The so called 'GOD' from religions

The so called 'GOD' from religions

Due to each society getting knowledge of good and evils by accident from their conscience

that could be the very reason in Kirangaz society they eat their neighbour while in nyani ngabu society they honor their neighbour

It is said that evolution of human being started in Africa
Can one volunteer telling me where the evolution of moral laws started from ?
Kiranga
Nyani Ngabu
Kwanza kabisa, andika katika lugha unayoifahamu.

Ama sivyo utatuletea vituko hapa.

Hayo madudu gani sasa uliyoandika?

Kwani kuandika kiingereza lazima?
 
Hata mnaoamini mungu wenyewe hamkubaliani mungu wa kweli ni yupi.

Mtatushawishi vipi sisi tusioamini mungu kwamba mungu yupo?

Uislamu, Ukristo na uyahudi haziwezi kuwa na mungu wa kweli kwa sababu idea ya huyu mungu inajipinga yenyewe.

The Abrahamic godhead is an inherrent contradiction.

Ni kama "pembetatu duara". Haipo, inasemeka tu.
 
Kwanza kabisa, andika katika lugha unayoifahamu.

Ama sivyo utatuletea vituko hapa.

Hayo madudu gani sasa uliyoandika?

Kwani kuandika kiingereza lazima?
Mkuu haukumwelewa au ndo umeshindwa kumjibu swali lake kwa kukutafuta vijimakosa na kuhamisha mada!
 
Mkuu haukumwelewa au ndo umeshindwa kumjibu swali lake kwa kukutafuta vijimakosa na kuhamisha mada!
Kuna aina fulani ya uandishi inafanya msomaji ahoji uwezo wa muandishi.

Nikiona mtu anaandika kwa namna hiyo naanza kujiuliza kwamba hata nikimjibu ana brain cells za kunielewa.

Swalo lake uliloliona linaweza kuwa na ugumu wa mimi kuliepa ni lipi?

Maana mimi nilivyosoma Kiingereza cha ajabu nimetaka kutapika mpaka swali lenyewe nikawa silioni tena.
 
Tena mnyukano mkali.
Hakuma mnyukano kama wanaosema mungu yupo wamepewa nafasi ya kuthibitisha na hawajaweza.

Hakuna mnyulano kama wanaosema kina mungu hawajaweza ku reconcile the problem of evil.

Hakuna mnyukano kama wanaosema kuna mungu wenyewe hawakubaliani mungu sahihi no yupi kabla hata ya kuwajibu wanaosema mungu hayupo.

Wanaosema kuna mungu wamenyukwa tu.

For starters hawawezi kuthibitisha kwamba mungu yupo.
 
Kwanza kabisa, andika katika lugha unayoifahamu.

Ama sivyo utatuletea vituko hapa.

Hayo madudu gani sasa uliyoandika?

Kwani kuandika kiingereza lazima?
Umejitahidi kuelewa meweza ukapata tundu la kutokea.
Ujuzi wa mema na mabaya hautokani na hauwezi kutokana na kitu chochote isipokuwa ni sehemu ya uumbaji.
Kama huiamini uwepo wa muumba eleza namna ujuzi WA mema na mabaya binadam kaupataje ?
 
Umejitahidi kuelewa meweza ukapata tundu la kutokea.
Ujuzi wa mema na mabaya hautokani na hauwezi kutokana na kitu chochote isipokuwa ni sehemu ya uumbaji.
Kama huiamini uwepo wa muumba eleza namna ujuzi WA mema na mabaya binadam kaupataje ?
Kwa nini unasema ujuzi wa mema na mabaya hauwezi kutokana na kitu chochote isipokuwa uumbaji?

Mema ni yapi na mabaya ni yapi?

Kwa nani?

Na kwa nini uumbaji utoke kwa mungu tu na si kitu kingine chochote?
 
Hata mnaoamini mungu wenyewe hamkubaliani mungu wa kweli ni yupi.

Mtatushawishi vipi sisi tusioamini mungu kwamba mungu yupo?

Uislamu, Ukristo na uyahudi haziwezi kuwa na mungu wa kweli kwa sababu idea ya huyu mungu inajipinga yenyewe.

The Abrahamic godhead is an inherrent contradiction.

Ni kama "pembetatu duara". Haipo, inasemeka tu.
Kutokukubaliana kuhusu yupi Mungu wa kweli haiwezi kuwa sababu ya kutokuwepo kwake.
"Mr pembe Tatu duara"

"Inherent contradiction " inatokana kukariri kwako sifa za Mungu pasipo fikra.
Umekumbushwa ulimwengu ambaobumetokea kwa ajali hauna maovu kwa kuwa kipimo cha utambuzi wa maovu kinakuwa hakuna kwa kuwa ili uitwe uovu lazima utendwe na binadam dhidi ya binadam jappo kuna kuhangsika kwingi kutafita maana mbdala.
Kama uovu ukitendwa dhidi ya binadam na ukajua ni uovu ina maanisha umeweka thamani kwa binadmu husika na hiyo inakinzana na marlezo yenu kuhusu chanzo cha binadam.kuwa ni matokeo yasiyopangiliwa.

Tatizo lako ni kukariri ndiyo sababu huwezi kuelewa mambo madogo kama ya mema na msbaya kutohusika na ninyi kwa kuwa binadam asiyeumbwa anaendeshwa na matamanio ya mwili wake na kutii matamanio ndiko humfanya atende chochote sasa ninyi msiomjua Mungu mmepata wapi ujuzi wa mema na mabaya
Zindukana wewe
 
Hakuma mnyukano kama wanaosema mungu yupo wamepewa nafasi ya kuthibitisha na hawajaweza.

Hakuna mnyulano kama wanaosema kina mungu hawajaweza ku reconcile the problem of evil.

Hakuna mnyukano kama wanaosema kuna mungu wenyewe hawakubaliani mungu sahihi no yupi kabla hata ya kuwajibu wanaosema mungu hayupo.

Wanaosema kuna mungu wamenyukwa tu.

For starters hawawezi kuthibitisha kwamba mungu yupo.
Ufundishweje wewe ?

Evil is a problem to believers

Unajuaje kuwa ni hili ni evil na jingine ni good ,wakati mnakuwa mnatii kiu ya miili yenu ?
 
Kwa nini unasema ujuzi wa mema na mabaya hauwezi kutokana na kitu chochote isipokuwa uumbaji?

Mema ni yapi na mabaya ni yapi?

Kwa nani?

Na kwa nini uumbaji utoke kwa mungu tu na si kitu kingine chochote?

Mema au mabaya wakati wote ni kutoka kwa binadam au dhidi ya binadam
Mpaka uite ni ubaya ni kwa kuwa unaamini kuwa tendo hudika linaharifu thamani au utu wa binadam
Kwa mtazamo wa wakana Mungu binadam ni matokeo ya mchakato usio na lengo maalum hivyo binadam matendo yake hutokana na msukumo toka kwenye vinasaba kwa kadri ya mazingira na nyakati

Ukweli ni kinyume na mtazamo huo, ukweli waonyesha binadam wanakitu ambacho kinafanana kwa wengi walio kawaida nacho ni kwamba wanatambua thamani zilizopo kwa kuwa kwao binadam na ndipo wote kwa umoja wao hujikuta wakitambua baadhi ya mambo kuwa ni maovu na mengine kuwa ni mema.
Ndipo nikakuonyesha kwamba ingekuwa matendo dhidi ya binadam ni matokeo ya ajali jamii yako kula majirani zao ingekuwa sio uovu bali wanatii kiu ya vinasaba vyao !

Mema ni yale yasiyo halifu utu wa MTU na mabaya ni Yale yanayohslifu na kumwondolea bimadam thamani yake.
Kwa binadam au dhidi ya binadam

Kitu kinginecho chenyewe kitakuwa ni matokeo na sio kisababishi kisichosababishwa.
Hicho kitu kingine ili kiwe na sifa ya kuumba kinafaa kiwe chenyewe sio matokeo ya Uumbaji.
 
Each one of you would like to convince each other who is right and who is wrong.That is the definition of BELIEF.
 
H1N1 said:
Wewe jamaa ni kama mbwa MZEE hufundishiki. Huwezi kukiri udhaifu wa mawazo ukionyeshwa kwa picha kubwaaa
We binti,jifunze adabu kwanza,sio unatukana watu usio wajua

Swali la msingi alilouliza Kiranga hamjalijibu mpaka sasa,

Mdahalo utaendeleaje kama hamtaki kujibu maswali ya msingi?

Msingi wa swali la Kiranga ni huu;

Suppose,kuna radi imepiga katika msitu

Ikasababisha moto mkubwa[Forest fire]

Moto huo ukasambaa kwa kasi na kwenda kuteketeza kambi ya wakimbizi

Idadi kubwa ya watu waliokufa ikawa ya kina mama wenye mimba na watoto wachanga

Kama Mungu mwenye ujuzi wote yupo,basi aliliona hili tukio mapema kabla halijatokea na akajua jinsi ya kulizuia.

Mungu mwenye upendo kwa viumbe wake,asingependa hili tukio liwapate watu wake,haswa wale watoto wachanga.

Na Mungu mwenye nguvu zote,asingeshindwa kulizuia hili tukio baya

Lakini tukio limetokea,kwanini?

Mungu alitaka kulizuia lakini akashindwa?

Au alikuwa na uwezo wa kulizuia lakini hakutaka?

Au vyote kwa pamoja?
 
Kiranga said:
Hakuna mnyukano kama wanaosema mungu yupo wamepewa nafasi ya kuthibitisha na hawajaweza.
Mkuu,tangu uanze kuomba uthibitisho bado tu hawajakupa?

Hawa watu ni timamu kweli?

Hakuna mnyukano kama wanaosema kuna mungu hawajaweza ku reconcile the problem of evil.
Na hili ndiyo swali la msingi,wanalotakiwa kulijibu

Cha kushangaza wanalikwepa,hata yule dada kashindwa[Mish]?

Hakuna mnyukano kama wanaosema kuna mungu wenyewe hawakubaliani mungu sahihi ni yupi kabla hata ya kuwajibu wanaosema mungu hayupo
Maajabu sasa,kila dini inadai Mungu wao ni mwenye nguvu zote

Hii kitu kimantiki ipo sahihi kweli?

Tunaweza kuwa na computers mbili,zinazoweza kushinda kila mchezo wa drafti[chess] bila kutoa sale?

Na tukizipambanisha,ipi itashinda kama kila computer ina uwezo wa kushinda bila kutoa sale hata mechi moja?

Wanaosema kuna mungu wamenyukwa tu.

For starters hawawezi kuthibitisha kwamba mungu yupo.
Tuwaiteje sasa?misukule?
 
Unaposema hayupo Mungu,ndio umethibitisha kuwepo,ni sawa kusema fulani hana akili,ni kuwa iko akili lakini kwa fulani ndio haziko hizo akili.
Kwa hiyo wewe unayesema Mungu hayuko,hayuko kwako,lakini yupo,hayupo kwako kwa sababu hutaki kukubali yupo,wakati Mungu yupo.
 
Tukisema kuna akili,ni nani akili kaiona,hakuna aliyeiona akili,lakini twajuwa akili ipo,kutokana na matokeo tunayoyaona,kutoka kwa hiyo akili.

Na tukisema Mungu yupo,ni Yupo kutokana na MATOKEO tunayoyaona kutoka kwa huyo Mungu.Maisha yako yote mwana wa Adamu,yanaendeshwa,na mpaka unafikia kufa,unakufa bila kupenda,upende usipende utakufa.Kwa hiyo yupo anayeendesha maisha yako,naye ni huyo unayesema hayupo,wakati matokeo ya kuwepo kwake,yanaonekana.
Ukisema Mungu hayupo,huo ni uthibitisho tosha wa kuwepo Mungu.
 
Mkuu,tangu uanze kuomba uthibitisho bado tu hawajakupa?

Hawa watu ni timamu kweli?


Na hili ndiyo swali la msingi,wanalotakiwa kulijibu

Cha kushangaza wanalikwepa,hata yule dada kashindwa[Mish]?


Maajabu sasa,kila dini inadai Mungu wao ni mwenye nguvu zote

Hii kitu kimantiki ipo sahihi kweli?

Tunaweza kuwa na computers mbili,zinazoweza kushinda kila mchezo wa drafti[chess] bila kutoa sale?

Na tukizipambanisha,ipi itashinda kama kila computer ina uwezo wa kushinda bila kutoa sale hata mechi moja?


Tuwaiteje sasa?misukule?
Katika uislamu ni tofauti unavyofikiria,uislamu unasema na kufundisha Mungu mmoja tu,kwa viumbe wote,kwa mwenye dini na asiye na dini,Mungu ni mmoja.
 
Kukataa kutukuwepo Mungu,wakati MATOKEO ya kuwepo kwake,yanaonekana.
Moja ya mfumo aliouweka Mungu kwa binadamu ni kwenda choo,kama ungeweza kujizuia kwenda choo,usiende maiha yako yote,hapo ungeweza kusema,hayupo unakuendesha maisha yako.
Ukisema hakuna Mungu,huo ndio uthibitisho wa kuwepo Mungu.
 
Unaposema hayupo Mungu,ndio umethibitisha kuwepo,ni sawa kusema fulani hana akili,ni kuwa iko akili lakini kwa fulani ndio haziko hizo akili.
Kwa hiyo wewe unayesema Mungu hayuko,hayuko kwako,lakini yupo,hayupo kwako kwa sababu hutaki kukubali yupo,wakati Mungu yupo.

Duara yenye pembe tatu ipo?

Bachelor aliyeoa yupo?

Bikra aliyezaa yupo?

Mtoto mchanga mwenye wajukuu yupo?

Pembe tatu yenye nyuzi zaidi ya 180 ipo katika Euclidean geometry?

Hivyo vitu vyote kimantiki haviwezekani,kwa hiyo Kiranga akisema hivyo havipo ina maana havipo kwake tu?

Mungu Hayupo si kwasababu umeshindwa kutoa uthibitisho

Hayupo kwasababu anajipinga yeye mwenyewe ni sawa na Pembe tatu duara.
 
Kukataa kutukuwepo Mungu,wakati MATOKEO ya kuwepo kwake,yanaonekana.
Moja ya mfumo aliouweka Mungu kwa binadamu ni kwenda choo,kama ungeweza kujizuia kwenda choo,usiende maiha yako yote,hapo ungeweza kusema,hayupo unakuendesha maisha yako.
Ukisema hakuna Mungu,huo ndio uthibitisho wa kuwepo Mungu.

Nina mashaka na utimamu wako.
 
Back
Top Bottom