The Guardian: Kuhusu kushuka kwa idadi ya watu wa Nchi ya Korea Kusini

The Guardian: Kuhusu kushuka kwa idadi ya watu wa Nchi ya Korea Kusini

Kila kitu duniani kimepangwa na Mungu???, je uzinzi, wizi, ujambazi, nk, vyote vimepangwa na Mungu???
Mungu anajua mipango yote ya mwanadamu tangu anazaliwa, yaani anaijua fika future yangu. So mpangaji ni yeye.
 
Mungu anajua mipango yote ya mwanadamu tangu anazaliwa, yaani anaijua fika future yangu. So mpangaji ni yeye.


Kujua jambo na kupanga jambo ni sawasawa???, mfano mimi nikijua kwamba mtu fulani ataiba na kweli akaiba je mimi ndiye nitakuwa nimepanga au nimemfanya aibe???
 
Kujua jambo na kupanga jambo ni sawasawa???, mfano mimi nikijua kwamba mtu fulani ataiba na kweli akaiba je mimi ndiye nitakuwa nimepanga au nimemfanya aibe???
Usijifananishe na Mungu.
 
Katika pitapita yangu mitandaoni, nikakutana na taarifa hii kwenye gazeti maarufu la THE GUARDIAN yenye kichwa cha habari: South Korea's population falls for first time in its history | South Korea | The Guardian ambayo inaongelea kuhusu kushuka kwa idadi ya watu nchini Korea ya Kusini kwa mara ya kwanza katika historia.

Taarifa hii inasema mpaka kufikia mwaka 2067, asilimia 46 ya wakorea watakuwa watu wa umri wa zaidi ya miaka 64 na idadi ya watu kushuka kutoka 51 milioni mpaka 39 milioni endapo hali ya sasa inachagiza kushuka kwa idadi yao itaendelea kuwa hivyo. Na kwa wakati huo huo idadi ya watu kwa bara Africa kuongezeka na umri wa wastani kuwa ni miaka 25 (sikumbuki chanzo cha taarifa hii nilikiona wapi maana sikitilia maanani mpaka nilipoona taarifa ya SK). Sasa tatizo hili sio kwa taifa hilo tu bali ni kwa mataifa mengi ya Ulaya kama Ufaransa.

Sasa mimi kama kijana mtanzania, nikaona hiyo ni fursa kwetu na kwa kizazi chetu katika mitizamo miwili.
1. Mataifa mengi ya Ulaya na Asia yanazidi kupoteza nguvukazi na hivyo kuwa tegemezi kwa Africa katika masuala mengi hasa mazao ya chakula.

USHAURI:

Naiomba serikali na mashirika binafsi itoe mafunzo kwa vijana na watoto wetu tangu elimu ya awali mbinu mpya na za kisasa za kilimo ili uzalishaji wa mazao mbalimbali kuongezeka kwa matumizi ya ndani na nje ya nchi hasa katika mazao ya kimkakati.

Kuwe na mashamba ya serikali/watu binafsi watakaowezeshwa na serikali au taasisi binafsi ambayo yaweza kutoa internship kwa vijana kwenda kujifunza kilimo kwa vitendo na baada ya hapo vijana kuunganisha kimakundi na kuanzisha miradi yao binafsi kwa maslahi ya Taifa. Mkazo ukiwa zaidi katika kushikilia mnyororo mzima wa kuongeza thamani ili bidhaa iende kwa mlaji moja kwa moja.

2. Nguvukazi. Vijana wengi wa mataifa ya Africa wanatoka katika nchi zao na kwenda kufanya kazi kwenye mataifa ya Ulaya, Asia na Marekani kisha fedha wanazopata hutuma nyumbani. Fursa hii bado haijachangamkiwa sana na watanzania wengi labda ni kutoka na Taifa kutokuwa na mipango thabiti ya kutafuta fedha za kigeni kupitia diaspora au ipo lakini watendaji bado wamelala mpaka baba aseme kama kawaida yao ya kupenda kusukumwa au labda mimi sina uelewa sana juu ya kinachoendelea.

Yote kwa yote, ninaishauri serikali yetu iweke mipango ya muda mfupi na muda mrefu katika kutengeneza nguvukazi itakayoenda kuvuna fedha hizi za kigeni katika mataifa ambayo nguvu kazi yao inapungua kwa kasi. Ni muhimu vijana wakafuzwa maadili mema ya nchi yetu na uzalendo kwa taifa letu ili watakapokuwa huko waendelee kuwa watiifu kwa taifa letu na kwa uamini wao na uchapaji kazi basi Taifa lipate sifa. Lugha za kimataifa zitiliwe mkazo mashuleni kwetu ili iwe rahisi kuingia katika soko la ajira la nchi hizo.

Kwa leo naomba niishie hapo...

Disclaimer: Mimi sio shabiki wa chama chochote cha siasa ila ni muumini wa serikali iliyo madarakani kwa sababu ya imani yangu kunifundisha kuheshimu mamlaka zilipo, kwa kuwa zote zatoka kwa Mungu. Kwa ambao nimewakwaza kwa maoni yangu, waniwie radhi.

Ahsanteni

Mwisho
Mkuu kashasema "fyatueni tu" ameona mbali sana! Hayo kwa wakolea ni mazao ya uzazi wa mpango!
 
Huu ushauri ni Mzuri sana ila hauendani na nyakati

Ingefaa utolewe karne ya 18 au 19 hivi

Huwa sielewi dhana ya kusema Idadi ya sisi, wa-Afrika ni tishio kwa Ulaya na Amerika

Kwanini?

Katika karne ya 21, bado Kuna Watu wanaamini wingi ni Hoja?

China ina Watu wangapi? Kwanini walibadili Sera yao ya kuzaliana?

Unahisi huko Ulaya na Amerika wanashindwa kuzaliana?

Ukiweza kujibu maswali hayo utaondoa dhana potofu iliyopo kwako

Ngoja tu nikuibie siri kidogo

Dunia ya sasa inategemea zaidi innovation and Technology,

Tupo katika Zama za Artificial Intelligence, AI na ulimwengu wa 5G bado kidogo tu tuufikie

Duniani huko Watu wanahangaika katika hayo maswala

Sasa anatokea mtu anasema eti Afrika tuna nguvu kazi. Huu ni upuuzi

Hio nguvu kazi mnayojivunia tayari ishaanza kubadiliwa na Roboti

Muangalie Elon Musk na Jeff Bozos, chukua jumla ya utajiri wao pamoja na potential growth ya makampuni yao katika miaka 10 tu ijayo

Unahisi Hawa Watu wawili watakuwa wamezidi GDP ya nchi ngapi za huku Afrika? Hao ni Watu wawili

Unless kama mnataka tuzaliane ili Hao watoto zetu waje kuwa wafanyakazi (watumwa) wa hao wazungu

Serikali ishauriwe juu ya Sera nzuri za kuinua Elimu yenye tija ya kutatua matatizo yetu pia inayoendana na kasi ya mabadiliko ya technology

Next time, Tujikite katika kujadili vitu vya maana sio huu ujinga ambapo kila mmoja ni shahidi kwamba kati ya familia yenye watoto 3 na 12 ni ipi yenye maisha mazuri
Ongera sana mkuu ubarikiwe sana .ulaya
Wameanza kufanya tafiti za kupanda mboga huko anga za mbali sisi tuna waza kufyatua😂
Robot zina piga kazi kuliko mtu
 
Mkuu mimi sibishi kwamba suala la Population yao ni tatizo. HAPANA

Nakataa hoja zinazodai African Population is a threat kwa Europe & America

Pia siungi mkono Hoja yako ya kusema tuongeze idadi yetu afu tukawe nguvu kazi huko kwa wazungu.

Sijui kama naeleweka vizuri, naomba usome mchango wangu hapo ju

Nakataa hoja zinazodai African Population is a threat kwa

Mkuu samahani kwa Lugha niliyotumia hapo awali, ila Lengo ni Moja tu...

... Kuonesha msisitizo juu ya ninachokiamini
Hamna tatizo kiongozi. Tuko pamoja maana lengo letu ni kuelimishana.
Ila kushauri Afrika iongeze nguvu kazi ambao unashauri wakavune hela ulaya, Asia na America ni mtazamo mbaya sana

Kwani South Korea kwa level ya Uchumi waliofikia walienda kuchumia wapi? What about Singapore na hao China uliowayaja

Did they leave their country/continent to chase wealthy outside their boundaries?

Nope, they didn't!
Kuhusu hoja hii ni kwamba nianze kwa kukuuliza swali ila sitokusaidia kulijibu kama wewe ulivyofanya.

Swali: Ushawahi kujua technological expertise transfer inafanyikaje? Unadhani kama hatutoenda huko kupitia mgongo wa serikali tufanikiwa katika adhma ya kuinua taifa letu? Tukiwa na nguvu kazi kubwa nje ya nchi huoni ndo njia sahihi ya kuleta mageuzi katika taifa letu.

Labda kwa taarifa tu China imekuwa ikilaumiwa sana katika kuiba teknolojia za mataifa mengine hasa marrkani na ulaya ( sina ushahidi wa hili), unadhani hiyo teknolojia wanazoshutumiwa kuibwa walifungia nchini kwao bila ya kutuma watu kwenda kufanya kazi au kusoma katika maeneo ambayo wanaamini wana uwezo mkubwa kuliko wao?

Ukijibu maswali haya ndo unapata msingi wa hoja yangu
Tufanye vitu kwa hatua, tuwekeze katika elimu, tutatue matatizo yetu, tujenge Uchumi imara (achana na hizi propaganda za 2 Trillion za TRA)

Baada ya Hapo ndipo zije Sera za kuongeza idadi ya watu
Now we are talking. Ila tafadhali hoja ya kuhusu propaganda ya TRA sio vyema kuiweka hapa. Napenda sana kuongea kwa facts, otherwise kama utakuja na hoja yenye mashiko kuhusu jambo hilo. Ahsante.

Katika hoja yangu nimetumia neno zaidi mafunzo ya vitendo na wewe ukatumia neno elimu... as far as i am concern kunaweza kukawa na uelekeo unafanana.

Nikiwa chuoni tulijifunza kitu kinaitwa critical pathway nadhani katika somo la engineering. Hivyo natambua wazi umuhimu wa kufanya kila jambo kwa hatua. Ingawa katika andiko langu mahali nilipohamasisha serikali kuendelea kuhamasisha ongezeka la watu bali ongezeko ninaloliongelea ni hilo la matazamio (projections) kwa miaka ijayo. Mfano kwa mujibu wa world bank mpaka kufika mwaka 2100 afrika itakuwa na zaidi ya nusu ya idadi ya watu wote duniani. Je hilo sio tishio kwa nchi za Ulaya na Marekani.... ukitaka kujua mantiki hapa
Hii ni sehemu ya ripoti katika gazeti la Financial Times iliyoandikwa na David Pilling | Financial Times ya 2016
Africa’s population boom is both danger and opportunity

".....The numbers are startling. Africa’s population is young, with a median age of just 20. That compares with 43 in Europe. By 2035, more than half of all new jobseekers will be African..."

Sasa tujifungie tu ndani tukisema acha hatuhitaji kuenda kufanya kazi katika nchi za wenzetu ili kupata foreign currency na ujuzi wao.

If we're aiming for individually development, America & Europe are good for us ila kama our aim is about Tanzania/Africa in general basi hio strategy yako si sahihi
Kidole kimoja hakifunji chawa. Ni elimu ya shule ya msingi hii. Uonevu wanaofanyiwa wageni katika nchi mbalimbali lazima serikali iwe na mkono wake ili kuzuia mambo kama hayo. Damu ni nzito kuliko maji. Huwezi mwambie kijana wako anayetafuta maisha ukitaka nikusaidia basi kaa hapa nyumbani fanya shughuli hapa ila ukienda mbali na nyumbani hilo ni juu yako.
 
Huu ushauri ni Mzuri sana ila hauendani na nyakati

Ingefaa utolewe karne ya 18 au 19 hivi

Huwa sielewi dhana ya kusema Idadi ya sisi, wa-Afrika ni tishio kwa Ulaya na Amerika

Kwanini?

Katika karne ya 21, bado Kuna Watu wanaamini wingi ni Hoja?

China ina Watu wangapi? Kwanini walibadili Sera yao ya kuzaliana?

Unahisi huko Ulaya na Amerika wanashindwa kuzaliana?

Ukiweza kujibu maswali hayo utaondoa dhana potofu iliyopo kwako

Ngoja tu nikuibie siri kidogo

Dunia ya sasa inategemea zaidi innovation and Technology,

Tupo katika Zama za Artificial Intelligence, AI na ulimwengu wa 5G bado kidogo tu tuufikie

Duniani huko Watu wanahangaika katika hayo maswala

Sasa anatokea mtu anasema eti Afrika tuna nguvu kazi. Huu ni upuuzi

Hio nguvu kazi mnayojivunia tayari ishaanza kubadiliwa na Roboti

Muangalie Elon Musk na Jeff Bozos, chukua jumla ya utajiri wao pamoja na potential growth ya makampuni yao katika miaka 10 tu ijayo

Unahisi Hawa Watu wawili watakuwa wamezidi GDP ya nchi ngapi za huku Afrika? Hao ni Watu wawili

Unless kama mnataka tuzaliane ili Hao watoto zetu waje kuwa wafanyakazi (watumwa) wa hao wazungu

Serikali ishauriwe juu ya Sera nzuri za kuinua Elimu yenye tija ya kutatua matatizo yetu pia inayoendana na kasi ya mabadiliko ya technology

Next time, Tujikite katika kujadili vitu vya maana sio huu ujinga ambapo kila mmoja ni shahidi kwamba kati ya familia yenye watoto 3 na 12 ni ipi yenye maisha mazuri
Nimekukubali 100% upo sawa tena TECHNOLOGY ndio muhimu sasa duniani ukiwa na hiyo kila kitu unafanya na kuunda .India leo imekuwa best ktk IT duniani chuo chao toka 1950 walikufungua leo result yake wahindi wanaotka india ktk chuo hicho ni kipusa America wanatakiwa kila upande na kazi zinawasubiri.
 
Ongera sana mkuu ubarikiwe sana .ulaya
Wameanza kufanya tafiti za kupanda mboga huko anga za mbali sisi tuna waza kufyatua😂
Robot zina piga kazi kuliko mtu
Naelewa sana kuwa kuna mambo kama hayo yanayohusu teknolojia yanayoendelea katika nchi za wenzetu.

Labda nikupe mfano mmoja rahisi. Kwa miaka mingi sasa kumekuwa na matumizi ya teknolojia mpya katika kilimo kwa nchi za Ulaya na Marekani, lakini ni lini waliacha kuja Afrika kwenye jembe mkono kununua mazao ya biashara na chakula...? Unajua kwanini? If they have all teknology and expertise kwanini wasimalize kila kitu kwao.

Sijui ni kwamba hamuoni au imekaaje.... the taste of human nature haijawahi kukinaiwa hata mara moja ndugu yangu... wanaenda mbele lakini baada wanakuja kugundua kuwa mother nature is calling.

Leo hii nikwambie uende kununua chakula cha kwenye makopo supermarket utaenda hata kama uwezo huo unao. Kwahiyo hicho wanachokifanya wazungu ni mbio za sakafuni ambazo siku zote huishia ukingoni. Nature siku zote ndo mshindi.

Kama hujaelewa uliza tena. Nipo kwa ajili yako tuelimishane
 
ngoja wenyewe waje miafrika ndio tulivyo kushuka kwao kwa idadi ya watu hakuna kwa njia yoyote ile na uwezekano wa sisi kufaidika nako trust me
 
Nimekukubali 100% upo sawa tena TECHNOLOGY ndio muhimu sasa duniani ukiwa na hiyo kila kitu unafanya na kuunda .India leo imekuwa best ktk IT duniani chuo chao toka 1950 walikufungua leo result yake wahindi wanaotka india ktk chuo hicho ni kipusa America wanatakiwa kila upande na kazi zinawasubiri.
Hata mimi hapa naunga mkono hoja. Elimu ni muhimu sana. Na tuiboreshe sambamba na sera zetu.

Ila nina swali hapa. Kama maexpert wa India wanatakiwa sana Marekani hilo sio tatizo kwa wale ambao ni raia wa marekani ambao wanaujuzi wa teknolojia ingawa labda yao inaonekana sio nzuri kama ya wahindi...??? Population vs Job competition vs Nationality vs Technology
 
ngoja wenyewe waje miafrika ndio tulivyo kushuka kwao kwa idadi ya watu hakuna kwa njia yoyote ile na uwezekano wa sisi kufaidika nako trust me
Kama ungeweza kufafanua kidogo ndugu hoja yako. Hata hivyo kuwa Muafrika sio dhambi, jikubali na jivunie kile kilicho chako maana kama huwezi kupigana nae ungana nae. Kuwa na amani na furaha wakati wote ni jambo la msingi sana kwa afya yako na Taifa.
 
Ni kweli usemacho ni kitu kizuri kwa kweli,kinahitaji mikakati iliyo safi...idadi ya watu hasa Europe inapungua sana
Nashukuru sana kwa welewa wako... vipi kuhusu mtazamo wako juu ongezeko letu la watu kuwa tishio kwa nchi zao...
 
Huo Uchumi unaoongelewa kwamba China itakuwa Super Power ni hadithi tu, unakuwaje superpower huku wananchi wakiwa masikini?

USA ni tofauti, angalia Uchumi wa mtu mmoja mmoja kisha linganisha na huko China

Je China Wanakadiriwa kuja kuwa na GDP ipi hio 2029? Kwa population ipi? 1.4 Billion People

Vipi kuhusu USA, unaweza kufanya uoinganishi hapo (achana na hisia za mtazamo wako wa siasa)
Sisemi vitu bila ya kuwa na reference ndugu yangu. Nasoma anagalau kwa kiasi chake ili niweze kusema vitu vya uhakika. Ingawa hii haikuwa kwenye mada ya leo ila nikujibu tu kidogo... soma The Guardian kwa link hii China to overtake US as world's biggest economy by 2028, report predicts

China to overtake US as world's biggest economy by 2028, report predicts​

Centre for Economics and Business Research says it expects this to happen half a decade sooner than it forecast a year ago
Shipping containers at the Yangshan deep-water port in Shanghai.



Larry Elliott Economics editor
Sat 26 Dec 2020 00.01 GMT

1,840

China will overtake the US as the world’s biggest economy before the end of the decade after outperforming its rival during the global Covid-19 pandemic, according to a report.
The Centre for Economics and Business Research said that it nowexpected the value of China’s economy when measured in dollars to exceed that of the US by 2028, half a decade sooner than it expected a year ago..."

Haya sio maneno yangu wala sio siasa. Mimi siko politically affiliated na mrengo wowote. I am a neutral citizen who supports whoever is in power as I have elaborated above.

"?....Even so, living standards in China will remain much lower than in the US and western European countries. In the US, the average per capita income is just over $63,000, while in the UK it is just over $39,000...."

Kuhusu hoja ya hali ya maisha nakuunga mkono kupitia maneno hayo hapo juu yaliyoandika katika gazeti tajwa hapo juu. Ila hii haihaharamishi China kuwa Superpower
 
Miafrika bana, hivi mnajua teknolojia zinazidi kubuniwa ili kupunguza tegemezi kwa nguvu kazi za kibinadamu, kwamba mashini inaingizwa sehemu na kufanya kazi ya watu 1,000 kwa mpigo mmoja bila kukosea, sasa mnaagizana kuzaliana ili muwapeleke wapi watu wenu.

Kwa mfano hapo Tanzania kwenu LATRA wametangaza mfumo wa online kununua tiketi za mabasi ya kwenda mikoani, hamna tena tegemezi kwa wale maelfu ya waandika tiketi ambao hubeba vitabu kwapani, endeleeni kuzaliana na kufyatua watoto.....
Wamebadilishana siti. Kutoka kwa wanaobeba vitabu kwapani mpaka kwenda wanaokaa nyuma ya computer. Kinachoangaliwa hapa sasa je ni nini impact yake katika uchumi... mapato ya serikali yataongezekana hivyo huduma za jamii kuendelea kuboreshwa ikiwemo elimu maana mianya ya kukwepa kodi itapungua. How do you see that?

Kila jambo na nyakati zake
 
Kujua jambo na kupanga jambo ni sawasawa???, mfano mimi nikijua kwamba mtu fulani ataiba na kweli akaiba je mimi ndiye nitakuwa nimepanga au nimemfanya aibe???
Yeah wewe ndo umemfanya aibe ikiwa unataka kufikiria hivyo.... ila kama unataka tuelimishane niruhusu.

Huwa tunafundishwa ya kuwa kila jambo hufanyika katika ulimwengu wa roho kabla ya kujidhihirisha katika mwili. Ukijiambia wewe kuwa utaenda kuiba na ukadhamiria kufanya hivyo basi utaiba kweli. Lakini pia inawezekana pia ukamuombea mtu mabaya na yakamkuta.

Mfano mtu anaweza kwenda kwa mganga kumfanya mwingine awe chini ma inakuwa. Sasa je ukipanga kumuwazia mwenzio kuiba je nani kamfanya mwingine aibe kama akiende kuiba kweli hapo? Spiritual power - usimnenee mwenzako mabaya kwanini?... Majibu unayo.

Hata hivo dhana ya kuhusu mpango wa Mungu inahitaji kiongozi wa kiroho aweze kuongelea juu ya hilo lasivyo unawezaleta mkanganyiko kwako na kwa wengine. Ila kama unabisha ntakuuliza swali ukijibu basi ntaelewa kuwa wewe ni mwelewa wa mambo au unabisha tu.

Swali: Unaamini Mungu wako unayemuamini anaijua leo na kesho yako? Je haimaanishi ya kuwa tayari anafahamu mwezi ujao utaenda kuiba?
 
Wamebadilishana siti. Kutoka kwa wanaobeba vitabu kwapani mpaka kwenda wanaokaa nyuma ya computer. Kinachoangaliwa hapa sasa je ni nini impact yake katika uchumi... mapato ya serikali yataongezekana hivyo huduma za jamii kuendelea kuboreshwa ikiwemo elimu maana mianya ya kukwepa kodi itapungua. How do you see that?

Kila jambo na nyakati zake

Naona haujanielewa, hamna cha kubadilishana siti hapo, mimi binafsi n mtaalam wa hayo makitu ya software development, kwa mfumo kama huo mtu mmoja aliyekaa nyuma ya computer atafanya kazi ya hao wakata tiketi kama 1,000 pia kumbuka sio hao tu, kuna makampuni yaliyokua yanachapsha hizo tiketi ikiwemo na familia zao, yaani watu wengi tu watabak bila ajira.

Ni kweli serikali itaweza kupokea mapato ya kodi bila ukwepaji wowote na itazitumia kwenye kuboresha huduma za kijamii, hiyo yote sawa, ila hoja yangu ya msingi ilikua dhidi ya kauli ya mleta mada kwamba mzaliane ili nguvu kazi iongezeke, ndio nikamkumbusha kwamba nyakati za leo nguvu kazi ya binadamu inaendelea kufutwa na teknolojia, in fact taaluma zisizohusiana na teknolojia zitapata tabu sana siku za hivi karibuni.

Kwanza Corona imedhihirishia ulimwengu kuna aina ya huduma nyingi ambazo huwa sio muhimu kivile, binadamu tuna uwezo wa kuishi bila kuzitumia na badala yake tutumie teknolojia, nyie endeleeni kufyatua watoto.
 
Back
Top Bottom