This man is either a sadist or alimuua kibaka, akanywa bia kusherehekea?

This man is either a sadist or alimuua kibaka, akanywa bia kusherehekea?

Usishangae mzee, tunaongozwa na Saddist in Chief

1. Kupiga mpaka mashangazi Mtwara
2. Serikali haijaleta tetemeko Kagera
3. Dawa wa wasaliti Ikulu
4. Mapolisi wakiua wapandishwe vyeo
5. Nusu ya walioimba "tuna imani na Lowassa" wangepotea
 
Huyu sijui alipatikana vipi aiseee.. Katibu Mkuu wetu CCM, alisema anatakiwa kwenda shule, yaani atolewe uongozini, alafu aende shule huyu.. Hafai kabisa, anamharibia sana Mkuu wa nchi.. Ni aibu kubwa

Ndio wamejifunzia,kama baba yao alishatamka wazi walazwe chini majambazi wanyang'anye silaha haraka, atapiga shangazi za watu,watawasimulia wanaowatuma,iwish I kuldu bi igp wangewasimulia waliowatuma,kaka zao nao wakatamka watawapiga kipigo cha mbwa koko hadi wachakae hadi wabunge wa USA wakalaani kauli hio,unategemea nini toka Kwa wadogo zao si ajabu maneno kama hayo,ndio maana ya ukosefu wa utawala wa Sheria huo.Hayo madogo hizo ni Salamu Kwa upinzani. Watoto uiga tabia za wazazi wao.
 
Watu wanapotetea utawala wa Sheria huwa na maana yao.Hawa sura pana ndio watatuvurugia Amani yetu.We umuulie MTU ndugu yake nao wakiamua kulipa kisasi kutakalika?
 
Duu..watendaji wa awamu hii,si mchezo! Kila mmoja anajaribu kumu impress Mheshimiwa Rais bila kujali namna ya kufikisha ujumbe. Sina hakika kama kuna chombo cha kuwachuja hawa mabwana kabla hawajapewa majukumu wanayopewa.Kwanini wasipelekwe Simiyu kwa Anthony Mtaka akawape somo la maadili ya uongozi?
umewai kuibiwa mkuu
 
Hawa ni watu ambao watakapoondolewa madarakani na kutupwa nje.. wataanza kuelezea kuwa "walipotea tu". Labda anafikiri kwa vile ni Mkuu wa Mkoa basi yuko juu ya sheria. Sasa polisi na mahakama zina kazi gani? Lengo zima la kuwa na sheria na vyombo vya dola ni kwa sababu jamii imeendelea na haitaki kila mtu kuwa mshtaki, jaji na mnyongaji! Huyu ni kiongozi mbovu. Ila asipoangalia anaweza kuishia kama Ditopile.
umewai kuibiwa mkuu then what if mwizi kaja na panga ile unatoka kwenda kupambana nae kakukata bapa pwaaaa utamuangalia tu kisa unataka demokrasia na utawala wa sheria
 
sio kigezo wewe haujawahi kuiba?
so tuendelee kuibiana au sio ha ha ha ha ha iba nikuibie basi nyumba yako usiweke ma grill manake tunaambiana tanzania ni nchi ya amani wakati nyumba tunaweka mageti na magrill acha unafiki uende mbinguni komredi
 
Wanabodi,
Siamini ninachokisikia hapa kwa kiongozi huyu!.



Japo wote tunamasikio inawezekana sio wote tunaweza kusikiliza kitu tukasikia, hivyo kwa faida ya wengine naomba kusema kwa kifupi tuu mimi nilichosikia na kilicho nifanya nipandishe bandiko hili.

Kiongozi huyu anasema kibaka akiingia kwako hata kama ni kuiba chumvi, anakuwa ameomba mambo matatu.
1. Ameamua kuiba
2. Ameamua kuua
3. Ameamua kuuwawa

Amewaambia polisi wa mkoa wake kuwa kufuatia magereza kufurika, wayajibu maombi ya vibaka wote mkoani kwake kwa kuwapatia ombi lao la tatu yaani wauwawe!.

Kubwa kuliko ni akajitolea mfano yeye mwenyewe jinsi alivyomuua kibaka aliyevamia nyumbani kwake kwa kumpiga risasi mbili na kufa papo hapo, na yeye ili kukamilisha furaha yake kwa kufungua bia moja kunywa kwa kujipongeza!.

Kwa watu wanaojua kitu kinachoitwa psychoanalysis ya binaadamu, unaweza kumbaini a person of unsound mind kwa jinsi anavyoongea.

Kwa jinsi mtu huyu alivyoongelea hili tukio la kumuua kibaka na Kusherehekea kwa kunywa bia, I seriously doubt the soundness of his mind, this is a sadist!.

Naombeni sana msi question mamlaka yake ya uteuzi huwa inawaokota wapi watu kama hawa, kwa sababu huwa hakuna kipimo cha soundness of state of mind kabla ya uteuzi hi nina amini kabisa alipoteuliwa, mteua hakujua state of mind ya mteuliwa huyu!.

Kwa vile state of mind is not static, ni dynamic, inawezekana kabisa wakati anateuliwa he was OK, akaja kubadilika mbele ya safari, kama hata baada ya kuyasema haya ataachwa aendelee, huu utakuwa ndio uthibitisho kuwa hali hii inafahamika vyema, hivyo mwacheni apige kazi.

Kitu nitakachowaomba wana jf wenzangu mfuatilie, ni kitu kinachoitwa Karma kinavyoshughulikia watu kama hawa, hivyo bandiko hili liwekeni pending kwenye kumbukumbu zenu, ili siku karma itakapo anza ku hit back, tutakumbushana.

P

Kwa hapa umeamua kumsema hivi ili wanajukwaa tuone hauko biased ila nafahamu nyuma ya ubongo wako unajutia kuandika kitu kama hiki kwa kuwa inakuletea doa kwenye safari yako ya matumaini ya kutafuta uteuzi,kama mteuzi wake hajasema chochote kufuatia kauli hiyo,je vipi kuhusu wewe msaka uteuzi?
 
Acha ujinga, sasa mfungwa kulala siku nzima unaona sawa, yaani afanye uhalifu halafu kodi zetu zimlishe, duniani kote wafungwa hufsnyishwa kazi sana tu, wengine mnawaona wanatujengea mabrabara
Acha uongo duniani kote wapi huko? Wamarekani wafungwa wanafanya kazi kwa kulipwa wakiwa huko kifungoni japo ni in cents and a dollar or two an hour lakini sio kazi za bure za kushurutishwa..point ni extrajudicial beatings or killings ndio zinakemewa hapa!
 
Back
Top Bottom