TANZIA Thomas Mashali afariki dunia baada ya kushambuliwa na watu wasiojulikana

TANZIA Thomas Mashali afariki dunia baada ya kushambuliwa na watu wasiojulikana

Determinantor

Platinum Member
Joined
Mar 17, 2008
Posts
59,045
Reaction score
94,974
Radio Free Africa kipindi cha michezo asubuhi hii wametangaza kifo cha ghafla cha Bondia Thomas Mashali. Thomas ni bondia aliyeleta changamoto kwenye gemu na kuifanya ichangamke.

Chanzo cha Kifo chake inadaiwa kuwa kimesababishwa na kipigo cha wananchi hapa maeneo ya Kimara.


=======
Mashali aliyezaliwa kwa jina Christopher Fabian Mashale aliuawa baada ya kupigwa akiwa huko Kimara jijini Dar es Salaam. Inasemekana wakati akinywa pombe, ulizuka ugomvi na mtu mmoja ambaye anadaiwa kupiga kelele kusema Mashali ni mwizi na watu kuanza kumshambulia.

Ndugu zake wanadai kuwa walimkuta akivuja damu nyingi.

Taarifa zinadai kuwa alipelekwa katika hospitali ya Sinza Palestina kabla ya kupelekwa Muhimbili ambako mauti ilimkuta. Inasemekana kuwa hadi jioni alikuwa na bondia mwenzake, Francis Cheka.

Chanzo: Bongo5

PIA SOMA
- Uelewa wangu juu ya kundi la watu wasiojulikana

~ Matukio ya Watu kupotea na wengine kudaiwa kutekwa, nini kinaendelea kuhusu usalama wa raia

- Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana
 
kipigo tena? alikuwa Mwizi au wananchi kawakoses nn tena huyu jamaa?
 
Kwa taarifa za kunyapia nyapia inasemekan mpiga ngumi huyu kafa jana usiku.
Inasemekan alipigwa na watu wenye hasira kali baada ya kujaribu kuiba

Kama kuna mtu anajua msiba utakuwa wapi atujuze wapenda ndondi tukatoe heshima za mwisho kwa mpiga ngumi huyu.
 
  • Thanks
Reactions: dtj
Apumzike kwa amani..

[HASHTAG]#sad[/HASHTAG]
 
Hebu toa Taarifa inayoeleweka, kama alikuwa mwizi au mbakaji tusitoe pole wala RIP
 
Aliyekuwa bondia maarufu Thomas Mashali amefariki dunia usiku wa kuamkia leo maeneo ya kimara. Chanzo bado hakijafahamika. Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi. Amina
Source: Radio Free Africa
 
Back
Top Bottom