Thread maalum ya wapenda Pikipiki kubwa

C
Dah parefu mzee. Nitatafuta basi ka cc300 ila nahisi shape itakua mbaya. Nimependa haka.

Zile naked CB sio mdau sana.
CBR300 haina mzuka ni single cylinder engine. Bora uchukue CBR250RR ni inline 2 cylinder hata toleo la nyuma au CBR400RR inline 4.

Ukichukua tofauti na hiyo iwe toleo Racing Replica (RR) ndio zina sound ya kibabe za kuanzia 2&4 inline cylinder hata iliwa chini ta 600cc
 

Sio kweli, most expensive bike inaitwa Dodge Tomahawk. Bei yake ni $550,000.
Google uione
 
Wakuu, kuna watu Insta wanajiita biketz wanadai wana import bikes kutoka Japan kuja Bongo. Nimekua naangalia bei zao naona no cheap sana. Na wanasema unalipia kwanza ndio pikipiki inakuja.

Mfano ni hizi hapa:

Hii BMW inauzwa Mil 8.


Na hii Ducati Mil 8.5



Kuna uwezekano ikawa kweli, lakini bei zao naona kama ndogo san.

Kuna mtu anawajua?
 
Hawa si wana ofisi kariakoo kabla ya Msimbazi, nitapita dukani kwao kisha jioni nitakupa mrejesho. Au nitamuuliza kuna dogo ni fundi bike hizi kubwa
 
Hap matapeli kaka nimepita pale dukani Msimbazi jioni wale wanaitwa Bikers Corner Ltd. Hata kwenye page zao za mitandaoni wanapatikana kwa jina hilo.

Cbr600 ipo njiani utamcheki boss wao namba hii 067 453 2555. Pale wana Kawasaki Ninja 400cc na Honda CB400 super four
 
Wacheki hawa namba ya boss wao nimekupa, kama utataka used za South Africa nicheki mwezi huu kuna gari itafatwa pick up pikipiki itapakiwa huku utalipia ushuru Tunduma
 
Boss shukrani sana aisee. Angalau nimepata pa kuanzia.
 
Hapo mwanzo sikuwaga na mapenz na pikpik kabisa lkn saiv aseh huniambi kitu kuhusu pikpik napenda saaan,hii mashine ni tam sana japo Mwenyez Mungu aniepushe na mabalaa huko road msuli wa paja hapo ulishachanika ila ni kudra za Allah zinatunusuru
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…