TLS: Kwa Mujibu wa Katiba, sasa Tanzania haina baraza la Mawaziri, Rais Samia atakiwa kuteua Waziri Mkuu ndani ya siku 14

Vipi bado upo na TLS au kwa mama?
 
Hajafuata, haya Sasa tuone huko kuparangana
 
Waziri mkuu ni jambo jingine. Katiba ikon clear kabisa kuwa waziri mkuu akiondoka/akiondolewa na baraza linavunjika. Hili la rais halina kifungu kama cha waziri mkuu. Ila nadhani ufafanuzi wa TLS uko sahihi.
Bado TLS wapo sahihi?
 
Vipi leo umepata jibu au bado?
Naona umekuja hapa kama kipofu, hujuia hata nini kilisemwa TLS na nini ambacho Mama amefanya leo.

kuweka kumbukumbu sawa hapa JF, TLS walisema kuapishwa kwa Mama Samia Suluhu kuwa rais maana yake ni kuvunjwa kwa baraza la mawaziri la zamani. Na kuundwa kwa baraza jipya kunaanza kwa kuteua waziri mkuu mpya ambaye kisheria anapitishwa bungeni kwanza kabla ya kuapishwa, na ndio mawaziri wengine wafuate kuteuliwa na wote wataapa kwa rais mpya!

Sasa leo mama Samia katangaza baraza lake la mawaziri (kabla ya kuteua kwanza waziri mkuu wake na kwenda bungeni kupitishwa)! Alichokifanya mama Samia ni kama anajichanganya, hajui afanye nini na kipi asifanye. Anadandia ukweli na kuuchanganya na uongo.
 
Wewe bado hujielewi, mama Samia alichofanya ni mabadiliko kidogo kwenye Baraza na sio kutangaza baraza jipya. Hivi huwa mnapeleka likizo hizo akili zenu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…