The Guardian: Kuhusu kushuka kwa idadi ya watu wa Nchi ya Korea Kusini

The Guardian: Kuhusu kushuka kwa idadi ya watu wa Nchi ya Korea Kusini

Freiston

JF-Expert Member
Joined
Oct 25, 2020
Posts
302
Reaction score
340
Katika pitapita yangu mitandaoni, nikakutana na taarifa hii kwenye gazeti maarufu la THE GUARDIAN yenye kichwa cha habari: South Korea's population falls for first time in its history | South Korea | The Guardian ambayo inaongelea kuhusu kushuka kwa idadi ya watu nchini Korea ya Kusini kwa mara ya kwanza katika historia.

Taarifa hii inasema mpaka kufikia mwaka 2067, asilimia 46 ya wakorea watakuwa watu wa umri wa zaidi ya miaka 64 na idadi ya watu kushuka kutoka 51 milioni mpaka 39 milioni endapo hali ya sasa inachagiza kushuka kwa idadi yao itaendelea kuwa hivyo. Na kwa wakati huo huo idadi ya watu kwa bara Africa kuongezeka na umri wa wastani kuwa ni miaka 25 (sikumbuki chanzo cha taarifa hii nilikiona wapi maana sikitilia maanani mpaka nilipoona taarifa ya SK). Sasa tatizo hili sio kwa taifa hilo tu bali ni kwa mataifa mengi ya Ulaya kama Ufaransa.

Sasa mimi kama kijana mtanzania, nikaona hiyo ni fursa kwetu na kwa kizazi chetu katika mitizamo miwili.
1. Mataifa mengi ya Ulaya na Asia yanazidi kupoteza nguvukazi na hivyo kuwa tegemezi kwa Africa katika masuala mengi hasa mazao ya chakula.

USHAURI:

Naiomba serikali na mashirika binafsi itoe mafunzo kwa vijana na watoto wetu tangu elimu ya awali mbinu mpya na za kisasa za kilimo ili uzalishaji wa mazao mbalimbali kuongezeka kwa matumizi ya ndani na nje ya nchi hasa katika mazao ya kimkakati.

Kuwe na mashamba ya serikali/watu binafsi watakaowezeshwa na serikali au taasisi binafsi ambayo yaweza kutoa internship kwa vijana kwenda kujifunza kilimo kwa vitendo na baada ya hapo vijana kuunganisha kimakundi na kuanzisha miradi yao binafsi kwa maslahi ya Taifa. Mkazo ukiwa zaidi katika kushikilia mnyororo mzima wa kuongeza thamani ili bidhaa iende kwa mlaji moja kwa moja.

2. Nguvukazi. Vijana wengi wa mataifa ya Africa wanatoka katika nchi zao na kwenda kufanya kazi kwenye mataifa ya Ulaya, Asia na Marekani kisha fedha wanazopata hutuma nyumbani. Fursa hii bado haijachangamkiwa sana na watanzania wengi labda ni kutoka na Taifa kutokuwa na mipango thabiti ya kutafuta fedha za kigeni kupitia diaspora au ipo lakini watendaji bado wamelala mpaka baba aseme kama kawaida yao ya kupenda kusukumwa au labda mimi sina uelewa sana juu ya kinachoendelea.

Yote kwa yote, ninaishauri serikali yetu iweke mipango ya muda mfupi na muda mrefu katika kutengeneza nguvukazi itakayoenda kuvuna fedha hizi za kigeni katika mataifa ambayo nguvu kazi yao inapungua kwa kasi. Ni muhimu vijana wakafuzwa maadili mema ya nchi yetu na uzalendo kwa taifa letu ili watakapokuwa huko waendelee kuwa watiifu kwa taifa letu na kwa uamini wao na uchapaji kazi basi Taifa lipate sifa. Lugha za kimataifa zitiliwe mkazo mashuleni kwetu ili iwe rahisi kuingia katika soko la ajira la nchi hizo.

Kwa leo naomba niishie hapo.

Disclaimer: Mimi sio shabiki wa chama chochote cha siasa ila ni muumini wa serikali iliyo madarakani kwa sababu ya imani yangu kunifundisha kuheshimu mamlaka zilipo, kwa kuwa zote zatoka kwa Mungu. Kwa ambao nimewakwaza kwa maoni yangu, waniwie radhi.

Ahsanteni

Mwisho
 
Ni kweli usemacho ni kitu kizuri kwa kweli,kinahitaji mikakati iliyo safi...idadi ya watu hasa Europe inapungua sana
Thanks brother. Ni muhimu kulisema hili kwa nguvu ili serikali yetu iweze kulifanyia kazi kupitia wizara ya husika kwa kutunga sera mathubuti za kufikia malengo haya.
 
Nilimsikia bwana mmoja anaitwa Jiwe akiwashauri watu wafyatue watoto huku wakifanya kazi kwa bidii na kuipuuza corona
Hhahahaha ni sawa. Idadi yetu kuongezeka ni tishio kwa mataifa ya Ulaya ukizingatia kizazi chetu kina nguvukazi kubwa sana ambayo ikitumika vyema itafanya nchi yetu iweze kuendelea kukua kiuchumi.

Kuhusu corona, hakika mapambano yalikuwa makali lakini, Mungu ambariki kiongozi wetu aliyeweza kuona mbali na hata sasa tu salama... hekina na busara zake zimetuokoa. Wakati mwingine mtaje tu kwa jina maana umenena jambo la ukweli, huna haja ya kuhofia kuliko kumuita kwa jina hilo. Siyo vyema kwa maoni yangu.

Ahsante kwa kuchangia kwenye uzi huu.
 
Huu ushauri ni Mzuri sana ila hauendani na nyakati

Ingefaa utolewe karne ya 18 au 19 hivi

Huwa sielewi dhana ya kusema Idadi ya sisi, wa-Afrika ni tishio kwa Ulaya na Amerika

Kwanini?

Katika karne ya 21, bado Kuna Watu wanaamini wingi ni Hoja?

China ina Watu wangapi? Kwanini walibadili Sera yao ya kuzaliana?

Unahisi huko Ulaya na Amerika wanashindwa kuzaliana?

Ukiweza kujibu maswali hayo utaondoa dhana potofu iliyopo kwako

Ngoja tu nikuibie siri kidogo

Dunia ya sasa inategemea zaidi innovation and Technology,

Tupo katika Zama za Artificial Intelligence, AI na ulimwengu wa 5G bado kidogo tu tuufikie

Duniani huko Watu wanahangaika katika hayo maswala

Sasa anatokea mtu anasema eti Afrika tuna nguvu kazi. Huu ni upuuzi

Hio nguvu kazi mnayojivunia tayari ishaanza kubadiliwa na Roboti

Muangalie Elon Musk na Jeff Bozos, chukua jumla ya utajiri wao pamoja na potential growth ya makampuni yao katika miaka 10 tu ijayo

Unahisi Hawa Watu wawili watakuwa wamezidi GDP ya nchi ngapi za huku Afrika? Hao ni Watu wawili

Unless kama mnataka tuzaliane ili Hao watoto zetu waje kuwa wafanyakazi (watumwa) wa hao wazungu

Serikali ishauriwe juu ya Sera nzuri za kuinua Elimu yenye tija ya kutatua matatizo yetu pia inayoendana na kasi ya mabadiliko ya technology

Next time, Tujikite katika kujadili vitu vya maana sio huu ujinga ambapo kila mmoja ni shahidi kwamba kati ya familia yenye watoto 3 na 12 ni ipi yenye maisha mazuri
 
Nashukuru sana kwa maoni yako. Maoni yako ni umuhimu sana ingawa umetumia lugha rahisi lakini yenye kuonyeshwa kukerwa labda na jambo nililoliwasilisha mezani. Ila sio mbaya.

Kuhusu hoja ya kuwa idadi sio issue nadhani kuna haja ya wewe kufanya utafiti. Idadi ya watu ni ndo inatambulisha ukubwa wa soko na nguvukazi katika taifa na ndio maana hoja hii imekuwa ndio hoja ya dunia kwa sasa.

China kwa mfano kwa idadi yao na viongozi thabiti walionao ndo kumewafanya ndo iwe nchi yenye uchumi mkubwa dunia nyuma ya marekani na kuna taarifa imetoka hivi karibuni kuwa mpaka kufika 2029 kama sijakosea China ndo itakuwa nchi yenye uchumi mkubwa zaidi duniani. Namba hazidanganyi ndugu.

Ukisikia serikali inafanya sensa basi uelewe, idadi ya watu mahala popote ni muhimu hasa nguvukazi. Idadi ya watu ndio jeshi. Na kama ni mfuatiliaji wa mambo duniani utajua tu kuna agenda nyingi za kuweza kupunguza idadi ya watu hasa wa barani africa na asia kwa kutumia njia mbalimbali ikiwamo mag0njw@.

Kuhusu suala la elimu pia hoja zangu vizuri na utaliona hilo kwamba;

"Naiomba serikali na mashirika binafsi itoe mafunzo kwa vijana na watoto wetu tangu elimu ya awali mbinu mpya na za kisasa za kilimo ili uzalishaji wa mazao mbalimbali kuongezeka kwa matumizi ya ndani na nje ya nchi hasa katika mazao ya kimkakati."

Natumai utakuwa umenielewa ndugu yangu. Number matters
 
Huu ushauri ni Mzuri sana ila hauendani na nyakati

Ingefaa utolewe karne ya 18 au 19 hivi

Huwa sielewi dhana ya kusema Idadi ya sisi, wa-Afrika ni tishio kwa Ulaya na Amerika

Kwanini?

Katika karne ya 21, bado Kuna Watu wanaamini wingi ni Hoja?

China ina Watu wangapi? Kwanini walibadili Sera yao ya kuzaliana?

Unahisi huko Ulaya na Amerika wanashindwa kuzaliana?

Ukiweza kujibu maswali hayo utaondoa dhana potofu iliyopo kwako

Ngoja tu nikuibie siri kidogo

Dunia ya sasa inategemea zaidi innovation and Technology,

Tupo katika Zama za Artificial Intelligence, AI na ulimwengu wa 5G bado kidogo tu tuufikie

Duniani huko Watu wanahangaika katika hayo maswala

Sasa anatokea mtu anasema eti Afrika tuna nguvu kazi. Huu ni upuuzi

Hio nguvu kazi mnayojivunia tayari ishaanza kubadiliwa na Roboti

Muangalie Elon Musk na Jeff Bozos, chukua jumla ya utajiri wao pamoja na potential growth ya makampuni yao katika miaka 10 tu ijayo

Unahisi Hawa Watu wawili watakuwa wamezidi GDP ya nchi ngapi za huku Afrika? Hao ni Watu wawili

Unless kama mnataka tuzaliane ili Hao watoto zetu waje kuwa wafanyakazi (watumwa) wa hao wazungu

Serikali ishauriwe juu ya Sera nzuri za kuinua Elimu yenye tija ya kutatua matatizo yetu pia inayoendana na kasi ya mabadiliko ya technology

Next time, Tujikite katika kujadili vitu vya maana sio huu ujinga ambapo kila mmoja ni shahidi kwamba kati ya familia yenye watoto 3 na 12 ni ipi yenye maisha mazuri
Nashukuru sana kwa maoni yako. Maoni yako ni umuhimu sana ingawa umetumia lugha rahisi lakini yenye kuonyeshwa kukerwa labda na jambo nililoliwasilisha mezani. Ila sio mbaya.

Kuhusu hoja ya kuwa idadi sio issue nadhani kuna haja ya wewe kufanya utafiti. Idadi ya watu ni ndo inatambulisha ukubwa wa soko na nguvukazi katika taifa na ndio maana hoja hii imekuwa ndio hoja ya dunia kwa sasa.

South Korea kwa mfano wao wanatoa fungu fulani fedha kwa wananchi wao ili wazae watoto na kuishi maisha ya ndoa. Kwanini wanataka kuongeza idadi hao hasa nguvu kazi. Hivi jiulize kwa mfano leo walisema basi nasihangaike kuhusu idadi hebu fikiria hayo maroboti ndo yatakayokuwa yanatunza hiyo 46% ambayo ni wazee? Vipi baada ya miaka mingine tena huoni ndo kizazi chao kinazidi kupotea. Kama idadi ya wanaokufa ni kubwa kuliko ya wanaozaliwa maana yake ni nini? Tafakari vizuri hapo.

China kwa mfano kwa idadi yao na viongozi thabiti walionao ndo kumewafanya ndo iwe nchi yenye uchumi mkubwa dunia nyuma ya marekani na kuna taarifa imetoka hivi karibuni kuwa mpaka kufika 2029 kama sijakosea China ndo itakuwa nchi yenye uchumi mkubwa zaidi duniani. Namba hazidanganyi ndugu.

Ukisikia serikali inafanya sensa basi uelewe, idadi ya watu mahala popote ni muhimu hasa nguvukazi. Idadi ya watu ndio jeshi. Na kama ni mfuatiliaji wa mambo duniani utajua tu kuna agenda nyingi za kuweza kupunguza idadi ya watu hasa wa barani africa na asia kwa kutumia njia mbalimbali ikiwamo mag0njw@.

Kuhusu suala la elimu pia hoja zangu vizuri na utaliona hilo kwamba;

"Naiomba serikali na mashirika binafsi itoe mafunzo kwa vijana na watoto wetu tangu elimu ya awali mbinu mpya na za kisasa za kilimo ili uzalishaji wa mazao mbalimbali kuongezeka kwa matumizi ya ndani na nje ya nchi hasa katika mazao ya kimkakati."

Mwisho kabisa, maisha mazuri yanategemea sana unaongelea katika mrengo gani. Mfano tu rahisi, Mo akiwa na watoto 12 na wewe ukawa na watoto 3 kina na watakuwa na maisha mazuri...? Nadhani jibu utakuwa nalo.

Natumai utakuwa umenielewa ndugu yangu. Number matters. Tukutane karne ya 27
 
Huu ushauri ni Mzuri sana ila hauendani na nyakati

Ingefaa utolewe karne ya 18 au 19 hivi

Huwa sielewi dhana ya kusema Idadi ya sisi, wa-Afrika ni tishio kwa Ulaya na Amerika

Kwanini?

Katika karne ya 21, bado Kuna Watu wanaamini wingi ni Hoja?

China ina Watu wangapi? Kwanini walibadili Sera yao ya kuzaliana?

Unahisi huko Ulaya na Amerika wanashindwa kuzaliana?

Ukiweza kujibu maswali hayo utaondoa dhana potofu iliyopo kwako

Ngoja tu nikuibie siri kidogo

Dunia ya sasa inategemea zaidi innovation and Technology,

Tupo katika Zama za Artificial Intelligence, AI na ulimwengu wa 5G bado kidogo tu tuufikie

Duniani huko Watu wanahangaika katika hayo maswala

Sasa anatokea mtu anasema eti Afrika tuna nguvu kazi. Huu ni upuuzi

Hio nguvu kazi mnayojivunia tayari ishaanza kubadiliwa na Roboti

Muangalie Elon Musk na Jeff Bozos, chukua jumla ya utajiri wao pamoja na potential growth ya makampuni yao katika miaka 10 tu ijayo

Unahisi Hawa Watu wawili watakuwa wamezidi GDP ya nchi ngapi za huku Afrika? Hao ni Watu wawili

Unless kama mnataka tuzaliane ili Hao watoto zetu waje kuwa wafanyakazi (watumwa) wa hao wazungu

Serikali ishauriwe juu ya Sera nzuri za kuinua Elimu yenye tija ya kutatua matatizo yetu pia inayoendana na kasi ya mabadiliko ya technology

Next time, Tujikite katika kujadili vitu vya maana sio huu ujinga ambapo kila mmoja ni shahidi kwamba kati ya familia yenye watoto 3 na 12 ni ipi yenye maisha mazuri
Sehemu ya taarifa katika gazeti hilo la The Guardian:

".......The trend, which has also led to a population decline in neighbouring Japan, is adding to pressure on the government to address the long-term demographic challenges posed by a rapidly ageing society and one of the lowest fertility rates in the world......"

(kwa maana isiyo rasmi) hapa hali ya waSouth Korea kuona kuna tatizo la kizazi chao kuwa na idadi kubwa ya wazee inayokuwa kwa kasi hivyo kuifanya serikali yao iangazie njia za muda mrefu changamoto hiyo ikiwa ni pamoja hali ya kuzaliana kuwa ya kiwango cha chini kabisa duniani.

".....The administration of the president, Moon Jae-in, recently announced initiatives to encourage couples to have bigger families, including a one-off payment of 1m won [£675] for pregnant women and monthly cash allowances for children aged under 12 months....."

Na hapa wakashauriwa kuwa na familia kubwa zaidi. Na hata kutangaza kuwa ukiwa na mimba utalipwa na kwa watoto chini ya miezi 12 unapewa allowance kwa kila mwezi.
 
Nashukuru sana kwa maoni yako. Maoni yako ni umuhimu sana ingawa umetumia lugha rahisi lakini yenye kuonyeshwa kukerwa labda na jambo nililoliwasilisha mezani. Ila sio mbaya.
Mkuu samahani kwa Lugha niliyotumia hapo awali, ila Lengo ni Moja tu...

... Kuonesha msisitizo juu ya ninachokiamini
Kuhusu hoja ya kuwa idadi sio issue nadhani kuna haja ya wewe kufanya utafiti. Idadi ya watu ni ndo inatambulisha ukubwa wa soko na nguvukazi katika taifa na ndio maana hoja hii imekuwa ndio hoja ya dunia kwa sasa.

South Korea kwa mfano wao wanatoa fungu fulani fedha kwa wananchi wao ili wazae watoto na kuishi maisha ya ndoa. Kwanini wanataka kuongeza idadi hao hasa nguvu kazi. Hivi jiulize kwa mfano leo walisema basi nasihangaike kuhusu idadi hebu fikiria hayo maroboti ndo yatakayokuwa yanatunza hiyo 46% ambayo ni wazee? Vipi baada ya miaka mingine tena huoni ndo kizazi chao kinazidi kupotea. Kama idadi ya wanaokufa ni kubwa kuliko ya wanaozaliwa maana yake ni nini? Tafakari vizuri hapo.
Hoja yako hapa ni nzuri sana.

China kwa mfano kwa idadi yao na viongozi thabiti walionao ndo kumewafanya ndo iwe nchi yenye uchumi mkubwa dunia nyuma ya marekani na kuna taarifa imetoka hivi karibuni kuwa mpaka kufika 2029 kama sijakosea China ndo itakuwa nchi yenye uchumi mkubwa zaidi duniani. Namba hazidanganyi ndugu.

Huo Uchumi unaoongelewa kwamba China itakuwa Super Power ni hadithi tu, unakuwaje superpower huku wananchi wakiwa masikini?

USA ni tofauti, angalia Uchumi wa mtu mmoja mmoja kisha linganisha na huko China

Je China Wanakadiriwa kuja kuwa na GDP ipi hio 2029? Kwa population ipi? 1.4 Billion People

Vipi kuhusu USA, unaweza kufanya uoinganishi hapo (achana na hisia za mtazamo wako wa siasa)
Ukisikia serikali inafanya sensa basi uelewe, idadi ya watu mahala popote ni muhimu hasa nguvukazi. Idadi ya watu ndio jeshi. Na kama ni mfuatiliaji wa mambo duniani utajua tu kuna agenda nyingi za kuweza kupunguza idadi ya watu hasa wa barani africa na asia kwa kutumia njia mbalimbali ikiwamo mag0njw@.

Haya yote ni sawa Kiongozi

Ila kushauri Afrika iongeze nguvu kazi ambao unashauri wakavune hela ulaya, Asia na America ni mtazamo mbaya sana

Kwani South Korea kwa level ya Uchumi waliofikia walienda kuchumia wapi? What about Singapore na hao China uliowayaja

Did they leave their country/continent to chase wealthy outside their boundaries?

Nope, they didn't!

Walijikita katika Elimu inayotatua matatizo yao husika, pia wamewekeza katika Elimu inayoendana na kasi ya ukuaji wa teknolojia

Kwanini Afrika pekeetu tuje na hio strategy ya kwenda kuchuma Pesa mabara mengine?

Hili ndilo NAPINGA kwa nguvu zote

If we're aiming for individually development, America & Europe are good for us ila kama our aim is about Tanzania/Africa in general basi hio strategy yako si sahihi
Kuhusu suala la elimu pia hoja zangu vizuri na utaliona hilo kwamba;

"Naiomba serikali na mashirika binafsi itoe mafunzo kwa vijana na watoto wetu tangu elimu ya awali mbinu mpya na za kisasa za kilimo ili uzalishaji wa mazao mbalimbali kuongezeka kwa matumizi ya ndani na nje ya nchi hasa katika mazao ya kimkakati."

Mwisho kabisa, maisha mazuri yanategemea sana unaongelea katika mrengo gani. Mfano tu rahisi, Mo akiwa na watoto 12 na wewe ukawa na watoto 3 kina na watakuwa na maisha mazuri...? Nadhani jibu utakuwa nalo.

Hapa tupo na Hoja inayofanana, kuhusu Population growth ni All about timing kwa hali iliyopo sasa hapa Tanzania watu wanapata milo 3 kwa tabu then unataka kushauri kuongeza Population?

Tufanye vitu kwa hatua, tuwekeze katika elimu, tutatue matatizo yetu, tujenge Uchumi imara (achana na hizi propaganda za 2 Trillion za TRA)

Baada ya Hapo ndipo zije Sera za kuongeza idadi ya watu.
Natumai utakuwa umenielewa ndugu yangu. Number matters. Tukutane karne ya 27

Hahha

Shukrani Mkuu
 
Huu ushauri ni Mzuri sana ila hauendani na nyakati

Ingefaa utolewe karne ya 18 au 19 hivi

Huwa sielewi dhana ya kusema Idadi ya sisi, wa-Afrika ni tishio kwa Ulaya na Amerika

Kwanini?

Katika karne ya 21, bado Kuna Watu wanaamini wingi ni Hoja?

China ina Watu wangapi? Kwanini walibadili Sera yao ya kuzaliana?

Unahisi huko Ulaya na Amerika wanashindwa kuzaliana?

Ukiweza kujibu maswali hayo utaondoa dhana potofu iliyopo kwako

Ngoja tu nikuibie siri kidogo

Dunia ya sasa inategemea zaidi innovation and Technology,

Tupo katika Zama za Artificial Intelligence, AI na ulimwengu wa 5G bado kidogo tu tuufikie

Duniani huko Watu wanahangaika katika hayo maswala

Sasa anatokea mtu anasema eti Afrika tuna nguvu kazi. Huu ni upuuzi

Hio nguvu kazi mnayojivunia tayari ishaanza kubadiliwa na Roboti

Muangalie Elon Musk na Jeff Bozos, chukua jumla ya utajiri wao pamoja na potential growth ya makampuni yao katika miaka 10 tu ijayo

Unahisi Hawa Watu wawili watakuwa wamezidi GDP ya nchi ngapi za huku Afrika? Hao ni Watu wawili

Unless kama mnataka tuzaliane ili Hao watoto zetu waje kuwa wafanyakazi (watumwa) wa hao wazungu

Serikali ishauriwe juu ya Sera nzuri za kuinua Elimu yenye tija ya kutatua matatizo yetu pia inayoendana na kasi ya mabadiliko ya technology

Next time, Tujikite katika kujadili vitu vya maana sio huu ujinga ambapo kila mmoja ni shahidi kwamba kati ya familia yenye watoto 3 na 12 ni ipi yenye maisha mazuri
Na ili ujue hili tatizo ni kubwa miaka miwili (2018) iliyopita ilikuwa zamu ya Japan: the Guardian

Sehemu ya taarifa yao:

"Japan suffered its biggest population decline on record this year, according to new figures that underline the country’s losing battle to raise its birth rate.

The number of births fell to its lowest since records began more than a century ago, the health and welfare ministry said, soon after parliament approved an immigration bill that will pave the way for the arrival of hundreds of thousands of blue-collar workers to address the worst labour shortage in decades...."

Nguvukazi inahitajika kwa "blue-collar workers" maroboti hayawezi kufanya kila kitu. Na ndo maana nkatoa wito kwa serikali na mashirika binafsi kuona hii fursa hivyo kuandaa kizazi chetu kwa ajili ya haya mambo.

"....Japan has the highest proportion of older people – or those aged 65 and over – in the world, followed by Italy, Portugal and Germany...."

Nmetumia nguvu nyingi sana kukujibu tafadhali ndugu yangu tumia akili sasa nawewe kuelewa nisemacho kwa maana tatizo la uzee lipo Italy, Portugal na Germany pia... unataka nini tena. Tufanye kazi ili tukizaa tuweze kuwahudumia watoto wetu ambao ni zawadi kutoka kwa Mungu. Ahsante
 
(kwa maana isiyo rasmi) hapa hali ya waSouth Korea kuona kuna tatizo la kizazi chao kuwa na idadi kubwa ya wazee inayokuwa kwa kasi hivyo kuifanya serikali yao iangazie njia za muda mrefu changamoto hiyo ikiwa ni pamoja hali ya kuzaliana kuwa ya kiwango cha chini kabisa duniani.
Mkuu mimi sibishi kwamba suala la Population yao ni tatizo. HAPANA

Nakataa hoja zinazodai African Population is a threat kwa Europe & America

Pia siungi mkono Hoja yako ya kusema tuongeze idadi yetu afu tukawe nguvu kazi huko kwa wazungu.

Sijui kama naeleweka vizuri, naomba usome mchango wangu hapo juu
 
Miafrika bana, hivi mnajua teknolojia zinazidi kubuniwa ili kupunguza tegemezi kwa nguvu kazi za kibinadamu, kwamba mashini inaingizwa sehemu na kufanya kazi ya watu 1,000 kwa mpigo mmoja bila kukosea, sasa mnaagizana kuzaliana ili muwapeleke wapi watu wenu.

Kwa mfano hapo Tanzania kwenu LATRA wametangaza mfumo wa online kununua tiketi za mabasi ya kwenda mikoani, hamna tena tegemezi kwa wale maelfu ya waandika tiketi ambao hubeba vitabu kwapani, endeleeni kuzaliana na kufyatua watoto.
 
Ndo
Kwa mfano hapo Tanzania kwenu LATRA wametangaza mfumo wa online kununua tiketi za mabasi ya kwenda mikoani, hamna tena tegemezi kwa wale maelfu ya waandika tiketi ambao hubeba vitabu kwapani, endeleeni kuzaliana na kufyatua watoto

Hiki ndicho kitu ninachosema

Huu ushauri ungetolewa kwenye karne ya 18 au 19 hivi ungekuwa ni sahihi

Sio kwa Zama zetu za leo
 
Huu ushauri ni Mzuri sana ila hauendani na nyakati

Ingefaa utolewe karne ya 18 au 19 hivi

Huwa sielewi dhana ya kusema Idadi ya sisi, wa-Afrika ni tishio kwa Ulaya na Amerika

Kwanini?

Katika karne ya 21, bado Kuna Watu wanaamini wingi ni Hoja?

China ina Watu wangapi? Kwanini walibadili Sera yao ya kuzaliana?

Unahisi huko Ulaya na Amerika wanashindwa kuzaliana?

Ukiweza kujibu maswali hayo utaondoa dhana potofu iliyopo kwako

Ngoja tu nikuibie siri kidogo

Dunia ya sasa inategemea zaidi innovation and Technology,

Tupo katika Zama za Artificial Intelligence, AI na ulimwengu wa 5G bado kidogo tu tuufikie

Duniani huko Watu wanahangaika katika hayo maswala

Sasa anatokea mtu anasema eti Afrika tuna nguvu kazi. Huu ni upuuzi

Hio nguvu kazi mnayojivunia tayari ishaanza kubadiliwa na Roboti

Muangalie Elon Musk na Jeff Bozos, chukua jumla ya utajiri wao pamoja na potential growth ya makampuni yao katika miaka 10 tu ijayo

Unahisi Hawa Watu wawili watakuwa wamezidi GDP ya nchi ngapi za huku Afrika? Hao ni Watu wawili

Unless kama mnataka tuzaliane ili Hao watoto zetu waje kuwa wafanyakazi (watumwa) wa hao wazungu

Serikali ishauriwe juu ya Sera nzuri za kuinua Elimu yenye tija ya kutatua matatizo yetu pia inayoendana na kasi ya mabadiliko ya technology

Next time, Tujikite katika kujadili vitu vya maana sio huu ujinga ambapo kila mmoja ni shahidi kwamba kati ya familia yenye watoto 3 na 12 ni ipi yenye maisha mazuri
Mkuu umenena vyema sana. Dunia ya sasa inakimbizana na inventions and innovations alafu mtu anakuja kuongelea swala la idadi ya watu as tuko 16th Century.

Hata hiko kilimo anachokiongelea kama hatutahamasisha kilimo chenye kutumia dhana bora, njia za kisiasa tukiachana na hiki cha mazoea tutabaki hapahapa tukiendelea kupeana takwimu za kufoji na kuaminishana ujinga.
 
Back
Top Bottom