mheshimiwa mbowe karibu sana ,kwa kweli jambo ni sehemu pekee ambapo hoja za msingi zinajadiliwa bila woga ,nafikiri bora sisi wengine tufiche majina ,huku nyie makamanda mtapata mambo mengi ya kuiweka sawa nchi ,ni matumaini yetu kuwa hoja ZETU HUKU ZITAPATA mbebaji.
muheshimiwa huku tuna uchungu sana na nchi yetu ,mara nyingi nakaa najiuliza tungepata hata asilimia 10% ya wananshi wawe na ufahamu kama wa wana forum ,tusingekuwa tunaletewa mikataba kama ya kina cifu mangunga,ea richmond.naomba kutoa changamoto ya kupatikana gazeti lisilohitaji faida na radio [mf butiama ] ambayo itakuwa funded ili maono kama haya yawafikie wananchi wengi wale wa vijijini ,tatizo kubwa haya magazeti mengi yanayotegemea matangazo ya serikali na hata lile RAI tuliloliamini sasa yamegeuka ya mtandao,hata lile la kwako ukitaka kuliendesha kibiashara ni vigumu kama utakuwa too critical....
la mwisho mmenisikitisha sana CHADEMA na wapinzani kwa ujumla kutokwenda mahakama ya east africa kupinga ule uchaguzi ,,,bado muda upo naomba tuitumie mahakama ile ,hii ni mara ya pili ccm kupitisha wapinzani dhaifu kumbuka ya zitto kabwe kukosa ubunge wa africa na sasa hili.
karibu sana!!!