Timu kama Brighton inafundisha kuiishi na kuitekeleza mifumo, sera na taratibu za timu

Timu kama Brighton inafundisha kuiishi na kuitekeleza mifumo, sera na taratibu za timu

Southern Highland

JF-Expert Member
Joined
Mar 22, 2017
Posts
14,938
Reaction score
25,405
Hii ni moja ya timu zinazonivutia sana kwenye ligi kuu uingereza nje ya kushabikia Chelsea. Sera yao ni kukuza na kulea vipaji pamoja na kuuza kama anapatikana mteja. Kinachonivutia zaidi ni namna wanaweza kusumbua vigogo na kutawala kwa kiasi fulani ligi ya EPL japo wanakua wamepitia vipindi tofauti kwa wachezaji wao na benchi la ufundi. Wanaweza kuuza wachezaji na hata makocha lakini kukuta wanasua sua ni mara chache sana.

Toka kipindi cha Graham Potter, akaja De Zerbi na sasa wana kocha mdogo kuliko wote EPL Fabian Hurzeler wanaonekana tayari wamepshajipata. Hii timu haiogopi kuuza wachezaji wala kuondokewa na makocha. Wachezaji kama Lallana, Mac Allister, Caicedo, Cucurella n.k ni kati ya biashara nzuri walizofanya kwa vilabu vingine.

Sio kila timu inakua na malengo ya kubeba makombe.

Screenshot_20240824_173828_Instagram.jpg
 
Kila ligi huwa Kuna hiyo team ingawa zingine hushindwa kujua wakati wa kuuza na kuhifadhi nguvu eg mtibwa
Issue ya Mtibwa nadhani ni management yao inashindwa kupata vyao hai vya mapato. Wanakuza wachezaji wazuri ila kuwa mantain waje kupiga hela nzuri wanashindwa
 
Westham Kuna kipindi walikuwa na sera Kama hiyo, Southampton nao pia walikuwa na sera hizo kwa kifupi timu hizo malengo yao ni biashara ni Kama mtibwa ila Sasa iko chini.
Walishawahi kufanya ivyo ila sasa hawa mantain status kwa sababu wananunua wachezaji ambao wamesha mature kwenye timu nyingine. Ila hawa Brighton wananunua kwa bei ya chini halafu zile potential ambao wana umri mdogo kabisa
 
Kale kajamaa Mitoma ni noma sana, tukienda kucheza nao sisi Arsenal huwa namhofia yeye tu.

Ila mwanetu Welbeck hajawahi kutuangusha, huwa anatunyooshe watu sana.
Ngoja awafunge yeye mwenyewe ndio mtashangaa.
 
Hii ni moja ya timu zinazonivutia sana kwenye ligi kuu uingereza nje ya kushabikia Chelsea. Sera yao ni kukuza na kulea vipaji pamoja na kuuza kama anapatikana mteja. Kinachonivutia zaidi ni namna wanaweza kusumbua vigogo na kutawala kwa kiasi fulani ligi ya EPL japo wanakua wamepitia vipindi tofauti kwa wachezaji wao na benchi la ufundi. Wanaweza kuuza wachezaji na hata makocha lakini kukuta wanasua sua ni mara chache sana.

Toka kipindi cha Graham Potter, akaja De Zerbi na sasa wana kocha mdogo kuliko wote EPL Fabian Hurzeler wanaonekana tayari wamepshajipata. Hii timu haiogopi kuuza wachezaji wala kuondokewa na makocha. Wachezaji kama Lallana, Mac Allister, Caicedo, Cucurella n.k ni kati ya biashara nzuri walizofanya kwa vilabu vingine.

Sio kila timu inakua na malengo ya kubeba makombe.
Mkuu, nami napenda sana jinsi wanavyocheza. Sisi Arsenal huwa tunapata taabu sana kwa hii timu. Ila kumbuka kmligi ni ya England na siyo Uingereza.
 
Back
Top Bottom