The Emperor Jean-Bedel Bokassa

The Emperor Jean-Bedel Bokassa

Watu walikua wanaufanya Udikteta kweli kweli[emoji23][emoji23][emoji23][emoji16].
Nchi inageuzwa mtaji... yani ukipindua ukipata madaraka tu. ushakua Dangote[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23].

Na hayo ni kwa uchache tu,utayakuta mengine mazito tu
 
Haya ni mabaki ya swimming pool inavyoonekana leo aliyojenga kijijini nyumbani alikozaliwa... imejaa maji ya mvua yameota mpaka ukurutu wa kijani kwa sababu leo hakuna mfanyakazi wa kusafisha hiyo swimming pool.

Hivi vyeo vinapita tu jamani...

images


Source: Daily Mail

Inside the crumbling palaces of Africa’s dictators | Daily Mail Online
hiyo swimming imeota chakula cha kuku mifugo! azolla dah!
 
Watoto wake wapo wapi hata kutelekeza mali za babayo. Kwa nini hayo majumba wasiyasimamie
 
Maisha haya ni mafupi sana usipoyafaidi yenyewe hua na tabia ya kutufaidi.....
Well done Bokasa umepitia ugumu wa uyatima kisha ukaponda raha sana, ukapiga kila papa uliyotaka then ukazeeka katika umasikini tena, ila raha na tabu za dunia umezifaidi kenge wewe kula tano [emoji109][emoji109]
alizeekaje ktk umaskin wakati alikuwa tajiri?
 
Mleta mada hukumalizia kuwa alifikisi nchi mpaka ikakosa pesa ya kujiendesha. Bokassa aliomba msaada wa hela kwa Gadafi, masharti aliyopewa ilikuwa kubadili dini.
Rais alislimu Libya, alirudi nchini kwake anaitwa Mohamed Saladine Bokassa

Alirudia u Katoliki kabla mauti hayajamfika
hahahaha hii ilikuwa noma
cc:niyombare
 
afika kwakweli imelaaniwa
huyu bokasa aliamuru Lori LA jeshi likanyage watoto wa shule waliogoma kutoka darasan kwenda barabaran kumshangaa
Aliwaweka ndani wanafunzi kwa kukataa kununua uniforms zilizoshonwa na mke wake
 
Si ajabu kumkuta peponi, maana njia za Mungu si njia za mwanadamu (Mungu si Athuman). Pengine alitubu kweli na kuiamini injili kabla ya kifo chake
watu wengine wamejipa kazi za Allah
 
Miongoni mwa watawala waliokuwa na visa na vituko vingi katika bara hili la Afrika ni mfalme wa kujipachika wa Afrika ya Kati, Jean-Bedel Bokassa.

Jean Bedel Bokassa akiwa anaongoza nchi masikini kabisa duniani, alifanya sherehe ya kujisimika kama mfalme mwaka 1977 kwa kutumia kiasi cha sawa na shilingi bilioni 32 za Kitanzania za wakati huu. Lile taji lake la Ufalme peke yake liligharimu kiasi cha shilingi bilioni tatu!.

Jean Bedel Bokassa alikuwa dikteta wa Jamuhuri ya Afrika ya Kati.
Alikuwa na wake kumi na saba (17) na watoto hamsini (50).

Alifanywa yatima wafaransa walipomuua baba yake akiwa na miaka sita (6) baada ya baba yake kufa mama yake naye alijiua.

Alipata kupigana vita ya pili ya dunia chini ya Wafaransa. Baadaye alikuja kumpindua rais aliyekuwa ndugu yake mwaka 1965. Alijipa cheo cha field marshall na kutengeneza uniform maalumu sababu ya wingi wa medals alizojipa. Akienda kutembelea nchi alikuwa anagawa almasi.

Alikuwa ana majumba zaidi ya sita Ufaransa. Pia alikuwa na majumba mengine nchi mwake, katika majumba yake mengine yaliyokuwa nchini mwake, Jumba lake mojawapo lilikuwa na bwawa la mamba na simba wa kufugwa, alitumia mamba hao na simba kuulia wapinzani wake.

Wake zake walikuwa Mchina, Mjerumani, Msweden, Mtunisia na Mromania. Aliwaweka nyumba tofauti na alikuwa akiwatembelea kila siku na kusababisha foleni kubwa barabarani kutoka na wingi wa safari hizo huku akiambatana na misafara.

Alipinduliwa na wafaransa baada ya kuua wanafunzi waliokua wanaandamana. Alifungia wanafunzi 30 kwenye jela ya mtu mmoja.

Walipompindua kwenye friji yake walikuta nyama za watu.

Mwishoni mwa maisha yake alitumia kusoma bible na huku akiwa anajiita mtume wa yesu. Hatimae alifariki mnamo mwaka 1996 kutokana na ugonjwa wa moyo.
Kwa kuongeza
Alikua na kitanda cha dhahabu na almasi tupu no mbao

Lakini alikufa masikini wa kutupwa
 
Back
Top Bottom