Thomas: Baba yangu Arcado Ntagazwa, alikuwa akisumbuliwa na tatizo la changamoto ya kupumua na alipata matibabu mbalimbali

Thomas: Baba yangu Arcado Ntagazwa, alikuwa akisumbuliwa na tatizo la changamoto ya kupumua na alipata matibabu mbalimbali

dubu

JF-Expert Member
Joined
Oct 18, 2011
Posts
3,502
Reaction score
3,483
1613292370429.png
Dar es Salaam, aliyekuwa Mwenyekiti wa bodi ya wadhamini Chadema, Arcado Ntagazwa amezikwa nyumbani kwake Kimara jijini Dar es Salaam huku sababu ya kifo chake ikielezwa kuwa ni changamoto ya upumuaji.

Waziri huyo wa zamani aliyehamia Chadema mwaka 2010 akitokea CCM, alifariki dunia Jumatano Februari 10, 2021 katika hospitali ya Mloganzila alikokuwa akipatiwa matibabu.

Akisoma wasifu marehemu leo, Thomas amesema baba yake alikuwa akisumbuliwa na tatizo la changamoto ya kupumua na alipata matibabu mbalimbali.

"Februari 2, 2021 baba alizidiwa na kupelekwa hospitali ya Regency lakini hakupata kitanda tukashauriwa tumpeleke hospitali ya Mloganzila na kupokelewa kwenye kitengo cha dharura," amesema Thomas.

Amesema Februari 9, 2021 baba yake aliyewahi kuwa mbunge wa Muhambwe alizidiwa na kuhamishiwa chumba cha uangalizi maalum (ICU) hadi umauti ulipomkuta Februari 10,2021.

Ntagazwa amewahi kuwa naibu waziri wa fedha, ujenzi na uchukuzi, ardhi na waziri wa nchi ofisi ya makamu wa rais.

Chanzo: Gazeti la Mwananchi

Zaidi, soma:

 
... At least wameamua kuwa wawazi kuhusu chanzo cha kifo cha Mzee. Kujua tatizo ni hatua muhimu sana katika kukabiliana nalo! Apumzike kwa amani Mzee Ntagazwa.
Hawajawa wazi. Hakuna ugonjwa unaoitwa changamoto ya kupumua. Magonjwa yote kwenye hatua zake za mwisho upumuaji huwa wa shida na hatimaye husimama kabisa - ukisimama ndipo tunasema mgonjwa kaaga dunia.

Hivyo hawajawa wazi. Hawajasema aliugua corona kwa mjibu wa vipimo.
 
"Februari 2, 2021 baba alizidiwa na kupelekwa hospitali ya Regency lakini hakupata kitanda tukashauriwa tumpeleke hospitali ya Mloganzila na kupokelewa kwenye kitengo cha dharura," amesema Thomas.

Hapo ndio penye changamoto nzima kuliko hata ile ya kupumua. Wachache zaidi mtanielewa
 
Muhambwe imepata mapigo sana maana mhandisi nditiye nae katokea huko
 
Back
Top Bottom