TLS - Kongamano la kitaifa kujadili matukio ya utekwaji na upoteaji wa raia nchini Tanzania

TLS - Kongamano la kitaifa kujadili matukio ya utekwaji na upoteaji wa raia nchini Tanzania

(LIVE VIDEO IPO CHINI)

Leo tarehe 5 Oktoba 2024, mawakili wote wa Tanzania bara, hasa wa jijini Dar es Salaam, wanakutana katika jengo la Ubungo Plaza, Dar es Salaam, ili kujadili suala la utekwaji na upoteaji wa raia nchini Tanzania. Tukio hili la kitaifa linaandaliwa na Tanganyika Law Society (TLS) na limehudhuriwa na wanachama wa TLS pamoja na wageni waalikwa kutoka taasisi mbalimbali.
Lengo kuu la kongamano hili ni kujadili hatua za kisheria, historia ya matukio haya, na mikakati ya kuzuia na kuwajibisha wahusika, sambamba na kuangalia namna ya kuwasaidia waathirika na familia zao.

Tukio hili ni la umuhimu mkubwa katika kulinda haki za binadamu na kupambana na vitendo vya upoteaji wa raia nchini.

Kongamano linaanza rasmi saa 9:00 asubuhi na litakuwa mubashara kupitia uzi huu pamoja na Wakili TV kwenye YouTube kwa wale ambao hawawezi kuhudhuria.


#WakoWapi #TLSSymposium #UtekwajiNaUpoteaji

Kongamano linaanza saa tisa asubuhi?
 
”Kama nchi, hakuna sheria inayoshughulikia upoteaji na utekwaji wa watu nchini” - Jaji mstaafu Makaramba​
 
“Tatizo kuu ni pamoja na kukataa tatizo lenyewe, serikali inakataa kuwa hakuna tatizo la watu kupotea ama kutekwa”

“Tanzania inatakiwa kuanzisha sheria mahususi kuhisiana na masuala ya upoteaji na utekwaji wa watu na kuhakikisha vitendo hivyo vinafanywa kosa kisheria”.

Jaji mstaafu - Makaramba
 
“Tatizo kuu ni pamoja na kukataa tatizo lenyewe, serikali inakataa kuwa hakuna tatizo la watu kupotea ama kutekwa”

“Tanzania inatakiwa kuanzisha sheria mahususi kuhisiana na masuala ya upoteaji na utekwaji wa watu na kuhakikisha vitendo hivyo vinafanywa kosa kisheria”.

Jaji mstaafu - Makaramba
Hapa ndio penye shida kubwa
 
Mimi sijaelewa
Wanatengeneza mkakati au wanafundishana kwa slides?
Ni muhimu kufundishana ili kuona ni kwa namna gani vitendo hivi ni kinyume na sheria kabla ya kuingia kwenye mkakati wa namna ya kudeal navyo.​
 
“Mtu anapopotea na kutojulikana ni wapi alipo, jukumu hilo linaamia kwa serikali kufanya uchunguzi”

Watu wote waliopotezwa pamoja na familia zao zinatakiwa kufidiwa pale ambapo muhanga anapo potezwa”

Dr.Nshalla,Esq
 
Yakiitishwa maandamano hujitokezi unamwachia Mwenyekiti wa Maisha Mbowe na mtoto wake ila vitu lainilaini kama hili Kongamano uko mstari wa mbele. Bibi Erythrocyte uwe unajitokeza hata kwenye maandamano anayoitisha Mwenyekiti wa Maisha Mbowe!
Off point..!!!
Hayakuhusu endelea na issue za uchawi.
Ok karibu nikupe tiba
 
Yakiitishwa maandamano hujitokezi unamwachia Mwenyekiti wa Maisha Mbowe na mtoto wake ila vitu lainilaini kama hili Kongamano uko mstari wa mbele. Bibi Erythrocyte uwe unajitokeza hata kwenye maandamano anayoitisha Mwenyekiti wa Maisha Mbowe!
Off point..!!!
Patachimbika ,Ponda ndani ,mwamakula ndani ,pambalu ndani,muliro ndani.
Ngoma inogile
 
Back
Top Bottom