vocha ni kama Biashara ya mafuta,faida yake ni ndogo sana lkn ukiuza mzigo mkubwa faida unaiona,kipindi hicho hii mishe ilikuwa 🔥 🔥 ila now days ni ya kawaida sana,kuuza mzigo wa milioni 5 kwa siku ilikuwa ni jambo la kawaida,nilichanganya shule na biashara kwasababu sikuwa na gutts tena za kusubiri mpk nimalize.
Chuo kilipoisha,
Kwa kweli sikuwa hata na chembe ya kutafuta ajira ijapokuwa matokeo yalikuwa mazuri,washkaji niliomaliza nao walikimbilia ajira,mimi nikaingia rasmi kwenye biashara ya vocha za jumla, wakati namaliza chuo mtaji ulikuwa kama 3M hv lkn ndani ya miezi sita mtaji ukafika 10M miezi sita mingine ikafika 20M,kwa waliofanya mishe hii backdays wanajua kama ukiuza mzigo wa milioni basi faida ni elfu 20,nilikuwa nauza mpk 8M kwa siku,kukunja laki hadi laki na nusu perday ilikuwa kawaida,dat time nikanunua kiwanja,nikajenga maflemu kama nane,then kwa nyuma niliplan kujenga apartments za kupangisha,nilinunua hiace(daladala)ili nitanue wigo,it was amazingl!coz I was just 23,nikazidi kusema "business is a quickest way onto riches" ila sikujua kuwa business is also a riskiest way onto riches,kwa ufupi ile side A ya biashara niliimaster ipasavyo,nilipiga kazi sana mpk watu wakahisi natumia ndumba,kwasababu ofisini watu walikuwa wanajaa,foleni kama nmb,hakika biashara na maisha kwa ujumla viliniendea poa,mtaani kila mtu alitamani afanye biashara kwakile alichokiona kinatokea kwangu,nilitengeneza jina kwa muda mfupi sana ghafla yakaanza mapicha picha,mara nikute damu kwny kiti ninachokalia pale ofisini,Mara hirizi,pesa zikawa zinapotea kimazingara,hua siamini uchawi lkn hiki kilichokuwa kinatokea ni uchawi bila chenga,nilifukuza wafanyakazi lkn haikusaidia(nilihisi wananipiga)nilipiga moyo konde lkn changamoto zilizidi to the extent nikaanza kuogopa biashara,kwa kweli nilibaki njia panda,ila Kuna wazo likanijia,juu ya nini cha kufanya......................
*****************************
Biashara zina ups and downs,niliona upande mmoja,sasa dunia inanionyesha upande wa pili,nini kitaendelea baada ya kupata wazo.............usikose
Jamaa washakufuata PM story ishapoteza utamu yaan wakishakufuata PM tu kwisha habari
 
Back
Top Bottom