The rise and fall of Colonel Muamar Gadaffi

The rise and fall of Colonel Muamar Gadaffi

Hakuna demokrasia kule Libya wala nini. Jamaa ni dikteta na lazima atoke. Kama kuna demokrasia kama unavyo dai wewe, kwanini watu wanaandamana?

Jibu lipo wazi, ka-dafu lazima achapwe mijeredi mpaka ajifuinze adabu.

Amen!!!!
 
Haya mapumziko kidogo sasa.
cf0d24594782f10b169c7eb.jpg

Haya mkuu naona mambo ya Vegas siyo!!
 
Umoja wa Afrika eti sasa ndiyo wanakuja na kauli ya kutaka mashambulizi dhidi ya Libya yasitishwe mara moja. Walikuwa wapi kumshauri mfalme wao Ghaddafi asitumie nguvu dhidi ya waandamanaji au kutii agizo la umoja wa mataifa la kusitisha mashambulizi dhidi ya raia wake?.

Hii ni aibu sana kwa viongozi wa Afrika, badala ya kuchukua leadership role wao walikaa kimya, sasa jamaa yao anakula kichapo wanaona kuwa huenda hii ndiyo itakuwa ni standard hasa kwao ambao wamezoea kutawala kwa ngumi ya chuma. Kama walibya na waarabu wanaunga mkono mashambulizi haya wao ni kina nani kuyalaani?

Walitaka Ghadafi abakie madarakani kwa kuua raia wake ili na wao watumie kama mfano kwa raia wao kuwa atakayeleta fyoko watamshughulikia kama Ghadafi alivyowashughulikia waliompinga, sasa kipigo hiki hakivumii upande wao kabisa.
 
Nimemshuhudia jirani yangu wa kushoto akinyolewa bila maji na mara sijakaa sawa jirani yangu wa kulia naye huyoo yanamkuta, kweli bado sishtuki tu ? Ningekuwa mimi ningejisemea lo, miaka arobaini na zaidi yatosha hakuna haja ya kuzidi kung'ang'ania madaraka. Haraka haraka ningekaa chini na wapinzani wangu na kwa pamoja kupanga namna ya kufanikisha mabadiliko ya utawala kwa amani.

Lakini siyo Gadafi, kwa akili yake hakuna mwingine kama yeye na hata kama itatokea yeye asiwepo kwa sababu yoyote ile, ukoo wake upo na wanaye watano si wapo ? Kwa watu kama Gadafi ambaye hata kuingia madarakani alitumia hila, ni vigumu kwao kufikiria kuwa kuna wazalendo Libya zaidi yake. Hao kina Ben Ali na Mubarak walishindwaje kutumia vyombo vya dola dhidi ya wananchi wao ?

Gadafi angekuwa mjanja angeng'amua mapema kabisa kuwa hawezi kuyazuia mabadiliko kwani muda wake Libya ulikuwa umefika. Nina hakika angefanya la maana kama angeyasikiliza madai na kutilia maanani hoja za Walibya waliochoka na utawala wake. Angefanya hivyo bila kumwaga damu ya watu wasio na hatia, angeweza kujijengea heshima na kubaki shujaa nchini humo.

Kama atakuwa alishajichimbia shimo kama Sadam Hussein, haraka atumbukie humo ajiifiche kama panya na hapo labda ataweza kujiongezea siku chache. Hapa kwetu tofauti ni kuwa badala ya Gadafi tuna CCM na siku zinavyosogea ndivyo wanavyozidi kutumia kila hila kubaki madarakani. Hata hivyo siku zao za kujificha pangoni zinakaribia kwa kasi mpya na ari zaidi mfano wa sikio la kufa.
 
AFP Wire:
The African Union: Calling for immediate stop to attacks on Libya.
Sky reporting RAF Tornados fired StormShadow after flying 3000m from RAF Marham - longest range RAF bombing since 1982.​
 
Check out this peace of info...Kipengele kinachotafsiri hiyo security council resolution 1973(2011)ammbapo kuna pahala wanasema watatumia "all means neccessary except foreign troops and occupation."
http://www.guardian.co.uk/world/2011/mar/17/libya-united-nations-air-strikes-live#block-17
http://www.guardian.co.uk/world/2011/mar/17/libya-united-nations-air-strikes-live#block-17

Source: AP news

My Take:Kama nilivyojiuliza hapo nyuma,je mapinduzi haya ni kweli ni ya wananchi wa Libya?Mimi nasapoti mapinduzi ya kweli ya wananchi na si blah blah za wahuni wachache.
 
amelewa madaraka na anaona Libya belongs to him and his own sons, na si vinginevyo. Hilo ndio tatizo la watawala wengi wa kiafrika, wanangang'ania kukaa miaka nenda miaka rudi kama vile wao ndi wenye uhalali wa kuongoza. siku zake zimekwisha.
 
AFP Wire:
The African Union: Calling for immediate stop to attacks on Libya.
Sky reporting RAF Tornados fired StormShadow after flying 3000m from RAF Marham - longest range RAF bombing since 1982.​

AU ni kichekesho bora wake kimya tu kama alivyokaa kimya Chavez na China maswahiba wa Gadafi
 
"We have launched Tomahawk Land Attack Missiles from a Trafalgar Class submarine and Stormshadow missiles from Tornado GR4s. The fast jets flew 3,000 miles from RAF Marham and back making this the longest range bombing mission conducted by the RAF since the Falklands conflict. This operation was supported by VC10 and Tristar air-to-air refuelling aircraft as well as E3D Sentry and Sentinel surveillance aircraft.

"HMS Westminster is off the coast of Libya and HMS Cumberland is in the region ready to support operations. Typhoon aircraft are also standing by to provide support.
 
Check out this peace of info...Kipengele kinachotafsiri hiyo security council resolution 1973(2011)ammbapo kuna pahala wanasema watatumia "all means neccessary except foreign troops and occupation."
Source: AP news

My Take:Kama nilivyojiuliza hapo nyuma,je mapinduzi haya ni kweli ni ya wananchi wa Libya?Mimi nasapoti mapinduzi ya kweli ya wananchi na si blah blah za wahuni wachache.
Kwa kifupi NATO wanawasafishia njia Rebels waende Tripol kuchukua nchi?
 
hawa washenzi wamerekani na wenziwe wanatakiwa kulaaniwa.

na kama ningekuwa nna sauti umoja wa mataifa tungetangaza kusitisha uhusiano na nchi zote zitazoishambulia libya.

pia tungezitaka nchi za afrika kupeleka jeshi libya kupambana na uvamizi wa kishenzi wa mbwa hawa

waaafrika tuamke tusiendeshwe na kutawala na hawa wapumbavu kwa maslahi yao
 
03:16 The Guardian Qatar's prime minister has told local new channel al-Jazeera that Qatar will definitively participate in the military action in Libya
"Qatar will participate in military action because we believe there must be Arab states undertaking this action, because the situation there is intolerable…. it has become an open war involving mercenaries. I think that this is an issue that must stop very quickly," Prime Minister Sheikh Hamad bin Jassim al-Thani said,
 
Kwa kifupi NATO wanawasafishia njia Rebels waende Tripol kuchukua nchi?
Inategemea na msimamo wa wananchi wa Libya,soma posting yangu iliyopita na comment aliyotoa Dr....inawezekana tumelishwa propaganda,kuna wananchi wasiotaka mambo hayo ya vita,nchi inaweza kugawanyika kwasababu sidhani kama rebels nao watapata sapoti everywhere lets say Tripoli,sidhani.
 
hawa washenzi wamerekani na wenziwe wanatakiwa kulaaniwa.

na kama ningekuwa nna sauti umoja wa mataifa tungetangaza kusitisha uhusiano na nchi zote zitazoishambulia libya.

pia tungezitaka nchi za afrika kupeleka jeshi libya kupambana na uvamizi wa kishenzi wa mbwa hawa

waaafrika tuamke tusiendeshwe na kutawala na hawa wapumbavu kwa maslahi yao

Mkuu tatizo nchi zetu ni ombaomba.
Waafrika hatujakatazwa kuwapa kichapo US na washirika wake. Cha msingi jiulize maswahiba wa Gadafi wakao wapi? I mean China, Chavez, Ahamedinajad, Russia, Tanzania etc.
 
Back
Top Bottom