The Only Thing We Have to Fear is Fear itself

The Only Thing We Have to Fear is Fear itself

Naamini it has been a good decision for Chadema to remain silent na kuwapa wao nafasi waseme maana ndiyo wenye shida na si Chadema. Wamesha sema yale ambayo CCM waliwataka waseme na kupokelea Dodoma fine inatosha Chadema nashauri endeleeni kufanya kazi badala ya kulumbana haina maana . wao wameondoka wamesha toa maelezo dhidi ya Chama sasa ni watu kupima ukweli huo . Maana watu walianzia Ukabila ukashindwa na leo wameanza na mambo ambayo hata haya ingii akilini . kazi kwenu na Chadema itawapata viongozi haswa na walio lala mbele wanaisaidia Chadema kuvamiwa last minutes .
 
Mkandara rudia kusoma tafadhali.Utanielewa wacha haraka na kurukia kileleni . Asante Mzee
 
Kama viongozi wa CCM ni corrupt na wanunuliwa kirahisi kwanini Chadema isijaribu kuwanunua? Tunakumbuka wakati wa uchaguzi baadhi ya viongozi walijaribu kuwashawishi at least publicly viongozi wa CCM waliobwaga kwenye kura za maoni kujiuna nao!! Kushawishi wapinzani wako kuachana na misimamo yao ya kisiasa, ni sehemu ya mchezo wa kisiasa!!

Nimeshawaambia CCM haina nia wala mpango wa kuona vyama vya upinzani vimeimarika! Wapinzani waendelee tu kuilaumu CCM kwa matatizo yao!! Lunyungu.. mimi kusema "nimetafutwa na CCM" haina maana nilikuwa nasema kweli, nilikuwa najaribu kukuonesha sarcastically, jinsi gani madai ya Mbowe hayawezi kuchukuliwa maanani!!

a. Ni mwana CCM gani aliyejaribu kumfuata, na alimuahidi nini? Hivi kuna ugumu gani kurekodi mazungumzo na kiongozi huyo wa CCM na kuyaweka hadharani (niko radhi kuyaweka yasikike) ili watu wajue ubovu wa CCM!! Kila siku kudai kiongozi huyu au yule wa CCM "amejaribu kuninunua nihame" bila kuwa na ushahidi zaidi wa maneno yenu inachosha!!

Kama wana CCM wanaweza kuwashawishi na kuwa majasiri kuwa approach viongozi wa upinzani na kuwapa deals, inaonesha ni jinsi gani CCM imebobea katika mbinu na mikakati ya kisiasa! wapinzani lazima wajifunze!! Ama sivyo wataendelea kulalamika na mwaka huu watapoteza viongozi wengine!

Acheni kulalamika, you wanted to get into the political game.. now you better play stop whining!!
 
Mwanakijiji,
Kati ya CCM na Chadema nani yuko loaded financially? Ukishajibu hulo utakuwa umejijibu mwenyewe.
 
Wanabodi,
Naomba mchango wenu kuhusu kuondoka kwa hawa jamaa toka Chadema - Kabourou, Laurent Marwa,Chacha Okong'o na Chacha Mwitesya.

Wananchi wanatakiwa kupata ukweli. Tumeyasikia toka CCM, sasa inabidi tupate toka upande wa Chadema!...
Hawa watu ni viongozi wa aina gani?... na hayo madai yao yana ukweli kiasi gani?


Kuna mambo ya maana zaidi kuyafanya kuliko kujibishana na hao wanaohama vyama vya upinzani. Hao wanaohama tayari wanatatizo la kisaikolojia; inabidi kwanza waridhishe nafsi zao kwamba walichokifanya ni sahihi. Sasa katika kufanya hivi lazima wataropoka chochote kuhalalisha matendo yao na kujiridhisha. Sasa kwa nini chadema wakae kujibu mambo. Kaborou aliongea mengi, lakini wananchi wake wa Kigoma wakamjibu waziwazi kuwa "sababu zako haziingii akilini" na wakamwambia kuwa "kinachokusumbua ni njaa,acha kuipakazia chadema". Sasa na hao wa Musoma, wananchi wa kule wana majibu mazuri zaidi kuliko chadema makao makuu.
 
Tatizo lenu Chadema mnakuwa na imani za ushabiki badala ya kuangalia issues kwa uzito wake...
Waswahili ndio wanaokupeni kura na mkiliacha swala hili wazi kama mnavyodai basi hakuna haja ya J. J Mnyika kuja hapa.
kumbukeni tu sisi waswahili kusema ndio kazi yetu na Inalipa kama hutaweza kusimama imara!...
CCM wanashindwa kuja hapa kwa madai kama yenu na trust me wengi wetu tumepata ufunuo wa kutosha kiasi kwamba itawachukua CCM kazi kubwa kutubadilisha mawazo yetu... na wakiendela kuachia eti - Chadema ni waropokaji basi wasitegemee mwisho mzuri.
hapa sio Mahakamani lakini kama tulivyokwisha sema toka awali, ukipata picha ya pande mbili ni rahisi kupeta pumba toka ktk mchele...
Sielewi kwa nini inakuwa ngumu kwenu kufahamu vitu hivi!..
Lunyungu,
Why should I believe you?... ikiwa wewe huna la kusema na zaidi ya hapo sikujui kiasi hicho, tena basi baadhi ya hawa jamaa nawafahamu. Nitapima kitu gani ikiwa nimepewa kitu kimoja toka Upande mmoja ambacho siwezi kuwa na hakika nacho.
Kumbukeni jamani hawa jamaa ndio viongozi wetu na kama nyie mtakuwa na habari mbaya kwa wananchi na mmezificha eti kuwahifadhi basi nanyi hamna maana vilevile!..
Ikiwa they are good leaders isipokuwa wameshawishika kwa fedha, bado sioni sababu ya wao kuweka madai yao. Wangeweza kuondoka kimya kimya na tusingeyafahamu yote waliyodai..
Hata kama kuna makosa yalitendeka ndani ya Chadema kwa nini nanyi msituambie kuwa marekebisho ama uchunguzi unafanyika kama vile mnavyomtaka JK kuwajibika!...
Guys tusiwe tunajadili mambo kwa ushabiki, haikatazwi lakini kidogo kuweni na uwezo wa kutoka nje ya hilo kabati lenu.
Tunapouliza maswali mengi ni kwa sababu tumeanza ku-notice Chadema kuwa ni chama ambacho kinaweza kuwa na Uwazi zaidi pia mwelekeo mzuri
 
Well said Mwanasiasa , waende Musoma na hasa Tarime wajue kuna nii huko. Chama Kipo washenzi wameenda CCM .
 
Ahahahahahah....ahahahahahahaha....Mwanakijiji vs. Lunyungu
It's hilarious!!!!!!!!
 
Kuna sababu nyingi zinazofanya watu wajiunge na chama fulani (chochote kile au cha siasa), na pia kufanya waondoke. Wengine ni kwa sababu ya maslahi binafsi ikiwemo kipato (fedha), cheo (mfano Ubunge) au umaarufu. Inafaa pia tukubaliane na kutokubaliana, wakati mwingine. Habari hii kutoka Uhuru inasaidia kuelewa hilo kuhusiana na mjadala unaoendelea hapa.


Chadema bado kwafukuta
Na Karume Malembeka, Kigoma
HALI ya kisiasa ndani Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), mkoani hapa imezidi kuwa mbaya tangu aliyekuwa makamu mwenyekiti wa taifa wa chama hicho, Dk.Walid Amani Kabourou alipojiengua na kujiunga na CCM.
Katika hatua inayoonyesha kudhoofika kwa chama hicho, kimemvua uanachama
mwenyekiti wake wa wilaya ya Kigoma Vijijini, Jeremiah Midaho, kwa
kinachoelezwa kukiuka maadili ya uongozi.
Mwenyekiti wa chama hicho mkoani Kigoma, Jaffari Kasisiko, aliwaambia
waandishi wa habari mjini hapa kuwa uanachama wa Midaho ulikoma kuanzia
Januari 5, mwaka huu, baada ya uongozi wa mkoa kutangaza suala hilo rasmi.
Kasisiko alisema uamuzi huo wa kumfukuza mwenyekiti huyo wa wilaya,
ulifikiwa na kikao cha kamati ya utendaji ya mkoa ya CHADEMA kilichokutana mjini Kigoma Desemba 28, mwaka jana.
Mwenyekiti huyo wa CHADEMA mkoa alisema Midaho amefukuzwa kwa
mujibu wa Katiba ya chama hicho, kifungu cha 5.4.3 kinachoelezea kukoma
kwa uanachama.
Kasisiko alisema Midaho akiwa mwenyekiti, morari na
utendaji wake ndani ya chama ulishuka kwa kiasi kikubwa, ambapo
mchango aliokuwa akiutoa haukuwepo kabisa, badala yake alianza kuwa
mzigo ndani ya chama.
Alibainisha kuwa awali, kiongozi huyo alikuwa na mchango mkubwa
ndani ya chama akifanya mambo mengine kwa kujitolea fedha zake za
mfukoni, lakini kuanzia Julai, mwaka jana utendaji wa kiongozi huyo
ulipotoka.

Mbali ya kushindwa kushiriki katika kazi za kuhamasisha uhai wa chama
na kwenda kinyume cha maadili ya uongozi, pia kiongozi huyo anadaiwa
kushindwa kuhudhuria mikutano muhimu ya CHADEMA katika ngazi za
mkoa na taifa.
Inaelezwa kuwa kujitoa kwa Dk. Kabourou CHADEMA na kujiunga na CCM, kunaweza kuwa pia kunachangia jambo hilo, kutokana na uswahiba wa karibu walionao watu hao.

Habari za ndani ambazo gazeti hili imezipata zinaeleza kuwa katika
uchaguzi mkuu uliopita, Midaho ambaye alishindwa kwenye kura za maoni za
chama hicho na Zitto Kabwe, alikuwa akipigiwa chapuo na Dk. Kabourou huku
Zitto akiungwa mkono na Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe.
Suala hilo lilizua mtafaruku baina ya kambi hizo mbili, na inaelezwa kuwa
hata baada ya uchaguzi kumalizika, na Zitto kushinda ubunge katika jimbo la
Kigoma Kaskazini, Midaho alikuwa haambatani na viongozi wenzake.


Habari za duru za kisiasa mkoani hapa zinasema Midaho alionekana kuwa na dalili za kutaka kujiunga na CCM, jambo lililowafanya viongozi wa CHADEMA
waamue kumfukuza, kuliko kupata aibu ya kuondoka kwake akiwa bado kiongozi.


Miongoni mwa nafasi alizowahi kushika Midaho kabla ya kufukuzwa
ni pamoja na ukatibu uenezi wa wilaya Kigoma vijijini, mgombea ubunge
jimbo la Kigoma Kaskazini mwaka 2000
, meneja wa kampeni wa Dk. Kabourou katika uchaguzi wa jimbo la Kigoma mjini na mjumbe wa mkutano mkuu wa taifa wa CHADEMA.
 
Nyani ondoa shaka . Hapa kuna unazi mkubwa naunafiki, mtu hata kura wala kadi ya kura huna ,ukifika TZ unakaa siku mbili kaa unakwenda at all , halafu unaanza kulinganusha siasa za US na TZ na kuleta unafiki kwamba wapinzani hawana mwelekeo sasa tuue vyama na kurudi huko yeye na ndugu wanako nufaika na kuacha Nchi inazama ? Ujinga huu rudi uje hapa uwanjani tupambanie hapa si US.
 
Nyani

Huyu Lunyungu anataka kutubabaisha tu yeye ndiye hasa anakula fedha ya walipa kodi. Yuko hapo ubalozini UK na watu wanaomtumia kesha kula pesa Sasa anamshambulia mwanakijiji ambaye inaonekana amemzidi kihoja na ana biashara zake Yeye Lunyungu ana nini? Wacha ngebe Lunyungu huo mrija ukikatwa unarudi bongo tu. Hatujaona hata tunda moja au mchango muafaka ambao umelifanyia taifa toka uje nje. Mwanakijiji ana redio etc. na watu wanapata habari murua kutoka kwa watu mbali mbali wa TZ. Unafikiri angekongomalia TZ angeweza hayo? Wacha unafiki. Wewe umeingia kwa jazba kwani kadi ya kura issue? Uliza majority ya wachangiaji hapa wako nje ya nchi ondoa pwagu na pwaguzi yako. kama wewe mkweli hebu weka jina lako sahihi kama mzee mwanakijiji.
 
Ole wewe ni mgeni hapa . Kaa tulizana na ujue watu wanaongelea nini . Mimi siwezi kuifanya kazi Ubalizoni maana huko so sehemu yangu . Huyu Mwana KJJ niachie wewe humjui .Radio yake ni sawa lakini anataka itumike vibaya na hapa ni kukata issue na kuleta kampeni za kijinga . Ole tafadhali tuendelee wanao nijua wamesha ona wewe una matongotongo maana unarukia issues .
 
Lunyungu

Wewe na mimi nani mgeni? Umejiunga rasmi 5/12/2006 na mimi rasmi16/12/2006 wacha ngebe weka facts mzee. Tulisaidie taifa kwa kuwa wakweli. kama hutaki kujibu ni sawa tu lakini mimi sijioni mgeni humu tangu mwaka jana unaweza kuangalia michango yangu.
 
Tatizo nasema hujui sana . Wewe unajidanganya na tarehe hizo ? Tuko hapa tangia Jambo ina anza tumehamia toka BCSTIMES . Nakuache unedelee kuwaka na tarehe ya kuingia hapa . Ndiyo maana nakuita wewe ni Mgeni sana hapa . Mzee Mwana KJJ ni wangu nakula naye tu hadi tuta acha ushabiki wa kijinga na kuangalia Tanzania na si ma Vyama .
 
Sasa kama wewe ni aluatan unaogopa nini kujibu swali dogo kama hili?
 
Sitabisha nawe kwa hili bali nasonga mbele tuonane kwenye michango mingine mzee Ole .
 
Sasa kama wewe mzee ambaye unajiita mkongwe (aluatan) unakataa kujibu swali dogo kama hili na kuweka kisasi kwenye mijadala ijayo ni mfano gani kwa taifa na wale tunaowapiga mawe? Umeamua kuvunja heshima ya hiki kijiwe? OK hapana noma.
 
Back
Top Bottom