Thomas Sowell: Jinsi Ujamaa wa Nyerere ulivyoiharibu Tanzania

Thomas Sowell: Jinsi Ujamaa wa Nyerere ulivyoiharibu Tanzania

Ifio
Hii mada ndio nimeamini kweli hii nchi watu uwezo wa kufikiri ni mdogo sana,huyo Mzungu ni Mpumbavu kama wanaomuunga mkono walivyo Wapumbavu zaidi yake,

Unapomzungumzia Nyerere lazima Akili itulie sio anaropoka ropoka kama kuna kitu kimeingia sehemu za Siri,

Swali la kwanza la kujiuliza kama Great Thinkers mnavyojiita humu ndani,nini maana ya Uhuru kwa wakati ule kipindi watu weusi wametoka kunyanyaswa, kufanywa watumwa na kila baya kutoka kwa hao mabwana zenu weupe?

Kwann tulipigania Uhuru?

Nyerere anakabidhiwa nchi tulikuwa na wataalamu wangapi wazalendo wa kuleta hayo maendeleo ya haraka haraka?

Kwanini tulikuja na Azimio La Arusha?

Mmesoma au kusikiliza hotuba ya Nyerere ya miaka 10 ya kujitawqla tangu nchi ilipopata Uhuru maendeleo ambayo tuliweza kupiga kuzidi miaka ya hao mbwa weupe waliyotutawala?

Anguko la jumuia ya Afrika mashariki?

Vikwazo vya kiuchumi hasa upatikanaji wa vipuri katika mitambo ya viwanda vyetu tulivyokuwa tumeanza kuanzisha hao mbwa kutotupa kwa wakati ili viwanda vife?

Kupanda kwa bei ya Mafuta miaka ya 70s kulikopelekea mtikisiko wa uchumi karibu Dunia nzima je?

Vita vya Uganda na Ukame uliokuja baadae?

Nyerere tunamuheshimu kama kiongozi aliyejharibu kujenga Misingi ya hii nchi licha ya changamoto zilizokuwepo kipindi hiko,bila ya Nyerere sisi tuliopo kwenye sekta ya Madini tusingeweza kupata Leseni za umiliki wa Uchimbaji wa Dhahabu au hata kumiliki Ardhi pengine,

Huko nchini China raisi wa kwanza Mao anaheshimika sio sababu ya kujenga Fly Over au Bullet Trains,watu wengi walikufa chini yake ila yeye alipigania China kwanza na maendeleo ya mtu mmoja mmoja baadae,Deng Xiaoping kaleta mabadiliko ila misingi ya Mao unafanya kazi mpaka leo.

Nchi haijengwi na mtu mmoja na ndio maana alitoka madarakani akawaachia wengine,lakini mpaka leo watu wapumbavu bado mnalaumu.

Swali la kujiuliza kabla hujamlaumu Nyerere wewe binafsi umefanya nini kuisaidia hii nchi?

Zidumu Fikra Za Mwalimu!
 
Ukimsoma Deng Xiaoping vizuri ukamsoma na Mao Zedong vizuri ukasoma kipindi ilichopitia China wakati wa Mao hasa miaka kumi ya mwisho wa utawala wake na ukasoma kipindi ilicho pitia China chini ya Deng hasa miaka ya mwanzo ya utawala wake ukarudi kusoma tena ulicho andika utaona umeandika ujinga.
Nafikiri ujinga wa kwanza ni wewe mwenyewe kutokujua nilichoandika,tena sio ujinga inawezekana ukawa mpumbavu, nimesema Mao ndie kajenga misingi ya China,huyo mwingine kafungua nchi kipindi watu wana mindset ya nchi kwanza kutoka kwa Mao,kama nimeandika ujinga kwanini Mao bado anaendelea kuheshimika nchini China?
 
Nimezaliwa wakati President Mkapa ni Raisi, hivyo siwezi nikasema nina jua yaliyojiri wakati wa Urais wa Nyerere.

But, kutoka hadithi za Babu na Babaangu, na kutoka vitabuni n.k. Nyerere was the Greatest, still the greatest amongst African and World leaders alike Today.

His intellect and vision were unmatched then and still unmatched Today.

Hata hivyo sihitaji mzungu aje kuniambia mazuri au mabaya yake.

Ushahidi upo wazi leo hii.

Watanzania wanajitambua.
wewe umezidisha sifa tena. Sisi wengine tumekulia katika kipindi chake na kuyaona mengi sana ambayo nyinyi generations za sasa munadhania ni uongo.
 
Bila wakoloni mngekuwa mshapotea kwa kuugua UKIMWI,vipindupindu na Malaria.Bila mkoloni mpaka kesho mngekuwa mnakunya machakani.Mkoloni mpaka kesho anaendelea kutujengea mashimo ya choo😂😂😂upendo ulioje huo.Kula ule wewe ila karaha ya mavi yako anaona mtu yupo huko maelfu ya maili Ulaya😣😣😣

Ashukuriwe mkoloni kwa kututoa tongotongo na kutustaarabisha maana mpaka kesho bila mkoloni Waafrica wangekuwa kundi moja na punda,nyani na sokwe.

Ashukuriwe mkoloni maana bila yeye magari,ndege na treni ingekuwa ni maajabu walau saivi tunaenda nao bampa tu bampa ukitoa ukiritimba wa kodi ya TRA leo tungekuwa tunamenya maganda na kuendesha gari mpya zerooo KM🤗

Mkoloni hana tunachomdai kwakua hatuna kitu tumewaprove wrong tangu wametuachia nchi zaidi ya kutaka na kupenda kujifananisha nao.

Ikiwapendeza wakoloni warudi AFRICA.Wajitwalie tena hili bara maana muafrika ameonyesha hawezi ishi bila mzungu.


📌📌MKOLONI AACHWE APUMZIKE AMILIFANYIE MENGI MAZURI HILI BARA LA GIZA.
👇
 

Attachments

  • Screenshot_20241012-181144 (1).jpg
    Screenshot_20241012-181144 (1).jpg
    52.3 KB · Views: 1
Kuendelea kumlaumu Nyerere kwa katiba mbovu ni kuonyesha jinsi gani sisi tuliopo sasa tusivyo na uwezo wowote.

Kama tunajua ni mbovu kwa nini hatutengenezi nyingine iliyo bora zaidi?

Hapo Nyerere hastahili lawama yoyote ile.
Utabadilishaje katiba kwa aina hii ya bunge tulilo nalo lililojaa wabunge wa Ccm wanaopatikana kwa favour ya katiba iliyopo?.
Sio rahisi kukata mkono unaokulisha
 
Kuna makala ya Profesa Babu anasema Western trained Nyerere hakujua kabisa propaganda za nchi za Kikominist katika safari yao ya kwanza kutembelea China anasema alionyeshwa vijiji vya ujamaa viko na nyumba,maji umeme,shule,hospitali, barabara nzuri,maduka.Kumbe ni vya kuigiza tu.
Anasema Nyerere alienda amevaa western suit lakini kurudi Tanzania akaja amebatizwa na ki Mao,hakuvaa tena western suit.
Kwa lugha nyepesi Nyerere was Compromised by Chinese.Alifuata njia nyingine ya siasa za kijamaa alizokuwa hazielewi vizuri.
Kitabu Cha 'Kaptula la Marx" Cha Prof Kenzirahabi
 
Shida ya watu weusi lipo Kichwani,tunapenda kulalamika bila ya kuja na suluhisho,hata kujaribu tunashindwa na mtu akijaribu ikitokea matokeo hayajakuwa mazuri ndio hapo hapo tunapoonesha kuwa hana Akili wakati wewe mwenye Akili umeshindwa kujaribu chochote.
NENO!

Mwalimu Nyerere alijitahidi kuyafanya yake, na sisi tuyafanye Yetu...

Ikiwa kweli tunajifahamu, sisi tunasimama juu ya mabega yake kiutaasisi.

HAPANA, Nyerere alikuwa mtu mwenye akili, fasaha ya kimafikara na ukomavu wa mawaidha na dhamiri kupita vituko vya hoja na viroja -- hoja na viroja vya mengi yanayozungumzwa humu mpaka hapa...

Kiufundi, ukweli wa mambo haupo kwenye 'Hoja ama Malumbano ya Hoja'--Upo kwenye 'Uono na Ufikirifu Mifumo'...

Kwenye Uono na Ufikirifu MIfumo, kila Shauri linamuktadha wake wa kufaa 'vina vya tafsiri' kwa wakati...

Shughuli ya Rais wa Kwanza wa Jamhuri ya Muungano, Mwalimu Kambarage Nyerere, ilikuwa na mabidishi/imperatives yenye kuzingatia Mazingira Tofauti ya (1) Ndani na hata (2) Nje ya 'Jamii Mabadilikoni : Taifa Changa la Watanzania/Waafrika'...

Hata Thomas Sowell, kama ilivyo kwa wasomi/msomi yeyote ambaye hajajiongeza kwa uono na ufikirifu mfumo, mashauri yake ya kihoja ni namna ile ya 'utambuzi wenye kuona mambo kwa sehemu'... Daima mashauri hayo yanaweza kubabaisha zile kambi za watu tofauti tofauti--kambi za udadavuaji wa mambo kwa hata ile misingi ya 'kukusanya data ama/na kujizima data' kidhamira ya utafiti na uchambuzi; na tena mahitimisho yake mahsusi ya visomo empirikali...

Ni kituko, mbele ya jicho la wenye ku-JUA ilivyobora, kuchanganya mashauri pasipo muktadha maridhawa wa ujuaji wa mambo... Ni ontolojia ya Ujinga/Unaivu! Mambo ya kuendekeza porojo na kuhorojoka...

Jamii na Ujamaa wake; ni fanusi tata ya sura-jamii, hadhi na utukufu wake... Ujamaa ni jambo la 'kufikirika' ama kusemwa 'uadilifu ulioni nadra/adimu' kupata kutimilika...

Ujamaa unahitaji jamii iwe na kiasi cha juu cha u-homojinesi ya kuyaishi mashauri ya Uhuru, Udugu, Haki na Amani...

Mambo ya Uhuru, Udugu, Haki na Amani ni mbegu ya utu-bora ambao wakati mmoja hata mwingine 'hupanda ama kuvuna' matokeo tofauti ya 'Mema/Maovu ya Ustawi wa Jamii'...

Uadilifu wa kiuongozi ni kuchunga idili la jambo/taifa -- maadili na miiko ya Sura, Hadhi na Utukufu wa Utaifa--iwe katika Nchi-taifa changa ama Nchi-Taifa iliyokomaa...

Ikiwa (m)wanajamii hajiongezi ili kulifikia hata lile daraja la kung'amua kuwa 'kuishi na maisha' ni mambo ya kuchagua na kujichagulia; basi wataacha kuwajibika na 'Wito wa Kiraia' na kujibwaga kwenye ulimwengu wa kunyoosheana vidole na kupakaziana lawama kwa mambo yao wenyewe kwenda kombo wakati mmoja hata mwingine.

Umoja na Uhuru--si kibwagizo cha 'Ngonjera Fulani' ya kitaifa... Ni shauri la uadilifu, linalotuwajibisha sisi sote tunaojitambulisha kuwa ni raia wa taifa la Tanzania...

Tusidanganyike nakupotezana kwenye 'Nguvu ya Hoja' ama 'Hoja ya Nguvu' , kwenye mashauri nusu nusu; kwa kuwa humo, kwenye michezo/mikato hiyo, kunaweza kuwa ni mambo ya 'Nyani haoni Kundule'...

Tuutafute mwangaza wa kujua ilivyobora juu ya mambo yote na yote... Hii ni nidhamu ya kuiishi 'Hekima'--hekima ya Utu bora.

Hekima inaleta Umoja...

Hekima inaleta Amani...

Hekima ni Uhuru !

Hmmm
 
tafadhali tupatie mfano wa hizo faida zilizopatikana kwenye umiliki wa ardhi, ambao kwa sasa ni utapeli na dhuluma kwa asilimia kubwa
Watu wachache hawajahodhi ardhi kubwa na kuwaacha raia wengi bila ardhi kama ilivyo Kenya. Kuhodhi ardhi na dhuluma za ardhi zilianza kuja baadaye sana baada ya Nyerere kuachia madaraka.
 
Mwl. Dr Julius Kambarage Nyerere aliyemuingiza chaka la Ujamaa ni Wazanzibari waliokuwa wamesomea uhanaharakati Cuba,East Germany, Soviet, Yugoslavia n.k
Mmoja wao ni Profesa Abdullah Babu waziri wa Uchumi na mipango.

Pili muungano na Zanzibar,wao walifungua ubalonzi wa Ujerumani Mashariki wakati Tanganyika tulikuwa na Ujerumani Magharibi.
Mara baada ya Tanganyika kupata uhuru the mighty West Germany ilikuja kwa nia mmoja kuijenga Tanganyika kiuchumi,viwanda,Elimu iwe mfano wa kuigwa duniani.Mjerumani alikuuja kwa mbwembwe tena akitaka kumuonyesha Mwingereza kuwa hawakufanya lolote kwa miaka 70.
Mara huko Zanzibar nayo ikafungua ubalozi na East Germany.mbaya wa West Germany.
Mbabe West Germany akamtaka Raisi Nyerere afunge ubalozi wa East Germany mara mmoja. Nyerere akawajibu wasimchagulie rafiki.
West Germany ikafuga ubalozi Dar ndio hivyo Mjerumani akatutosa mmoja kwa mmoja.

Karata ya pili Nyerere aliwakimbilia Israel wahimarishe vyama vya Ushirika,kilimo cha kisasa kwa peasants. Kuanzisha Jeshi la kujenga Taifa .
Cooperative Unions zikashahimili,Mashamba darasa ya kilimo yakafunguliwa,ukakamavu wa kujenga utaifa kwa wasomi kupitia JKT ukatamalaki.
Lakini 1967 six days war kati ya Israel na Nchi za Misri, Jordan na Syria,Tanzania ikavunja uhusiano na Israel.

Nyerere karata ya tatu akiambatana na Abdullah Babu kwenda China ya Mao kutafuta ufadhili wa kujenga reli ya Tazara na mengine yakafuata ndio ikazaliwa Azimio la Arusha ambalo ndio siasa ya ujamaa na kujitegemea.
Mzee Mohamed Said tupe mwanga zaidi kuhusu huyu "mzee wako" Abdullah Babu aliyeshiriki kutuingiza kwenye zimwi la Ujamaa.
 
Uelewe Jambo moja unapojadili haya mambo.
Ujamaa na ukomunisti Ni vitu viwili tofauti.
Kiingereza Socialism na Communism.
Tanzania haijawahi kuwa nchi ya ukomunisti bali Ujamaa.
Kuna nchi nyingi tu duniani hata Ulaya zenye Ujamaa na wajamaa zilizo endelea. Ndani ya Marekani, Germany na kwingineko wapo watu wanachama wa chama cha kijamaa.
Mfumo wa Nyerere japo uliitwa ujamaa ila kiutendaji ulikaa zaidi kama Ukomunisti kwa kuangalia sera za vijiji vya ujamaa (villagization), serikali kuendesha biashara hadi za maduka ya mtaani yaliyoitwa ya ushirika na mfumo wa chama kimoja. Ujamaa wa nchi za Ulaya kama Denmark, Norway na Sweden ni ''Welfare states" ambapo sehemu kubwa ya uchumi bado ni soko huria lakini serikali inahakikisha raia wote wanapata huduma bora za afya na elimu bila kujali kipato chao, pia demokrasia imeshamiri.
 
Naongeza tu

Ieleweke.Kwa wale wasiojua, Muasisi wa Ujamaa alikuwa Otto Van Bismark wa Ujerumani. Na baadae kuigwa na Nchi zingine.

ujiridhie kuhusu hilo

Wazungu walijua bila ya uwepo wa aina fulani wa Ujamaa na Kujitegemea, Capitalist system ina lenda ku Collapse.

=======

Itoshe, kuna wajinga na wapuuzi waliomezeshwa nakukaririshwa maneno, kwamba Ujamaa na kujitegemea ni Itikadi ya Kisiasa kama ilivyo itikadi ya WaCommunist wa Ulaya mashariki. Sio kweli kabisa.
Hawajui wanachokiongelea.
Umedanganya waziwazi uko shuleni sijui mnasomaga nini
Karl marx ndo muanzilishi wa huu ujamaa yeye ndo aliyepropose comunism manifesto acha uongo

Ussr chini ya vladimir lenini na stalin mwaka 1917 ndo watu wakwaza kuweka idea ya ujamaa kwenye matendo
 
Nafikiri ujinga wa kwanza ni wewe mwenyewe kutokujua nilichoandika,tena sio ujinga inawezekana ukawa mpumbavu, nimesema Mao ndie kajenga misingi ya China,huyo mwingine kafungua nchi kipindi watu wana mindset ya nchi kwanza kutoka kwa Mao,kama nimeandika ujinga kwanini Mao bado anaendelea kuheshimika nchini China?
Hata Nyerere bado ana endelea kuheshimika Tanzania hapa hatuzungumzii habari za kuheshimika ulichoandika sasa na muda uliopita ni muendelezo wa ujinga
 
Mfumo wa Nyerere japo uliitwa ujamaa ila kiutendaji ulikaa zaidi kama Ukomunisti kwa kuangalia sera za vijiji vya ujamaa (villagization), serikali kuendesha biashara hadi za maduka ya mtaani yaliyoitwa ya ushirika na mfumo wa chama kimoja. Ujamaa wa nchi za Ulaya kama Denmark, Norway na Sweden ni ''Welfare states" ambapo sehemu kubwa ya uchumi bado ni soko huria lakini serikali inahakikisha raia wote wanapata huduma bora za afya na elimu bila kujali kipato chao, pia demokrasia imeshamiri.
Social democracy.
 
Mao mwenyewe alikuwa kashaingia chaka , mamilioni waliokufa kutokana na sera zake tushukuru hatukupitia hayo
Nyerere dini ilimuingia iliyotengeneza hofu ndogo.

Huyu alivutiwa na ukomunisti wa huko Uchina alipoenda lakini kuiacha dini ilikuwa ngumu kwake alikuwa mkomunisti uchwara
 
Misingi mikuu ya Ujamaa na Ukomunisti inafanana kwa kiasi kikubwa Sana, almost kama Ujamaa na Ukomunisti ni Kitu kimoja. There is a very slight difference between them.

Aidha, Tanzania ni nchi ya UKOMUNISTI, labda wewe hauna uelewa wa kutosha kuhusiana na masuala haya ya Ukomunisti/Ujamaa.
Sera ya Mwl.Nyerere ya Azimio la Arusha ni Copy and paste from USSR, China, Cuba and North Korea.

Nakupa Homework: Fanya Utafiti wako wa kina kuhusu Sera ya Itikadi ya Juche kwenye Ukomunisti na Kisha linganisha na Sera za Mwl. Nyerere juu ya Siasa zake za Ujamaa na Kujitegemea (misingi 3 ya Ukomunisti: Jaju, Jiraw na Jurip)
Tanzania ilikuwa na ukomunisti uchwara wa China na North Korea na iliongozwa na mkomunisti uchwara
 
Back
Top Bottom