The Only Thing We Have to Fear is Fear itself

The Only Thing We Have to Fear is Fear itself

CHADEMA: Tunasisitiza CCM ilitumia rushwa



Edward Ibabila, MUC na Magreth Kinabo


CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimeendelea kushikilia msimamo wake kuwa, matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa 2005, hayakuwakilisha matakwa ya wapiga kura na kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kilitumia rushwa kwenye uchaguzi huo.


Msimamo huo upo kwenye taarifa ya chama hicho iliyotolewa jana kwenye vyombo vya habari na Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa chama hicho, Erasto Tumbo.


Taarifa hiyo inasema, CHADEMA inashangazwa na kauli iliyotolewa na Katibu Mwenezi wa CCM, hivi karibuni, ya kupinga ukweli huo uliowekwa hadharani na Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, baada ya kumaliza awamu ya kwanza ya ziara yake ya kuwashukuru wananchi.


“Ni kweli kwamba CCM ilitoa rushwa katika uchaguzi na hili hata wakati wa kampeni CHADEMA tulilipinga, rushwa hii ilikuwa ni bidhaa mbalimbali kama khanga, sukari na maeneo mengine hata fedha taslimu. CCM ilijitetea wakati huo na kuiita ni takrima, mara baada ya uchaguzi Mahakama Kuu imethibitisha takrima ni rushwa,” imeeleza sehemu ya taarifa hiyo.


Inaeleza kuwa, hivi karibuni kwenye Mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCM, uliofanyika mjini Dodoma, Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho, Rais Jakaya Kikwete, aliwahimiza wanachama wa chama hicho kutojaribu kutumia rushwa kwenye uchaguzi wa chama hicho mwaka huu kwa sababu anawajua.


“Tumekuwa mstari wa mbele kuweka wazi masuala ambayo yana mazingira ya rushwa ikiwemo mikataba yenye utata, hususan kwenye sekta ya nishati na madini. Tulimsaidia rais kwa kuweka kama agenda yetu ya msingi kuwa mikataba ipitiwe upya, lakini kinachoendelea ni tofauti.


“Hata rais aliposema kwamba anawafahamu wala rushwa na anawapa muda wa kujirekebisha, tulimsaidia kwa kumueleza wazi kwamba rushwa ni kosa la jinai hivyo kama wapo hawapaswi kwa namna yoyote kupewa muda wa kujirekebisha,” inaeleza taarifa hiyo.


“Tunaendelea kuitikia mwito wa kushirikiana na chama tawala kukabiliana na rushwa, tunaitaka CCM na serikali yake ianzie kwa kuweka wazi kwa umma wamiliki wa Richmond ni hasara kiasi gani tumepata kama taifa na iundwe tume ya kuchunguza suala zima,” ilisema.


Taarifa hiyo inaeleza kuwa, Watanzania hawapaswi kuaminishwa kwamba suala la Richmond ni kitu kidogo, huu ni mkataba wa zaidi ya bilioni 260/-, fedha hizi zingeweza kugawiwa kwenye mikoa kama zile bilioni moja zilizotolewa na serikali kwa kila mkoa na kuendeleza wananchi.


Taarifa hiyo pia ilipinga taarifa zilizotolewa na baadhi ya vyombo vya habari kuwa CHADEMA, ilianzishwa wakati wa ukoloni kwa malengo ya kuendeleza Wachagga (Chagga Development Manifesto – CHADEMA).


Inaeleza taarifa hiyo kuwa chama hicho kilianzishwa na kusajiliwa mara baada ya Tanzania kuingia katika mfumo wa vyama vingi vya siasa na jina la chama hicho lilibuniwa na Simon Madete, ambaye ni Msukuma.


“Awali CHADEMA tulipuuza uzushi huu, lakini kutokana na kauli hizi kurudiwarudiwa, tunaamini kuwa uongo na upotoshaji huu unaweza kugeuzwa na umma wa Watanzania ukaaminishwa kuwa ndio ukweli.


“Safu za juu za uongozi wa kitaifa za CHADEMA zina viongozi sita, wenyeviti na makatatibu kati yao Mchagga ni mmoja tu ambaye ni Mwenyekiti wa chama Taifa, Mbowe, wengine ni Muiraq, Myao, Mpemba na Muunguja,” ilisema taarifa hiyo.
 
Janja ya nyau tikisa makiaaa aaa aaa a a a a eh! Ha ha ha ……………….
 
Lunyungu aka kiliba

Wewe usivamie watu tu, ulikuwa unajifanya aluatan maswali madogo tu haya unajizungusha weka ukweli hapa. tangu lini aluatan akashindwa na maneno madogo kama hayo anahitaji tafsiri?

Nenda muulize anayekulipa kwani huna muda utarudi nyumbani ndiyo unafiki utakapokwisha. KASHESHE ZENU ZA UBALOZINI HUKO HUKO SIO HAPA.
 
Ole weweeeeeeee ole wako kijana . Unajau maswali huwa hayajibiwai unavyo taka wewe ia kadiri mjibu maswali anavyo taka kujibu sasa hujaelewa majibu yangu ama ?
 
Mzee mwana KJJ njoo dar mimi niko Dar Mzee usiwakilize hao watu wasio kuwa na taarifa sahihi . Nasema njoo tusemee hapa sote Mzee . Tupingane kwa uso kwa macho Mzee. OK tuendelee na mada haya mengine unaweza kuni PM .Karibu Dar
 
Sasa wewe mwenye taarifa sahihi eh! Ugomvi wako na wahaya etc wa ubalozini utakupeleka pabaya. hapa tunakata issue za kitaifa sio za kibinafsi.
 
Tukumbuke kuwa Kabourou na Nkomola walipotangaza kuhamia CCM walipokelewa na Makamba pale Bomangombe, Hai, Kilimanjaro. Wakatoa sababu zao za kuikandya Chadema. (Nkomola alishakwenda SAU). Walipomaliza tu, Makamba (jinsi asivyo na dogo) akawaambia wananchi" Hawa wapinzani wanaohamia CCM wanakuja kuganga njaa zao wenyewe..."

Laiti Mwanakijiji angeyatafakari maneno haya ya Makamba. Anazijua njaa zao...
 
Kichwamaji, hivyo viongozi wote walioko Chadema ambao hawajahama hadi hivi sasa, wameshiba na tusitarajie kiongozi yeyote kuhama?
 
Wanaganga njaa? Na hii baada ya kuwakaribisha? CCM kuna mambo.
 
Kichwamaji, hivyo viongozi wote walioko Chadema ambao hawajahama hadi hivi sasa, wameshiba na tusitarajie kiongozi yeyote kuhama?

Mwanakijiji, jadili hoja iliyo mbele yetu. Usilete za CCM wanaulizwa hili wanaleta lile. Nasema hivi, Katibu Mkuu wa CCM anasema hivyo. Wewe unampinga? Unawajua hao kuliko yeye anayewakaribisha? Tunajadili hoja ya Makamba hapa, aliyokuwa anawaeleza kina mwanakajiji wengine. Ningetarajia mwanakijiji amuulize swali makamba, atafakari kauli yake hiyo, aache ushabiki tu. Akue, akomae!
 
Kichwamaji,
Ebu tufunulie juzuu hii basi?...
Kweli hata mimi nimetoka mtupu zaidi ya kuifikiria kuwa wale jamaa walikuwa na njaa kali Chadema ndio maana wamehama...
Je, ni kweli Chadema kuna njaa!... kama hakuna basi Makamba alikuwa na maana nyingine tofauti ambayo bado inanipa shida!
 
Ebwana hivi huyu Kiliba si ndio Tafiti Then Jadili sasa Lunyungu amekuwaje Kiliba tena?
 
Kumbe we unamfahamu. Alinibatiza hilo jina sasa mimi nilikuwa sijui maana yake kwa hiyo niliamua kumwita hilo jina lake as Lunyungu aka kiliba - jasho litamtoka. Inaelekea ana ugomvi na wahaya etc. Angalia post zangu utaona yalikoanzia na kuna mwingine Tabasamu amenipachika majina ya jamaa wengine humu.

Anyway unajua Mzee Es amesema anarudi kabla ya jumapili kusettle issues tutaona sasa wale waliokuwa wanamkashifu.
 
Lakini mkandara alisema atamshika shati kabla hajafika airport.
 
Wacha.....Queen Es wala asikukoseshe raha.....hana lolote zaidi ya mikwara tu. Eti anachimba biti atarudi kusettle deni....deni my foot. Bring it on
 
Back
Top Bottom