These Are The Top USAID Recipients—From Religious Groups To Major U.S. Companies—As Trump Targets Agency

These Are The Top USAID Recipients—From Religious Groups To Major U.S. Companies—As Trump Targets Agency

Hivi niwaulize ndugu zangu USA wanapata wapi haya mabilioni ambayo wanatapanya Dunia nzima kwa style hii??? Imagine Kanisa linapewa Bil 4 dola unadhani PAPA atasema jambo akisikia USA wanaua watu????
Hizo sio za kanisa na hakuna hata cent inayo ingia kanisani
 
Aga Khan haihudumii wa vipato vya chini kumuona specialist wa dental ni zaidi ya TZS 170,000 per single visit wananchi wangapi wanaweza mudu hiyo gharama?
Hata hiyo ruzuku isingetosha halafu elewa aga khan haikuanzishwa ili kuhudumia maskini hamna issue za charity pale ni biashara ile kama ilivyo saifee, tmj, hindumandal na regency sasa ushawahi kusikia saifee, tmj au regency wanaombwa na serikali watoe huduma pungufu ya bei then wapewe ruzuku?
Unafikiri Aga Khan hata wangeombwa wangekubali? unafikiri Aga khan wanapenda kuhudumia wagonjwa hohe hahe tena wengi ka nyuki? ile ni hospital ya wanaojimudu kichumi ni ya wachache ile huwezi linganisha na KCMC au Bugando inayohudumia mpaka mwananchi maskini wa kutupwa hohehahe wa kazuramimba.
KCMC, Bugando lengo ni kuhudumia maskini kabisaa na kuna sadaka kibao za watu mle na ndiyo maana zilianzishwa ilikuwa ni watu walitoa sadaka zao kuwasaidia wengine.
Aga Khan ni pure business na ni kwa ajili ya wachache
Infact vitu vya Aga Khan ni kwa ajili ya wachache na wenye hela na hasa jamii yao na sio akina pangu pakavu. Akina pangu pakavu wao watibiwe za kanisa na serikalini.
Wachache wapi nisha wahi tibiwa aga khan Arusha pale nilikuwa nanoesa za kawaida tu, ila nilitibiwa.Unaijua Nairobi Hospital? ukifika kule utaiona Ag khan tena kama ya watu masikini.
 
Wachache wapi nisha wahi tibiwa aga khan Arusha pale nilikuwa nanoesa za kawaida tu, ila nilitibiwa.Unaijua Nairobi Hospital? ukifika kule utaiona Ag khan tena kama ya watu masikini.
Utaifananisha aga khan na hivi vituo vya afya vya serikali ambapo kila mtu anaenda kutibiwa? hivi ambavyo mama mjamzito anaenda anapata kujifungua bure? bei za aga khan zinalingana na za hospital za serikali? Ushasema uliwahi kutibiwa kwa hivyo ni mara moja ulienda au ni mara chache sana huwa unaenda huko. Kwa Tanzania bado Aga Khan, Regency, TMJ ni hospital za gharama kwa walio wengi na wengi bima zinawasaidia. Siyo kwamba hakuna hospital zingine za gharama mfano Sali na nyingine zipo ila hizol ni level zingine kwa maana ya gharama.
Halaf tunaongelea muktadha wa Tanzania ukileta ya Kenya nami nitakuletea ya S.A. n.k
 
Back
Top Bottom