The Remainder...

MwanajamiiOne

Platinum Member
Joined
Jul 24, 2008
Posts
10,470
Reaction score
6,580
Mwanamke huwa kama pasi huchelewa kupata joto na hutunza joto kwa muda zaidi hata baada ya kumaliza kupiga pasi. Kwa wengi wetu huwa inatokea either kusahau au kujifikiria wao wenyewe. Utakuta baba akirudi toka kazini na kumkuta mkewe nyumbani humsalimia na kwenda zake chumbani kubadilisha nguo za kazini.

After that anapata chakula cha usiku (Dinner) then anaanza kutazama TV au kupitia magazeti yake na kuyasoma.

Muda wa kulala umefika anaenda kuoga na kuvaa pajama zake; mke naye anaenda kuoga na kufanya sawa na mume. Wanapanda kitandani, mume anampapasa mke, mke naya anajua mzee anataka maana ndiyo sex code yake akinigusa kwa mtindo huu maana yake anataka tuwe mwili mmoja na anajisikia kama kusumbuliwa maana alikuwa hajui kama mzee atataka kutokana na kutowasiliana hata hivyo anamkubalia.

Baada ya dakika chache wamemaliza, wapo kimya na mzee anapiga usingizi.
Mke anajiona kama ametumiwa tu kwani hakukuwa na raha yoyote ni kuumizwa tu kwani mwili haukuwa connected hisia.

Mwanaume ni rahisi kusisimka kimapenzi wakati mwanamke huhitaji kusisimuliwa. Mwanaume husisimuliwa na moja ya mlango wake wa fahamu kupitia kuona (sight) wakati mwanamke husisimuliwa kupitia milango yote mitano ya fahamu Kuguswa, kusikia, kuona, kuonja, kunusa na wororo (tenderness) wa mwanaume. Mwanaume ni mfano wa bulb ya umeme uki-switch tu mara moja inawaka wakati mwanamke ni mfano wa pasi ya umeme ambayo huchukua muda hadi ipate joto na hutumia muda zaidi to cool off.
Hii ni muhimu sana ukitaka kuwa mpenzi mzuri na mpenzi mzuri hujua na kuzingatia jinsi ya kumridhisha mwenzake.

Mwanamke anaongozwa na highway ya emotions, atajisikia vizuri sana kama alikuwa na idea kwamba kutakuwa na kuwasha pasi yake ya umeme mapema.
Itakuwaje kama wakati wa kuondoka asubuhi mume akampa mke busu la uhakika na kumnong’oneza mkewe kwamba “vipi unaonaje leo usiku ukawasha pasi mapema kwani nina hamu sana kupiga pasi nguo kwani naona bulbu yangu ina mwanga wa uhakika leo".

Nahisi mke atashinda anaweza jinsi ya kuhakikisha pasi yake inawaka chapchap usiku na ikitokea na mchana akaambiwa neon linguine mwororo inaweza kuwa jioni yenye mwako wa mahaba.

Lakini kwa wengi wetu huwa ni kinyume na hayo na ndio maana wakati mwingine ukipapasa usiku unaambiwa “baba nanii leo kichwa kinaniuma sana” au “nimechoka sana” au “unapata zero participation na kuambiwa maliza haraka” au pasi inakuwa kavu kabisa matokeo yake ni pasi inagoma kuwaka na kuanza kuumizana.

Jifunze kuwa mwanaume mwororo (tenderness) wasiliana na mke, tafuta muda wa kumsikiliza, cheka naye, cheza naye, ongea naye, mpe mgusu (touch), mkumbatie na kumbusu hata kama si wakati wa sex ni wako na ni wewe uliamua kuishi naye.

Mwanaume humtengeneza mwanamake!

Source: The Hill Of Wealth
 
Good stuff! Ila wengine tunajua wajibu wetu.....sasa na wale wadada kila siku anaumwa kichwa hajisikii bila sababu, baba anamlamba hadi macho bado tu inakuwaje?
 
MJ1,
Unawakilisha shosti..... toa somo hadi kieleweke!

Mamii kwani ni mie shost? hiyo web niloweka hapo kama source ina vitu vizuri sana kuhusiana na mahusiano. Kila nikiyasoma yaliyomo humo huhishi kwamba yanatugusa sana. Kwa kweli wenzetu hawa huwa wanajisahau. Ni wazuri sana na ni wabunifu wanajua kukupagawisha but akishakuoa na kukuzoea haya yote husahaulika. Sijui ni ubuzy au ni nini?

Matokeo yake mahusiano yakidorora utasikia lawama kwa wife oh umezembea sana, mara mwanamke ubunifu asa huo ubunifu si kwa mwanamke tu jamani hata wanaume!!

Nachelea nsijepigwa ngumi hapa akija Mbu, Fidel, Msanii, Bonnie e.t.c ntashambuliwa mie hadi nikome. Jamani si wanaume wote wanajisahau auh baadhi.

Hivi ukisoma hapo inaonyesha kama huwa ni mwanaume tu ndie anapataga hisia, je mdada akitaka kuwasha pasi yake usiku ni ishara gani anatakiwa atoe ili kumjulisha mwenzie kuwa usiku kuna overtime? Au wao haijalishi?
 
Good stuff! Ila wengine tunajua wajibu wetu.....sasa na wale wadada kila siku anaumwa kichwa hajisikii bila sababu, baba anamlamba hadi macho bado tu inakuwaje?


Kweli kabisa Masanilo ni baadhi yenu si wote.
Hawa wa hivyo huwa wanakuwa na sababu ambayo hajataka kuisema. Inawezakana kabisa kuwa kuna kitu umemkosea but hakwambii na huichukulia tendo kama ndo adhabu sahihi kwako. Chunguza labda kuna ambacho uliahidi hujatimiza na yeye amechoka kukumbushia!

Lakini tell us the truth hivi wa hivi si ukimgusa the right button anakuwa hana ujanja au ni mpaka akili itoe go ahead?
 

MJ1
hata mhadhiri si inabidi atayarishe somo kwa kutafuta material ya kutosha kutoka kila kona?
Nakupongeza kwa kutafuta info na kuiweka hapa ili watu wakasome wa improve mahusiano yao.
Suali zuri umeuliza..inakuwaje kabla hujawa wake wa maisha mpagawisho unakuwa baabkubwa ila baada ya... mambo hugeuka?
Ni kama kutega ndege na ulimbo/chambo... humtafutia kile kitu chake akipendacho na kumtegeshea..akishampata..huyo ndege atajiju!..hahahah just kiddn!
 
Good stuff! Ila wengine tunajua wajibu wetu.....sasa na wale wadada kila siku anaumwa kichwa hajisikii bila sababu, baba anamlamba hadi macho bado tu inakuwaje?


kwa kujifagilia sikuwezi

Mwanajamii topic nzuri sana hii nadhani kina baba watajifunza kuacha ubinafsi.
 
MJ 1,

Ushauri mzuri sana. Binafsi nitajitahidi kubadilika.

Lakini pia najiuliza nini nafasi ya mwanamke katika suala hili? Yeye hawezi kuwa initiator kwa kuweka appointment asubuhi 'mzee' anapotoka kwamba jioni/usiku angependa pasi iwashwe? Mara nyingi wanawake wanakuwa 'waoga' kuanza hata kwa mume wake wa ndoa. Ni kwa nini?

Binafsi huwa najisikia vizuri sana mke wangu akianza yeye kusema anahitaji/anahamu ya majamboz.
 
Hakuna cha fagizi wala nini....ngoja mama Masa atakuja awape ushuhuda...naye ni memba hapa.....hakuna cha ubinafsi jamani wakina mama nao wanamchango mkubwa tu...si lazima baba awe ndo kisusio bwana....wee jaribu kuwa naked unatingisha tigisha tiGo mbele yangu hata gazette halitosomeka na TV itazimika....kupigana mashine hadi majogoo!


kwa kujifagilia sikuwezi

Mwanajamii topic nzuri sana hii nadhani kina baba watajifunza kuacha ubinafsi.
 


SMU nakupongeza kwa kukiri kuwa umejisahau kidogo (mara nyingi wingi wa shughuli na maisha hutufanya tukajisahau). Ndio maana nikasema ni kujikumbusha tu.

Hata mie naamini kabisa kuwa mke naye anayonafasi ya kutoa indicator kuwa mzee jioni una kazi ya ziada hata kwa kukutumia kisms cha uchokozi. Ni kweli wengi wetu huwa na kijiaibu but with the use of sms tu unawezakufikisha ujumbe kwa mzee.
 
MJ1
Kwani wewe una pasi ya aina gani?
Phillips,National au..............
Pasi nyingine zinachelewa kupata moto.
 
MJ1
Ni kweli kwa baadhi ya watu ila kama ujuavyo hata wanawake nao wanatakiwa kuwaandaa pia waume zao. Mfano lazima wawe ni wabunifu wa kubadilisha staili mabalimbali. Pia decoration za chumbani nazo ni muhimu. Na hapa mhusika mkuu ni mama! Vile ambavyo utajiweka ndivyo ambavyo utamwatract mwenzio.
Lakini pia niulize jamani pajama za nini humo chumbani mwenu? Msije mkanambia na kofuli nazo mnavaa! Jamani tunatakiwa kufeel ngozi ya mwenzio na sio chini ya nguo. Na riha tamu yatosha kuamsha hisia. Sio mama katoka kukamua ng'ombe anakuja na harufu yake ya zizini halafu utegemee jamaa asisimke!
 
MJ1
Kwani wewe una pasi ya aina gani?
Phillips,National au..............
Pasi nyingine zinachelewa kupata moto.

...... Ah nijuavyo mie wote tuna za umeme aina tu ndo tunatofautiana. Hata hiyo yote ya yote ni kwamba tunachelewa kupata moto si kama ninyi wenzetu mkiona tu badi suruali zinakuwa matatani. Sie mpaka 'tuguswe' vilivyo. Bahati mbaya wanaume wengine wakisikia wanawake shurti uwaguse basi wao kurupu hukimbilia kugusa kule- yaani unawezakuta mtu karudi kwanza kachelewa we ushalala basi kono hiloo keshapeleka kule anasugua sugua yaani ni karaha tupu. Kukusa si lazima uguse kwa mkono na si lazima uguse kule jamani ah peck kiss ya shingoni can do better than the finger in there. Hata maneno matamu tu kwani si wanasemaga kuna kitu ninaitwa cyber lovemaking? hii inakuwagaje kwani? hatuwezikuifanya kwenye simu zetu kama matayarisho ya kupasi?
 

Eeka shemeji umemaliza yote. i couldnt put it better than this. Aksante sana.

Jamani kina dada/mama somo hili hapa katoa Eeka.
 

Wanasahau hawa "Ukiolewa kulala bila chupi ni wajibu"
 
Ah ninyi mbona wapo wanaolala na bukta? ukiwauliza wanakwambia huwezijua bwana lolote lawezatokea mfano moto ukiwaka usiku unawezajikuta umetoka nje bila nguo asa sijui wanawake hawatatoka nje!
 
...pasi hiyo pasi gani, 'ushapanda' kitandani yenyewe haijawaka tu? 🙂
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…