Thomas Sowell: Jinsi Ujamaa wa Nyerere ulivyoiharibu Tanzania

Thomas Sowell: Jinsi Ujamaa wa Nyerere ulivyoiharibu Tanzania

Lawama kwa nyerere zinasaidia nini kipindi hiki
Ili kujisahihisha yapasa kujua ulipokosea. Matatizo tuliyo nayo leo ya kiutawala (hivyo kimaendeleo) ni matokeo ya siasa mbovu na utawala wa hovyo wa JK Nyerere. Tukumbuke aliwahi kupewa jina la “Haambiliki”. Alijiaminisha kuwa yeye pekee ndiye alikuwa na uwezo na nia ya kuiongoza nchi kuondokana na aliowaita maadui watatu. Hakuvumilia maoni tofauti na yake. Aliwasweka ndani waliokuwa na udhubutu wa kumkosoa (Bibi Titi, Chipaka, Kamalisa et al). Kambona ilibidi akimbilie uhamishoni Uingereza. Jk akazungukwa na ‘machawa’ kama kina Kawawa ambao kazi yao kubwa ilikuwa ni mapambio ya kumsifu bwana mkubwa kwa kila aliloamua lifanyike. Kufikia miaka ya 80 uchumi wa nchi ukadorora kiasi kwamba watu walipanga misururu mirefu kujipatia mahitaji muhimu kama sukari, betri, viberiti nk. Itoshe tu kusema Nyrere alichangia moja kwa moja, na akiwa peke yake, kuiua nchi ilokuwa ikiitwa Tanganyika. Na leo utawala wa nchi na mapungufu yake yote vimejengwa juu ya msingi aloujenga na kuuacha Mwl Julius Kambarage Nyerere.
 
Lawama kwa nyerere zinasaidia nini kipindi hiki
Ili kujisahihisha yapasa kujua ulipokosea. Matatizo tuliyo nayo leo ya kiutawala (hivyo kimaendeleo) ni matokeo ya siasa mbovu na utawala wa hovyo wa JK Nyerere. Tukumbuke aliwahi kupewa jina la “Haambiliki”. Alijiaminisha kuwa yeye pekee ndiye alikuwa na uwezo na nia ya kuiongoza nchi kuondokana na aliowaita maadui watatu. Hakuvumilia maoni tofauti na yake. Aliwasweka ndani waliokuwa na udhubutu wa kumkosoa (Bibi Titi, Chipaka, Kamalisa et al). Kambona ilibidi akimbilie uhamishoni Uingereza. Jk akazungukwa na ‘machawa’ kama kina Kawawa ambao kazi yao kubwa ilikuwa ni mapambio ya kumsifu bwana mkubwa kwa kila aliloamua lifanyike. Kufikia miaka ya 80 uchumi wa nchi ukadorora kiasi kwamba watu walipanga misururu mirefu kujipatia mahitaji muhimu kama sukari, betri, viberiti nk. Itoshe tu kusema Nyrere alichangia moja kwa moja, na akiwa peke yake, kuiua nchi ilokuwa ikiitwa Tanganyika. Na leo utawala wa nchi na mapungufu yake yote vimejengwa juu ya msingi aloujenga na kuuacha Mwl Julius Kambarage Nyerere.
 
Mwl. Dr Julius Kambarage Nyerere aliyemuingiza chaka la Ujamaa ni Wazanzibari waliokuwa wamesomea uhanaharakati Cuba,East Germany, Soviet, Yugoslavia n.k
Mmoja wao ni Profesa Abdullah Babu waziri wa Uchumi na mipango.

Pili muungano na Zanzibar,wao walifungua ubalonzi wa Ujerumani Mashariki wakati Tanganyika tulikuwa na Ujerumani Magharibi.
Mara baada ya Tanganyika kupata uhuru the mighty West Germany ilikuja kwa nia mmoja kuijenga Tanganyika kiuchumi,viwanda,Elimu iwe mfano wa kuigwa duniani.Mjerumani alikuuja kwa mbwembwe tena akitaka kumuonyesha Mwingereza kuwa hawakufanya lolote kwa miaka 70.
Mara huko Zanzibar nayo ikafungua ubalozi na East Germany.mbaya wa West Germany.
Mbabe West Germany akamtaka Raisi Nyerere afunge ubalozi wa East Germany mara mmoja. Nyerere akawajibu wasimchagulie rafiki.
West Germany ikafuga ubalozi Dar ndio hivyo Mjerumani akatutosa mmoja kwa mmoja.

Karata ya pili Nyerere aliwakimbilia Israel wahimarishe vyama vya Ushirika,kilimo cha kisasa kwa peasants. Kuanzisha Jeshi la kujenga Taifa .
Cooperative Unions zikashahimili,Mashamba darasa ya kilimo yakafunguliwa,ukakamavu wa kujenga utaifa kwa wasomi kupitia JKT ukatamalaki.
Lakini 1967 six days war kati ya Israel na Nchi za Misri, Jordan na Syria,Tanzania ikavunja uhusiano na Israel.

Nyerere karata ya tatu akiambatana na Abdullah Babu kwenda China ya Mao kutafuta ufadhili wa kujenga reli ya Tazara na mengine yakafuata ndio ikazaliwa Azimio la Arusha ambalo ndio siasa ya ujamaa na kujitegemea.
Ukisikia mtu anapinga UJAMAA ujue umekutana na mtu mpumbavu
 
Back
Top Bottom