The Guardian: Kuhusu kushuka kwa idadi ya watu wa Nchi ya Korea Kusini

The Guardian: Kuhusu kushuka kwa idadi ya watu wa Nchi ya Korea Kusini

Labda nikurahisishie kazi ndugu yangu. Ni hivi Mungu ndiye muweza wa yote, Mungu ndiye mpangaji wa yote, Mungu ndiye hujua kesho yetu, Mungu kila kitu... na hata shetani alishaongeaga na Mungu aende kumjaribu Ayubu na akaruhusiwa ingawa kwa masharti.

Sasa mimi nawewe tuna haja gani ya kuzozana. Hebu kwa mfano ukija kiimani hata serikali iliyo madarakani sass unadhani Mungu hakujua yenyewe ndo itakuwepo, je asingeweza kuzuia isiwepo, kwanini kaacha iwepo, ana makusudi yake na ndo hapo mimi naww hatupaswi kuhoji... Mipango ya Mungu hatuwezi kupingana nayo...


Na mimi ngoja nikurahishie kazi rafiki yangu.

Unasema:- Mungu ndiye muweza wa yote, Sio kweli kwamba Mungu ni muweza wa yote, kama Mungu ni muweza wa yote, je Mungu anaweza kusema uongo??, Mungu anaweza kuiba??, Mungu anaweza kuua watu hovyo???, Mungu anaweza kufa??, Mungu anaweza kuumba Mungu mwingine kama yeye???, Mungu anaweza kukugeuza wewe ukawa Yesu??nk,

Hivyo sasa utaona kwamba kuna baadhi ya vitu Mungu hawezi kufanya ili kulinda heshima na utukufu wake, hivyo sio kila kitu Mungu anaweza kufanya.

Unasema:- Mungu ndiye mpangaji wa yote, Sio kweli kwamba Mungu ndio mpangaji wa Yote, Mungu hawezi kupanga uhalifu na mambo yote ya kishetani, mfano kuzini, kuiba KURA, kula rushwa, kuua nk, hivyo sio kila kitu hupangwa na Mungu, Mungu hupanga mambo mema tu kwasababu yumwema.

Unasema:- Hujua kesho yetu, ndiyo hujua jana yetu, leo yetu na kesho yetu, na kujua kwake jana, leo na kesho yetu hakuhusiani na matendo yetu ya jana, leo na kesho yetu, matendo yetu husukumwa na nia na dhamira za nafsi zetu na ndio maana tunaamini ipo siku ya hukumu ambapo kila mtu ataulizwa juu ya matendo yake aliyofanya pindi alipokuwa duniani na hatimaye kulipwa malipo yanayompasa, kama kujua kwa Mungu kungalihusiana na matendo yetu basi wala kusingalikuwepo na malipo siku ya mwisho kwani kujua kwa Mungu na u husiano na matendo yetu ingalikuwa ni kikwazo cha watu kuadhibiwa au kulipwa malipo.mema, hiyo ndio falsafa ya malipo ya mema na maovu kwa mtu katika siku ya malipo.

Unasema Mungu aliongea na Shetani, Ndiyo, shetani mwenyewe ni Ibilisi au Lucifer, Shetani ni Generic name (jina la ujumla), lakini Mungu hajaumba Shetani kwani Mungu huwa haumbi vitu viovu na vibaya, Shetani ni kiumbe chochote kiovu na ushetani ni uovu na Mungu alimruhusu shetani awepo miongoni mwetu ili awe ni mtihani au ngazi yetu kwa ajili ya kupanda kuelekea juu kwenye wema, utajuaje kwamba jambo fulani ni jema kama hakuna ubaya wake???, utajuaje wizi ni mbaya kama hakuna wizi au hujaibiwa??, au utajuaje kupigwa ni kubaya kama hujapigwa??, Mungu alipaswa amuache shetani miongoni mwetu na ndiyo maana pia akawaleta mitume, manabii na malaika kupambana na shetani na watu tujifunze mema ya manabii na tuache mabaya ya shetani na hapo ndipo tutakapo panda madaraja ya kiroho duniani na akhera.
 
Ingekuwa idadi kubwa ni deal Kuna watu ndugu zao wakifariki wanashindwa hata kulea watoto wa ndugu zao wanategemea jamii nyingine ije kuwalelea hata Wazungu watoke nje kuwaletea misaada, kikubwa tunaokoelekea ni uchumi wa Kila mtu na familia upoje na siyo idadi kubwa ya watu ambao technology inakwenda kuteka nafasi nyingi za kazi hata huko nje mifumo yao inategenezwa kuendesha maisha kwa technology,

wakati wewe unahangaika kuajili house girl wenzako mifumo ya nyumbani na nje ya nyumbani wametengeneza mtu ajitegemee mfano kuosha vyombo na kufua kwa mashine, maji yapo kwenye masink kwa kuoga na kuosha mikono, kabati za kunyoosha nguo yaani wanapambana Kila mtu kumiliki maisha mazuri na yakujitegemea Sasa wewe unawaza kwenda kuajiliwa kwamba hawana watu, watu wapo kwa idadi inayowatosha wao kuendesha maisha yao bila wasoma mita, cashier, house girl na kazi nyingi zilizowekwa kwenye technology.
 
Labda nikurahisishie kazi ndugu yangu. Ni hivi Mungu ndiye muweza wa yote, Mungu ndiye mpangaji wa yote, Mungu ndiye hujua kesho yetu, Mungu kila kitu... na hata shetani alishaongeaga na Mungu aende kumjaribu Ayubu na akaruhusiwa ingawa kwa masharti.

Sasa mimi nawewe tuna haja gani ya kuzozana. Hebu kwa mfano ukija kiimani hata serikali iliyo madarakani sass unadhani Mungu hakujua yenyewe ndo itakuwepo, je asingeweza kuzuia isiwepo, kwanini kaacha iwepo, ana makusudi yake na ndo hapo mimi naww hatupaswi kuhoji... Mipango ya Mungu hatuwezi kupingana nayo...
Kuwa muweza wa yote siyo kwamba ndo aweke serikali iliyopo, hiyo ilikuwa zamani wakati Mungu aliendesha mwenyewe utawala wa nchi Ila kwasasa tangu watu waamue kujifanyia wenyewe na Mungu akawaacha wafanye wenyewe, serikali ya Mungu inaendeshwa kwa mifumo ya Mungu mwenyewe hata kujenga nyumba za ibada zingejengwa na serikali na mifumo yote ya mambo ya imani ingejengwa na serikali.
 
Mamlaka ya kuteka na kuua wakina azory gwanda, na ben saanane, mamlaka ya kuiba kura, mamlaka ya kujenga uwanja wa ndege vijijini kwao ilhali hamna wateja na watoto wanakaa chini shuleni zote hizo. Zimetoka kwa mungu?
Nonsense.
 
Ndo


Hiki ndicho kitu ninachosema

Huu ushauri ungetolewa kwenye karne ya 18 au 19 hivi ungekuwa ni sahihi

Sio kwa Zama zetu za leo
Hivi mtu haoni tumehangaika na suala la kujenga madarasa na shule kwa miongo 3, shule hazitoshi tu yote hii ni sababu ya ongezeko la watu, Serikali kila Mwaka inajenga shule na hospitali tu ambazo kama ongezeko la watu halitodhibitiwa haitotokea vikatosha, tunachangamoto kubwa ya ajira, Rasilimali na fursa zilizopo hazitoshelezi idadi ya watu waliopo na bado watu wanataka tuzaliane. Kati ya jambo ambalo sisi tunapaswa kuwa nalo makini sana ni idadi ya watu
 
Kwa hiyo mkuu unatushauri tuzamie mambele uko ..tukawazalishe wazungu na hao makorea?
 
Kwa hiyo mkuu unatushauri tuzamie mambele uko ..tukawazalishe wazungu na hao makorea?
Nadhani tumeelewana... lakini wengi wemechagua kipinga nisichokishabikia... lengo langu tuzamie mbele kwa msaada wa serikali na sio kuzaliana. Kuzaliana ni swala natural sana kwa Africa. We don't care...
 
Mamlaka ya kuteka na kuua wakina azory gwanda, na ben saanane, mamlaka ya kuiba kura, mamlaka ya kujenga uwanja wa ndege vijijini kwao ilhali hamna wateja na watoto wanakaa chini shuleni zote hizo. Zimetoka kwa mungu?

Warumi13​

1 Kila mtu hana budi kutii serikali inayotawala. Kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na serikali zote zilizopo zimewekwa na Mungu.

2 Kwa hiyo anayepinga mamlaka inayotawala ana pinga chombo kilichowekwa na Mungu; na watu wanaoasi watajiletea hukumu.

3 Kwa maana watawala hawatishi watu wanaotenda mema bali wale wanaotenda maovu. Kama hupendi kuishi kwa kumwogopa mwenye mamlaka, basi tenda mema naye atakusifu.

4 Maana mwenye mamlaka ni mtumishi wa Mungu kwa manufaa yako. Lakini kama ukitenda maovu, basi ogopa kwa maana hatembei na silaha bure. Yeye ni mtumishi wa Mungu anayetekeleza adhabu ya Mungu juu ya watenda maovu.

5 Kwa hiyo ni lazima kutii wenye mamlaka, si kwa sababu ya kuogopa adhabu tu bali pia kwa ajili ya dhamiri.

6 Kwa sababu hiyo hiyo mnalipa kodi, kwa maana watawala ni watumishi wa Mungu ambao hutumia muda wao wote kutawala.

7 Wal ipeni wote haki zao; mtu wakodi mlipe kodi; na mtoza ushuru mli pe ushuru; astahilie kunyenyekewa, mnyenyekee; astahiliye hesh ima, mheshimu.

Qur'ani
"Enyi mlioamini Mtiini Allah, na mtiini Rasuli (Wake Muhammad) na Wale waliopewa mamlaka kutoka miongoni mwenu, ......" (Qur'ani, 4:59
Credit to mama D
 

Warumi13​

1 Kila mtu hana budi kutii serikali inayotawala. Kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na serikali zote zilizopo zimewekwa na Mungu.

2 Kwa hiyo anayepinga mamlaka inayotawala ana pinga chombo kilichowekwa na Mungu; na watu wanaoasi watajiletea hukumu.

3 Kwa maana watawala hawatishi watu wanaotenda mema bali wale wanaotenda maovu. Kama hupendi kuishi kwa kumwogopa mwenye mamlaka, basi tenda mema naye atakusifu.

4 Maana mwenye mamlaka ni mtumishi wa Mungu kwa manufaa yako. Lakini kama ukitenda maovu, basi ogopa kwa maana hatembei na silaha bure. Yeye ni mtumishi wa Mungu anayetekeleza adhabu ya Mungu juu ya watenda maovu.

5 Kwa hiyo ni lazima kutii wenye mamlaka, si kwa sababu ya kuogopa adhabu tu bali pia kwa ajili ya dhamiri.

6 Kwa sababu hiyo hiyo mnalipa kodi, kwa maana watawala ni watumishi wa Mungu ambao hutumia muda wao wote kutawala.

7 Wal ipeni wote haki zao; mtu wakodi mlipe kodi; na mtoza ushuru mli pe ushuru; astahilie kunyenyekewa, mnyenyekee; astahiliye hesh ima, mheshimu.

Qur'ani
"Enyi mlioamini Mtiini Allah, na mtiini Rasuli (Wake Muhammad) na Wale waliopewa mamlaka kutoka miongoni mwenu, ......" (Qur'ani, 4:59
Credit to mama D
Kwani kuna anayetaka kuongeza au kupunguza neno kwenye torati? Au kuna anayetamani kuipindua kabisa😂😂😂
 
Katika pitapita yangu mitandaoni, nikakutana na taarifa hii kwenye gazeti maarufu la THE GUARDIAN yenye kichwa cha habari: South Korea's population falls for first time in its history | South Korea | The Guardian ambayo inaongelea kuhusu kushuka kwa idadi ya watu nchini Korea ya Kusini kwa mara ya kwanza katika historia.

Taarifa hii inasema mpaka kufikia mwaka 2067, asilimia 46 ya wakorea watakuwa watu wa umri wa zaidi ya miaka 64 na idadi ya watu kushuka kutoka 51 milioni mpaka 39 milioni endapo hali ya sasa inachagiza kushuka kwa idadi yao itaendelea kuwa hivyo. Na kwa wakati huo huo idadi ya watu kwa bara Africa kuongezeka na umri wa wastani kuwa ni miaka 25 (sikumbuki chanzo cha taarifa hii nilikiona wapi maana sikitilia maanani mpaka nilipoona taarifa ya SK). Sasa tatizo hili sio kwa taifa hilo tu bali ni kwa mataifa mengi ya Ulaya kama Ufaransa.

Sasa mimi kama kijana mtanzania, nikaona hiyo ni fursa kwetu na kwa kizazi chetu katika mitizamo miwili.
1. Mataifa mengi ya Ulaya na Asia yanazidi kupoteza nguvukazi na hivyo kuwa tegemezi kwa Africa katika masuala mengi hasa mazao ya chakula.

USHAURI:

Naiomba serikali na mashirika binafsi itoe mafunzo kwa vijana na watoto wetu tangu elimu ya awali mbinu mpya na za kisasa za kilimo ili uzalishaji wa mazao mbalimbali kuongezeka kwa matumizi ya ndani na nje ya nchi hasa katika mazao ya kimkakati.

Kuwe na mashamba ya serikali/watu binafsi watakaowezeshwa na serikali au taasisi binafsi ambayo yaweza kutoa internship kwa vijana kwenda kujifunza kilimo kwa vitendo na baada ya hapo vijana kuunganisha kimakundi na kuanzisha miradi yao binafsi kwa maslahi ya Taifa. Mkazo ukiwa zaidi katika kushikilia mnyororo mzima wa kuongeza thamani ili bidhaa iende kwa mlaji moja kwa moja.

2. Nguvukazi. Vijana wengi wa mataifa ya Africa wanatoka katika nchi zao na kwenda kufanya kazi kwenye mataifa ya Ulaya, Asia na Marekani kisha fedha wanazopata hutuma nyumbani. Fursa hii bado haijachangamkiwa sana na watanzania wengi labda ni kutoka na Taifa kutokuwa na mipango thabiti ya kutafuta fedha za kigeni kupitia diaspora au ipo lakini watendaji bado wamelala mpaka baba aseme kama kawaida yao ya kupenda kusukumwa au labda mimi sina uelewa sana juu ya kinachoendelea.

Yote kwa yote, ninaishauri serikali yetu iweke mipango ya muda mfupi na muda mrefu katika kutengeneza nguvukazi itakayoenda kuvuna fedha hizi za kigeni katika mataifa ambayo nguvu kazi yao inapungua kwa kasi. Ni muhimu vijana wakafuzwa maadili mema ya nchi yetu na uzalendo kwa taifa letu ili watakapokuwa huko waendelee kuwa watiifu kwa taifa letu na kwa uamini wao na uchapaji kazi basi Taifa lipate sifa. Lugha za kimataifa zitiliwe mkazo mashuleni kwetu ili iwe rahisi kuingia katika soko la ajira la nchi hizo.

Kwa leo naomba niishie hapo.

Disclaimer: Mimi sio shabiki wa chama chochote cha siasa ila ni muumini wa serikali iliyo madarakani kwa sababu ya imani yangu kunifundisha kuheshimu mamlaka zilipo, kwa kuwa zote zatoka kwa Mungu. Kwa ambao nimewakwaza kwa maoni yangu, waniwie radhi.

Ahsanteni

Mwisho
ushasikia ulaya ,Korea wananjaaa,kule hawalimi kwa mikono
 
Ok, if that is the case then, Kujua jambo kwa Mungu hukuhusiani na utendaji wake kwa hilo jambo.
Hivi kwanini mitume hawakuwa sawa na sisi wengine kwa maana wao walikuwa ni watu wenye tabia njema tu tofauti na sisi ambao wengine ni wema na wengine ni waovu au wakati mwengine ni wachamungu na wakati mwengine hubadilika na kuwa waovu.

Je mitume kuwa hivyo ni jambo ambalo limepangwa na Mungu kuwa hivyo au Mungu hahusiki?
 
Hivi kwanini mitume hawakuwa sawa na sisi wengine kwa maana wao walikuwa ni watu wenye tabia njema tu tofauti na sisi ambao wengine ni wema na wengine ni waovu au wakati mwengine ni wachamungu na wakati mwengine hubadilika na kuwa waovu.

Je mitume kuwa hivyo ni jambo ambalo limepangwa na Mungu kuwa hivyo au Mungu hahusiki?


Ni hivi, Mitume ni watu waliotumwa na Mungu ili watuongoze njia sahihi sisi tusiokuwa mitume, kutimiza jambo hilo Mungu mara zote huwaongoza hao mitume kutofanya makosa ya kudhamiria, makosa ya kudhamiria ni yale ambayo mtendaji anatenda huku akijua kwamba anatenda kosa.

Ama kuhusu makosa ya kibinadamu mitume nao wanaweza kufanya.

Mungu amewalinda mitume kufanya makosa ya kudhamiria ili wawe ni kioo chetu katika kutenda maagizo ya Mungu, lakini tukumbuke kwamba huo ulinzi pia unatokana na juhudi na maombi yao kwa Mungu ili awalinde na kutenda mambo mabaya ni kwa namna hiyohiyo ya maombi hata sisi tusiokuwa mitume tunaweza kuiga njia hiyo ya mitume kumuomba Mungu atulinde na kutenda maovu na tushike njia nzuri na amri za Mungu, hiyo inaitwa "Istighfaar" (kuomba maghofira).

Kifupi ni kwamba mitume ni vioo vyetu vya kujitazamia kasoro zetu ili tujisahihishe na tushika njia anazotaka Mungu tuzishike, Mungu kwa hekima zake ndivyo amepanga hivyo.
 
Hawa watu hawawezi kutegemea Africa kwa chakula, kilimo chao kipo highly mechanized na very efficient

Unaweza kuta 1% tu ya watu ndio wanaxalisha chakula cha nchi nzima

Pia wahamiaji ni wengi kuliko mahitaji yao, wengi wanazama baharini na kufia huko wakijaribu kufika Ulaya na mwishoni wengi wanarudishwa tena

Nchi nyingine kunaibuka siasa za mrengo mkali wa kulia amba wanapinga wahamiaji wakidai wanaharibu utamaduni wao na wanaenda kuwa tegemezi
 
Nadhani tumeelewana... lakini wengi wemechagua kipinga nisichokishabikia... lengo langu tuzamie mbele kwa msaada wa serikali na sio kuzaliana. Kuzaliana ni swala natural sana kwa Africa. We don't care...
ni wachache sana watakaoelewa mkuu
 
Back
Top Bottom