Tito Magoti na Theodory Giyan wafikishwa Mahakamani, wafunguliwa mashtaka 3 yakiwemo ya Uhujumu Uchumi na Utakatishaji Fedha

Tito Magoti na Theodory Giyan wafikishwa Mahakamani, wafunguliwa mashtaka 3 yakiwemo ya Uhujumu Uchumi na Utakatishaji Fedha

Inasikitisha sana. Historia itahukumu huu utawala kama moja ya tawala za hovyo kabisa kupata kutokea nchini.
 
Kwa muda wote ambao Tito Magoti na Theodory Giyan wamekuwa kizuizini wamehojiwa kuhusu harakati zao mitandaoni, uhusiano wao na Maria Sarungi, Fatma Karume, na Zitto Kabwe na uvumi wa kwenye mitandao, LHRC imeeleza.

FB_IMG_1577200971564.jpg
 
V for Vendetta
 

Attachments

  • main-qimg-f8bac507c644008113198ec0dee7d857-c.jpg
    main-qimg-f8bac507c644008113198ec0dee7d857-c.jpg
    177.2 KB · Views: 1
Nchi haiongozwi kwa mihemuko inaongozwa kwa sheria. Kidomodomo kimemponza, kwani unafikiri wote wasiondika ni wajinga? Hakuna chuki hapo angekuwa mama yako katukanwa vile wakati wewe unafahamu fika huyu kijana anapata pesa kwa njia za udanganyifu ungemwachia? Msiingize mambo ya kimataifa kwani huko kwao na wenyewe si wana sheria zao?

Kwahiyo kosa ni kidomodomo au kujipatia pesa kwa njia ya udanganyifu? Sheria zipi tunazoongozwa nazo? za utakatishaji au uhujumu uchumi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama wamehojiwa haya, halafu wanafunguliwa kesi ya uhujumu uchumi hii ni aibu kwa vyombo vyetu vya dola. Inaonesha sura fulani ya unyanyasaji na uonevu kuzingatia itikadi za vyama. Kiukweli kama hivi ndivyo mambo yalivyo Mwenyezi Mungu aingilie kati, sidhani kama tunaenda sawa kama taifa
 
Back
Top Bottom