'The Economist' Takes Gloves off on Kikwete...

'The Economist' Takes Gloves off on Kikwete...

Wa vijijini ndio worse off!

Nime generalize? Afadhali wa mjini wanashinda wanakunywa chai chapati kazini na kusoma "Sani," wa vijijini hata kazini hawaji, hawagusi kitu, kazi wao ni kunywa pombe, kukalia vigoda. Wanachojua ni kusimamia tohara za vi teenager vya kike na kushinda kwenye ngoma, hususan wanaume. Unasema walipigania uhuru? Angalia hawa waliopigania uhuru wanavyo walaani wazee wa vijijini walivyolegalega toka enzi za uhuru the '60s:

``Ukweli wenyewe ni kwamba vijijini kina mama hufanya sana kazi. Pengine hutimiza saa 12 au 14 kutwa. Hawana Jumapili, na hawana livu. Kina mama wa vijijini hufanya kazi zaidi kuliko mtu mwingine ye yote katika Tanzania.

Lakini kina baba wa vijijini (na baadhi ya kina mama wa mijini) nusu ya maisha yao ni livu. Nguvu hizi za mamilioni ya kina baba vijijini na maelfu ya kina mama wa mijini ambazo hivi sasa hazifanyi kazi yo yote ila kupiga soga, kucheza ngoma na kunywa pombe, ni hazina kubwa yenye manufaa zaidi kwa maendeeo ya nchi yetu kuliko hazina za mataifa matajiri`` TANU, ARUSHA, Januari 29, 1967

Kwa hiyo, si mjini si vijijini, wavivu, tusisafishane. Tena wa vijijini nusu yao nzima ni wafanyakazi wafu. Shughuli za mjini ni send off, shughuli za vijijini ni ngoma. Mdundiko na Sindimba na Rythm and Blues na Mayenu. Difference without distinction.

Mtanzania akikwambia "naenda kwenye shughuli" usidhani anaenda kupima kiwanja au shamba. Tafrija. "Kikao" ni get-together ya mikakati ya tafrija ya kipaimara cha mtoto. Akisema anaenda kwenye rehearsal usidhani ni practice ya kitu cha maana zaidi ya upambe wa tafrija. Kama sio ndoa ya mke wa pili basi ni Iddi pili. Maulidi haziishi. Kuna Pasaka mpaka Jumatatu. Na Jumatano za Majivu, na Ijumaa za Mateso. Na Ubarikio wa vinjiti.

Hizo ndizo "shughuli," ukisikia Mtanzania anakwambia anaenda kwenye "shughuli." Sote na Kikwete wetu ni slow.

Makabila 120+,watu milioni 40+,na wote wawe na tabia moja.Hivi inahitaji rocket science ku-prove how wrong your thesis is?

Kwa taarifa yako,huwezi kuijadili (and kuihukumu,for that matter ) jamii pasipo to take into consideration power relations ndani ya jamii husika.Kuna tofauti kati ya matokeo na chanzo,kupenda/kutaka na kulazimishwa,nk.Labda tusaidie basi kutueleza chanzo cha hiyo "slowness",uvivu,uzembe,majungu,umbea,nk vinavyokwanza maendeleo yetu nikiamini kwamba unakubaliana nami kuwa HAVIJATOKEA TU GHAFLA.Is it Genetics?Superstition?

Halafu ni vigumu kufikia mwafaka,au hata to agree to disagree,na mitizamo kama "...Tena wa vijijini nusu yao nzima ni wafanyakazi wafu...".That's not overgeneralization ila ni sheer abuse of anaytical skills.Vijiji gani unavyozungumzia?Gezauleole na Kazimzumbwi,au Msolwa Ujamaa?Of course,baadhi ya mababu na mabibi zetu huko vijijini ni wafu (kwa mapenzi ya Mungu na wakati mwingine lack of medical facilities) lakini kuwaita wafu katika uhai wao....anyway,ndio freedom of speech!
 
Last edited:
Maana sahihi zaidi ni hii hapa:



Sawa, umeelewa? Au nisema, umejielewa?

$2.4bil ni sawa na 40% ya $ 6 bil, ndio. Okay...

Whoa whoa whoa... hold it, stop stop!

Ilijitegemea kwa 100% vipi wakati umeshasema tegemezi la bajeti ni 40%-44% ? That's dopey. Takwimu zimekuonyesha kwamba tegemezi ni 44%, there is no need for conceptual heavy lifting here, tegemezi ni 44%, sasa imekuwaje tegemezi sifuri?

Fuzzy math!

"Tanzania ili-survive bila 2/3 (almost 67%) ya misaada iliyoahidiwa," iliahidiwa kiasi gani? 100% ni ngapi hapo?

Na umejueaje? Huwezi fanya hisabati za asilimia kama hujui au huwezi kujua asilimia 100% ni nini. Tunaongelea sehemu, sehemu ya nini?
Tunachojua ni kwamba $ 2.4 bil kati ya zilizoahidiwa hakitolewa. Hatujui ngapi zilitolewa. Asilimia zako unaziunga unga zisipohusika.

Sisi ni tegemezi karibia nusu ya bajeti yetu, tunaishi na kufa na misaada, period.

Wanaposema 44% ya budget ni pesa kutoka kwa wahisani, unafikiri wanasema bila kujua inatoka wapi? The pledged funds were 44 percent of $6 billions. Na karibia 44% [$2.4 billions] ya $6 billions haikutolewa na walioahidi. Kama takribani pesa zote zilizoahidiwa hazikutolewa, hii ina maana kuwa utegemezi ni asilimia takribani sifuri.

The good thing ni kwamba, angalau sasa unakubali kuwa $2.4 billion kati ya zilizoahidiwa hazikutolewa [na si kwamba zilitolewa halafu hazikutumika]. Unachotakiwa kuelewa sasa ni kuwa, kiasi kilichoahidiwa ni 44% ya $6 billion. Then, we will be on the same page.

"Sisi ni tegemezi karibia nusu ya bajeti yetu, tunaishi na kufa na misaada, period."

Yes. Sisi ni tegemezi karibia nusu ya bajeti [44%], at least on papers. Ukweli ni kwamba, hii misaada haipokelewi na Serikali. If I am wrong, then The Economist is also wrong. And since this debate stems from the article by The Economist , you will also be wrong.
 
Last edited:
Hiyo sababu ya saba, Watanzania, ndio kiini cha tatizo. Si CCM, si Kikwete, si serikali.

ECONOMIST wametutandika fimbo wote, kwamba Watanzania ni watu slow, tusio na mwendo wa kwenda mbele, hatuna "dynamism." Hatuna ujuzi, tumezidiwa na Wakenya na Waganda, tunawaogopa. Tuko slow wanasema mpaka tumeshindwa hata kutumia hela tulizoomba, $ 2.4bil. Ukweli si kejeli, ashakum si matusi.

Kikwete sio dawa, sio ugonjwa. Miundombinu yetu ya reli na bandari imechoka mbaya, "rickety," wanasema. Reli, bandari, ndege, barabara, magari ya usafirishaji yalianza kuchoka toka enzi Nuhu anaibuka kutoka kwenye Gharika ya Kwanza ya Dunia. Kikwete kakikuta hiki kifafa cha miundombinu, na hana dawa.

Wananchi wa Tanzania, sio Kikwete, wote tumejaa uvivu, uchovu, ukilaza, uzembe wa mawazo na kazi. Jumatatu unaingia saa sita, jana ulilala msibani ukihani marehemu Mzee Dau, baba wa shangazi yake mke mdogo wa jirani yako. Jummanne inabidi uombe udhuru kumpeleka Pili hospitali. Jumatano unaenda kwenye mazishi, haupo kazini nusu siku. Alhamisi unaondoka mapema kuwahi lifti ya Mama Tarimo maana ukiikosa hii basi usafiri jioni udhia mtupu, isitoshe yabidi uwahi kwenye send off. Ijumaa unatakiwa harusini, ulitoa mchango. Wiki ijayo huna udhuru, utajitahidi kutulia kazini unasoma "Acha Umbea" na "Alasiri," ukichoka unachomoka kidogo kutafuta supu ya utumbo, ukirudi ni kusogoa na kunywa chai na maandazi. Nusu ya maisha yako ya kazi ni livu, na mshahara utapata wote. Sio wewe tu utapata mshahara mzima, na marehemu Mzee Dau nae atalipwa.

Sasa kama hapo tatizo ni Kikwete basi waandishi wa makala hiyo wametutusi wote maana wamesema Mrisho atachaguliwa tena, wameongea kwa ukomo wa uhakika, atachaguliwa tena, na itakuwa ni kwa kishindo cha mmomonyoko wa ardhi ya uchaguzi, landslide. Kwa nini, kwa sababu Chama cha Mapinduzi kimewachota watu akili, wanasema kimetukuka katika longolongo dufu, "ponderous propaganda."

Na wametuasa kusikiliza wenyenchi ndani ya chama kutaka kuwapeleka tena wananchi kwenye Ujamaa kwa kigezo cha mporomoko wa ubepari duniani. Wachambuzi wa The Econonimist wanasema genda ulole.

umeona Barack Obama aliamuru ile kampuni ya bima kama sikosei warudishe bonases!! Kwahiyo bado kikwete anastahili lawama, kashindwa kufanya kile watu walicho kitegemea.
 
Lakini jamani hayo maisha bora ya wakenya yako wapi?? Katika 40m ya wakenya ni wangapi wanamaisha bora zaidi kutuzidi?? Kama ni usharp.... na ujambazi wa kutumia silaha nzito ni usharp??

Ni kweli serikali yetu ina matatizo hasa ya kuyumbishwa na mafisadi, ukiangalia walivyo uza TIPPER, mikataba ya madini, TICTS, ATC, TRC, n.k. ni ufisadi tu na kama tukipata rais kama magufuli mambo yatabadirika!!

Si kweli kwamba watanzania wote ni wavivu, mfumo wetu wa kazi katika ofisi nyingi ndo mbovu. Mambo mengi yana endeshwa kisiasa. Angalia wananchi na wasomi mbali mbali walivyo pinga kubinafsishwa kwa ATC, si ni sisi watanzania tulipinga lakini kwa kuwa rais mkapa alikuwa na azima yake ya ufisadi, alitumia mabavu akauza na je leo iko wapi?? Hao economist mbona hawa kulisemea hilo?? nani asiyejua kwamba nao ni wakoloni tu! World Bank na IMF walishabikia, uzeni benki, uzeni reli, uzeni ATC,..leo wako wapi na sera zao??

Watanzania tunacho hitaji sasa hivi ni rais na waziri mkuu kama magufuli (kama hata badirika) na enzi ya sokoine au mrema.
 
Wakuu,Askofu Kishoka na mwandishi wa 'ze uchumi' nimewapata.Ninachokiona hapa ni cynisism,kwamba hatuwezi hiki hatuwezi kile,ya kweli hayo? Nakataa,we can.Mambo ya msingi ya kufanya yapo na tukiamua tunaweza. Kwa mfano badala ya kung'ang'na eti mpaka tupate bilioni mia moja ndo tuanze mradi wa kujenga kilomita 100 za barabara kwa nini tusikusanye bilioni kumi tukajenga kilomita 10 na kila mwaka tukaendelea hivyo hivyo kidogo kidogo? baada ya miaka kumi hiyo barabara si itakuwa imetoka Mwanza na kufika Shinyanga na huku tunafanya matengenezo kwa kutumia vifaa vyetu wenyewe? jamani waswahili si ndivyo tunavyojenga nyumba zetu? vivyo hivyo kwa madarasa,zahanati,miundo mbinu ya maji n.k.We are not that poor,ni mipango tu.Kwa nini kwa mfano tusiseme enough is enough hatutaki kuagiza mchele tena toka nje hivyo tuamue kulivaa bonde la mtoto Rufiji kwa tukajenga dams na irrigation system na kulikata bonde katika blocks kisha watu waka lease na kulima mpunga?Yote yanawezekana ni mipango tu,lakini above all tujenge positivity na tuache kuwa watu wa kulalamika tuuuuuu!Sincerely speaking change comes from the people,tusiwategemee sana wanasiasa(itikadi zao notwithstanding),tujibidiishe wenyewe,tutafute,tutapata na nchi itaendelea.Kamwe tusijione wanyonge ambao hatuwezi ,kumbuka pamoja na ulaini wake maji hupasua miamba!

Sahihi kabisa nimekupata, tukiamua inawezekana. umetolea mfano wa kama tunataka kujenga barabara ya km 100 na inahitaji bil.200 kwa nini tusijenga hado hado km 10 kila mwaka?? Kawambwa uko wapi?? wewe ni mhandisi au unatuambia kwamba kile kibanda chako cha mbezi ulijenga kwa mkupuo?? mbona ulijenga aste aste?? hivyo hivyo kwenye miradi ya serikali, tutafika. Napinga hoja eti watanzania ni wazembe, niko kwenye ki-nchi fulani hapa watu ni wazembe mpaka basi lakini nchi inaendelea, issue hapa ni mipango na kuondoa ufisadi.
 
Sawa,sie wavivu,wazembe,watu wa majungu,nk according to Dilunga et al.Hawa je:

The Speaker's scapegoat: Official who signed off MPs' expenses didn't even have accountancy qualification
By Simon Walters
Last updated at 2:48 AM on 10th May 2009

The row over MPs' expenses intensified last night as it was revealed that the parliamentary finance chief who signs off their claims had no formal accountancy skills - and that he feared he would be sacked when he warned the Commons Speaker the system was being abused.
Andrew Walker, who runs the Commons Fees Office responsible for MPs' wages and expenses, told Speaker Michael Martin more than five years ago that he must act to curb excessive claims.
But Westminster sources say the Speaker told him not to meddle, and 'punished' him by refusing to speak to him for weeks at a time.


article-1179937-04DFDB6B000005DC-703_224x304.jpg

article-1179937-04DFC801000005DC-682_224x304.jpg




Andrew Walker (left) warned Speaker Michael Martin more than five years ago that he must act to curb excessive claims
It is understood that Mr Walker felt he could be dismissed from his £125,000-a-year job as director general of resources at the Commons after issuing the warning.
Now friends say he has been made a 'scapegoat' by MPs who have justified scandalous expense claims on the grounds that Mr Walker approved them.



The disclosures came as:
  • Labour's support plummeted to 23 per cent - its lowest since polling began.
  • Cabinet Minister Hazel Blears was accused of avoiding £18,000 of capital gains tax, having persuaded the taxman a flat she sold was her main home, while claiming parliamentary expenses on it as her second home.
  • The Mail on Sunday established that Andrew Walker's boss Dr Malcolm Jack has homes in London, Portugal and South Africa as well as a grace-and-favour mansion in Westminster.
The properties owned by Dr Jack, who earns £150,000 a year as Commons clerk and chief executive, are worth more than £1.8million. His £2.8million grace-and-favour mansion in Parliament Street recently underwent a taxpayer-funded £100,000 refurbishment, including a £39,000 kitchen.
The upgrade sparked fury from some MPs.


More...

Dr Jack, who is in overall charge of parliamentary accounting, has called in police to investigate the leak of MPs' expenses, prompting claims that it was intended as a distraction.

The 62-year-old, who lives with partner Robert Borsje, is close to Mr Martin and remained loyal during the controversy over the Speaker's own expenses claims. He and Mr Walker were given more power over expenses following a reorganisation of Commons officials ordered by Mr Martin.

Astonishingly, Mr Walker was put in charge of MPs' expenses even though he was not qualified to hold the post. He was sent to college to take a £15,000 course in business studies, at taxpayers' expense, while in his job.
Lifelong civil servant Mr Walker became finance and administration director at the Commons in 1997 after a low-profile role as assistant director of human resources at the Inland Revenue.

But his degree in Ancient Near Eastern Studies from Birmingham University was of little use when faced with the complex financial matters of the Commons Fees Office.
One source said: 'Andrew did his best to keep control of things but it was an impossible job, and he was not really equipped to do it. He knew there were things going on that shouldn't be and drew them to the Speaker's attention.
'The Speaker didn't want to know. His own expenses were coming under scrutiny and the last thing he wanted to do was draw attention to the issue. Andrew was told to keep his nose out and to turn a Nelsonian blind eye.
'The Speaker would go for ages without speaking to him, his way of "punishing" Andrew. It was a disgrace. Now MPs are blaming him for the trouble they are in by saying he approved their expenses. He has every right to be angry.'
Another source said: 'A while back it looked as if Andrew might lose his job and you can't blame him for thinking that he might as well keep his head down. Why should he sacrifice his career for the sake of others?'
Mr Walker's return to favour with the Speaker coincided with Mr Martin's surprise choice of Dr Jack - who is also a successful writer who spends much of the parliamentary breaks at his homes in Portugal and South Africa - as Commons clerk and chief executive.
The Speaker ordered a shake-up after Serjeant-At-Arms Peter Grant Peterkin was effectively sacked in 2007 for querying Mr Martin's expenses.
In the reorganisation, Dr Jack and Mr Walker - who was promoted to his current job - were given more power over staff as well as MPs' pay and expenses. Critics said the Speaker had surrounded himself with cronies.
Instead of selecting someone with a financial background, the Speaker gave Mr Walker the go-ahead to study for a Master of Business Administration degree at Warwick University, approving the £5,000-a-year fees and granting him time off from the Commons for his studies.
Mr Walker, who is 55 and married with three children, lives in Berkhamsted, Hertfordshire. He was unavailable for comment, while the Speaker's office declined to comment.
 
Sawa,sie wavivu,wazembe,watu wa majungu,nk according to Dilunga et al.Hawa je:




Ndo maana mimi nasema TZ bado we can still do better kama tukiamua kila mtu kwa nafasi yake tubadilike. Kama unaona bosi analeta mambo ya siasa ni kumpasha live na kazi inaendelea.

Hasa upande wa kuendeleza miradi ya maendeleo, tubajeti kulingana na uwezo na kama mradi unagharimu pesa nyingi basi tuutekeleze kwa awamu. Niliuliza kwa ndg. kawambwa mbona yeye alijenga kakibanda kake pale mbezi kwa awamu?? mbona kwenye miradi ya serilaki anataka aibuke na bil. 200?? kwa nini tusijenge kwa awamu (km 10 kwa mwaka?)
 
1. Mlalahoi, UK transparency ndo imefichua hayo madudu, na vema wameadmit watayafanyia kazi! Taabu ya Madudu ya Viongozi Tz ni usiri, na hata Slaa alipozungumzia maslahi ya wenzake, wao walimzomea!

2. JK wakati wa IMF meeting dar, aliulizwa na Bob kwa nini anasema anawajua wakwepa kodi Port ya dar na hawachukulii hatua ..kama raisi? Je JK ni mwoga naye? Ndo Jk alijiumauma tu.. na kutabasamu tu..hakuwa na jibu!
 
What a breathe of fresh air on the Forum, thank you mkuu, you always are a calm hand in the midst of calamity. Badala ya kupoteza muda kwa kushabikia katika threads zingine naomba nichangie hapa:
Economist ni wanafiki sana, nadhani ukipiga search mwaka 2006 waliandika article ambapo walimsifia JK ya kuwa ni John F Kennedy of Africa!!!! I am not joking! That does not mean that I dsmiss this article out of hand in fact I have continued to read the Economist ever since. However we have to be cautious and say haijashushwa kutoka Mungu, so we should always weigh what and why they write it.
Mimi naamini ya kuwa Western world has ended its love affair with the 'young and dynamic' leader of Tanzania and they finally see him for what he is - an ineffective leader. But this is not about him, we have to look at some of the very important points raised in particular the competetiveness of Tanzania within the region.
Another alarming issue is that Aid or donor money was not disbursed! Why and what happened. Mi naamini kuwa hata hao donors inabidi tuwabane na kuwalazimisha wachapishe katika magazeti wametoa misaada kiasi gani kwa nchi yetu ili tuweze kufuatilia pesa zetu maana any aid is given to the people of Tanzania na siyo serikali na watendaji wake.
I also think it is high time for donors to consider not giving money to the govenrment. They should disperse funds with the private sector, na hizi NGOs pia haifai, inatakiwa iwe Foundations that are audited na zipite some form of test that qualifies them to handle money on behalf of the Tanzanian people.
All in all I think that the analysis is fair although it is still trying to paint a rosy picture somewhatlakini at least there is acknowledgement that there is trouble and even bigger problems ahead.

susuviri thanks for the good piece. Inabidi vilevile tuelewe kuwa "an efficient government" according to wazungu ni ile ambayo ina wafanikishia "looting of resources". Kenya haijawahi kukata mifija ya kinyonyaji ya wazungu tangu wapate uhuru, ndio maana, kila siku wanaisifia, na hawawezi kuibeza kamwe. After having said that, serikali ya kikwete ni kweli ni bomu sana. Kwanza sio serikali bali genge la wahumi, majangali na majambazi.
 
Wakuu zangu msilumbane kwa kitu kilichozungumzwa nusu nusu hapa.. Mnapozungumzia hizo 2.4/m ambazo hazikutumika iwe hazijatolewa au zimetolewa hakuna mahala economist wamesema hizo fedha ni asilimia 40 ya Budget ya mwaka unaohusika.. Yawezekana kabisa kuwa hizi fedha ni limbikizo toka mwaka 2006 au 2007 au 2008 kwani mara nyingi fedha hizi hutolewa/huahidiwa ktk jumla ya miaka fulani inaweza kuwa mitano, kumi au ishirini..

Kwa hiyo sioni sababu kabisa ya kuweka maneno zaidi ktk tafsiri ya maneno haya:- Tanzania is not even spending all the aid it is given. Last year, $2.4 billion of pledged funds were not disbursed. Na yawezekana kabisa hili neno disbursed tunalitafsiri vibaya kulingana na sentesi hii kwani yawezekana hiyo pay off inayozungumziwa hapa ni toka serikalini kwenda ktk Ujenzi wa nchi na sio kutoka kwa Wahisani...Nje ya hapo sentesi nzima ya maelezo ya economist hayaeleweki kabisa..
La muhimu kwetu ni kufahamu kwamba The economist wamezungumza kitu kile ambacho wengi hapa JF huwa hawaamini wanataka ushahidi na nadhalika toka kwa wananchi ambao maisha yao wenyewe ndio ushahidi unaotafutwa..
 
Tatizo letu ni kuwa tunapenda mno majibu mepesi. Majibu ambayo kila wakati tunaonyeshwa kuwa sisi ni victims! Majibu ambayo yanawanyooshea vidole wengine kwa matatizo yetu na sio sisi.

Leo tunawatolea macho watanzania wenye asili ya kiasia watano ati wao ndio chimbuko la ufisadi! Conveniently tunasahau kuwa Rais wetu, waziri wetu wa fedha, gavana wetu na bila shaka hadi tarishi anaebeba mafaili katika ofisi zote hizo ni mmatumbi. Tunasahau kuwa waziri Mkuu aliyepita, Waziri wa nishati na madini, Katibu Mkuu wake, Attorney General, mawakili na wataalamu wengine katika mawizara mengine na mashirika ya umma ni wamatumbi wenzetu. Lakini tunamuandama mtanzania mwenzetu tuliyetofautiana nae rangi kana kwake yeye ndiye aliyetushinikiza kuingia kwenye mkenge wa Richmond!

Leo Attorney General aliyepita na Gavana wa benki aliyepita wameonekana kuwa na vijisenti huko nje ambavyo inasemekana kuwa ni sehemu za mgao wao kutokana na mauzo ya rada! Lakini hapana, sisi tunamuona tena mtanzania mwenye asili ya asia kuwa ndio mhusika mkuu!

Leo wote tunajua kuwa waziri wetu wa madini alisaini miataba mibovu hotelini KWAKE! Mikataba ambayo ilikataliwa na wataalam wake. Lakini leo tunajaza thread tukiwasema hao wageni kuwa wao dio wanaotumalizia urithi wetu.

Leo tunalalamikia mgao wetu katika madini lakini hatujiulizi kuhusu athari ya matumizi mabaya ya mercury yanayofanywa na hao ndugu zetu tunaowaita wachimbaji wadogo wadogo!

Leo tunalilia urithi wetu wakati ni sisi wenyewe tunaotoa vibali kujenga mahoteli, viwanja vya ndege kwenye mbuga zetu. Tunang'ang'ania kujenga kiwanda katika mazalio pekee ya aina fulani ya flamingo DUNIANI. Tunatoa vibali kuubomoa mji wetu na kujenga maghorofa ambayo hatuna infrastructure ya kuhudumia!

Leo, wakati wenzetu wote wanabana mikanda, sisi tumo mbioni kutumia mabilioni kwa mradi hewa wa vitambulisho.

Leo wakati watoto wetu wanakufa kwa utapia mlo, tuliowachagua wanadai mamilioni tunayowalipa hayatoshi! Badala ya kujilinganisha na huyo wanaemwakilisha, waheshimiwa hawa wanajilinganisha na wezi wenzao wa taifa jirani! Na mbaya zaidi, mwakani tutawarudisha tena bungeni kuendeleza libeneke!

Hapana, ndugu zangu. Mpaka hapo tutakapoweza kuangaliana wenyewe na kudai majibu yasiyo na kificho, majibu ambayo yatatueleza kinaga ubaga matatizo yetu sisi raia wa nchi hii bila kujali rangi, jinsia au kabila, hatutatoka hapa tulipo!

Amandla.......
 
Last edited:
The Economist wamemaliza kila kitu. Matatizo yanayotutatiza yanajulikana, njia za kuyatatua zipo, kwa nini hayatatuliwi ? Hili gazeti ni very reliable on economic issues.Jirani zetu wakiandikwa possitively on economic issues inabidi tushtuke. What is wrong with Tanzania?

" Matatizo yanayotutatiza yanajulikana, njia za kuyatatua zipo, kwa nini hayatatuliwi ? "

ni kwasababu tumekosa agent of change ambaye/ambao watatumia njia hizo kutatua matatizo!
 
Tatizo letu ni kuwa tunapenda mno majibu mepesi. Majibu ambayo kila wakati tunaonyeshwa kuwa sisi ni victims! Majibu ambayo yanawanyooshea vidole wengine kwa matatizo yetu na sio sisi.

Leo tunawatolea macho watanzania wenye asili ya kiasia watano ati wao ndio chimbuko la ufisadi! Conveniently tunasahau kuwa Rais wetu, waziri wetu wa fedha, gavana wetu na bila shaka hadi tarishi anaebeba mafaili katika ofisi zote hizo ni mmatumbi. Tunasahau kuwa waziri Mkuu aliyepita, Waziri wa nishati na madini, Katibu Mkuu wake, Attorney General, mawakili na wataalamu wengine katika mawizara mengine na mashirika ya umma ni wamatumbi wenzetu. Lakini tunamuandama mtanzania mwenzetu tuliyetofautiana nae rangi kana kwake yeye ndiye aliyetushinikiza kuingia kwenye mkenge wa Richmond!

Leo Attorney General aliyepita na Gavana wa benki aliyepita wameonekana kuwa na vijisenti huko nje ambavyo inasemekana kuwa ni sehemu za mgao wao kutokana na mauzo ya rada! Lakini hapana, sisi tunamuona tena mtanzania mwenye asili ya asia kuwa ndio mhusika mkuu!

Leo wote tunajua kuwa waziri wetu wa madini alisaini miataba mibovu hotelini KWAKE! Mikataba ambayo ilikataliwa na wataalam wake. Lakini leo tunajaza thread tukiwasema hao wageni kuwa wao dio wanaotumalizia urithi wetu.

Leo tunalalamikia mgao wetu katika madini lakini hatujiulizi kuhusu athari ya matumizi mabaya ya mercury yanayofanywa na hao ndugu zetu tunaowaita wachimbaji wadogo wadogo!

Leo tunalilia urithi wetu wakati ni sisi wenyewe tunaotoa vibali kujenga mahoteli, viwanja vya ndege kwenye mbuga zetu. Tunang'ang'ania kujenga kiwanda katika mazalio pekee ya aina fulani ya flamingo DUNIANI. Tunatoa vibali kuubomoa mji wetu na kujenga maghorofa ambayo hatuna infrastructure ya kuhudumia!

Leo, wakati wenzetu wote wanabana mikanda, sisi tumo mbioni kutumia mabilioni kwa mradi hewa wa vitambulisho.

Leo wakati watoto wetu wanakufa kwa utapia mlo, tuliowachagua wanadai mamilioni tunayowalipa hayatoshi! Badala ya kujilinganisha na huyo wanaemwakilisha, waheshimiwa hawa wanajilinganisha na wezi wenzao wa taifa jirani! Na mbaya zaidi, mwakani tutawarudisha tena bungeni kuendeleza libeneke!

Hapana, ndugu zangu. Mpaka hapo tutakapoweza kuangaliana wenyewe na kudai majibu yasiyo na kificho, majibu ambayo yatatueleza kinaga ubaga matatizo yetu sisi raia wa nchi hii bila kujali rangi, jinsia au kabila, hatutatoka hapa tulipo!

Amandla.......

Fundi Mchundo:

Unayosema ni kweli lakini punguza kutumia kabila la wamatumbi katika mifano yako.

Tanzania ina makabila zaidi 120. Zinapofanyika shughuli za mafanikio Rungwe, mmatumbi hatajwi kama na yeye anaweza kufanya mafanikio hayo.

Yanapotokea makosa na mhehe au mzigua, mmatumbi anakuwa wa kutolewa mfano.

Hilo ni kabila la watu na si vizuri kuwa-victimize kwa makosa yanayofanywa na watu wengine ambao wamesoma na ambao walishasahau mila na desturi za makabila yao.
 
Rev. Kishoka:

Mimi sipo Tanzania. Lakini nikichukua posts za JF kama public sentiment ya watanzania, maoni yangu yangekuwa sawa na mwandishi wa Economist kuhusu JK.

Kuna uwezekano mkubwa mwandishi ali-compile maoni yaliopo JF au watu wenye fikra za wana JF na kuyatolea article kwenye Economist.

Swali je watanzania ambao wanapiga kura na kumchagua rais wana-sentiment gani kuhusu JK?
 
Rev. Kishoka:

Mimi sipo Tanzania. Lakini nikichukua posts za JF kama public sentiment ya watanzania, maoni yangu yangekuwa sawa na mwandishi wa Economist kuhusu JK.

Kuna uwezekano mkubwa mwandishi ali-compile maoni yaliopo JF au watu wenye fikra za wana JF na kuyatolea article kwenye Economist.

Swali je watanzania ambao wanapiga kura na kumchagua rais wana-sentiment gani kuhusu JK?
Mkuu watanzania gani tena si ndio wenye mawazo kama haya yetu tu yaani mawazo ya kimapinduzi zaidi na kukataa rasilimali za hii nchi kutumika ovyo
 
Fundi Mchundo:

Unayosema ni kweli lakini punguza kutumia kabila la wamatumbi katika mifano yako.

Tanzania ina makabila zaidi 120. Zinapofanyika shughuli za mafanikio Rungwe, mmatumbi hatajwi kama na yeye anaweza kufanya mafanikio hayo.

Yanapotokea makosa na mhehe au mzigua, mmatumbi anakuwa wa kutolewa mfano.

Hilo ni kabila la watu na si vizuri kuwa-victimize kwa makosa yanayofanywa na watu wengine ambao wamesoma na ambao walishasahau mila na desturi za makabila yao.

Nawaomba msamaha wamatumbi wenzangu wote kwa kutumia kabila letu kama mfano wa watanzania weusi. Tofauti na anavyodhani Zakumi, matumizi yangu ya kabila letu si victimisation bali kufanya suala la uasili kuwa karibu zaidi. Matumizi yangu ya neno mmatumbizi hayahusiani na kabila la mmatumbi. Katika mifano yangu mtu yeyote ambae ni mweusi Tanzania ni mmatumbi! Sasa badala ya neno mmatumbi sijui Mkuu Zakumi ungependekeza niwatofautishe watanzania weusi na wale wasio weusi? Neno mtanzania mweusi linakubalika?

Amandla.....
 
Nawaomba msamaha wamatumbi wenzangu wote kwa kutumia kabila letu kama mfano wa watanzania weusi. Tofauti na anavyodhani Zakumi, matumizi yangu ya kabila letu si victimisation bali kufanya suala la uasili kuwa karibu zaidi. Matumizi yangu ya neno mmatumbizi hayahusiani na kabila la mmatumbi. Katika mifano yangu mtu yeyote ambae ni mweusi Tanzania ni mmatumbi! Sasa badala ya neno mmatumbi sijui Mkuu Zakumi ungependekeza niwatofautishe watanzania weusi na wale wasio weusi? Neno mtanzania mweusi linakubalika?

Amandla.....

Vipi mijitu myeusi?
 
Nawaomba msamaha wamatumbi wenzangu wote kwa kutumia kabila letu kama mfano wa watanzania weusi. Tofauti na anavyodhani Zakumi, matumizi yangu ya kabila letu si victimisation bali kufanya suala la uasili kuwa karibu zaidi. Matumizi yangu ya neno mmatumbizi hayahusiani na kabila la mmatumbi. Katika mifano yangu mtu yeyote ambae ni mweusi Tanzania ni mmatumbi! Sasa badala ya neno mmatumbi sijui Mkuu Zakumi ungependekeza niwatofautishe watanzania weusi na wale wasio weusi? Neno mtanzania mweusi linakubalika?

Amandla.....

Call a spade a spade.
 
Back
Top Bottom